Yoda
JF-Expert Member
- Jul 22, 2018
- 37,582
- 46,180
- Thread starter
- #41
Ukizaa wawili au mmoja unakuwa katika nafasi nzuri ya kufanya saving ya maana ambayo unaweza kuiwekeza na/au kuja kuwasaidia baadaye kama watahitaji msaada wako. Ukiwa na watano huwezi kufanya saving yoyote ya maana, kila utakachokipata itakuwa kwa ajili ya kuwalisha tu, hata mavazi au makazi bora itakuwa vigumu kuwapatia na baadaye wakija kutaka msaada wowote kwako hutaweza kuwapatia na badala yake wewe ndiye una uwezekano mkubwa wa kugeuka mzigo tena kwao wakiwa na haso zao.
Tatizo lako naona unachukulia hii issue kama kucheza kamari; "ukizaa watano, watatu wawe machinga na bodaboda, na wengine ndio wafanikiwe"
Unaweza zaa mmoja huyo huyo akawa bodaboda, au ukazaa wawili wote wakawa bodaboda na machinga, pale ambapo ajira zinatoka kwa kuajuana uta-guarantee vipi uhakika wa mwanao kuipata hata kama ana elimu?
Narudia tena, uzazi wa mpango sio kigezo/uhakika wa kupata ajira kwa kijana wa kitanzania asie na connection.