Mag3
Platinum Member
- May 31, 2008
- 13,064
- 22,757
Baba yangu alinitembelea hapa Dar es Salaam kwenye miaka ya 90. Alifika kipindi ambapo kulikuwepo na mashindano ya kumtafuta 'Miss Tanzania'. Bahati mbaya ni wakati huo kulitokea malumbano kuhusu mavazi ya vimwana hawa wakiwa jukwaani kwamba hayaendani na mila zetu !! Kwa kuwa shindano lilikuwa likionyeshwa 'live' kwenye TV kwa aibu niliamua kubadilisha 'channel' nikihofia baba kuchukizwa na vimwana walivyovaa. Lo, nilishangaa babu aliponikataza nisifanye hivyo na nikagundua anafuatilia kwa makini sana kilichokua kinaendelea.
Baada ya onyesho kwisha nilitaka sana kujua kwa nini mzee wangu aliyekua na umri karibu miaka 100 afuatilie jambo kama hilo. Akasema, " Mwanangu hilo onyesho limenikumbusha mengi wakati wa ujana wangu kabla ya kuja hawa wazungu. Nashukuru kuwa sasa mnaamka na kuanza kuzienzi mila zetu na desturi ambazo wao waliziita za kishenzi " Nilipomweleza kuwa hayo anayoyaona yanapigwa vita kuwa si utamaduni wetu na tunaiga tu, alihamaki na kunitaka nimpeleke kwa huyo mhuni anayesema hivyo. Alisisitiza kuwa ni hao wazungu ndio walikuwa wanaiga utamaduni wetu.
Ingefaa tuwe tunafikiria mara mbili kabla ya kukurupuka kuponda tamaduni zetu wenyewe na kuziita za kigeni. Huu ni mfano moja tu na naomba wenye mifano mingine kama hii watuhabarishe.
Baada ya onyesho kwisha nilitaka sana kujua kwa nini mzee wangu aliyekua na umri karibu miaka 100 afuatilie jambo kama hilo. Akasema, " Mwanangu hilo onyesho limenikumbusha mengi wakati wa ujana wangu kabla ya kuja hawa wazungu. Nashukuru kuwa sasa mnaamka na kuanza kuzienzi mila zetu na desturi ambazo wao waliziita za kishenzi " Nilipomweleza kuwa hayo anayoyaona yanapigwa vita kuwa si utamaduni wetu na tunaiga tu, alihamaki na kunitaka nimpeleke kwa huyo mhuni anayesema hivyo. Alisisitiza kuwa ni hao wazungu ndio walikuwa wanaiga utamaduni wetu.
Ingefaa tuwe tunafikiria mara mbili kabla ya kukurupuka kuponda tamaduni zetu wenyewe na kuziita za kigeni. Huu ni mfano moja tu na naomba wenye mifano mingine kama hii watuhabarishe.