Uteuzi wa Jaji kuwa Mwanasheria Mkuu na Uhuru wa Mahakama

HANGAYA THE CHIEF

JF-Expert Member
Sep 10, 2021
329
947
Katiba ya JMT ibara ya 109 (2) inampa Rais mamlaka ya kuteua Jaji Kiongozi na Majaji wengine wa Mahakama kuu, Muhimili huu wa utoaji haki unatakiwa kuwa huru katika kutekeleza shughuli zake hiyo ibara ya 107B imetamka bayana kuwa mahakama zote zitakuwa huru pasipo kuingiliwa na muhimili wowote. Uhuru wa Mahakama ni pamoja na watoa huduma wake yaani majaji wanapashwa wawe huru, hivyo katiba ibara 110 imewahakikishiria muda wa kukaa kazini na kutekeleza shughuli zao kwa uhuru.

Hivyo pamoja na kuwa na nguvu ya uteuzi ibara109 (2), kuondolewa katika shughuli za ujaji lazima ibara 110 (5) au ibara 110 (5) visomwe kwa pamoja na ibara na ibara ndogo 7, au ibara ndogo ya 6 na 8. kulingana na mazingira.

Kwa kifupi, maana ya mahakama kuwa huru ni watendaji wake kuwa na uhakika wa kazi zao (security of tenure)

Je, uteuzi wa Feleshi ni kuondolewa kazini?
kwa haraka haraka unaweza kuona kala shavu, lakini kimsingi kaondolewa kazini kwa maana sio jaji tena (kwa hiyo anatoka kwenye muhimili wa mahaka ) na kwenda muhimili mwingine yaani serikali.

Nini maana ya uteuzi wake?
Maana ya uteuzi huu ni kwamba ukomo wa majaji kukaa kazini (security of tenure) uko chini ya Rais, anaweza kuteua na kutengua majaji wakati wowote anaotaka.

Nini maana yake kwa Muhimili wa Mahakama?

Muhimili wa mahakama hauko Huru, kwa sababu sasa majaji wataogopa kufanya shughuli zao za utoaji haki kwa uhuru kwa sababu wana mamlaka ya utenguzi, (no security of tenure is guranteed).

Maoni yangu?
Mosi, uteuzi wa Jaji Feleshi kuwa Mwanasheria Mkuu ni kinyume cha Katiba na kuingilia Uhuru wa mahakama kwa maana ya watendaji wake (kuteuliwa kushika nyadhifa zingine tofauti na shughuli zao)

Mahakama iachwe huru, tunawatanzania zaidi ya mililion 60 tupanue wigo kuona kama wapo wanaofaa.

Pili, wanaomshauri Mheshimiwa Rais wetu mpendwa, tumieni taaluma zanu vizuri kwa malengo mapana ya nchi yetu

MUNGU IBARIKI TANZANIA NA WATU WAKE
 
Katiba ya JMT ibara ya 109 (2) inampa Rais mamlaka ya kuteua Jaji Kiongozi na Majaji wengine wa Mahakama kuu, Muhimili huu wa utoaji haki unatakiwa kuwa huru katika kutekeleza shughuli zake hiyo ibara ya 107B imetamka bayana kuwa mahakama zote zitakuwa huru pasipo kuingiliwa na muhimili wowote. Uhuru wa Mahakama ni pamoja na watoa huduma wake yaani majaji wanapashwa wawe huru...
Kwani Werema si alikuwa senior Judge of the HC akaenda kuwa Mwanasheria Mkuu, so sio swala la kushangaa,hata akiondolewa anarudia ujaji wake.pia Jaji kiongozi ni jaji wa mahakama kuu.ni kama Jaji anapelekwa kuwa Msajili wa vyama vya siasa etc.
 
Kwani Werema si alikuwa senior Judge of the HC akaenda kuwa Mwanasheria Mkuu, so sio swala la kushangaa,hata akiondolewa anarudia ujaji wake.pia Jaji kiongozi ni jaji wa mahakama kuu.ni kama Jaji anapelekwa kuwa Msajili wa vyama vya siasa etc.
Hapa nchini majaji hawana hadhi inayowapasa na hawana uhuru sitashangaa jaji akiteuliwa kuwa mkuu wa mkoa au balozi kama ilivyotokea.
 
Kwani Werema si alikuwa senior Judge of the HC akaenda kuwa Mwanasheria Mkuu, so sio swala la kushangaa,hata akiondolewa anarudia ujaji wake.pia Jaji kiongozi ni jaji wa mahakama kuu.ni kama Jaji anapelekwa kuwa Msajili wa vyama vya siasa etc.
So kwa kuwa tulikosea huko nyuma ndiyo tuendelee kukosea mkuu? Hii mambo ikiendelea hivi haka ka-nchi hakatakuja kuendelea kamwe asilani.
 
