Utumbuaji: Tuache Siasa Kwenye Professionalism, Sio Kila Mtumbuliwa ni Jipu!

No sikutaka umeme upande bei, bali Tanesco na Ewura ni taasisi ya serikali yenye serikali ambayo ni regulatory yenye mandate yake, autonomy yake na independence yake ambapo serikali ina jicho na mkono wake pale kwa mtindo wa eyes on hands off, serikali kujua kila kilichokuwa kinafanyika hatua kwa hatua, lakini maamuzi yalipofikiwa kwa kufuata taratibu zote ndipo serikali hiyo hiyo inaibuka na eyes on hands on kusimamisha.

Ningekuwa mimi bosi wa Tanesco na Ewura, ningeziandika barua za kumbwagia kazi yake jana ile ile ili Jumatatu asubuhi angezikuta mezani kwake kuliko kusubiri kutumbuliwa kwa aibu na udhalilishaji.

Hili la kupanda umeme hakuna kitu ambacho Prof. Muhongo na rais Magufuli walikuwa hawajui kwa sababu maamuzi yoyote ya kuomba kupandisha umeme yanatoka kwenye bodi ambapo bodi zote zina waserikali, mtu wa ikulu, ambao wote waliripoti hivyo wanajua kila kitu bali kudhalilishana tuu


Paskali
Mkuu hapa umeongea kama mchambuzi mbobezi nakupa mkono kwa kutolea ufafanuzi huu utumbuaji ovyo ovyo
 
Hivi ni sahihi kila anaetenguliwa kukaa kimya bila nae kujitokeza hadharani na kueleza ya upande wa pili?

Hivi wote ambao nafasi zao zimetenguliwa kila mmoja alikuwa ana makosa?

Mh.sana yeye yuko sahihi kila siku katika maamuzi yake?

Hivi yule alietenguliwa siku za nyuma na baade kuteuliwa kushika wadhifa mwingine si ushahidi kuwa kuna baadhi wanaonewa?

where is natural justice?
Hawawezi, watatupwa Kisongo bila dhamana. Nawashauri wanyamaze, kunako majaliwa time will tell
 
Nabishana na STDVII????
Njoo kwenye hoja acha matusi Juzi hapa mlikua mnalaumu UMEME kupanda leo mnakuja na bla bla bla wakati Muhongo kakataa.

Tanesco na ewura kama wana hoja waje na andiko Fedha zitokanazo na Ongezeko zitafanya kazi gani?
Kwa nini wanaongeza Bei ya UMEME kipindi hiki tunavutia wawekezaji?

Hatutaki kulinganishiwa bei ya UMEME ya Kenya na Uganda sisi tuna Gesi, Makaa ya mawe nk.

Pima elimu yako na yangu ya STDVII...
 
Gharama za uzalishaji wa umeme 'per unit' sio kubwa kulingana na charges. Tatizo ni madeni na mikataba mingi inayoliumiza shirika.

Sisi kama wananchi, hatukufanya makosa yoyote wakati hiyo mikataba inafanyika, ni hao 'professionals' waliokosea na sasa wanataka kutuumiza kwa charges kubwa.

Wasomi wengi hawakutumia nafasi zao za taaluma kwa weledi na kufuata kanuni na sheria za kazi....

...let them be punished!!!
 
Kazi inayohitaji njia ngumu kuwa solved , mpe mtu mvivu uone. The same to TANESCO, who simply resort to raise electricity charges rather than cracking down their heads and come up with atleast 50 yrs solution. Hawajiulizi kuwa watakuwa wanapandisha charges kila mwaka hadi lini? Huyu wa EWURA aliye accept charges zipande ajiuzulu haraka, taa nyekundu zimeshawaka.
 
Kwan political inakuchuka taaluma gani?. Hii ni "sandakalawe" nani kaona...si ajabu wakati mwingine hao walipata fursa kifigisufigusu..kwa kuwakatiri wengine acha dhambi iwatafune tuu...uzur Tz tuko wengi wenye proffesional..hivyo acha na wengine wajipime pumzi na kina.
 
Kwa hili la Tanesco na ewura namuunga mkono rais, labda nimesahau ila sina kumbukumbu kuona siku moja walau ewura imeigomea Tanesco kwenye kupandisha bei ya umeme, kila mwaka wanachofanya ni kupunguza percentage tu kutoka zile walizoomba, kwa akili ya kawaida kila mwaka Tanesco watakua wanaleta ombi la kupanda kwa gharama za uzalishaji wa umeme lenye figures nyingi ili
hata ukipunguza wabaki na kitu.!

Ewura wajitathmin pia wameegemea upande mmoja (suppliers) huku kwa wananchi wapo kama ishara tu.
 
Wanabodi,

Hili ni angalizo tuu kuhusu utumbuaji majipu wa rais Magufuli, sio kila mtumbuliwa ni jipu, wengine wanatumbuliwa kwa circumstances tuu, wengine wanatumbuliwa for political capitalisation tuu na wengine kweli ni majipu hivyo wanatumbuliwa kihalali.

