Utamaduni na tasnia ya filamu Tanzania

Damaso

JF-Expert Member
Jul 18, 2018
1,590
2,088
Habari wakuu, naomba mnisamehe kwa kuwa kimya sana, majukumu ya hapa na pale. Kama kawaida naomba kuleta uzi kuhusu jamii zetu. Leo nimeona ni vyema nikazungumzia tasnia yetu ya filamu hapa Tanzania (Bongo Movie).

Kiukweli tupo nyuma kabsa katika kuwapatia watoto wetu utamaduni na mila ikiwemo kuelewa historia ya jamii mbalimbali haswa jamii ambazo wamezaliwa nao kupitia luninga.

Amini usiamini kuna watu hata majina matatu ya babu zao ama bibi zao hawayajui, inasikitisha sana ila mtu huyo huyo anafahamu majina ya familia nzima ya kardashian.

IMG_0140.jpg



Janga kubwa hili.

Nilifurahi na kuumia kwa wakati mmoja nilipotazama tasnia ya filamu ya Hollywood ambao wanatumia filamu na tamthilia pamoja na nyimbo kuendeleza utamaduni na kuyafanya majina ya watu mashuhuri yaendelee kuishi.

Majina kama Joseph Brant, Lone Horn, Bill Bowlegs, Geronimo, Lozen, Osceola, pamoja na Red Cloud ni majina ambayo ni maarufu kwani hata katika filamu mbalimbali basi husika zao zimeonekana! Wakionesha ushujaa na morali ya kupambana.

Upande wa muziki ndo wamewaenzi kila kona;
1. “Indian Outlaw” kutoka kwa Tim McGraw
IMG_0153.jpg



2. “America the Beautiful” kutoka kwa Jody Brown Indian Family.
IMG_0154.jpg



Kwetu huku Tanzania, nimepata kutazama filamu ya Mkwawa pekee ambapo mwanadada Seko Shamte alipambana akiwa na waigizaji kama vile, Mutaju Issac Marobhe, Paul Clithero pamoja na Doug Bramsen.

Seko Shamte
IMG_0139.jpg


Mkwawa: Shujaa wa Mashujaa

IMG_0144.jpg


Kwa Hollywood na dunia huko kuna filamu chungu mbovu kuhusu mashujaa wa makabila ya wahindi wekundu;

Dance with Wolves (1990)

IMG_0134.jpg



Shalako (1968)
IMG_0135.jpg


Against a Crooked Sky (1975)
IMG_0136.jpg


Two Rode Together (1961)
IMG_0137.jpg


Grayeagle (1977)
IMG_0138.jpg




Na zingine nyingi tu.
Kweli tumeshindwa hata kutengeneza filamu kuhusu mashujaa wetu ili vizazi na vizazi viendelee kusoma kuhusu utamaduni wetu.
1. Kimweri Mputa Magogo
2. Mganila Nonga Bukoli
3. Ludomya Ng’hwele
4. Thomas Marealle Mbegha
5. Mangi Meli
6. Chief Mirambo
Tatizo lipo wapi mpaka tunakosa filamu zinazoelezea utamaduni wetu na makabila zaidi ya 128 bado hatujaruhusu filamu zituoneshe wahusika wa zamani waliobeba utamaduni wa makabila yetu.

Hawa wahindi wametuacha mbali;

1. Lagaan (2001)
IMG_0145.jpg



2. Manjhi: The Mountain Man (2015)
IMG_0146.jpg


3. Lakshya (2004)
IMG_0147.jpg



Tumebakia kuoneshwa mambo ambayo ya tofauti tu tena yasiyo na umuhimu kwetu. Leo dada na mama zetu wanafurahia tamthilia ya La Sultana: The story of Kosem, lakini ni 5% tu au chini ya hapo wanajua kuwa hiyo sio tamthilia ya kutugwa tu bali ni maisha halisi ya Kösem Sultan moja kati ya mwanamama aliyekuwa na nguvu sana kwenye utawala wa Ottoman.

Kösem Sultan
IMG_0142.jpg



La Sultana: The story of Kosem

IMG_0141.jpg



Nina imani kuwa jamii forums kuna watu wenye ushawishi ebu kidogo tujitahidi kuwasawishi hawa waongozaji na wadau wa filamu na hata Wizara husika maana tumekosa kabsa ladha na hamu ya kufuatilia filamu na tamthilia za Kitanzania.
Mtu yupo radhi anunue bando aende Net Naija kuchukua
Operation Fortune: Ruse de Guerre au Chokehold ila sio filamu ya Kitanzania.

Leteni filamu zenye utamu kama filamu hizi; Misukosuko, Nsyuka na Odama.

IMG_0152.jpg


IMG_0151.jpg

IMG_0150.jpg

IMG_0148.jpg

IMG_0149.jpg


Naomba kuwasilisha…..
[mention]Mshana Jr [/mention] [mention]Tit 4 Tat [/mention] [mention]MalcolM XII [/mention]
 

Attachments

  • IMG_0143.jpg
    IMG_0143.jpg
    7.1 KB · Views: 7
Damaso ni furaha kubwa kukuona tena hapa jukwaani ukiwa bukheri wa afya.. Niko hapa nimefika kwa wakati.. Nitarejea...
 
