Uzazi wa mpango ni suluhu ya matatizo mengi ikiwemo umachinga uliokithiri

Yoda

JF-Expert Member
Jul 22, 2018
37,619
46,258
Binadamu yoyote tofauti na wanyama ili aweze kukua vizuri, apate maendeleo na astawi anahitaji msaada, uangalizi na muongozo wa muda mrefu wa wazazi, familia, ndugu, marafiki, majirani na Serikali.

Anahitaji apatiwe chakula bora, mavazi bora, makazi, na elimu bora tangu akiwa mdogo hadi angalau miaka 18. Akimaliza masomo yake anahitaji apewe mazingira mazuri/awezeshwe kujipatia kipato kupitia kazi za hadhi nzuri "decent jobs". Wenye jukumu hili ni Familia yake na Serikali. Wanaposhindwa kutimiza jukumu hilo ndipo tunaona taifa likizalisha vijana lukuki ambao ni wamachinga, wauza pipi na maji barabarani, bodaboda na mama ntilie wanaopikia kuni katikati ya majiji.

Lawama nyingi zinaelekezwa serikalini kunapoteka matatizo yanayohusu kufuata utaratibu kwa makundi haya lakini ni vyema tujikite katika chanzo cha tatizo ambacho ni 1.sera za kiuchumi zilizoshindwa kufungua sekta za uchumi mkubwa wa viwanda, kilimo na huduma 2.

Kupuuza uzazi wa mpango kwa raia wengi. Ni lazima sote tukubali zama za kuzaa rundo la watoto ambao hujui hatma yao watakapofikisha miaka 20 zimepitwa na wakati. Hizi na zama za kuwa na watoto ukiwa na mpango kichwani wa jinsi gani watoto hao hawataishia kuwa makabwela wanaotanga tanga.
 
Unaweza kuzaa mtoto mmoja ukamsomesha mpaka degree au masters na asipate ajira.

Hivyo atarudi tu mtaani.

Suluhisho sio uzazi wa mpango, mbona wazee wetu walikuwa wanazaa dazani ya watoto na walikuwa wanawatengenezea future nzuri tuu? Yani ilikuwa toto ambalo linakuwa halina future basi limejitakia lenyewe.

Unforgettable
 
Binadamu yoyote tofauti na wanyama ili aweze kukua vizuri, apate maendeleo na astawi anahitaji msaada, uangalizi na muongozo wa muda mrefu wa wazazi, familia, ndugu, marafiki, majirani na Serikali..
Kufyatua watoto kupo zaidi kwa watu mafukara na wasio na elimu hasa maeneo ya vijijini, kwenye miji angalau presha ya maisha ya kujitafutia kwa ajili ya familia yanafanya watu angalau wawe makini kwenye kuleta watoto duniani.
 
Na suluhu ya mashamba yasio na watu wakuyalima ni ipi? Wote wamehamia mjini wameacha wazee wasio na nguvu ndio walime, suluhu ni ipi?
 
Na suluhu ya mashamba yasio na watu wakuyalima ni ipi? Wote wamehamia mjini wameacha wazee wasio na nguvu ndio walime, suluhu ni ipi?
Kilimo kina hitaji mtaji mkubwa kuliko kibanda cha mpesa watu wanajitahidi ila serikali inawakatisha tamaa aina msaada wowote kwa wa kulima, alafu mnategemea watu wafanye kilimo chamaana....... tatizo sio watt wengi hapana ni mipango ya hovyo ya serikali, hawaja ona kilimo kama kipaombele cha nchi
 
Kwa nini usimpe ajira wewe kwa kumuwezesha mtaji ? Kwani lazima akaajiriwe na watu wengine au serikali? Hawezi kusimamia biashara au mashamba yako?
Unaweza kuzaa mtoto mmoja ukamsomesha mpaka degree au masters na asipate ajira.

Hivyo atarudi tuu mtaani.

Suluhisho sio uzazi wa mpango, mbona wazee wetu walikuwa wanazaa dazani ya watoto na walikuwa wanawatengenezea future nzuri tuu? Yani ilikuwa toto ambalo linakuwa halina future basi limejitakia lenyewe.

Unforgettable
 
Binadamu yoyote tofauti na wanyama ili aweze kukua vizuri, apate maendeleo na astawi anahitaji msaada, uangalizi na muongozo wa muda mrefu wa wazazi, familia, ndugu, marafiki, majirani na Serikali..ataishia kuwa makabwela wanaotanga tanga.
Idadi ya watt ni kichocheo cha maendeleo China isingekua super power isingekua na idadi ya hao watu, tunashindwa kua na mipango mizuri kuleta maendeleo tunaanza kusinginzia kuzaa watt huo ni mtizamo wa zamani sanaa.
 
