Utatu wenye utata: Umri, Pesa na Mapenzi

Utatu wenye utata: Umri, Pesa na Mapenzi

Wanaruka ruka tu,ila kiuhalisia kabisa kimantiki ktk sekta kuu halis za mahusiano hakuna hela,

Katika sekta kuu za njaa nne za ubongo hakuna fedha,mahusiano halis yaliyobeba dhima halis ya upendo hayaangalii chochote zaid ya muhemko ulivyo kati yenu.. Na ndio maana kama ni hela inabeba mapenz mbona wenye fedha weng wamekwama ktk sekta hyo?
 
Hahahahahaha
Mbavu zangu my foot.
Akiwa hajui kuita baby, love sharti uwe na pesa?????

yes
but kiukweli mapenzi yanaambatana na maneno na pesa kama huna pesa you have to be Romantic fanya utafiti wanaume ambao hawana pesa na wako soo romatic wanamiliki wanawake wazuriii na wala wapenzi wao hawalalamiki hawapewi hela but Mtu mjeuri sio romantic na pesa hana khaa wataishia kusema sina bahati
 
Wapo wahenga walisema penzi haliangalii pesa hata kidogo na wakaja vijana wakaimba pesa ni mbolea ya mapenzi. Mimi naungana na vijana wenzangu kusema pesa ni mbolea ya mapenzi penzi bila pesa ni sawa na mahindi bila mbolea yatakuwepo na utavuna lakini tofauti kubwa na aliyeweka mbolea.

Wakati tumepanga uswahilini choo na bafu chumba kimoja tena nje ya nyumba ukienda kuoga unatazamwa kila upande mwingine anaoga chumbani na mkewe kwenye basin la kuogea huku wakisuguana suguana mgongoni.

Wakati mpenzi wako anakuja kwako kwa daladala wakati mwingine anatembea kwa miguu anakuja kwako amechoka hoi mwingine anamfata kwa gari au anakuja na taxi. Tusidanganyane hatuwezi pata ile kitu sawa lazima mwenye mpunga azidishiwe manjonjo.

Wakati mwenye pesa anamhudumia vyema mkewe anakula vizuri hana stress sisi tunakimbizana kudaiana change ya 5000 alipoenda kununua vitu gengeni mmmmh kuna shida.

Japo kuwa na pesa siyo kigezo cha kupendwa lakini kwa maoni yangu tukubali tu pesa ni mbolea ya mapenzi.

Wakati mwenzako anaenda na mpenzi wake serena hotel na sehemu zingine wewe unampeleka guest ya 2500 shuka zinanuka halafu utegemee mambo mazuri thubutuuuu

Hata sisi maskini tunapendwa pia tena sana lakini walionazo wanafaidi zaid kuliko sisi. Kwani hata shamba lisilo na mbolea litatoa mazao lakini lililopata mbolea litazaa zaidi.
 
Umeandika ukweli mtupu mkuu. Acha tutafute mbolea ili mahindi yastawi vizuri.
 
Back
Top Bottom