Uteuzi wa Dk Asha Rose-Migiro, Kenani Kihongosi ni wa Kimkakati huenda wakatenguliwa baada ya malengo kutimia

Uteuzi wa Dk Asha Rose-Migiro, Kenani Kihongosi ni wa Kimkakati huenda wakatenguliwa baada ya malengo kutimia

jindundu

JF-Expert Member
Joined
Aug 1, 2025
Posts
679
Reaction score
580
CCM imemteua Dk Asha Rose- Migiro, kuwa Katibu Mkuu wake kuchukua nafasi ya Dk. Emanuel Nchimbi, Mgombea Mwenza wa Mama Samia.

Aidha Chama hicho kimemteua Kenani Kihongosi, Mkuu wa Mkoa wa Arusha kuwa Katibu wa Itikadi na Uenezi.

Mabadiriko haya ni ya Kimkakati zaidi kuelekea Uchaguzi Mkuu;

1: Dk. Asha- Rose Migiro.

Ni Kada wa CCM ambaye amewahi kuwa Naibu Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa, na kuiletea heshima kubwa nchi yetu Kimataifa.

Ikumbukwe kuwa kwa sasa CCM inabebwa na wanawake. Dk. Asha Rose- Migiro anaenda kuleta ushawishi kwa wanawake ambao kwa kiasi kikubwa ni miongoni mwa kundi linalolamikia hali ya mambo na mwenendo wa CCM na Serikali yake kwa ujumla.

2: Kenani Kihongosi.

Ni kijana anayepandishwa haraka haraka ndani ya CCM kwa malengo maalum. Sote tunajua vema kuwa karibu robo tatu ya wapiga kura waliojiandikisha kupiga kura ni vijana. Kundi hili linaongoza kulalamika dhidi ya utendaji wa CCm na Serikali yake kwa ujumla.

Kenani Kihongosi anaenda kutumika kama chambo cha CCM kushawishi vijana wakapige kura ukizingatia kuwa hata ndani ya Chama hiki Kuna wanaoimba wimbo wa CHADEMA wa No reform, no election.

3: Tahadhali kutokana na Humphrey Polepole kulisanua kuwa kuna liwaya linalounganisha INEC, CCM na NIDA.

Katika Press yake ya mwisho, Humphrey Polepole alisema CCM wanaiba kura Kwa mfumo wa li-waya lililounganishwa katika Taasisi hizo tatu.

Kama tuhuma hizi ni za kweli, basi huenda Chama hiki sasa kina tafuta njia mbadala ya kupata kura kwani li-waya hilo huenda lisiwasaidie walau kwa kipindi hiki.

Hata hivyo, kutokana na hali ya mambo na mfumo wa CCM hii ya Sasa, mwelekeo wa Serikali ijayo na Mwamko wa wengi ndani ya CCM na jamii nzima kwa ujumla kuelekea 2030, wawili Hawa yaani Dk. Asha Rose- Migiro na Kenani Kihongosi huenda wakatenguliwa mara baada tu ya malengo ya waliowateua kukamilika. Tuombe uzima.
 
CCM imemteua Dk Asha Rose- Migiro, kuwa Katibu Mkuu wake kuchukua nafasi ya Dk. Emanuel Nchimbi, Mgombea Mwenza wa Mama Samia.

Aidha Chama hicho kimemteua Kenani Kihongosi, Mkuu wa Mkoa wa Arusha kuwa Katibu wa Itikadi na Uenezi.

Mabadiriko haya ni ya Kimkakati zaidi kuelekea Uchaguzi Mkuu;

1: Dk. Asha- Rose Migiro.

Ni Kada wa CCM ambaye amewahi kuwa Naibu Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa, na kuiletea heshima kubwa nchi yetu Kimataifa.

Ikumbukwe kuwa kwa sasa CCM inabebwa na wanawake. Dk. Asha Rose- Migiro anaenda kuleta ushawishi kwa wanawake ambao kwa kiasi kikubwa ni miongoni mwa kundi linalolamikia hali ya mambo na mwenendo wa CCM na Serikali yake kwa ujumla.