Hili la kuwatumbua watu maprofession tena wenye weledi wa hali ya juu katika professionals zao for political capitalization, ni udhalilishaji wa hali ya juu wa professional za watu.

Hii ni kufuatia tetesi ya utumbuaji mwingine wa maprofessionals unaotarajiwa kufanywa na Mhe. rais any moment from now.


Nasisitiza Tanzania ili tupate maendeleo ya kweli, ni lazima tuwe wakweli kwa kuacha kuingiza siasa kwenye taaluma za watu, kama gharama za uzalishaji umeme per unit ni Kubwa kuliko tozo ya umeme, ukweli ni kwamba umeme lazima upende bei tutake tusitake, hili la Tanesco kuendelea kulishwa kwa spoon feed na serikali huku ikilazimishwa kuuza umeme kwa bei ya hasara, sio sustainable na ni short lived! .

Ili Tanzania tuweze kupiga hatua za kweli za maendeleo na kusonga mbele ni kwanza lazima tuwe wakweli, na pili tuache siasa kwenye kila kitu! .

Let's stop politicizing everything, politicians do politics and leave professionals Alone! .
Heri ya Mwaka Mpya.
Paskali
Sikuelewi mbona mkuu pascal mayala?Watu wanalipana bonus wakati hakuna ziada inayopatikana?No way walimchelewesha tu huyu jamaa.Ilikuwa hakuna shirika la kuongoza rahisi kama Tanesco!Mapato yakizingua tu unaongeza bei,mahitaji yakiongezeka tu Kata umeme,MTU akitaka umeme anunue nguzo na kulipia nyaya!Hats ukiweka muuza nyanya anakuwa meneja tu
 
Capacity charge ya iptl...mbona wazir aliyeko madarakan aliwajibika..then.. karudi kama vile iptl hakuhusika?...hajui mzigo wa tanesco na mikataba mibovu ilhali serikali inasema pesa za escrow ni za singh sio serikali...kuna double standards za uongozi?... ...kweli siasa ikizid ni vituko...sema mnajionesha wazi wazi namna gani mlivyo!
ha ha ha.....wakati anapendekeza hiyo bei professionally he could have mentioned clearly and fairly kwamba ongezeko hili ni kwa ajili ya kuwalipa IPTL reaction yetu ingekuwa tofauti...niwekee hoja za Tanesko hapa specific zinazoongelea kupanda kwa bei ni kwa sababu ya IPTL....Kwamba tumeanza kuwalipa upya mwezi januari 2017????
 
Wakuu hii issue ikijadiliwa
Kwa upande hatuwezi kufika.

Huyu pascal alichokieleza ndani kuna ukweli wake.

Tutakuwa tumeshindwa kutumia akili zetu vizuri kama tutakubaliana na mwenye nyumba kwamba mtu mmoja tu kaamka akapandisha umeme kwa hili nakataa HAPANA

Naamin huu mchakato ulipitia sehemu zote muhimu na watumbuaji walikuwa wakijua kila hatua iliyokuwa ikiendelea.

Kilichofanyika ni kumtoa kafara tu mhusika na bahati mbaya sana hawa MAJIPU wanaotumbuliwa huwa hawajitokezi na kusema UKWELI.

Laiti wangekuwa wanatokea tungejua vingi na tungefunga midomo ya kukunja vidole tulivyokuwa tunawanyooshea.

Habari ya kujilipa 40m mpaka 60m hapa tu ndo unajua serikali hii na zilizopita hazina maana hata kidogo.

Yaani 40-60m kama sehemu ya kujipongeza aisee wakati kuna watu wana matatzo kibao yanatokea.

Kiuhalisia napata wakati mgumu sana kuamini matukio ya nchi hii hasa ya kisiasa tena hasa awamu hii inayoendesha kwa kelele za media na mitandao
 
Mwacheni atumbue , hawezekani watu bonus 60 ml??? Walimu mshara laki 5??????????
 
Jamani serikali inahitaji utulivu ili kufikia malengo yake, kama idara na managements mbali mbali za serikali hazitatulia itakua ngumu sana kufikia malengo.Tumbua huyu weka huyu,hamisha huyu weka yule kwa maoni yangu kunaweza kuleta shida mno kiutendaji.

Haya yote dawa ni moja tu, katiba mpya!! Mfumo uliopo unawapa nafasi kubwa sana viongozi wa idara kstika taasisi mbalimbli za umma kufanya watakavyo,ni mfumo uliopitwa na wakati!! Jamani hawa wanafanya kwa sababu taratibu za kimfumo zinawaruhusu.
 
Yani eti mwanasiasa hajasomea udaktari,ualimu,ukandarasi halafu anaibuka kutoka Lumumba huko anapiga kelele,na kumwondoa mtu ktk kazi yake.
Ni ujinga wa kupitiliza na tabia hii ikome ikome ikomeee.
Nani akome sasa??
Watanzania kama vinyonga-sijui huwa mnawaza nn vichwani mwenu.!!!
 
Back
Top Bottom