Hivi ndoa ni nini?
Nimekutana na stori moja ya jamaa zangu mke na mume ambao hawakubahatika kufika Kanisni kufunga ndoa lakini wemeishi kwa miaka isiyo pungua 7 na wana watoto wawili. Katika kipindi chote hicho wazazi wa pande mbili walisha tambuana na kiasi cha mahali kilisha tolewa.
Tukirudi nyuma wawili hao kama mahusiano mengi ya ki Africa yalivyo mume alikua mkubwa na alianza kujitegemea muda mrefu huku mke akiwa bado shuleni, hivyo mahitaji madogo madogo mume wakati huo boy friend aliwajibika kutimiza kwa mwenzake. Miaka ika enda shule ikaisha, mwanamke aka ajiriwa lakini walisha amua kuishi pamoja kama mke na mume na sasa wana watoto.
Ajira ya mke ilikua mkoa wa Mbeya wakati mume akiwa Dar es Salaam, mume aka fanya jitihada za kumuhamisha na waka ishi pamoja, ikumbukwe kua licha ya umbali wa awali wote walitambulika mke na mume licha ya kuto kwenda kifunga ndoa Kanisani.
Katika safari ya miaka hiyo 7 kume kua na changamoto nyingi kama mahusiano mengi yalivyo. Lakini baada ya kufanikiwa uhamisho na kauanza mikakati ya kimaisha kwa pamoja mke akawa ana goma kuchangia katika maendeleo ya familia akidai kwamba hawezi changia chochote kwa kua hakuna ndoa, hajitambui yeye ni nani katika maisha Yale? Ikumbukwe kua mume alimtumikia mke kipindi chote cha mahusiano akiwa shule na hata baada ya kuanza kazi na hata kukamilisha hatua za utambulisho kifamilia ( mahari) na hata uhamisho kama mjuavyo uhamisho ulivyo mgumu.
Lakini sasa mke anasema yeye hawezi changia chochote kwa kua hajijui kua yeye ni nani katika familia hiyo. Na kwa taarifa zaidi kwamba alisha aza kununua vitu kimya kimya kama vile viwanja bila hata kumpa taarifa mwenzake. Lakini wakati hayo yanafanyika mume alisha kua na vijimali ambavyo kwa asilimia 100% ame muhusisha kwa ushauri au hata kumtaarifu katika kuvitafuta vitu hivyo kitu ambacho tunaweza kuita jamaa amekua muwazi hasa kwa mwenzake.
Katika kuepusha migogoro hiyo jamaa alisha changia ununuzi wa vitu fulani kwa jina la mkewe ili kumjenga kiimani mkewe lakini bado mke hawezi changia kitu cha kimaendeleo kama familia kama maelezo ya awali.
Mume aka endelea na kupambana, siku za karibuni aka kutana na mtu naweza sema mdada wa makamo ambaye nae ame kua akitaka mwenza wa kupambana nae kimaisha bila kujali utofauti wa vipato. Mwanamke huyo ni mdada anae jiweza kwa kweli, alicho vutiwa ni jitihada za mshikaji ingawa kipato chake ni kidogo.
Sasa mshikaji kaleta hoja aki hitaji msaada wa mawazo je akubali offer ya mdada huyu ( shemeji yetu) au avumilie na kutekeleza takwa la kufunga ndoa la Mke wake a.k.a mzazi mwenzie?
Mwaga ushauri mdau maana mdada hahitaji hata ndoa anacho hitaji ni upendo wa kweli na uwepo wa mwaname katika maisha yake ili wasukume gurudumu pamoja...