2: Kenani Kihongosi.

Ni kijana anayepandishwa haraka haraka ndani ya CCM kwa malengo maalum. Sote tunajua vema kuwa karibu robo tatu ya wapiga kura waliojiandikisha kupiga kura ni vijana. Kundi hili linaongoza kulalamika dhidi ya utendaji wa CCm na Serikali yake kwa ujumla.

Kenani Kihongosi anaenda kutumika kama chambo cha CCM kushawishi vijana wakapige kura ukizingatia kuwa hata ndani ya Chama hiki Kuna wanaoimba wimbo wa CHADEMA wa No reform, no election.

3: Tahadhali kutokana na Humphrey Polepole kulisanua kuwa kuna liwaya linalounganisha INEC, CCM na NIDA.

Katika Press yake ya mwisho, Humphrey Polepole alisema CCM wanaiba kura Kwa mfumo wa li-waya lililounganishwa katika Taasisi hizo tatu.

Kama tuhuma hizi ni za kweli, basi huenda Chama hiki sasa kina tafuta njia mbadala ya kupata kura kwani li-waya hilo huenda lisiwasaidie walau kwa kipindi hiki.

Hata hivyo, kutokana na hali ya mambo na mfumo wa CCM hii ya Sasa, mwelekeo wa Serikali ijayo na Mwamko wa wengi ndani ya CCM na jamii nzima kwa ujumla kuelekea 2030, wawili Hawa yaani Dk. Asha Rose- Migiro na Kenani Kihongosi huenda wakatenguliwa mara baada tu ya malengo ya waliowateua kukamilika. Tuombe uzima.
Iff you are to know...Kuna mtu anadhibitiwa hapo na soon asipokuwa makini atatoswa Ili mipango ya watu iendelee bila tatizo...I warn them not this time, nimeona ndege Yao imeungua hewani, too little too late to catch the train...Hapa ndipo nilipo doubt motive ya HP...Aliyemsema hadharani najua siyo preference ya hao anaodai wameiteka nchi
 
Kama hawasikii, wanalazimisha, na sisi tunaimba kama kasuku Uchaguzi haipo! Wewe unafanya nini kuzuia Uchaguzi? Unadhani kusema tu hivyo na kuimba kama kasuku kutasaidia Nini? Itafika wakati kauli kama hizi zionekane ni za wavuta bangi
Hakuna uchaguzi
Sasa unatutukana Tena twavuta bange wkt tushakwambia
No election
 
Hakuna uchaguzi
Sasa unatutukana Tena twavuta bange wkt tushakwambia
No election
Nimeulizq, kusema hakuna Uchaguzi tuuuuu kama kasuku Kuna saidia Nini? Kipi kina support neno lako?
 
Natabiri Kuna mtu ataweka mpira kwapani, na tutaanza mchakato ambao pia ni fake....This time the Holy Sea have got them in, hawachomoki hata kidogo!
Labda hivyo
 
Usijitoe ufahamu.
Mwaka huu kuna uchaguzi? Vyama gani vinagombea?
Eti vijana watatetewa na kihongosi, kehongosi si ndio huyu huyu aliye wacharaza vijana viboko hadharani?
Mnu akishakula nyama ya mtu hawezi kuacha.
 
Kwa akili yako unadhani wanahitaji kupiga kura? Kuna maana yoyote ya kupiga kura?
Hakuna maana. Sawa sasa huo mtazamo na hii movement iko kwa watanzania wangapi?
 
Usijitoe ufahamu.
Mwaka huu kuna uchaguzi? Vyama gani vinagombea?
Eti vijana watatetewa na kihongosi, kehongosi si ndio huyu huyu aliye wacharaza vijana viboko hadharani?
Mnu akishakula nyama ya mtu hawezi kuacha.
Nakubali, hayo unayoyasema yamewafikia watanzania wangapi?
 
Hakuna uchaguzi
Sasa unatutukana Tena twavuta bange wkt tushakwambia
No election
Tunaimba weeee kama kasuku humu, je huko nje ambako ndiko Kuna wapiga kura huu wimbo upo?
 
Back
Top Bottom