UVCCM: Maoni juu ya Reform [Survey]

UVCCM: Maoni juu ya Reform [Survey]

Status
Not open for further replies.
Wanavyo vioo vya kujitazama...

Ujana wa Kambarage, Kawawa, Moringe, Salim, Warioba nk wawatazame, wajifunze kutoka kwao kwani nchi bado inawaangalia hawa (wazee) kama mfano wa vijana bora walioacha historia... Leo tunaona vijana wetu wakiwa vibaraka, makuwadi wa makundi maslahi ktk chama...

Vijana x3, tuko tayari, kulitumikia... taifa x3 Tanzania!

Nyimbo hizi ziliimbwa na vijana wa kweli.., sasa tunaona vijana wachovu kupita, Bashe akiwemo na sijui kama aliwahi hata kushiriki 'chipukizi' huyo...uvccm yoote labda kakijana ni hako ka Nape wengine mmh!
 
Kwa nini amekuja kwa turufu ya Maxence Melo?

Kwa kweli umoja wa Vijana wa CCM unamatatizo makubwa sana kiasi kwamba i dont see any positive things in this organ. lakini kwa heshima ya JF nitayatoa yangu baadhi tu kama ifuatavyo;
  1. Within UVCCM there is no political discipline, every body is a master imefika mahali utasikia Arusha wamesema hivi, pwani wamesema hivi, Mara wanasema hivi na Moshi wanasema hivi, it is chaos.
  2. Viongozi wa UVCCM wamewekwa kwa maslahi ya makundi ndani ya chama wengi hawana sifa hata ya kuwa mabalozi wa nyumba kumi cheo cha chini katika itifaki ya CCM
  3. Watoto wa viongozi wengi wanautumia umoja wa vijana kwa masilahi ya wazazi wao
  4. Sielewi mamlaka makubwa ya Ridhiwani ndani ya umoja wa vijana anayatoa wapi, amewawekea kivuli kikubwa viongozi wa jumuia kiasi kuwa wanajigonga kwake hata pale ambapo nia yake si mbaya kwa umoja huo
  5. Ili kutenganisha Kofia walizonazo wazazi wao wekeni zuio la kuwataka watoto wa viongozi wa juu wa chama na serikali wasijitokeze kugombea uongozi wa kisiasa mara baada ya wazazi wao kuchaguliwa au kuteuliwa kushika nyadhifa za juu za chama au serikali ili kupunguza mgogoro wa kimasilahi. (The president's child is a president of all children, and a president's wife is a president of all women. Some go even further to say that a president's dog is a president of all dogs and because of this automic preveledge they are all automatically, on moral grounds excluded to participate in any competetive challenges because they stand a better chance of being favoured by the prevailing circumstances.)
  6. Viongozi wa chama na serikali wanatumia UVCCM kwa masilahi yao
  7. Umoja wa Vijana hauna vision wa mision ya kisiasa
  8. Wengi wao hawaijui siasa.
  9. Umoja wa Vijana hawana chuo cha uongozi wa kuwaimarisha wanachama wake kiitikadi na kuinua vipaji vya uongozi miongoni mwa vijana tatizo hili liko hata kwenye Chama.
  10. Umoja wa vijana uweke mfumo mzuri wa kuwafanyia vetting viongozi wao
  11. umoja wa vijana haumsaidi mwenyekiti wa Chama kwa kumueleza mapungufu ya viongozi waandamizi wa chama na serikali
  12. Umoja wa vijana sasa hivi nao wengi wameingiwa na kasumba ya kuamini fedha kama sauti ya kila kitu
  13. umoja wa vijana sasa hivi wanachojua ni kuandaa greenguard kufanya fujo na ubabe, si umoja wa kujenga hoja na kushawishi
  14. Vitina ndiyo karama ya kuchaguliwa au kuteuliwa kuongoza umoja wa vijana
  15. Nendeni musome vitabu vya umoja wa vijana enzi za Mwalimu
  16. Makamanda wa umoja wa vijana wengi ni hoi kisiasa na kwa hiyo hawezi kuwa role model kwa vijana wala maisha yao ya kila siku.
 
