magnifico
JF-Expert Member
- Jan 14, 2013
- 7,438
- 13,178
Mkuu nimemuonesha Aden Rage hapo ulipoandika "Intellectuals" amecheka hadi machozi yamemtoka.Kuna Watu mna Upumbavu kweli kweli hivi dunia ya leo kuna haja ya Timu Kujificha ikiwa inafanya Mazoezi yake? Liverpool FC ikicheza na Manchester United FC timu zote hizi zikijiandaa na huo Mpambano wao ( Derby ) huwa zinajificha? Kwa Mtizamo wa hovyo kama huu wako Soka la la Tanzania Kukua na kuwa la Kisayansi ni ngumu.
Kiufundi na Kisayansi pia kwa Mpira wa Siku hizi kuna Kitu kinaitwa Football Intelligence au Team Intelligence Department ambapo Wapinzani wako hawana haja ya Kutizama Mazoezi yako bali Mikanda tu ya Video ya Mechi zako au ujio wao Physically kuja Kutizama Mechi zako za Ligi na hata za Kimataifa ulizocheza kupitia Mtu aitwae Team Performance Analyst ( ambaye Simba SC pia wanae kutokea nchini Zimbabwe ) zinatosha Kwao Kukusoma ulivyo Kiubora na Kimapungufu.
Mwisho Mashabiki wa Simba SC ni Waungwana, Wastaarabu na Simba SC ndiyo Klabu yenye Intellectuals wengi ndani na hata nje ya Tanzania hivyo hawawezi Kumvunjia Heshima CEO Wao ( Wetu ) Barbara Gonzalez kama ufikiriavyo Wewe Mwana Yanga SC Mnafiki ila hapa umejifanya ni Simba SC Mwenzetu.