So kwa kuwa tulikosea huko nyuma ndiyo tuendelee kukosea mkuu? Hii mambo ikiendelea hivi haka ka-nchi hakatakuja kuendelea kamwe asilani.
Jaji anateuliwa na Nani? Tuanzie hapo. Mbona Jaji Lubuva alipoteuliwa NEC ulikaa kimya? Mwangesi, Nsekela? Au ulitaka AG atoke kwenye vikosi?
 
Uchambuzi mzuri sana,suala la Jaji Werema kuwahi kuwa mwanasheria mkuu bado ni mapungufu hayo hayo aliyozingatia mtoa mada.
 
Jaji anateuliwa na Nani? Tuanzie hapo. Mbona Jaji Lubuva alipoteuliwa NEC ulikaa kimya? Mwangesi, Nsekela? Au ulitaka AG atoke kwenye vikosi?

Mkuu inabidi utuelewe vzr hapo. Wote tunamfahamu anayewatua hilo lina shida lakini kwa kikatiba hiki cha kikoloni hakuna kitu tunaweza kufanya kwa sasa. Tatizo letu ni kuwa wakishateuliwa waachwe huko wasiwe candidates tena wa teuzi zingine ili wawe huru kwenye majukumu yao. Ni mby sana jaji anafanya maamuzi khs executive arm ya government huku anafahamu kwamba yeye pia ni potential candidate kwenye teuzi zingine za hiyo executive branch ya government.

Kwa kulitambua hilo haya tunayoyaona hayakuwepo sana kipindi cha Mwinyi, Mkapa na hata Kikwete pia. Awamu ya 5 na 6 marais ni miungu watu wao hawakosei which is very big problem.

Nimesema mara kadhaa na ninarudia tena kwamba Tanzania kama nchi lazima kuna mahali tulimkosea sana Mungu vinginevyo asingetupa adhabu kali kiasi hiki cha kuwa na viongozi wasiowajali wanaowaongoza.
 
Hii loophole inayotumika na Rais inabidi kuangaliwa upya.

Maana kesho anaweza kutimuliwa kwenye kazi ya AG

Swali ni je? Hawezi kukataa uteuzi mpya?
 
Katiba ya JMT ibara ya 109 (2) inampa Rais mamlaka ya kuteua Jaji Kiongozi na Majaji wengine wa Mahakama kuu, Muhimili huu wa utoaji haki unatakiwa kuwa huru katika kutekeleza shughuli zake hiyo ibara ya 107B imetamka bayana kuwa mahakama zote zitakuwa huru pasipo kuingiliwa na muhimili wowote. Uhuru wa Mahakama ni pamoja na watoa huduma wake yaani majaji wanapashwa wawe huru, hivyo katiba ibara 110 imewahakikishiria muda wa kukaa kazini na kutekeleza shughuli zao kwa uhuru.
Hivyo pamoja na kuwa na nguvu ya uteuzi ibara109 (2), kuondolewa katika shughuli za ujaji lazima ibara 110 (5) au ibara 110 (5) visomwe kwa pamoja na ibara na ibara ndogo 7, au ibara ndogo ya 6 na 8. kulingana na mazingira.

Kwa kifupi, maana ya mahakama kuwa huru ni watendaji wake kuwa na uhakika wa kazi zao (security of tenure)

Je, uteuzi wa Feleshi ni kuondolewa kazini?
kwa haraka haraka unaweza kuona kala shavu, lakini kimsingi kaondolewa kazini kwa maana sio jaji tena (kwa hiyo anatoka kwenye muhimili wa mahaka ) na kwenda muhimili mwingine yaani serikali.

Nini maana ya uteuzi wake?
Maana ya uteuzi huu ni kwamba ukomo wa majaji kukaa kazini (security of tenure) uko chini ya Rais, anaweza kuteua na kutengua majaji wakati wowote anaotaka.

Nini maana yake kwa Muhimili wa Mahakama?

Muhimili wa mahakama hauko Huru, kwa sababu sasa majaji wataogopa kufanya shughuli zao za utoaji haki kwa uhuru kwa sababu wana mamlaka ya utenguzi, (no security of tenure is guranteed).