Cha msingi wasipoteze muda wachukue muundo wa BAVICHA nao wabadili kidogo nadhani utawafaa sana

Hayo unayoshauri watayafanyia wapi? Walipewa nafasi miaka 50 yote wakaichezea. Maji yameshamwagika...Labda wakishakuwa mbers wa kambi ya upinzani wanapata nafasi ya kuona tena (kwa sasa ni vipofu) na ndipo tunaweza kuongea lugha ambayo tutaelewana.

Kwa sasa hayo magamaba hayawezi kuwapa nafasi ya kuelewa hoja ya maana labda itoke kwa King maker!
 
mghaka umemaliza..,sasa tunaona vijana wenye fikra za 'kijima',hawawezi kusimama wenyewe lazima kuwe na mtu nyuma yao..wakiyachezea maslahi na hatima ya nchi kwa vijisenti vya kupewa pewa..ni hatariii.
 
Hayo unayoshauri watayafanyia wapi? Walipewa nafasi miaka 50 yote wakaichezea. Maji yameshamwagika...Labda wakishakuwa mbers wa kambi ya upinzani wanapata nafasi ya kuona tena (kwa sasa ni vipofu) na ndipo tunaweza kuongea lugha ambayo tutaelewana.

Kwa sasa hayo magamaba hayawezi kuwapa nafasi ya kuelewa hoja ya maana labda itoke kwa King maker!

nadhani si vibaya wakituma viongozi wao waende BAVICHA ili wapewe semina elekezi zinaweza zikawasaidia wasiogope kujifunza toka kwa wapinzani kwani lazima wajue ya kuwa kutokuungwa kwao mkono na vijana basi upande wa wenzio wamefanikiwa kuungwa mkona na vijana wa kada mbali mbali za wasomi na wanavijiji

UVCCM ni wakati wa kusaidiwa na BAVICHA sasa
 
Max.....Mimi nina haya machache ambayo nadhani yanaweza kusaidia katika kuireform UVCCM..

1.Muundo.
Kwa muundo nadhani uliopo si mbaya sana,ila kunatakiwa kuwepo na muundo ufuatao:
i. UVCCM Taifa
ii.Baraza kuu la UVCCM
iii. Sekretarieti ya UVCCM Taifa
iv.UVCCM mkoa
v. Baraza la UVCCM mkoa
vi. UVCCM wilaya
vii. Baraza la UVCCM wilaya
viii. UVCCM kata
ix. Baraza la UVCCM kata
x. UVCCM tawi
xi. Baraza la UVCCM tawi.


2. Mfumo wa upataji viongozi

Si vibaya UVCCM wakawa na mfumo unaojitegemea wa kupata vioongozi na pia mfumo huo utofautiane na ule wa CCM ambao unakuwa na Mwenyekiti wa taifa,Makamu mwenyekiti wa bara na visiwani,katibu mkuu n.k...Ni vema UVCCM wakawa na Mwenyekiti(kama ilivyo sasa) ambaye
atachaguliwa na mkutano mkuu(Baraza kuu) la UVCCM.Pia awepo Makamu mwenyekiti ambaye pia atachaguliwa na Mkutano mkuu wa UVCCM,
awepo Makamu mwenyekiti mmoja tu na si lazima awepo wa Bara na Visiwani,na si vibaya ikiwa Mwenyekiti atatoka Bara Makamu wake akatoka
visiwani(upande wa pili wa Muungano).Pia awepo katibu mkuu ambaye atateuliwa na Mwenyekiti wa UVCCM taifa na jina lake kuthibitishwa na
mkutano mkuu wa UVCCM badala ya katibu huyo kuteuliwa na mwenyekiti wa CCM Taifa kama ilivyo sasa...Vile vile katibu wa fedha ambaye atateuliwa na Mwenyekiti wa UVCCM Taifa miongoni mwa wajumbe wa UVCCM Taifa ambaye kazi yake itakuwa ni kusimamia miradi yote ya UVCCM na pia atakuwa ndiye mweka hazina wa jumuia....Baraza kuu la UVCCM litaundwa na wajumbe ambao watachaguliwa katika ngazi ya wilaya...Pia uchaguzi mkuu wa UVCCM uwe unafanyika mwaka mmoja kabla ya uchaguzi mkuu wa CCM na si baada ya uchaguzi mkuu wa CCM...Shughuli za uenezi na uhamasishaji zitafanywa na kitengo maalum ambacho kitakuwa ni sehemu ya idara ya mawasiliano kwa umma....

