Utatu wenye utata: Umri, Pesa na Mapenzi

Utatu wenye utata: Umri, Pesa na Mapenzi

Nipo hapa nawashikaji tunapiga stori mbili tatu, ghafla kuna prado inapaki mbele yetu anashuka mshikaji wetu Side ambaye tumefahamiana kutokana na mihangaiko ya hapa na pale huku yeye akiwa ni mgeni mtaani kwetu, mlango wa pili anashuka mwanamke "mkali sana" mweupe peee amepakata mtoto, mwanamke huyo amevaa kijigauni cheupee kimeishia magotini. Side anatusalimia pale na kututambulisha huyu ndo shemeji yenu, tunamsalimia kisha Side anampatia funguo funguo ya gari shemeji yetu na kuondoka zake.

tumebaki na Side tunapiga stori na kumsifia kwa kupata chombo kikali namna ile, wakati wa stori nikanukuu maneno haya mawili ambayo hadi sasa nayatafutia ukweli, Side alisema hawa wanawake ukitaka kuwadhibiti lazima uwe na vitu viwili kati ya hivi
  1. Pesa za kumtunza
  2. Kukidhi haja yake ya mwili kikamilifu
ukifanikiwa kwa hivyo, mwanamke yeyote hakupi tabu tena.
.....Side ananyanyuka zake na kuondoka zake......
 
Jinsia ya kike ni ngumu Sana kuilewa kama wao wenyewe hawajielewi unafikili hivyo ndivyo vitawafanya watulie? Nina kisa kimoja ambacho kuna mshikaji alinipa nitakisimulia baadae
Hata mi nakuunga mkono.kwa mfano mmoja hai.mwanamke kama ulimkuta na jamaa yake ambaye choka mbaya kisha we ukamkwapua na hela zako na magari yako!hata umuoneshe mahaba ya aina gani lazima ataenda kwa yule ambae chemistry zao zinaendana
 
Back
Top Bottom