Umachinga utakuwepo tu hata kama patakuwepo na huo uzazi wa mpango, kama sekta binafsi na serikali kwa pamoja wanashindwa kuajiri angalau nusu ya wanaomaliza vyuoni kila mwaka, sioni ni kwa namna gani umachinga utamalizwa kwa uzazi wa mpango, labda watu wasizae kabisa.
 
Mashamba yapi yasio na watu nchi hii?
Unaelewa tofauti ya shamba na pori?
Unafikiri ukiwa na shamba au pori basi unaweza kulima tu na ukaushinda umaskini?
Unafahamu umaskini mkubwa nchi hii umejikita vijijini huko wanakolima na sio mijini?
Na suluhu ya mashamba yasio na watu wakuyalima ni ipi? Wote wamehamia mjini wameacha wazee wasio na nguvu ndio walime, suluhu ni ipi?
 
Uko sahihi mkuu, na hao wanaofyatuliwa zaidi na mafukara na wasio na elimu huko vijijini wengi ndio wanakimbilia na kuishia kuja kuwa wamachinga mijini.

Watoto wa matajiri na wa "middle class" hawawi wamchinga kamwe.
Kufyatua watoto kupo zaidi kwa watu mafukara na wasio na elimu hasa maeneo ya vijijini.......kwenye miji angalau presha ya maisha ya kujitafutia kwa ajili ya familia yanafanya watu angalau wawe makini kwenye kuleta watoto duniani.
 
Kama wewe ni maskini, fukara au mfanyakazi wa ngazi ya chini ukizaa watoto 5 kuna uwezekano mkubwa watatu wakaishia kuwa wamachinga na waendesha bodaboda na hao wawili ndio wakapata kazi au kufanya biashara ya maana. Uamuzi ni wako.
Umachinga utakuwepo tu hata kama patakuwepo na huo uzazi wa mpango, kama sekta binafsi na serikali kwa pamoja wanashindwa kuajiri angalau nusu ya wanaomaliza vyuoni kila mwaka, sioni ni kwa namna gani umachinga utamalizwa kwa uzazi wa mpango, labda watu wasizae kabisa.
 
Unaweza kuzaa mtoto mmoja ukamsomesha mpaka degree au masters na asipate ajira.

Hivyo atarudi tuu mtaani...
Umeongea vizuri sana ila ukumbuke ili uwe na watoto wenye future nzuri lazma nawe uwe na future nzuri kwanza!

Wazazi wetu walimudu kutokana na fursa zilizokuwapo huko nyuma wenye vichwa walisoma wakamaliza haraka na ajira zilikuwa ni za kumwaga tu!

Mtu anamaliza form 4 kuna michongo viwandani! Anamaliza 6 anapewa ofisi kabisa kama karani au mhasibu! Akipiga diploma tu maisha yake hayawezi kuwa na dhiki kabisa.

Ataoa mke vizuri, atazaa watoto wengi tu na atawamudu na kuwasomesha pia wakimaliza ajira zipo! Hili liliishia kizazi cha watoto wale wa 70’s na 80’s! Kizazi cha watoto wa 90’s na 00’s ndio hiki kinapitia mabalaa na mikosi! Shule utaend mpaka PhD ila kuyapanga maisha haitegemei elimu uliyonayo maana utaanzia kitaa. Inaumiza sana kuanzia pale failures na dropouts wenzio walipopitia miaka hio ya nyuma wakati mambo yalikuwa nafuu kidogo wewe unaanzia hard level ukiwa na stress lukuki za kukosa ajira miaka 4 baada ya kutoka chuo!
 
Umeongea vizuri sana ila ukumbuke ili uwe na watoto wenye future nzuri lazma nawe uwe na future nzuri kwanza!
wewe unaanzia hard level ukiwa na stress lukuki za kukosa ajira miaka 4 baada ya kutoka chuo!
ili uwe na watoto wenye future nzuri lazma nawe uwe na future nzuri kwanza!......nakusalimia sana mkuuu
 
Serikali ikiwa na mipango na sera za kiuchumi itatumudu hata mara nne ya ifadi tulivyo sasa.

Japan ni ndogo sana ukilinganisha na sisi, lakini ina watu zaidi ya 120m. Korea Kusini tunalingana idadi ya watu lakini kwa ukubwa inaingia kama mara tisa kwetu.

Lakini wao wanaishi vizuri kuliko wao. Na hizi nchi, Japan na Korea idadi kubwa sana ya watu ni wazee ambao hawazalishi bali wanatumi. Sisi average ya umri ni kama miaka 18 hivi, bado nguvu nyingi sana.

Serikali ni ya kulaumiwa kwa asilimia 100. Hatujafika idadi ya kuanza kupanga uzazi, ni uzembe tu.
 
Back
Top Bottom