Ni vema pia UVCCM wakarekebisha katiba yao ambayo ina mapungufu mengi sana na ioneshe hatua(za kinidhmu) ambazo zitachukuliwa kwa wanachama/viongozi wote ambao wataenda kinyume na maadili ya jumuia na CCM,hii ni pamoja kuwakumbatia mafisadi n.k....

3. Mfumo wa mawasiliano wa UVCCM

Kuwepo na kitengo cha mawasiliano ambacho kitakuwa chini ya Msemaji mkuu(Spokeperson) wa UVCCM..Msemaji mkuu ndiye atakuwa mkuu wa kitengo cha mawasiliano ndani ya UVCCM,yeye ndiye atakuwa mtoaji wa taarifa zote zinazohusiana na UVCCM...

Vile vile kuwepo na majarida mbali mbali yanayonilikiwa na UVCCM ambayo yatatumika kutoa taarifa kwa wanachama pamoja na kufanya kazi ya uenezi wa sera na itikadi za CCM.

Pia kuwepo na tovuti(website) ya UVCCM ambayo pia itatumika kufanya kazi ya kutoa taarifa pamoja na kufanya kazi ya uenezi....Wajivunze kutoka kwa wenzao wa ANC(ANC Youth League) ambao website yao ni nzuri na iko upadated ANC Youth League
Vile vile si vibaya wakaanzisha vipindi katika redio ya CCM,Redio Uhuru ambavyo vitasaidia kuweka mawasiliano baina yao na wanachama wao...


Ili hayo yote hapo juu yakamilike ni lazima waifanyie marekebisho katiba yao(UVCCM) ili angalau iendane na na hali ya sasa,wanaweza hata kuchukua baadhi ya vitu vilivyomo katika katiba ya ANCYL http://www.ancyl.org.za/docs/const/2008/constitution2010b.pdf

Aidha ni vema wakaanzisha chuo ambacho kitafanya kazi ya kuwaandaa viongozi wajao wa CCM,na kuwepo na sharti kwamba kila kiongozi wa UVCCM na CCM ajaye ni lazima awe amepitia katika chuo hiki ambacho kitafanya kazi kama kilichokuwa chuo cha(uongozi) chama cha Kivukoni ambacho kilitumika kuwaandaa viongozi mahiri,waadilifu na wenye uchungu na nchi yao.....Chuo hiki kitawaandaa viongozi na makada ambapo pamoja na mambo mengine watafundishwa maadili ya uongozi na hili linaweza kusaidia kuondokana na janga lililopo sasa la kuwa na viongozi wasio na uchungu na nchi yao na ambao wanaweka maslahi yao binafsi mbele kwa kushiriki vitendo vya ufisadi na mambo mengine mabaya ambayo ni kinyume na maadili ya uongozi...
 
nadhani si vibaya wakituma viongozi wao waende BAVICHA ili wapewe semina elekezi zinaweza zikawasaidia wasiogope kujifunza toka kwa wapinzani kwani lazima wajue ya kuwa kutokuungwa kwao mkono na vijana basi upande wa wenzio wamefanikiwa kuungwa mkona na vijana wa kada mbali mbali za wasomi na wanavijiji

UVCCM ni wakati wa kusaidiwa na BAVICHA sasa

Ili iweje?

Nitawashangaa sana BAVICHA kama wanaweza kweli kuwa na muda mchafu wa kuwachuna hao watu magamba badala ya kuendelea na maandalizi ya kuchukua nchi!
 
Tatizo mtafuata ushauri wetu au tumalize vijisent vyetu bure tuu

Umeona MR,

Hawa jamaa wanataka kutukera bure...Miaka kibao tumeshauri na kuwasihi watulie tuongoze nchi yetu kwa maslahi yetu wakakataa na kuendeleza ulaji wa hovyo kama viwavi jeshi. Sasa wanaona hali inazidi kuwa mbaya wanaanza kujipendekeza.

Dawa yao ni kuwasusa!
 