Maoni yangu?
Mosi, uteuzi wa Jaji Feleshi kuwa Mwanasheria Mkuu ni kinyume cha Katiba na kuingilia Uhuru wa mahakama kwa maana ya watendaji wake (kuteuliwa kushika nyadhifa zingine tofauti na shughuli zao)

Mahakama iachwe huru, tunawatanzania zaidi ya mililion 60 tupanue wigo kuona kama wapo wanaofaa.

Pili, wanaomshauri Mheshimiwa Rais wetu mpendwa, tumieni taaluma zanu vizuri kwa malengo mapana ya nchi yetu

MUNGU IBARIKI TANZANIA NA WATU WAKE
Mahakama pia inapaswa ijipange vizuri, kunaonekana kuna matatizo kibao ndani kwa ndani.
Mnacho kihubiri lazima mkitende nyinyi wenyewe, sio unahubiri mema unatenda uovu.
Mahakama badilikeni, wacheni majungu.
 
Katiba ya JMT ibara ya 109 (2) inampa Rais mamlaka ya kuteua Jaji Kiongozi na Majaji wengine wa Mahakama kuu, Muhimili huu wa utoaji haki unatakiwa kuwa huru katika kutekeleza shughuli zake hiyo ibara ya 107B imetamka bayana kuwa mahakama zote zitakuwa huru pasipo kuingiliwa na muhimili wowote. Uhuru wa Mahakama ni pamoja na watoa huduma wake yaani majaji wanapashwa wawe huru, hivyo katiba ibara 110 imewahakikishiria muda wa kukaa kazini na kutekeleza shughuli zao kwa uhuru.
Hivyo pamoja na kuwa na nguvu ya uteuzi ibara109 (2), kuondolewa katika shughuli za ujaji lazima ibara 110 (5) au ibara 110 (5) visomwe kwa pamoja na ibara na ibara ndogo 7, au ibara ndogo ya 6 na 8. kulingana na mazingira.

Kwa kifupi, maana ya mahakama kuwa huru ni watendaji wake kuwa na uhakika wa kazi zao (security of tenure)

Je, uteuzi wa Feleshi ni kuondolewa kazini?
kwa haraka haraka unaweza kuona kala shavu, lakini kimsingi kaondolewa kazini kwa maana sio jaji tena (kwa hiyo anatoka kwenye muhimili wa mahaka ) na kwenda muhimili mwingine yaani serikali.

Nini maana ya uteuzi wake?
Maana ya uteuzi huu ni kwamba ukomo wa majaji kukaa kazini (security of tenure) uko chini ya Rais, anaweza kuteua na kutengua majaji wakati wowote anaotaka.

Nini maana yake kwa Muhimili wa Mahakama?

Muhimili wa mahakama hauko Huru, kwa sababu sasa majaji wataogopa kufanya shughuli zao za utoaji haki kwa uhuru kwa sababu wana mamlaka ya utenguzi, (no security of tenure is guranteed).

Maoni yangu?
Mosi, uteuzi wa Jaji Feleshi kuwa Mwanasheria Mkuu ni kinyume cha Katiba na kuingilia Uhuru wa mahakama kwa maana ya watendaji wake (kuteuliwa kushika nyadhifa zingine tofauti na shughuli zao)

Mahakama iachwe huru, tunawatanzania zaidi ya mililion 60 tupanue wigo kuona kama wapo wanaofaa.

Pili, wanaomshauri Mheshimiwa Rais wetu mpendwa, tumieni taaluma zanu vizuri kwa malengo mapana ya nchi yetu

MUNGU IBARIKI TANZANIA NA WATU WAKE
Chini ya katiba iliyopo hicho ulichoandika ni ndoto, hiyo katiba iloyopo nayo imepewa likizo mpaka uchumi ukue na uchumi kukua ni ndoto pia.
 
Mahakama inapaswa ibadilike, inapaswa itende kile inacho kihubiri siku zote, sio unahubiri hiki unatenda kingine.
Mahakama wanapaswa wabadilike wasidhani wamejificha kwenye mwamvuli wa muhimili na hivyo kuamua kujifanyia wanavyo taka, kuoneana, kuumizana, kuharibiana na kupigana majungu.
Mahakama badilikeni.
Uhuru usitumike vibaya.
 
Tatizo linaanzia kwenye mahakama yenyewe Kama muhimili huru kudhindwa kujijua mamlaka yao na kukubali kutumiwa na serikali.
 
Mhimili wa serikali umechimbiwa chiini zaidi kwa hiyo hakuna shida. Huku nikukanyaga katiba tu tumeshazoea. Kuondoa hili tunahitaji devotion ya hali ya juu labda kwa kizazi kijacho sii hiki wanaoapa na kuivunja the next morning.
 
Back
Top Bottom