Habari wakuu, naomba mnisamehe kwa kuwa kimya sana, majukumu ya hapa na pale. Kama kawaida naomba kuleta uzi kuhusu jamii zetu. Leo nimeona ni vyema nikazungumzia tasnia yetu ya filamu hapa Tanzania (Bongo Movie).

Kiukweli tupo nyuma kabsa katika kuwapatia watoto wetu utamaduni na mila ikiwemo kuelewa historia ya jamii mbalimbali haswa jamii ambazo wamezaliwa nao kupitia luninga.

Amini usiamini kuna watu hata majina matatu ya babu zao ama bibi zao hawayajui, inasikitisha sana ila mtu huyo huyo anafahamu majina ya familia nzima ya kardashian.

View attachment 2609586


Janga kubwa hili.

Nilifurahi na kuumia kwa wakati mmoja nilipotazama tasnia ya filamu ya Hollywood ambao wanatumia filamu na tamthilia pamoja na nyimbo kuendeleza utamaduni na kuyafanya majina ya watu mashuhuri yaendelee kuishi.

Majina kama Joseph Brant, Lone Horn, Bill Bowlegs, Geronimo, Lozen, Osceola, pamoja na Red Cloud ni majina ambayo ni maarufu kwani hata katika filamu mbalimbali basi husika zao zimeonekana! Wakionesha ushujaa na morali ya kupambana.

Upande wa muziki ndo wamewaenzi kila kona;
1. “Indian Outlaw” kutoka kwa Tim McGraw
View attachment 2609645


2. “America the Beautiful” kutoka kwa Jody Brown Indian Family.
View attachment 2609646


Kwetu huku Tanzania, nimepata kutazama filamu ya Mkwawa pekee ambapo mwanadada Seko Shamte alipambana akiwa na waigizaji kama vile, Mutaju Issac Marobhe, Paul Clithero pamoja na Doug Bramsen.

Seko Shamte
View attachment 2609585

Mkwawa: Shujaa wa Mashujaa

View attachment 2609649

Kwa Hollywood na dunia huko kuna filamu chungu mbovu kuhusu mashujaa wa makabila ya wahindi wekundu;

Dance with Wolves (1990)

View attachment 2609563


Shalako (1968)
View attachment 2609578

Against a Crooked Sky (1975)
View attachment 2609582

Two Rode Together (1961)
View attachment 2609583

Grayeagle (1977)
View attachment 2609584



Na zingine nyingi tu.
Kweli tumeshindwa hata kutengeneza filamu kuhusu mashujaa wetu ili vizazi na vizazi viendelee kusoma kuhusu utamaduni wetu.
1. Kimweri Mputa Magogo
2. Mganila Nonga Bukoli
3. Ludomya Ng’hwele
4. Thomas Marealle Mbegha
5. Mangi Meli
6. Chief Mirambo
Tatizo lipo wapi mpaka tunakosa filamu zinazoelezea utamaduni wetu na makabila zaidi ya 128 bado hatujaruhusu filamu zituoneshe wahusika wa zamani waliobeba utamaduni wa makabila yetu.

Hawa wahindi wametuacha mbali;

1. Lagaan (2001)
View attachment 2609614


2. Manjhi: The Mountain Man (2015)
View attachment 2609613

3. Lakshya (2004)
View attachment 2609610


Tumebakia kuoneshwa mambo ambayo ya tofauti tu tena yasiyo na umuhimu kwetu. Leo dada na mama zetu wanafurahia tamthilia ya La Sultana: The story of Kosem, lakini ni 5% tu au chini ya hapo wanajua kuwa hiyo sio tamthilia ya kutugwa tu bali ni maisha halisi ya Kösem Sultan moja kati ya mwanamama aliyekuwa na nguvu sana kwenye utawala wa Ottoman.

Kösem Sultan
View attachment 2609597


La Sultana: The story of Kosem

View attachment 2609599


Nina imani kuwa jamii forums kuna watu wenye ushawishi ebu kidogo tujitahidi kuwasawishi hawa waongozaji na wadau wa filamu na hata Wizara husika maana tumekosa kabsa ladha na hamu ya kufuatilia filamu na tamthilia za Kitanzania.
Mtu yupo radhi anunue bando aende Net Naija kuchukua
Operation Fortune: Ruse de Guerre au Chokehold ila sio filamu ya Kitanzania.

Leteni filamu zenye utamu kama filamu hizi; Misukosuko, Nsyuka na Odama.

View attachment 2609620

View attachment 2609621
View attachment 2609622
View attachment 2609623
View attachment 2609624

Naomba kuwasilisha…..
[mention]Mshana Jr [/mention] [mention]Tit 4 Tat [/mention] [mention]MalcolM XII [/mention]
Aisee sijawahi kupenda filamu za Kituruki ila Kosema ni Game of thrones ya Kituruki. Nilianza kuichungulia kiutani utani ila story yake ni bomba. THe game of politics and power. Waturuki kumbe wako vizuri.
 
Back
Top Bottom