Mimi nina ushauri moja tu kwa misingi ifuatayo
  • Vijana duniani kote ni chachu ya mabadiliko na maendeleo
  • Vijana bila kujali itikadi zao wana mahitaji yanayofanana
  • Vijana wa leo ndio dira kwa vijana wa kesho
  • Vijana ndio kioo na darubini ya taifa la baadaye
Hivyo UVCCM lazima iache kuwaonea haya viongozi wao wanapotanguliza maslahi ya chama mbele ya taifa. Wawe tayari kushirikiana na vijana wenzao bila kujali itikadi, kabila, dini, rangi au jinsia kwa maslahi ya taifa. Wasiruhusu utiifu wao kwa chama kuwapofusha kiasi cha kutetea uongozi legelege usioweza kusimamia kikamilifu utawala wa sheria unaojali haki na usawa.
 
Haki ya Mungu nina maoni mazuri kwao ila kwa uvccm siwapi ,ni walafi, wanafiki,wanatamaa ya uongozi niko tayari kuitetea tanzania sio Uvccm wezi wakubwa ! kama nimekukwaza im sorry!
 
Max.....Mimi nina haya machache ambayo nadhani yanaweza kusaidia katika kuireform UVCCM..

1.Muundo.
Kwa muundo nadhani uliopo si mbaya sana,ila kunatakiwa kuwepo na muundo ufuatao:
i. UVCCM Taifa
ii.Baraza kuu la UVCCM
iii. Sekretarieti ya UVCCM Taifa
iv.UVCCM mkoa
v. Baraza la UVCCM mkoa
vi. UVCCM wilaya
vii. Baraza la UVCCM wilaya
viii. UVCCM kata
ix. Baraza la UVCCM kata
x. UVCCM tawi
xi. Baraza la UVCCM tawi.


2. Mfumo wa upataji viongozi

Si vibaya UVCCM wakawa na mfumo unaojitegemea wa kupata vioongozi na pia mfumo huo utofautiane na ule wa CCM ambao unakuwa na Mwenyekiti wa taifa,Makamu mwenyekiti wa bara na visiwani,katibu mkuu n.k...Ni vema UVCCM wakawa na Mwenyekiti(kama ilivyo sasa) ambaye
atachaguliwa na mkutano mkuu(Baraza kuu) la UVCCM.Pia awepo Makamu mwenyekiti ambaye pia atachaguliwa na Mkutano mkuu wa UVCCM,
awepo Makamu mwenyekiti mmoja tu na si lazima awepo wa Bara na Visiwani,na si vibaya ikiwa Mwenyekiti atatoka Bara Makamu wake akatoka
visiwani(upande wa pili wa Muungano).Pia awepo katibu mkuu ambaye atateuliwa na Mwenyekiti wa UVCCM taifa na jina lake kuthibitishwa na
mkutano mkuu wa UVCCM badala ya katibu huyo kuteuliwa na mwenyekiti wa CCM Taifa kama ilivyo sasa...Vile vile katibu wa fedha ambaye atateuliwa na Mwenyekiti wa UVCCM Taifa miongoni mwa wajumbe wa UVCCM Taifa ambaye kazi yake itakuwa ni kusimamia miradi yote ya UVCCM na pia atakuwa ndiye mweka hazina wa jumuia....Baraza kuu la UVCCM litaundwa na wajumbe ambao watachaguliwa katika ngazi ya wilaya...Pia uchaguzi mkuu wa UVCCM uwe unafanyika mwaka mmoja kabla ya uchaguzi mkuu wa CCM na si baada ya uchaguzi mkuu wa CCM...Shughuli za uenezi na uhamasishaji zitafanywa na kitengo maalum ambacho kitakuwa ni sehemu ya idara ya mawasiliano kwa umma....

Ni vema pia UVCCM wakarekebisha katiba yao ambayo ina mapungufu mengi sana na ioneshe hatua(za kinidhmu) ambazo zitachukuliwa kwa wanachama/viongozi wote ambao wataenda kinyume na maadili ya jumuia na CCM,hii ni pamoja kuwakumbatia mafisadi n.k....

3. Mfumo wa mawasiliano wa UVCCM

Kuwepo na kitengo cha mawasiliano ambacho kitakuwa chini ya Msemaji mkuu(Spokeperson) wa UVCCM..Msemaji mkuu ndiye atakuwa mkuu wa kitengo cha mawasiliano ndani ya UVCCM,yeye ndiye atakuwa mtoaji wa taarifa zote zinazohusiana na UVCCM...

Vile vile kuwepo na majarida mbali mbali yanayonilikiwa na UVCCM ambayo yatatumika kutoa taarifa kwa wanachama pamoja na kufanya kazi ya uenezi wa sera na itikadi za CCM.

Pia kuwepo na tovuti(website) ya UVCCM ambayo pia itatumika kufanya kazi ya kutoa taarifa pamoja na kufanya kazi ya uenezi....Wajivunze kutoka kwa wenzao wa ANC(ANC Youth League) ambao website yao ni nzuri na iko upadated ANC Youth League
Vile vile si vibaya wakaanzisha vipindi katika redio ya CCM,Redio Uhuru ambavyo vitasaidia kuweka mawasiliano baina yao na wanachama wao...


Ili hayo yote hapo juu yakamilike ni lazima waifanyie marekebisho katiba yao(UVCCM) ili angalau iendane na na hali ya sasa,wanaweza hata kuchukua baadhi ya vitu vilivyomo katika katiba ya ANCYL http://www.ancyl.org.za/docs/const/2008/constitution2010b.pdf

Aidha ni vema wakaanzisha chuo ambacho kitafanya kazi ya kuwaandaa viongozi wajao wa CCM,na kuwepo na sharti kwamba kila kiongozi wa UVCCM na CCM ajaye ni lazima awe amepitia katika chuo hiki ambacho kitafanya kazi kama kilichokuwa chuo cha(uongozi) chama cha Kivukoni ambacho kilitumika kuwaandaa viongozi mahiri,waadilifu na wenye uchungu na nchi yao.....Chuo hiki kitawaandaa viongozi na makada ambapo pamoja na mambo mengine watafundishwa maadili ya uongozi na hili linaweza kusaidia kuondokana na janga lililopo sasa la kuwa na viongozi wasio na uchungu na nchi yao na ambao wanaweka maslahi yao binafsi mbele kwa kushiriki vitendo vya ufisadi na mambo mengine mabaya ambayo ni kinyume na maadili ya uongozi...


Mkuu,

Bora umenipunguzia kazi maanake nilikuwa nimeahidi kwamba nitarudi

Hapo kwenye kupata Uongozi,si vibaya pia wakawa na Rais wa Vijana wa CCM (President:CCM Youth League)

Kuhusu mawasiliano suala la tovuti na msemaji wa Umoja wa vijana ni muhimu ili kupunguza zile embarrasement nyingine zinazosababishwa na katibu mkuu wa vijana.Pia zinampa opportunity ya kufanya masahihisho

Pia ikiwezekana wabadilishe na logo yao kabisa wawe na logo ambayo ni Unique na yenye mvuto,ikiwezekana walete hizo suggestion hapa kwa watu wenye background ya marketing and advertisement tuwasaidie but ziwe politically feasible ! ! !

Bado nitarudi........Tunahitaji CCM imara zaidi ili tuwe na upinzani Imara zaidi x 12.
 
Mimi nina ushauri moja tu kwa misingi ifuatayo
  • Vijana duniani kote ni chachu ya mabadiliko na maendeleo
  • Vijana bila kujali itikadi zao wana mahitaji yanayofanana
  • Vijana wa leo ndio dira kwa vijana wa kesho
  • Vijana ndio kioo na darubini ya taifa la baadaye
Hivyo UVCCM lazima iache kuwaonea haya viongozi wao wanapotanguliza maslahi ya chama mbele ya taifa. Wawe tayari kushirikiana na vijana wenzao bila kujali itikadi, kabila, dini, rangi au jinsia kwa maslahi ya taifa. Wasiruhusu utiifu wao kwa chama kuwapofusha kiasi cha kutetea uongozi legelege usioweza kusimamia kikamilifu utawala wa sheria unaojali haki na usawa.

Unadhani hao vijana na mashati yao ya kijani wanayopewa ofa wanaweza kuwa wameongoka jana au leo?

Hawa si ndio wananengua na kukenua meno kila siku kwenye disco za komba zenye nyimbo za hovyo kama ule wa "wapinzani tuwachane chane tuwatupe, na CCM tuwakumbatie tuwabusu"? Wanawezaje leo kuwa na mtazamo wa "Taifa kwanza" wakati wamezoe kutanguliza matumbo yao?
 
Mi si zumbukuku wa kuwachangia hawa watu. Si ndo hawahawa CCM ambao kila siku wanadai jf inapandikiza chuki kati ya wananchi na serikali yao, sasa iweje leo waje hapa kuomba msaada wa kimawazo au leo jf imebadilika, si ndo haohao wametuletea makapi wengi humu jf ambao wamekuwa waleta mashudu na kupoteza sifa za jf na kuonekana kama kijiwe cha wahuni.A friend of my enemy is my enemy too
 
Waweke NIA ya dhati ya kuleta MABADILIKO ya kweli. Muundo mfumo nk. vipo wala si lazima vibadilishwe. Hivi kuna chama kilichokuwa na muundo na mfumo wa kueleweka kama CCM? UVCCM wanahitaji NIA tu wao na wazazi wao CCM!
 
Hivi Max na Bashe naona hampo serious kabisa; hii ni style gani ya kukusanya taarifa? hata sijui report itaandikwaje na mchanganuo wa hoja na mawazo yatanywaje hapa lazima kuwe na vurugu mwisho wa siku maana nani atasema hili ndilo wazo zuri na hili si zuri?! Kwanini UVCCM/Bashe wasiwape reseachers (Consultants) hii kazi

Yes tunashukuru kwa kujali mawazo ya wana-JF lakini ebu wajaribu kuhusisha wataalam hasa reseachers ili wajuwe wanahitaji nini na kitachujwa kwa njia gani, then wanaweza kuwa na JF-online Questioner ambayo wataalam wa JF wata-limit access kwa maana ya kila member aweze kutoa mawazo yake mara moja tu! Hivi mwisho wa siku kukiwa na mawazo ya wana-JF mia tano hapa lakini kati ya hayo mawazo Ben wa Saanane (Samahani Ben, jina lako limekuwa jepesi kutumia kwa ajili ya mfano) katowa mawazo mia na hizo zingine mia nne kuna watu kadhaa wamegawana mwingine kumi, mwingine kadhaa, itakuwaje! Sijui nimetoka shule siku nyingi lakini naona haikubaliki kitaalam na italeta mkanganyiko na kuimaliza hiyo UVCC iliopo ICU.

Hakuna sehemu duniani mawazo ya kuboresha chombo au system yoyote yanakusanywa kwa namna hii, kama mjadala au kongamano labda kama anataka kuandika riwaya na siyo ripoti ya maboresho.Huwezi ku-code kitu hapa, hata sijui unaiita survey badala ya kongamano la wana-JF juu ya namna ya kuboresha UVCCM.
 
Kwanza UVCCM ni nini ? Akina nani ? Wako wapu ? Wanafanya nini? Je kuna umuhimu wa uwepo wa manufaa ya Taifa na hasa kwa watanzania wote wenye vyama na wasiokuwa na Vyama?
 
Kaka Maxence kwanza kabisa napenda kutambua kwamba hii hoja imeshapitwa na wakati, ushauri wote wa uvccm upo wazi kwa ku copy and paste ule wa baba zao wa CCM.

Ila tu kwa kumsaidia muomba ushauri tatizo mojawapo kubwa sana la UVCCM ni huyo Bashe mwenyewe na watu wanafiki wa aina yake wanaofikiri kwa matumbo yao. Yeye alitumwa hiyo kazi na mafisadi na kupatanishwa na Benno malisa kwa lengo la kuwa na big picture ya kumtayarishia Lowassa uraisi 2015. Ndio maana leo hii Benno na Riz1 imekua ndivyo sivyo, sasa yeye atakuaje tena chachu ya mabadiliko?

Kwanza atuambie juu ya utata wa uraia wake, pili aongee na hicho hicho chama kilichoajiri mamluki kuendesha nchi yetu, sisi hatumo na hatuna cha kushauri sisi sio wanachama wa UV wala CCM yenyewe atatuomba vipi ushauri kama sio siasa za kutaka baadae atambe kwamba anatudhibiti huku.
 
Is this for real?.............nina mashaka makubwa na uliberali wa UVCCM na CCM kwa ujumla.............Bashe....wewe ni mwanachama hapa JF..........inakuwaje umtumie Max kuleta ujumbe hapa..............je wewe ni liberali?...................hilo ni tatizo mojawapo mlilonalo UVCCM na wanachama wa CCM kwa ujumla............
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom