Utajiri wenye uchungu

NYEMO CHILONGANI
UTAJIRI WENYE UCHUNGU
0718069269

Sehemu ya Kumi na Tisa.

‘Dylan Was Caught With Beautiful Shawty’ ‘Alone In The Dark, What Did They Do?’ ‘Atlast, He Is Happy Maybe’ (Dylan Abambwa na Msichana Mrembo’ Ni Gizani, Walikuwa Wakifanya Nini?’ Hatimaye! Labda Ana Furaha) hivyo vilikuwa vichwa mbalimbali vya magazeti ya udaku, kila mtu aliyeyaona mitaani, tena yakiwa na habari iliyomhusu mtoto wa bilionea, iliwashangaza na hivyo kulinunua gazeti hilo.
Dylan alionekana kuwa na msichana mrembo, mwenye mchanganyiko wa rangi, walipomwangalia msichana huyo, alikuwa mrembo wa sura kiasi kwamba kila mmoja alishangaa, jamaa alimtoa wapi msichana huyo?
Hiyo ilikuwa habari kubwa ya siku hiyo, ukaribu wao, ulionyesha shaka kwa kila mtu aliyeziangalia picha zile, walichokifanya wataalamu wa mambo, wakachukua magazeti yenye picha hizo kisha kuanza kuzitolea ufafanuzi.
Kitu cha kwanza walichoanza nacho kilikuwa ni muonekano wa wote wawili, walisimama karibukaribu, mbali na hiyo, walionekana kama watu wenye uhusiano wa kimapenzi kitu kilichozua maswali kwani walijua kwamba huyo Dylan alitarajiwa kumuoa msichana mwingine siku chache zijazo.
“Au huyu ndiye msichana mwenyewe?” aliuliza jamaa mmoja.
“Sidhani! Nasikia huyo ni mrembo zaidi, anaitwa Katty, huyu ni Pauline, ndiye nani? Si huyu,” alisema jamaa mwingine, alionekana kumfuatilia sana Dylan.
Taarifa hizo ilipomfikia Dylan, alishangaa, hakuamini kama kitendo chake cha kusimama na msichana Pauline kingekuwa stori namna ile, alijifungia ofisini mwake, hakutaka kutoka ndani na kitu pekee kilichomuumiza ni juu ya Katty, kama angeona kile kilichoandikwa, nini kingetokea?
Wakati hayo yakiendelea, katty alikuwa nchini Italia, alikwenda huko tayari kwa kuonana na padri ambaye alitakiwa kufungisha ndoa yao miezi miwili mbele. Wakati wakiwa mitaani ndipo macho yao yakatua katika Gazeti la US Weekly ambalo hutoka kila siku na kusambazwa katika nchi zenye maendeleo, alipoliona, akamwambia rafiki yake alichukue kwani habari iliyoandikwa, ilimshtua.
Alipopewa mikononi na kuliangalia, hakuamini kile alichokiona, damu ikaanza kutembea kwa kasi mwilini mwake, hakuamini kama mwanaume aliyekuwa akimpenda, Dylan angeweza kuwa katika hali hiyo, tena na mwanamke ambaye hakuonekana kuwa mrembo kama yeye.
“Cassie, am I dreaming?” (Cassie, ninaota?) alimuuliza rafiki yake.
Hakuweza kuyazuia machozi yake kutiririka mashavuni mwake, maumivu aliyoyasikia hayakuweza kusimulika. Hata nguvu za kwenda kumuona Padri hakuwa nazo, alibaki akisononeka moyoni mwake tu.
“Katty, usijali, inawezekana ni marafiki tu...” alisema Cassie.
“Marafiki! Marafiki wanaweza kusimama hivi?” aliuliza Katty.
“Ni kawaida tu, usimfikirie vibaya Dylan, ni wako na bado anakupenda.”
Japokuwa rafiki yake, Cassie alimwambia hivyo lakini hakutaka kuamini, bado alihisi kwamba mpenzi wake huyo alikuwa akimsaliti. Hakutaka kumpigia simu kwanza mpaka pale atakapozungumza naye kwenye simu ili ajue kuhusu kile kilichokuwa kimetokea.
Wakati akiwa na padri huyo huku wakizungumza, simu yake ikaanza kuita, alipoangalia mpigaji, alikuwa mpenzi wake, Dylan. Hakuipokea simu hiyo, alibaki akiiangalia, alitaka kuzungumza na mwanaume huyo pale atakapotoka nje.
Walipomaliza kuzungumza na padri huyo, wakasimama na kutoka huku wakiwa wamekwishaelewana kwamba yeye ndiye atakayefungisha ndoa hiyo ambayo ilionekana kuwa na dalili zote za kufana.
“Dylan alinipigia simu...” alisema Katty.
“Amesemaje?”
“Nilikuwa ndani, sikuweza kupokea...”
“Hebu mpigie kwanza,” alisema Cassie, hata kabla Katty hajapiga, mara simu ya Dylan ikawa inaingia, harakaharaka akaipokea.
“Unasemaje?” aliuliza kishari.
“Samahani, naomba nikuelezee...” alisema Dylan.
“Unielezee kuhusu nini? Kuhusu nini nauliza? Au huyo malaya wako?” aliuliza Katty huku hata sauti yake tu ilisikika kama mtu mwenye hasira nyingi.
“Hapana! Usiseme hivyo!”
“Nisemeje? Nakuuliza swali, unamjua yule mwanamke humjui?” aliuliza msichana huyo.
“Namjua!”
“Ni nani kwako?”
“Mfanyakazi wangu!”
“Kwa hiyo umeamua kuanza kuchukua wafanyakazi?” aliuliza msichana huyo.
Ilikuwa ngumu kumtuliza, lakini kwa sababu Dylan alikuwa mtu mwenye busara, nguvu ya kuzungumza na watu, akamuweza Katty na kuanza kumhadithia kila kitu kuhusu msichana Pauline.
Hakutaka kumficha kitu chochote kile kwa kuamini kwamba ukweli ndiyo utakaomfanya kuwa huru. Katty akaridhika, historia fupi kuhusu msichana huyo ambayo alipewa, ikampa uhakika kwamba mpenzi wake huyo hakuwa na uhusiano na msichana huyo.
“Una uhakika?”
“Ndiyo mpenzi! Usiamini magazeti, ukienda hotelini kuonana na mgeni, watasema umekwenda kulala na mwanamke, usiyaamini haya magazeti,” alisema Dylan.
Kidogo moyo wa Katty ukawa na amani, akahisi furaha ikirudi tena moyoni mwake, kile alichozungumza mpenzi wake kilimpa uhakika kwamba kweli Pauline hakuwa wa mpenzi wake bali walikuwa watu wasiokuwa na uhusiano wowote ule japokuwa msichana huyo alikuwa akijikomba.
“Umefikia wapi?” aliuliza Dylan.
“Nimezungumza na padri, kila kitu kipo tayari!”
“Kweli?”
“Ndiyo! Kazi imebaki kwetu tu,” alisema Katty.
“Basi hakuna tatizo, kila kitu kitafanikiwa.”
Siku ziliendelea kwenda mbele, kila mtu akawa na hamu kuona harusi hiyo, magazeti yaliripoti kila kitu kilichokuwa kikiendelea. Kwa Dylan, hakuwa na furaha kabisa, kila siku, alikuwa akifikiria kuhusu tatizo la kiafya lililokuwa likimsibu.
Hiyo ilikuwa siri kubwa, hakutaka kumwambia mtu yeyote yule, ni watu watatu tu ndiyo waliokuwa wakilifahamu tatizo hilo, yeye, baba yake na mama yake mlezi.
Moyo wake ulimuuma sana lakini hakuwa na jinsi, siku zilikatika mpaka siku hiyo ambayo ilikuwa ikisubiriwa kwa hamu. Kila kitu kiliandaliwa na ni tukio hilo ndilo lililokuwa likisubiriwa.
Ilikuwa harusi kubwa, iliyoshika masikio ya watu lakini hakukuwa na watu zaidi ya ishirini waliohuhuria, ilikuwa harusi ya kitajiri, na hata hao watu wachache waliotakiwa kuhudhuria, walihudhuria kwa mwaliko maalumu.
“Umekubali kumuoa na kuwa mke wako katika shida na raha?” aliuliza padri.
“Ndiyo nimekubali!”
Hakuishia hapo, padri aliendelea kuuliza na jibu lilikuwa lilelile na hata alipokuja kwa Dylan naye, jibu halikubadilika, liliendelea kuwa vilevile. Makofi yakatawala, siku hiyo usiku, kilichofuatia ni sherehe kubwa na kuelekea katika Visiwa vya Bahamas kwa ajili ya fungate.
Kama kawaida, Dylan alipokwenda huko, kwenye begi lake kulikuwa na kiungo cha bandia ambacho ndicho angekitumia huko. Hilo, bado Katty hakujua chochote kile, kila alipofanya naye mapenzi, hakujua kama kilichokuwa kikitumika kilikuwa ni kiungo cha bandia kutokana na ulaini wa kifaa hicho.
*****
“Unaitwa nani?”
“Mike Johnson...”
“Una miaka mingapi?”
“Ishirini!”
“Sawa! Unaishi wapi hapa New York?”
“Livingstone...”
“Kule uswahilini?”
“Ndiyo!”
“Utaweza kutunza siri...”
“Hakuna tatizo...nitaweza tu....”
“Sawa! Unajua kwa nini upo hapa?”
“Hapana! Ila niliitwa na watu fulani, wakaniambia kuna kazi natakiwa kufanya na nitalipwa dola milioni moja, hakuna tatizo, mimi ni masikini na ninahitaji sana hizo hela, hivyo nipo tayari!”
“Yaani kisa umasikini, haijalishi ni kazi gani, wewe upo tayari?”
“Ndiyo daktari...”
Alikuwa miongoni mwa vijana masikini mno waliokuwa wakiishi katika Mtaa wa Livingstone hapo New York. Maisha yake yalitawaliwa na ufukara mkubwa, hakuwa na fedha, mara nyingi alifanya kazi mbalimbali ili kujikimu na maisha lakini hayakuwa na ahueni hata siku moja.
Umasikini ulimpiga, ulimtesa mno na hakuwa na tumaini lolote lile mbele yake. Alitamani kuwa na fedha, alitamani kuendesha magari ya kifahari na kuishi maisha ya gharama kama walivyokuwa wakiishi masupastaa wa mpira wa kikapu, wanamuziki lakini hilo halikuwezekana, maisha hayo alikutana nayo kwenye ndoto tu.
Japokuwa alikuwa masikini, huyu Mike alikuwa miongoni mwa watu waliokuwa na sura nzuri, alimvutia kila msichana aliyekuwa akimwangalia, wengi walitamani kuwa naye lakini Mike mwenyewe, yeye na wanawake ilikuwa ni kama paka na panya.
Aliamini kwamba unapojiingiza kwenye mahusiano ya kimapenzi unapoteza asilimia kadhaa ya vitu fulani katika maisha yako, utakuwa na stress, utashindwa kufanya mambo mengine mara mpenzi anapokuzingua hivyo, kuwa singo kama alivyoamua, kwake ilikuwa ndiyo njia sahihi ya kuweza kuishi maisha ya furaha.
“Do you know my father?” (unamfahamu baba yangu) aliuliza msichana mmoja, mzuri wa sura, alisimama mbele ya Mike.
“No! Who is he?” (hapana! Ni nani?)
“Mr. Godfrey Paul...” (Bwana Godfrey Paul)
“A bilionaire one?” (huyu bilionea?)
“Exactly.” (Sawasawa)
“So what can I help you miss?” (Kwa hiyo nikusaidie nini mrembo?)
“I need your help! I have fallen, I want you to pick me up,” (Ninahitaji msaada wako! Nimeanguka, nataka uniinue) alisema msichana huyo.
“How?” (Kivipi?)
“I love you, I want you to be mine, forever!” (Ninakupenda! Nataka uwe wangu, milele) alisema msichana huyo aliyeitwa Jesca.
Japokuwa msichana huyo alijitambulisha kama mtoto wa bilionea mkubwa nchini Marekani lakini Mike hakutaka kukubaliana naye, hakuhitaji msichana yeyote kwa kipindi hicho, hakuwa tayari kwa kuingia kwenye uhusiano wa kimapenzi.
Aliachana na Jesca na yeye kufanya mambo mengine. Umasikini uliendelea kumtesa kila siku, kwa kuwa alikuwa mrefu, aliamini kwamba mchezo wa kikapu ungemtoa lakini napo huko akaambulia patupu.
Maisha yalisonga mbele mpaka siku ambayo alifuatwa na watu wawili, waliovalia suti ambao walimvuta pembeni na kuanza kuzungumza naye. Mara ya kwanza alihisi kuwa hao ni watu wabaya, aliogopa lakini hakutaka kuuonyesha uoga wake mbele ya watu hao.
Walijitambulisha kwamba wao ni watu wema hivyo walitaka kufanya naye kazi. Hakujua ni kazi gani, hakuwa na fedha, alikuwa kijana masikini, je hiyo kazi ambayo alitakiwa kufanya na watu hao, ilikuwa kazi gani?
“Mfanye kazi na mimi?”
“Ndiyo!”
“Sasa mimi nina mtaji gani jamani?”
“Wala usijali, si kazi inayohitaji wewe kutupa fedha, ni kazi inayohitaji sisi kukupa fedha!” alijibu jamaa mmoja.
“Mmh!”
“Usiogope, jiandae, kesho saa mbili asubuhi tunakuja kukuchukua, kuna sehemu tutakwenda nawe. Kwanza chukua hii,” alisema mwanaume mmoja, hapohapo akamgawia kiasi cha dola mia tano, wakaondoka zao.
Huo haukuwa mwisho, bado alikuwa akijiuliza kuhusu watu hao lakini hakupata jibu kabisa. Wakati mwingine alihisi kwamba watu hao walikuwa wauza madawa ya kulevya, akaogopa lakini kwa kuwa walionekana kuwa watu safi, wamevaa suti hakutaka kujali sana wala kuhisi hivyo.
Maisha yakaendelea, kesho yake, muda uleule alioambiwa, watu hao wakafika mahali hapo, wakamchukua na kuondoka naye. Baada ya dakika kadhaa, gari hilo likasimama mbele ya Hospitali ya Marie Stoppes Medical Center na kutakiwa kuteremka, akafanya hivyo.
Wakaelekea ambapo huko akapelekwa kwa daktari mmoja ambaye alimchukua na kumuingiza ndani, kisha akaanza kuzungumza naye, mazungumzo marefu yaliyojaa maswali mengi.
“Kitu cha msingi ni kutunza siri, halafu baada ya kufanya kazi yetu, tunataka hata mji huu uhame,” alisema Dk. Fabian.
“Hakuna tatizo, nitatunza siri mpaka kifo changu!”
“Kweli?”
“Ndiyo! Nitatunza siri dokta!”
“Sawa! Unasema unaishi Livingstone, si ndiyo?”
“Ndiyo dokta!”
“Basi sawa...subiri hapo!”
Mike hakutakiwa kuwa na presha yoyote ile, alitakiwa kukaa kwenye benchi, baada ya muda fulani, wanaume wengine wakaja na kumchukua, wakampeleka katika chumba kimoja kilichokuwa kimya kabisa.
Muda wote huo Mike alikuwa akishangaa, hakujua ni kitu gani kilikuwa kikiendelea. Kwa mbali, akaanza kuingiwa na hofu, wakati mwingine alitamani kuwaambia kwamba basi hiyo kazi hakuitaka tena lakini akapiga moyo konde na hivyo kusikilizia nini ambacho kingetokea.
Baada ya saa moja, mlango ukafunguliwa, dokta Fabian akaingia akiwa na vipimo. Kitu cha kwanza kabisa akachukua damu yake na kuondoka nayo, aliporudi, alikuwa na majibu kwamba damu yake ilikuwa safi hivyo alistahili kuifanya kazi hiyo.
“Ila ni kazi gani?”
“Usijali Mike, utaijua tu. Si kazi ya hatari kabisa...si unataka fedha lakini?”
“Ndiyo!”
“Basi usijali...” alisema daktari huyo. Bado Mike alikuwa na hofu mno. Kuna kipindi alifikiria kukimbia tu kwani kila alipokuwa hapo, mapigo yake ya moyo yalikuwa yakidunda kwa nguvu mno.

Je, nini kitaendelea?
Tukutane Ijumaa hapahapa.
 
NYEMO CHILONGANI.
UTAJIRI WENYE UCHUNGU.
0718069269.

Sehemu ya Ishirini

Kila mmoja alionekana mwenye furaha kubwa huko Bahamas, walitembea kila sehemu, kwa siku zote walizokuwa huko, Dylan alikuwa akifanya mapenzi na mkewe, Katty usiku tu.
Hakutaka kufanya mchana, alijifanya kuwa bize mchana na hata alipoguswa hapa na pale, alikuwa mkali, ila usiku, tena huku taa zikiwa zimezimwa, alifanya kwa nguvu zote kwa kutumia kiungo cha bandia ambacho alikifunga kama mkanda fulani hivi.
Baada ya kukaa kwa mwezi mzima ndani ya kisiwa hicho huku wakiponda raha, wakaamua kurudi nchini Marekani kuendelea na shughuli zao kama kawaida. Maisha yake yakabadilika, hayakuwa kama yalivyokuwa kipindi cha nyuma.
Japokuwa alikuwa na furaha tele lakini tatizo moja ambalo lilimfanya kukosa raha katika maisha yake ni juu ya afya yake tu. Alijitahidi kuwaona wataalamu mbalimbali, hakukuwa na mtu aliyemtibu hivyo kubaki hivyohivyo.
Siku zikaendelea kukatika, miezi ikakatika, baada ya miezi sita ya ndoa, mkewe, Katty akaanza kulilia mtoto. Huo ulikuwa mtihani mkubwa kwake, kama kufanya mapenzi, walifanya, tena kwa nguvu zote, kwa nini mtoto hakupatikana?
Hali hiyo ikampa mawazo mazito Dylan, yeye alilijua tatizo lakini mkewe hakujua kitu chochote kile. Kazi yake kubwa kwa kipindi hicho ikawa ni kumfariji tu kwamba muda ukifika, Mungu atawapa mtoto, kwa kipindi hicho walitakiwa kuendelea kusubiri.
“Tatizo nini mume wangu?” aliuliza Katty.
“Hata mimi sijui mke wangu.”
“Kama vipi tukamuone daktari...” alishauri Katty.
“Unahisi tunaweza kuwa na tatizo?”
“Nahisi itakuwa hivyo...”
Hicho ndicho walichotakiwa kufanya hasa katika hali kama hiyo. Kesho yake walikuwa katika Hospitali ya Marie Stopes ambapo wakakutana na daktari wao, Fabian na kumueleza tatizo lao.
“Poleni sana, ila hali kama hiyo inawatokea watu wengi, ngoja niwafanyie vipimo,” alisema Dk. Fabian na hivyo kuanza kazi ya kuwafanyia vipimo.
Muda wote Dylan alikuwa na mawazo tele, moyo wake ulimuuma mno, hakuamini kama bilionea kama yeye ndiye aliyekuwa akipitia maisha hayo. Mbele yake aliiona aibu kubwa, kitendo cha kushindwa kumpa mimba mke wake kilimfanya kuona kwamba siku yoyote ile angeweza kugundulika kile alichokuwa akikifanya kitandani.
Baada ya daktari kuwafanyia vipimo na wiki moja iliyofuata, wakafuata matokeo ya vipimo vyao na kuonekana wote wapo vizuri, hapakuwa na mtu yeyote aliyekuwa na tatizo lolote lile.
“Unasema kweli daktari?”
“Ndiyo Dylan, hakuna mwenye tatizo kabisa,” alijibu Dk. Fabian,
Wakaondoka mahali hapo huku daktari akiwataka kufika hospitalini hapo mara kwa mara kwa ajili ya kupewa ushauri juu ya kitu walichotakiwa kufanya.
Hilo wala halikuwa tatizo, mara kwa mara walifika mahali hapo kama walivyokuwa wakiambiwa, pamoja na hali yote hiyo, matokeo hayakuweza kubadilika, hali ilikuwa ileile kwamba mimba haikupatikana.
“Sasa tatizo litakuwa nini?” aliuliza Katty.
“Hata mimi sifahamu! Au twende sehemu za maombezi..”
“Labda, inawezekana kuna tatizo.”
Wakawa watu wa kwenda kanisani, huko, wakafanyiwa maombezi lakini bado hali iliendelea kuwa vilevile. Waliishi maisha ya majonzi, muda mwingine Katty alikuwa mtu wa kulia tu.
Siku nyingine hakuwa akizungumza na mumewe, hasira zilimkaba kooni na muda mwingi alikuwa akimlaumu Mungu. Kazi yao kubwa ilikuwa ni kubadilisha hospitali, kote huko, matokeo yaliendelea kubaki vilevile lakini Dylan alifahamu nini lilikuwa tatizo.
“Hivi siku akinigundua, itakuwaje?” alijiuliza Dylan.
“Nafikiri itakuwa mwisho! Mungu wangu, nitaishi maisha haya mpaka lini? Ngoja nimuone daktari, nahisi kuna kitu natakiwa kufanya,” alisema Dylan.
Siku hiyo hakutaka kurudi nyumbani mapema, alichokifanya ni kupitia hospitalini ambapo huko akaonana na Dk. Fabian na kuanza kuzungumza naye. Hakutaka kumficha, alijiweka wazi kila kitu kilichokuwa kikiendelea katika maisha yake.
“Ooppss...” alishusha pumzi nzito daktari.
“Ndiyo hivyo! Ninahitaji msaada wako,” alisema Dylan.
“Unafikiri nitakusaidia vipi?”
“Nataka tufanye kitu kimoja...”
“Kipi hicho...”
“Tupandikize mbegu za kiume katika yai la mke wangu,” alisema Dylan.
“Mbegu zako?”
“Hapana! Za mtu mwingine...”
“Mmh!”
“Nini sasa?”
“Nahisi inaweza kuleta matatizo baadaye...”
“Matatizo gani?”
“Huyo mtu akitoa siri...!”
“Sitaki ajue hizo mbegu zinakwenda wapi, iwe siri, nitamlipa dola milioni moja,” alisema Dylan.
“Kweli?”
“Ndiyo! Haina jinsi, nataka kumuona mke wangu akiwa na furaha siku zote katika maisha yake,” alisema Dylan.
Hakuwa na jinsi, kitu pekee alichokihitaji kwa wakati huo ni kumuona mke wake akiwa na furaha. Alijua kwamba jambo alilotaka kulifanya lilikuwa na hatari lakini hakujali, alizihitaji hizo mbegu za kiume kwa gharama zozote zile.
Alichokifanya ni kumuachia jukumu hilo Dk. Fabian ambaye kazi yake kubwa ilikuwa ni kumtafuta mtu ambaye angeweza kuifanya kazi hiyo, mwanaume mwenye sura nzuri ili mtoto atakayezaliwa basi awe na sura nzuri.
Kazi hiyo ikaanza mara moja, alichokifanya Dk. Fabian ni kuwatafuta vijana ambao waliingia mtaani na kumpata Mike ambaye walizungumza naye na kumpeleka hospitali pasipo kumwambia kwamba lengo la yeye kuwa mahali hapo ni kwamba mbegu zake zilikuwa zikihitajika sana.
“Kwa hiyo ishu ni kutoa mbegu tu?” aliuliza Mike.
“Ndiyo! Utapata dola milioni moja...”
“Kweli?”
“Ndiyo!”
“Hakuna kingine?”
“Hakuna!”
Kwake, kwa umasikini aliokuwa nao wala halikuwa tatizo, lilikuwa jambo dogo sana. Kutoa mbegu hizo huku akiingiza dola milioni moja ambazo kwa fedha za Kitanzania ilikuwa ni zaidi ya bilioni mbili, ilikuwa ni bahati mno.
Alichoambiwa ni kuingia ndani ya chumba kimoja kilichokuwa na televisheni, akapewa chombo na kisha kuwashiwa televisheni hiyo na kuwekewa filamu ya utupu huku akitakiwa kujichua.
Akaanza kazi huku akiwa peke yake. Dakika tano nyingi, akafanikiwa kutoa mbegu zake ambazo zilichukuliwa na kuwekwa kwenye mashine maalumu na kutakiwa kuondoka mahali hapo huku akiambiwa kwamba kila kitu kilichoendelea, kiwe siri, asijue mtu yeyote yule. Akakubaliana nao. Ndani ya saa tatu, kiasi hicho cha fedha kaingizwa katika akaunti yake.
****
“Nimeanza kusikia kizunguzungu mpenzi,” alilalamika Katty, ilikuwa ni saa sita usiku.
“Kuna nini tena mpenzi wangu?” aliuliza Dylan huku akionekana kuwa na wasiwasi.
“Sijui! Tumbo linaniuma, nisaidie, tumbo linaniuma na nasikia kizunguzungu, nisaidie mume wangu,” alipiga kelele Katty.
Hakukuwa na kitu kingine cha kufanya zaidi ya kumchukua mkewe, Katty, akambeba na kumpeleka ndani ya gari lake na kuanza safari ya kuelekea katika Hospitali ya Marie Stoppes Medical Center.
Njiani, bado Katty alikuwa akilalamika kwa maumivu huku kile kizunguzungu kikiongezeka kadiri dakika zilivyokwenda mbele. Dylan alichanganyikiwa, aliendesha gari kwa kasi ya ajabu mpaka walipofika katika hospitali hiyo ambapo harakaharaka akawaita manesi ambao wakafika mahali hapo na kumpakiza kwenye machela na kuanza kuisukuma kuelekea nani.
Dylan alikuwa akifuatilia kwa nyuma, alionekana kuchanganyikiwa, hakujua tatizo lilikuwa nini mpaka mke wake kuwa kwenye tatizo kubwa namna ile. Machela ile ikaingizwa katika chumba kilichoandikwa Theatre kwa mlangoni na yeye kuambiwa kubaki mahali hapo.
“Nataka niende na mke wangu,” alisema Dylan.
“Hapana...unatakiwa kubaki hapa,” alisema nesi.
“Nesi...nesi, ninampenda mke wangu, ninataka kuwa karibu naye...” aliendelea kusema Dylan huku akionekana kuchanganyikiwa mno, ugonjwa wa ghafla wa mkewe ulimuweka katika hali mbaya mno.
Hakuruhusiwa kuingia ndani ya chumba hicho, alitakiwa kubaki mahali hapo huku manesi wale wakienda na Katty ndani ya chumba kile. Huku nje, Dylan alibaki akiwa ametulia, muda wote alionekana kuwa na mawazo. Manesi walipokuwa wakitoka nje, aliwang’ang’ania na kutaka kujua ni kitu gani kilikuwa kikiendelea.
“Kuna nini? Nini kimemtokea mke wangu?” aliuliza Dylan huku akionekana kuchanganyikiwa.
“Hakuna kitu, subiri, daktari atakwambia kila kitu,” alisema nesi.
“Atapona?”
“Utaambiwa, subiri hapo,” alisema nesi huyo, hakutaka kubaki mahali hapo kwa kuogopa maswali mengi, huyo akaondoka zake.
Dylan alibaki mahali hapo huku akiwa na mawazo tele, alijiinamia chini, alionekana kuwa na wasiwasi mno, wala haukupita muda mrefu, mlango ukafunguliwa na nesi mwingine kutoka, akasimama na kumdaka na kumuuliza maswali mengine lakini nesi huyo hakutaka kujibu swali lolote lile.
Baada ya dakika chache, Dk. Fabian akatokea mahali hapo huku akiwa kwenye mwendo wa kasi, Dylan alipoyainua macho yake, wakagonganisha macho na daktari huyo kumkonyeza, akaachia tabasamu kisha kuingia ndani ya chumba kile.
Huo ndiyo ulikuwa mpango waliotaka kufanya, Dylan hakutaka kukosea, alijua siku za hatari za mke wake kushika mimba hivyo alihakikisha siku hiyo anafanya kitu kimoja kikubwa.
Kwanza akamuwekea madawa ya usingizi ambayo yangemfanya kusikia maumivu ya tumbo kwa mbali na kuhisi kizunguzungu na mwisho wa siku kupoteza fahamu. Hilo ndilo lililofanyika, wakati amejisikia kizunguzungu, akapoteza fahamu ili Dk. Fabian afanye kazi yake ya kupandikiza mbegu za kiume katika mwili wa Katty.
Hilo lilifanyika kwa siri, ni Dk. Fabian na daktari mwenzake, Dk. Alexander ndiyo waliojua mchezo huo. Mara moja, tena kwa haraka sana kazi ikaanza kufanyika ndani ya chumba hicho.
Dylan alikaa nje ya chumba kile, alijiona kuwa na mafanikio makubwa, alimshukuru Mungu kwa kufanikisha mpango huo, kazi kubwa ilibaki kwa madaktari hao ambao walimuongezea nusu kaputi kitandani pale.
Baada ya saa moja, kila kitu kikawa tayari, madaktari hao wawili wakatoka, kitu cha kwanza baada ya kuonana na Dylan nje ya chumba hicho ni kuanza kumpongeza na kumwambia ainge ndani ya chumba kile.
“Tumefanikiwa...” alisema Dk. Fabian.
“Kweli?”
“Asilimia mia moja, tumefanikiwa!”
“Asante Mungu, siamini!”
“Amini sasa, imekuwa kazi nyepesi mno!”
Wakapongezena, baada ya saa mbili, Katty akarudiwa na fahamu, mtu wa kwanza kabisa kumuona ndani ya chumba hicho alikuwa mume wake. Japokuwa ilikuwa ni saa nane usiku lakini mwanaume huyo hakulala, alipomuona mkewe amefumbua macho, uso wake ukaonyesha tabasamu pana.
“Mume wangu! Nini kilitokea?” aliuliza Katty huku akimwangalia Dylan usoni.
“Sijui! Ila madaktari wamekupima wamegundua kwamba kizunguzungu kimesababishwa na akili yako kuchoka, umefanya kazi mfululizo,” alijibu Dylan bila kupepesa macho pembeni, alitaka kuaminika zaidi.
Hata madaktari walipoingia, majibu yao yalikuwa yaleyale kwamba alifanya kazi kwa kipindi kirefu hivyo alichoka sana hali iliyompelekea kusikia kizunguzungu.
Saa tisa usiku, akaruhusiwa na kurudi nyumbani.
Usiku wa siku hiyo, ulikuwa ni wa mahaba mazito, Dylan hakutaka kuichezea nafasi hiyo, akaanza kumpapasa mkewe kitandani na mwisho wa siku wakajikuta wakiwa kwenye dimbwi la mahaba na hatimaye kuanza kuvuana nguo, kilichofuatia ni sauti za mahaba huku Dylan akiwa makini sana katika kucheza na kifaa kile cha bandia.

Je nini kitaendelea?
Tukutane Junapili
 
Aisee

Huyu Dylan bora angekuwa tu mkweli kwa mkewe jamani

Madame santee
 
NYEMO CHILONGANI.
UTAJIRI WENYE UCHUNGU.
0718069269.

Sehemu ya Ishirini

Kila mmoja alionekana mwenye furaha kubwa huko Bahamas, walitembea kila sehemu, kwa siku zote walizokuwa huko, Dylan alikuwa akifanya mapenzi na mkewe, Katty usiku tu.
Hakutaka kufanya mchana, alijifanya kuwa bize mchana na hata alipoguswa hapa na pale, alikuwa mkali, ila usiku, tena huku taa zikiwa zimezimwa, alifanya kwa nguvu zote kwa kutumia kiungo cha bandia ambacho alikifunga kama mkanda fulani hivi.
Baada ya kukaa kwa mwezi mzima ndani ya kisiwa hicho huku wakiponda raha, wakaamua kurudi nchini Marekani kuendelea na shughuli zao kama kawaida. Maisha yake yakabadilika, hayakuwa kama yalivyokuwa kipindi cha nyuma.
Japokuwa alikuwa na furaha tele lakini tatizo moja ambalo lilimfanya kukosa raha katika maisha yake ni juu ya afya yake tu. Alijitahidi kuwaona wataalamu mbalimbali, hakukuwa na mtu aliyemtibu hivyo kubaki hivyohivyo.
Siku zikaendelea kukatika, miezi ikakatika, baada ya miezi sita ya ndoa, mkewe, Katty akaanza kulilia mtoto. Huo ulikuwa mtihani mkubwa kwake, kama kufanya mapenzi, walifanya, tena kwa nguvu zote, kwa nini mtoto hakupatikana?
Hali hiyo ikampa mawazo mazito Dylan, yeye alilijua tatizo lakini mkewe hakujua kitu chochote kile. Kazi yake kubwa kwa kipindi hicho ikawa ni kumfariji tu kwamba muda ukifika, Mungu atawapa mtoto, kwa kipindi hicho walitakiwa kuendelea kusubiri.
“Tatizo nini mume wangu?” aliuliza Katty.
“Hata mimi sijui mke wangu.”
“Kama vipi tukamuone daktari...” alishauri Katty.
“Unahisi tunaweza kuwa na tatizo?”
“Nahisi itakuwa hivyo...”
Hicho ndicho walichotakiwa kufanya hasa katika hali kama hiyo. Kesho yake walikuwa katika Hospitali ya Marie Stopes ambapo wakakutana na daktari wao, Fabian na kumueleza tatizo lao.
“Poleni sana, ila hali kama hiyo inawatokea watu wengi, ngoja niwafanyie vipimo,” alisema Dk. Fabian na hivyo kuanza kazi ya kuwafanyia vipimo.
Muda wote Dylan alikuwa na mawazo tele, moyo wake ulimuuma mno, hakuamini kama bilionea kama yeye ndiye aliyekuwa akipitia maisha hayo. Mbele yake aliiona aibu kubwa, kitendo cha kushindwa kumpa mimba mke wake kilimfanya kuona kwamba siku yoyote ile angeweza kugundulika kile alichokuwa akikifanya kitandani.
Baada ya daktari kuwafanyia vipimo na wiki moja iliyofuata, wakafuata matokeo ya vipimo vyao na kuonekana wote wapo vizuri, hapakuwa na mtu yeyote aliyekuwa na tatizo lolote lile.
“Unasema kweli daktari?”
“Ndiyo Dylan, hakuna mwenye tatizo kabisa,” alijibu Dk. Fabian,
Wakaondoka mahali hapo huku daktari akiwataka kufika hospitalini hapo mara kwa mara kwa ajili ya kupewa ushauri juu ya kitu walichotakiwa kufanya.
Hilo wala halikuwa tatizo, mara kwa mara walifika mahali hapo kama walivyokuwa wakiambiwa, pamoja na hali yote hiyo, matokeo hayakuweza kubadilika, hali ilikuwa ileile kwamba mimba haikupatikana.
“Sasa tatizo litakuwa nini?” aliuliza Katty.
“Hata mimi sifahamu! Au twende sehemu za maombezi..”
“Labda, inawezekana kuna tatizo.”
Wakawa watu wa kwenda kanisani, huko, wakafanyiwa maombezi lakini bado hali iliendelea kuwa vilevile. Waliishi maisha ya majonzi, muda mwingine Katty alikuwa mtu wa kulia tu.
Siku nyingine hakuwa akizungumza na mumewe, hasira zilimkaba kooni na muda mwingi alikuwa akimlaumu Mungu. Kazi yao kubwa ilikuwa ni kubadilisha hospitali, kote huko, matokeo yaliendelea kubaki vilevile lakini Dylan alifahamu nini lilikuwa tatizo.
“Hivi siku akinigundua, itakuwaje?” alijiuliza Dylan.
“Nafikiri itakuwa mwisho! Mungu wangu, nitaishi maisha haya mpaka lini? Ngoja nimuone daktari, nahisi kuna kitu natakiwa kufanya,” alisema Dylan.
Siku hiyo hakutaka kurudi nyumbani mapema, alichokifanya ni kupitia hospitalini ambapo huko akaonana na Dk. Fabian na kuanza kuzungumza naye. Hakutaka kumficha, alijiweka wazi kila kitu kilichokuwa kikiendelea katika maisha yake.
“Ooppss...” alishusha pumzi nzito daktari.
“Ndiyo hivyo! Ninahitaji msaada wako,” alisema Dylan.
“Unafikiri nitakusaidia vipi?”
“Nataka tufanye kitu kimoja...”
“Kipi hicho...”
“Tupandikize mbegu za kiume katika yai la mke wangu,” alisema Dylan.
“Mbegu zako?”
“Hapana! Za mtu mwingine...”
“Mmh!”
“Nini sasa?”
“Nahisi inaweza kuleta matatizo baadaye...”
“Matatizo gani?”
“Huyo mtu akitoa siri...!”
“Sitaki ajue hizo mbegu zinakwenda wapi, iwe siri, nitamlipa dola milioni moja,” alisema Dylan.
“Kweli?”
“Ndiyo! Haina jinsi, nataka kumuona mke wangu akiwa na furaha siku zote katika maisha yake,” alisema Dylan.
Hakuwa na jinsi, kitu pekee alichokihitaji kwa wakati huo ni kumuona mke wake akiwa na furaha. Alijua kwamba jambo alilotaka kulifanya lilikuwa na hatari lakini hakujali, alizihitaji hizo mbegu za kiume kwa gharama zozote zile.
Alichokifanya ni kumuachia jukumu hilo Dk. Fabian ambaye kazi yake kubwa ilikuwa ni kumtafuta mtu ambaye angeweza kuifanya kazi hiyo, mwanaume mwenye sura nzuri ili mtoto atakayezaliwa basi awe na sura nzuri.
Kazi hiyo ikaanza mara moja, alichokifanya Dk. Fabian ni kuwatafuta vijana ambao waliingia mtaani na kumpata Mike ambaye walizungumza naye na kumpeleka hospitali pasipo kumwambia kwamba lengo la yeye kuwa mahali hapo ni kwamba mbegu zake zilikuwa zikihitajika sana.
“Kwa hiyo ishu ni kutoa mbegu tu?” aliuliza Mike.
“Ndiyo! Utapata dola milioni moja...”
“Kweli?”
“Ndiyo!”
“Hakuna kingine?”
“Hakuna!”
Kwake, kwa umasikini aliokuwa nao wala halikuwa tatizo, lilikuwa jambo dogo sana. Kutoa mbegu hizo huku akiingiza dola milioni moja ambazo kwa fedha za Kitanzania ilikuwa ni zaidi ya bilioni mbili, ilikuwa ni bahati mno.
Alichoambiwa ni kuingia ndani ya chumba kimoja kilichokuwa na televisheni, akapewa chombo na kisha kuwashiwa televisheni hiyo na kuwekewa filamu ya utupu huku akitakiwa kujichua.
Akaanza kazi huku akiwa peke yake. Dakika tano nyingi, akafanikiwa kutoa mbegu zake ambazo zilichukuliwa na kuwekwa kwenye mashine maalumu na kutakiwa kuondoka mahali hapo huku akiambiwa kwamba kila kitu kilichoendelea, kiwe siri, asijue mtu yeyote yule. Akakubaliana nao. Ndani ya saa tatu, kiasi hicho cha fedha kaingizwa katika akaunti yake.
****
“Nimeanza kusikia kizunguzungu mpenzi,” alilalamika Katty, ilikuwa ni saa sita usiku.
“Kuna nini tena mpenzi wangu?” aliuliza Dylan huku akionekana kuwa na wasiwasi.
“Sijui! Tumbo linaniuma, nisaidie, tumbo linaniuma na nasikia kizunguzungu, nisaidie mume wangu,” alipiga kelele Katty.
Hakukuwa na kitu kingine cha kufanya zaidi ya kumchukua mkewe, Katty, akambeba na kumpeleka ndani ya gari lake na kuanza safari ya kuelekea katika Hospitali ya Marie Stoppes Medical Center.
Njiani, bado Katty alikuwa akilalamika kwa maumivu huku kile kizunguzungu kikiongezeka kadiri dakika zilivyokwenda mbele. Dylan alichanganyikiwa, aliendesha gari kwa kasi ya ajabu mpaka walipofika katika hospitali hiyo ambapo harakaharaka akawaita manesi ambao wakafika mahali hapo na kumpakiza kwenye machela na kuanza kuisukuma kuelekea nani.
Dylan alikuwa akifuatilia kwa nyuma, alionekana kuchanganyikiwa, hakujua tatizo lilikuwa nini mpaka mke wake kuwa kwenye tatizo kubwa namna ile. Machela ile ikaingizwa katika chumba kilichoandikwa Theatre kwa mlangoni na yeye kuambiwa kubaki mahali hapo.
“Nataka niende na mke wangu,” alisema Dylan.
“Hapana...unatakiwa kubaki hapa,” alisema nesi.
“Nesi...nesi, ninampenda mke wangu, ninataka kuwa karibu naye...” aliendelea kusema Dylan huku akionekana kuchanganyikiwa mno, ugonjwa wa ghafla wa mkewe ulimuweka katika hali mbaya mno.
Hakuruhusiwa kuingia ndani ya chumba hicho, alitakiwa kubaki mahali hapo huku manesi wale wakienda na Katty ndani ya chumba kile. Huku nje, Dylan alibaki akiwa ametulia, muda wote alionekana kuwa na mawazo. Manesi walipokuwa wakitoka nje, aliwang’ang’ania na kutaka kujua ni kitu gani kilikuwa kikiendelea.
“Kuna nini? Nini kimemtokea mke wangu?” aliuliza Dylan huku akionekana kuchanganyikiwa.
“Hakuna kitu, subiri, daktari atakwambia kila kitu,” alisema nesi.
“Atapona?”
“Utaambiwa, subiri hapo,” alisema nesi huyo, hakutaka kubaki mahali hapo kwa kuogopa maswali mengi, huyo akaondoka zake.
Dylan alibaki mahali hapo huku akiwa na mawazo tele, alijiinamia chini, alionekana kuwa na wasiwasi mno, wala haukupita muda mrefu, mlango ukafunguliwa na nesi mwingine kutoka, akasimama na kumdaka na kumuuliza maswali mengine lakini nesi huyo hakutaka kujibu swali lolote lile.
Baada ya dakika chache, Dk. Fabian akatokea mahali hapo huku akiwa kwenye mwendo wa kasi, Dylan alipoyainua macho yake, wakagonganisha macho na daktari huyo kumkonyeza, akaachia tabasamu kisha kuingia ndani ya chumba kile.
Huo ndiyo ulikuwa mpango waliotaka kufanya, Dylan hakutaka kukosea, alijua siku za hatari za mke wake kushika mimba hivyo alihakikisha siku hiyo anafanya kitu kimoja kikubwa.
Kwanza akamuwekea madawa ya usingizi ambayo yangemfanya kusikia maumivu ya tumbo kwa mbali na kuhisi kizunguzungu na mwisho wa siku kupoteza fahamu. Hilo ndilo lililofanyika, wakati amejisikia kizunguzungu, akapoteza fahamu ili Dk. Fabian afanye kazi yake ya kupandikiza mbegu za kiume katika mwili wa Katty.
Hilo lilifanyika kwa siri, ni Dk. Fabian na daktari mwenzake, Dk. Alexander ndiyo waliojua mchezo huo. Mara moja, tena kwa haraka sana kazi ikaanza kufanyika ndani ya chumba hicho.
Dylan alikaa nje ya chumba kile, alijiona kuwa na mafanikio makubwa, alimshukuru Mungu kwa kufanikisha mpango huo, kazi kubwa ilibaki kwa madaktari hao ambao walimuongezea nusu kaputi kitandani pale.
Baada ya saa moja, kila kitu kikawa tayari, madaktari hao wawili wakatoka, kitu cha kwanza baada ya kuonana na Dylan nje ya chumba hicho ni kuanza kumpongeza na kumwambia ainge ndani ya chumba kile.
“Tumefanikiwa...” alisema Dk. Fabian.
“Kweli?”
“Asilimia mia moja, tumefanikiwa!”
“Asante Mungu, siamini!”
“Amini sasa, imekuwa kazi nyepesi mno!”
Wakapongezena, baada ya saa mbili, Katty akarudiwa na fahamu, mtu wa kwanza kabisa kumuona ndani ya chumba hicho alikuwa mume wake. Japokuwa ilikuwa ni saa nane usiku lakini mwanaume huyo hakulala, alipomuona mkewe amefumbua macho, uso wake ukaonyesha tabasamu pana.
“Mume wangu! Nini kilitokea?” aliuliza Katty huku akimwangalia Dylan usoni.
“Sijui! Ila madaktari wamekupima wamegundua kwamba kizunguzungu kimesababishwa na akili yako kuchoka, umefanya kazi mfululizo,” alijibu Dylan bila kupepesa macho pembeni, alitaka kuaminika zaidi.
Hata madaktari walipoingia, majibu yao yalikuwa yaleyale kwamba alifanya kazi kwa kipindi kirefu hivyo alichoka sana hali iliyompelekea kusikia kizunguzungu.
Saa tisa usiku, akaruhusiwa na kurudi nyumbani.
Usiku wa siku hiyo, ulikuwa ni wa mahaba mazito, Dylan hakutaka kuichezea nafasi hiyo, akaanza kumpapasa mkewe kitandani na mwisho wa siku wakajikuta wakiwa kwenye dimbwi la mahaba na hatimaye kuanza kuvuana nguo, kilichofuatia ni sauti za mahaba huku Dylan akiwa makini sana katika kucheza na kifaa kile cha bandia.

Je nini kitaendelea?
Tukutane Junapili
Ila Katty nae anaonekana alikuwa anatulia sana aisee, yani akijilaza kajilaza anatulia tuliiiiii kama yule mrembo wa gwajiseeeee yani hana makeke wala mbwembwe... .. Ndomana hajaweza kulistukia dili la mkanda wa dude bandia la bwana Dylan..

All in all asante sana Madame S
 
Adhabu yote ya nini. Na huyo mke jamani ndio hashtuki. Hawezi kutofautisha ya plastic na original
 
NYEMO CHILONGANI.
UTAJIRI WENYE UCHUNGU.
0718069269.

Sehemu ya Ishirini

Kila mmoja alionekana mwenye furaha kubwa huko Bahamas, walitembea kila sehemu, kwa siku zote walizokuwa huko, Dylan alikuwa akifanya mapenzi na mkewe, Katty usiku tu.
Hakutaka kufanya mchana, alijifanya kuwa bize mchana na hata alipoguswa hapa na pale, alikuwa mkali, ila usiku, tena huku taa zikiwa zimezimwa, alifanya kwa nguvu zote kwa kutumia kiungo cha bandia ambacho alikifunga kama mkanda fulani hivi.
Baada ya kukaa kwa mwezi mzima ndani ya kisiwa hicho huku wakiponda raha, wakaamua kurudi nchini Marekani kuendelea na shughuli zao kama kawaida. Maisha yake yakabadilika, hayakuwa kama yalivyokuwa kipindi cha nyuma.
Japokuwa alikuwa na furaha tele lakini tatizo moja ambalo lilimfanya kukosa raha katika maisha yake ni juu ya afya yake tu. Alijitahidi kuwaona wataalamu mbalimbali, hakukuwa na mtu aliyemtibu hivyo kubaki hivyohivyo.
Siku zikaendelea kukatika, miezi ikakatika, baada ya miezi sita ya ndoa, mkewe, Katty akaanza kulilia mtoto. Huo ulikuwa mtihani mkubwa kwake, kama kufanya mapenzi, walifanya, tena kwa nguvu zote, kwa nini mtoto hakupatikana?
Hali hiyo ikampa mawazo mazito Dylan, yeye alilijua tatizo lakini mkewe hakujua kitu chochote kile. Kazi yake kubwa kwa kipindi hicho ikawa ni kumfariji tu kwamba muda ukifika, Mungu atawapa mtoto, kwa kipindi hicho walitakiwa kuendelea kusubiri.
“Tatizo nini mume wangu?” aliuliza Katty.
“Hata mimi sijui mke wangu.”
“Kama vipi tukamuone daktari...” alishauri Katty.
“Unahisi tunaweza kuwa na tatizo?”
“Nahisi itakuwa hivyo...”
Hicho ndicho walichotakiwa kufanya hasa katika hali kama hiyo. Kesho yake walikuwa katika Hospitali ya Marie Stopes ambapo wakakutana na daktari wao, Fabian na kumueleza tatizo lao.
“Poleni sana, ila hali kama hiyo inawatokea watu wengi, ngoja niwafanyie vipimo,” alisema Dk. Fabian na hivyo kuanza kazi ya kuwafanyia vipimo.
Muda wote Dylan alikuwa na mawazo tele, moyo wake ulimuuma mno, hakuamini kama bilionea kama yeye ndiye aliyekuwa akipitia maisha hayo. Mbele yake aliiona aibu kubwa, kitendo cha kushindwa kumpa mimba mke wake kilimfanya kuona kwamba siku yoyote ile angeweza kugundulika kile alichokuwa akikifanya kitandani.
Baada ya daktari kuwafanyia vipimo na wiki moja iliyofuata, wakafuata matokeo ya vipimo vyao na kuonekana wote wapo vizuri, hapakuwa na mtu yeyote aliyekuwa na tatizo lolote lile.
“Unasema kweli daktari?”
“Ndiyo Dylan, hakuna mwenye tatizo kabisa,” alijibu Dk. Fabian,
Wakaondoka mahali hapo huku daktari akiwataka kufika hospitalini hapo mara kwa mara kwa ajili ya kupewa ushauri juu ya kitu walichotakiwa kufanya.
Hilo wala halikuwa tatizo, mara kwa mara walifika mahali hapo kama walivyokuwa wakiambiwa, pamoja na hali yote hiyo, matokeo hayakuweza kubadilika, hali ilikuwa ileile kwamba mimba haikupatikana.
“Sasa tatizo litakuwa nini?” aliuliza Katty.
“Hata mimi sifahamu! Au twende sehemu za maombezi..”
“Labda, inawezekana kuna tatizo.”
Wakawa watu wa kwenda kanisani, huko, wakafanyiwa maombezi lakini bado hali iliendelea kuwa vilevile. Waliishi maisha ya majonzi, muda mwingine Katty alikuwa mtu wa kulia tu.
Siku nyingine hakuwa akizungumza na mumewe, hasira zilimkaba kooni na muda mwingi alikuwa akimlaumu Mungu. Kazi yao kubwa ilikuwa ni kubadilisha hospitali, kote huko, matokeo yaliendelea kubaki vilevile lakini Dylan alifahamu nini lilikuwa tatizo.
“Hivi siku akinigundua, itakuwaje?” alijiuliza Dylan.
“Nafikiri itakuwa mwisho! Mungu wangu, nitaishi maisha haya mpaka lini? Ngoja nimuone daktari, nahisi kuna kitu natakiwa kufanya,” alisema Dylan.
Siku hiyo hakutaka kurudi nyumbani mapema, alichokifanya ni kupitia hospitalini ambapo huko akaonana na Dk. Fabian na kuanza kuzungumza naye. Hakutaka kumficha, alijiweka wazi kila kitu kilichokuwa kikiendelea katika maisha yake.
“Ooppss...” alishusha pumzi nzito daktari.
“Ndiyo hivyo! Ninahitaji msaada wako,” alisema Dylan.
“Unafikiri nitakusaidia vipi?”
“Nataka tufanye kitu kimoja...”
“Kipi hicho...”
“Tupandikize mbegu za kiume katika yai la mke wangu,” alisema Dylan.
“Mbegu zako?”
“Hapana! Za mtu mwingine...”
“Mmh!”
“Nini sasa?”
“Nahisi inaweza kuleta matatizo baadaye...”
“Matatizo gani?”
“Huyo mtu akitoa siri...!”
“Sitaki ajue hizo mbegu zinakwenda wapi, iwe siri, nitamlipa dola milioni moja,” alisema Dylan.
“Kweli?”
“Ndiyo! Haina jinsi, nataka kumuona mke wangu akiwa na furaha siku zote katika maisha yake,” alisema Dylan.
Hakuwa na jinsi, kitu pekee alichokihitaji kwa wakati huo ni kumuona mke wake akiwa na furaha. Alijua kwamba jambo alilotaka kulifanya lilikuwa na hatari lakini hakujali, alizihitaji hizo mbegu za kiume kwa gharama zozote zile.
Alichokifanya ni kumuachia jukumu hilo Dk. Fabian ambaye kazi yake kubwa ilikuwa ni kumtafuta mtu ambaye angeweza kuifanya kazi hiyo, mwanaume mwenye sura nzuri ili mtoto atakayezaliwa basi awe na sura nzuri.
Kazi hiyo ikaanza mara moja, alichokifanya Dk. Fabian ni kuwatafuta vijana ambao waliingia mtaani na kumpata Mike ambaye walizungumza naye na kumpeleka hospitali pasipo kumwambia kwamba lengo la yeye kuwa mahali hapo ni kwamba mbegu zake zilikuwa zikihitajika sana.
“Kwa hiyo ishu ni kutoa mbegu tu?” aliuliza Mike.
“Ndiyo! Utapata dola milioni moja...”
“Kweli?”
“Ndiyo!”
“Hakuna kingine?”
“Hakuna!”
Kwake, kwa umasikini aliokuwa nao wala halikuwa tatizo, lilikuwa jambo dogo sana. Kutoa mbegu hizo huku akiingiza dola milioni moja ambazo kwa fedha za Kitanzania ilikuwa ni zaidi ya bilioni mbili, ilikuwa ni bahati mno.
Alichoambiwa ni kuingia ndani ya chumba kimoja kilichokuwa na televisheni, akapewa chombo na kisha kuwashiwa televisheni hiyo na kuwekewa filamu ya utupu huku akitakiwa kujichua.
Akaanza kazi huku akiwa peke yake. Dakika tano nyingi, akafanikiwa kutoa mbegu zake ambazo zilichukuliwa na kuwekwa kwenye mashine maalumu na kutakiwa kuondoka mahali hapo huku akiambiwa kwamba kila kitu kilichoendelea, kiwe siri, asijue mtu yeyote yule. Akakubaliana nao. Ndani ya saa tatu, kiasi hicho cha fedha kaingizwa katika akaunti yake.
****
“Nimeanza kusikia kizunguzungu mpenzi,” alilalamika Katty, ilikuwa ni saa sita usiku.
“Kuna nini tena mpenzi wangu?” aliuliza Dylan huku akionekana kuwa na wasiwasi.
“Sijui! Tumbo linaniuma, nisaidie, tumbo linaniuma na nasikia kizunguzungu, nisaidie mume wangu,” alipiga kelele Katty.
Hakukuwa na kitu kingine cha kufanya zaidi ya kumchukua mkewe, Katty, akambeba na kumpeleka ndani ya gari lake na kuanza safari ya kuelekea katika Hospitali ya Marie Stoppes Medical Center.
Njiani, bado Katty alikuwa akilalamika kwa maumivu huku kile kizunguzungu kikiongezeka kadiri dakika zilivyokwenda mbele. Dylan alichanganyikiwa, aliendesha gari kwa kasi ya ajabu mpaka walipofika katika hospitali hiyo ambapo harakaharaka akawaita manesi ambao wakafika mahali hapo na kumpakiza kwenye machela na kuanza kuisukuma kuelekea nani.
Dylan alikuwa akifuatilia kwa nyuma, alionekana kuchanganyikiwa, hakujua tatizo lilikuwa nini mpaka mke wake kuwa kwenye tatizo kubwa namna ile. Machela ile ikaingizwa katika chumba kilichoandikwa Theatre kwa mlangoni na yeye kuambiwa kubaki mahali hapo.
“Nataka niende na mke wangu,” alisema Dylan.
“Hapana...unatakiwa kubaki hapa,” alisema nesi.
“Nesi...nesi, ninampenda mke wangu, ninataka kuwa karibu naye...” aliendelea kusema Dylan huku akionekana kuchanganyikiwa mno, ugonjwa wa ghafla wa mkewe ulimuweka katika hali mbaya mno.
Hakuruhusiwa kuingia ndani ya chumba hicho, alitakiwa kubaki mahali hapo huku manesi wale wakienda na Katty ndani ya chumba kile. Huku nje, Dylan alibaki akiwa ametulia, muda wote alionekana kuwa na mawazo. Manesi walipokuwa wakitoka nje, aliwang’ang’ania na kutaka kujua ni kitu gani kilikuwa kikiendelea.
“Kuna nini? Nini kimemtokea mke wangu?” aliuliza Dylan huku akionekana kuchanganyikiwa.
“Hakuna kitu, subiri, daktari atakwambia kila kitu,” alisema nesi.
“Atapona?”
“Utaambiwa, subiri hapo,” alisema nesi huyo, hakutaka kubaki mahali hapo kwa kuogopa maswali mengi, huyo akaondoka zake.
Dylan alibaki mahali hapo huku akiwa na mawazo tele, alijiinamia chini, alionekana kuwa na wasiwasi mno, wala haukupita muda mrefu, mlango ukafunguliwa na nesi mwingine kutoka, akasimama na kumdaka na kumuuliza maswali mengine lakini nesi huyo hakutaka kujibu swali lolote lile.
Baada ya dakika chache, Dk. Fabian akatokea mahali hapo huku akiwa kwenye mwendo wa kasi, Dylan alipoyainua macho yake, wakagonganisha macho na daktari huyo kumkonyeza, akaachia tabasamu kisha kuingia ndani ya chumba kile.
Huo ndiyo ulikuwa mpango waliotaka kufanya, Dylan hakutaka kukosea, alijua siku za hatari za mke wake kushika mimba hivyo alihakikisha siku hiyo anafanya kitu kimoja kikubwa.
Kwanza akamuwekea madawa ya usingizi ambayo yangemfanya kusikia maumivu ya tumbo kwa mbali na kuhisi kizunguzungu na mwisho wa siku kupoteza fahamu. Hilo ndilo lililofanyika, wakati amejisikia kizunguzungu, akapoteza fahamu ili Dk. Fabian afanye kazi yake ya kupandikiza mbegu za kiume katika mwili wa Katty.
Hilo lilifanyika kwa siri, ni Dk. Fabian na daktari mwenzake, Dk. Alexander ndiyo waliojua mchezo huo. Mara moja, tena kwa haraka sana kazi ikaanza kufanyika ndani ya chumba hicho.
Dylan alikaa nje ya chumba kile, alijiona kuwa na mafanikio makubwa, alimshukuru Mungu kwa kufanikisha mpango huo, kazi kubwa ilibaki kwa madaktari hao ambao walimuongezea nusu kaputi kitandani pale.
Baada ya saa moja, kila kitu kikawa tayari, madaktari hao wawili wakatoka, kitu cha kwanza baada ya kuonana na Dylan nje ya chumba hicho ni kuanza kumpongeza na kumwambia ainge ndani ya chumba kile.
“Tumefanikiwa...” alisema Dk. Fabian.
“Kweli?”
“Asilimia mia moja, tumefanikiwa!”
“Asante Mungu, siamini!”
“Amini sasa, imekuwa kazi nyepesi mno!”
Wakapongezena, baada ya saa mbili, Katty akarudiwa na fahamu, mtu wa kwanza kabisa kumuona ndani ya chumba hicho alikuwa mume wake. Japokuwa ilikuwa ni saa nane usiku lakini mwanaume huyo hakulala, alipomuona mkewe amefumbua macho, uso wake ukaonyesha tabasamu pana.
“Mume wangu! Nini kilitokea?” aliuliza Katty huku akimwangalia Dylan usoni.
“Sijui! Ila madaktari wamekupima wamegundua kwamba kizunguzungu kimesababishwa na akili yako kuchoka, umefanya kazi mfululizo,” alijibu Dylan bila kupepesa macho pembeni, alitaka kuaminika zaidi.
Hata madaktari walipoingia, majibu yao yalikuwa yaleyale kwamba alifanya kazi kwa kipindi kirefu hivyo alichoka sana hali iliyompelekea kusikia kizunguzungu.
Saa tisa usiku, akaruhusiwa na kurudi nyumbani.
Usiku wa siku hiyo, ulikuwa ni wa mahaba mazito, Dylan hakutaka kuichezea nafasi hiyo, akaanza kumpapasa mkewe kitandani na mwisho wa siku wakajikuta wakiwa kwenye dimbwi la mahaba na hatimaye kuanza kuvuana nguo, kilichofuatia ni sauti za mahaba huku Dylan akiwa makini sana katika kucheza na kifaa kile cha bandia.

Je nini kitaendelea?
Tukutane Junapili
Dear kule kwa Wapemba umetugaya nitumie PM bas
 
NYEMO CHILONGANI
UTAJIRI WENYE UCHUNGU
0718069269

Sehemu ya Ishirini na Moja.

Dalili ya kwanza kabisa aliyoisikia baada ya wiki mbili ni kutapika, alijisikia uchovu mwingi, hakujua tatizo lilikuwa nini. Alichanganyikiwa, alihisi kwamba alikuwa akiumwa ugonjwa fulani wa hatari.
Kizunguzungu kikampata, muda mwingi akawa mtu wa kulala tu. Hakutaka kumsubiri mume wake, hapohapo akampigia simu na kumwambia alivyokuwa akijisikia.
“Mpigie simu daktari aje..” alisema Dylan.
Hicho ndicho alichokifanya, akachukua simu na kumpigia daktari wa familia na kumwambia kilichokuwa kikiendelea, Ndani ya dakika kadhaa, daktari huo akafika nyumbani hapo na kumfanyia vipimo.
Katty alikuwa pembeni, alikuwa akisubiri majibu, alitaka kujua tatizo lilikuwa nini. Moyo wake ulichanganyikiwa, alikumbuka vilivyo kwamba wiki mbili zilizopita alipata tatizo kama hilo, akahisi mwili wake ulikuwa na matatizo makubwa, hivyo alichokifikiria ni kwenda kuuchunguza mwili mzima.
“Kuna tatizo gani dokta?” aliuliza Katty.
“Siamini macho yangu!”
“Kuna nini?”
“Hebu njoo uone...” alisema daktari, Katty akasogea na kuanza kuangalia. Akamuonyeshea matokeo.
“Sielewi chochote, ndiyo nini?”
“Una mimba...”
“Unasemaje?” Katty aliuliza huku akionyesha mshtuko wa waziwazi.
“Una mimba, ndivyo kipimo kinavyonionyesha,” alisema daktari yule.
Katty akachanganyikiwa kwa furaha, hakuamini kile alichokisikia, hapohapo akajikuta akisimama na kumkumbatia daktari kwa furaha. Alibaki akipiga kelele kama chizi ndani ya nyumba hiyo, alikimbia huku na kule, alipagawa, akashindwa hata kumtaarifu mumewe.
“Asante Mungu! Asante Mungu!” alisema Katty, hapo ndipo akakumbuka kumpigia simu mume wake, akachukua simu yake na kumpigia.
“Mpenzi...” aliita mara baada ya simu kupokelewa.
“Kuna nini? Si unaumwa? Mbona unaonekana una furaha!”
“Nimemuita daktari..”
“Ikawaje?”
“Huwezi kuamini!”
“Kuna nini? Mbona unaniweka roho juu?”
“Nina mimba...nina mimba mume wangu...”
Dylan hakutaka kuzungumza suala hilo kwenye simu, alichokifanya ni kukata kisha kutoka ofisini mwake. Yeye mwenyewe alichanganyikiwa, hakuamini kama kile kitu alichokifanya yeye na madaktari kingeweza kufanikiwa kwa kiasi hicho.
Akaingia ndani ya gari, alikuwa na furaha tele na siku hiyo aliendesha gari kwa tahadhali kubwa, aliogopa kupata ajali na kufa pasipo kumuona mkewe akiwa mjauzito.
Alipofika nje ya nyumba yake, hata kabla geti halijafunguliwa, tayari aliteremka na kuingia kwa kutumia geti dogo. Mlinzi alibaki akimshangaa, hakujua bosi wake alikuwa na nini. Moja kwa moja akaingia ndani ambapo bado alimkuta mke wake akiwa na furaha na kuwapigia simu marafiki zake.
“Mke wangu...” aliita Dylan.
“Mume wangu! Nina mimba..” alisema Katty, hapohapo akamsogelea mumewe na kumkumbatia kwa furaha.
“Siamini! Dokta! Kweli mke wangu ana mimba?” aliuliza Dylan huku akimwangalia daktari ambaye bado alikuwa mahali hapo.
“Ndiyo! Mkeo ana mimba, nimempima.”
“Una uhakika?”
“Asilimia mia moja!”
Jibu hilo tu lilitosha kumfanya Dylan kumng’ang’ania mke wake kwa nguvu, hakutaka kumuachia mikononi mwake. Hatimaye alifanikiwa kile alichokuwa amekipanga.
*****
Mike alijiona kuwa bilionea mkubwa, hakuamini kama kitendo chake cha kutoa mbegu kwa ajili ya mtu asiyemfahamu kingemfanya kuwa tajiri kiasi hicho. Muda wote alikuwa mtu mwenye furaha, katika maisha yake yote aliishi maisha ya kimasikini mno, hakuamini kama muda huo naye alikuwa miongoni mwa watu waliokuwa na fedha.
Kichwa chake kilikuwa na akili kubwa, alijua kwamba hakuwa na fedha kabla na alimuomba sana Mungu apate fedha, na kweli katika kipindi hicho alipata kiasi kikubwa cha fedha hivyo jambo la kwanza kabisa alilolifikiria ni kuanzisha biashara.
Biashara ambayo ilikuja kichwani mwake ni kuwa mfanyabishara wa mafuta. Hakukuwa na kazi nyingine ambayo aliiona kuwa na faida kubwa na ambayo ilifanywa na watu wenye kiu ya kutaka kupata mafanikio kama hiyo.
Kitu cha kwanza alichokifanya ni kuonana na Bwana Peters Brown aliyekuwa mkurugenzi wa kampuni ya mafuta ya Oilcom na kuanza kuzungumza naye. Mazungumzo hayo yalichukua saa moja, lengo kubwa la mazungumzo hayo na mzee huyo ni kumwambia kwamba naye alitaka kuweka hisa katika kampuni hiyo, hata kama angepata kiasi kidogo cha fedha, kwake ingemsaidia.
“Kiasi gani?” aliuliza Bwana Peters.
“Nataka niweke dola laki tano...” alisema.
“Una uhakika utapata faida?”
“Kwa nini isiwezekane?”
“Ngoja nikwambie kitu kimoja!”
“Kitu gani?”
“Hii kampuni inakaribia kufilisika....”
“Unasemaje?”
“Ndiyo hivyo! Kama kweli unajiona unaweza kufanya biashara hii tena ukapata faida, basi nikuuzie kabisa,” alisema mzee huyo.
“Kiasi gani?”
“Dola milioni tano!”
“Mbona nyingi hivyo na wakati biashara yenyewe inakaribia kufilisika?” aliuliza Mike huku akionekana kushangaa.
“Ni kwa sababu ina faida.”
“Kama ina faida, kwa nini unataka kuachana nayo?”
“Ni mambo mengi sana, kubwa ni kwamba nataka nianzishe biashara nyingine, hii ya kusafirisafiri kwenda Uarabuni, nimechoka,” alisema mzee Peters.
Walizungumza mambo mengi kuhusu biashara hiyo. Kwa Mike, aliona kwamba ilikuwa biashara nzuri ambayo kama angeamua kuifanya basi ingekuwa na faida kubwa. Alichokifanya ni kuzungumza na mzee huyo na kumwambia kwamba lingekuwa jambo zuri kama angemuuzia kwa kumpa kiasi kidogo cha fedha na baadaye kummalizia.
“Hakuna tatizo....kikubwa uaminifu..”
Hapo ndipo alipoanza kufanya biashara hiyo ya mafuta, ilikuwa ni biashara ngumu kwa kipindi cha kwanza lakini Mike hakutaka kukata tamaa. Alisafiri huku na kule, alitafuta masoko na hatimaye ile kampuni ya Oilcom ambayo ilikuwa ikielekea kufilisika ikaanza kusimama.
Hakutaka kulegea, kila siku ilikuwa ni lazima kuwalazimisha wafanyakazi wake kufanya kazi kubwa usiku na mchana huku akipunguza gharama za uuzaji wa mafuta hayo kitu kilichomfanya kufanikiwa kwa haraka mno.
Alichukiwa na wauzaji wengine wa mafuta lakini hakujali, alichokuwa akikiangalia ni kupata fedha ya haraka kwani bado alikuwa na deni kubwa kutoka kwa Bwana Peters.
Mwaka wa kwanza ukakatika, wa pili ukaingia na hatimaye akafanikiwa kulipa deni lililobaki na hivyo kuanza kuingiza fedha katika akaunti yake. Biashara ilichanganya, akaingiza kiasi kikubwa cha fedha, hakuwa mtumiaji, alijua kwamba ili uwe na utajiri mkubwa ilikuwa ni lazima uwe na nidhamu ya fedha katika matumizi, na hicho ndicho alichokifanya.
Alianza chini kabisa lakini kadiri siku zilivyozidi kwenda mbele na ndivyo alivyozidi kufanikiwa zaidi. Hakulala usiku kucha, kila siku ilikuwa ni kufuatilia mauzo, yalikwendaje, wapi yaliishia na kwa namna gani alitakiwa kuyaendelea kutoka pale yalipogotea.
Baada ya kupita miezi sita, ndipo alipoamua kuangalia akaunti yake ilikuwa na kiasi gani kwani kwa kipindi kirefu hakuwa amefanya hivyo. Alipoangalia, hakuamini macho yake, kulikuwa na zaidi ya dola bilioni mbili, hakuamini, akapiga magoti chini na kumshukuru Mungu kwa kile alichokiona.
“Na mimi ni bilionea?” alijiuliza huku akionekana kushangaa.
Huo ulikuwa mwanzo, mwanzo wa kujinyima mpaka kufikia malengo yake. Hakuishia hapo, aliendelea kupambana kila siku, alitamani kuingiza kiasi kikubwa cha fedha zaidi na zaidi.
Mara kwa mara alikuwa mtu wa kwenda katika nchi za Kiarabu, huko, alikutana na wafanyabiashara wenzake na kuzungumza mengi kuhusu biashara hiyo. Alijiona kuwa mtu mwenye bahati kubwa, wakati mwingine, hakuamini kama kile kilichokuwa kikitokea kilitokea katika maisha hayahaya na si ndoto.
“Umependeza...” alisema msichana mmoja, alikuwa Mwarabu mwenye sura nzuri, alikuwa akimwambia Mike.
“Asante sana...”
“Umetoka wapi?”
“Marekani!”
“Karibu sana, naitwa Aisha, ni mwenyeji wa hapa Kuwait...” alisema msichana huyo huku akimpa mkono Mike.
Kipindi hicho alikuwa nchini Kuwait, alikwenda huko kwa kuwa kulikuwa na mazungumzo mazito kuhusu biashara ya mafuta aliyokuwa akifanya na Waarabu nchini humo.
Hakutaka kumtuma mwakilishi wake, kwa kuwa ulikuwa ni mkutano mkubwa alitaka kwenda yeye mwenyewe. Huku wakiwa katika mkutano huo ndipo alipokutana na msichana huyo aliyejitambulisha kwa jina la Aisha.
Alikuwa mzuri wa sura, alivalia nguo ya heshima na kichwani alivalia hijabu ya bluu, machoni alivalia miwani, kila alipotembea, alitembea kwa madaha na kuwaacha wanaume wengine mdomo wazi.
Huyo alikuwa mtoto wa mfalme wa Kuwait Sabah Al-Ahmad, alikuwa msichana mrembo mno ambaye alipendwa na wanaume wengi huko Kuwait. Japokuwa baba yake ndiye alikuwa kiongozi wa nchi hiyo lakini hakutaka kuishi kama mtoto wa mfalme bali alitaka kuishi kama mtu wa kawaida tu.
Alikuwa mfanyakazi katika Kampuni ya Mafuta ya Al Jazeebablon iliyokuwa ikifanya kazi ya kusambaza mafuta katika nchi mbalimbali duniani. Katika maisha yake yote mpaka kipindi hicho, Aisha hakuwahi kumjua mwanaume kwani muda mwingi alikuwa msichana wa kuchungwa, alipokwenda, alichungwa, hakutakiwa kusogeleana na mwanaume yeyote yule.
“Ila hata wewe umependeza....”
“Kweli?”
“Ndiyo! Hongera sana! Halafu sasa....”
“Halafu nini?” aliuliza Aisha huku akiachia tabasamu pana lililomvuruga kabisa Mike. Akameza mate.
“Au basi...”
“Hapana! Niambie, halafu nini?” aliuliza msichana huyo. Tayari hali ya Mike ikabadilika. Mwili ukaanza kumsisimka kupita kawaida. Watu wote waliokuwa mahali hapo, wakabaki wakiwaangalia wawili hao, nao wakajisahau kabisa kama walikuwa katika meza ndefu, kikaoni, tena kulikuwa na watu zaidi ya ishirini.
Wakabaki wakiangaliana tu.

Je, nini kitaendelea?
Tukutane Ijumaa hapa.
 
NYEMO CHILONGANI.
UTAJIRI WENYE UCHUNGU.

Sehemu ya Kumi na Nne.

Nyumbani hawakutulia, kila wakati Catherine alikuwa akipiga simu kwa baba yake kujua walifikia wapi, kama Dylan alikubali au alikataa. Moyo wake haukuwa na amani hata kidogo, hakutulia, alijifikiria kuhusu mvulana huyo, alimpenda mpaka hatua ya mwisho kabisa ambapo akipenda zaidi ya hapo angechanganyikiwa na kuwa kichaa.
Saa zikaendelea kukatika, kila alipomuuliza baba yake waliishia wapi, alimwambia asubiri kwani bado kulikuwa na vitu vichache vya kufanya. Catherine akatulia, akajipa moyo kwamba iwe isiwe ilikuwa ni lazima baba yake akamilishe kile kitu, hivyo akatulia.
Siku hiyo ilipokatika, Bwana James akawapigia simu na kuwaambia kwamba ni lazima waondoke waelekee nchini China kwani kulikuwa na kitu hakikukaa sawa. Hilo liliwachanganya Catherine na mama yake, hawakuelewa ni kitu gani kilichokuwa kikiendelea kwani hata safari hiyo ilikuwa ya ghafla sana.
“Kuna nini?” aliuliza bi Claire.
“Kuna kitu mke wangu!”
“Ni salama lakini?”
“Ndiyo! Wala msijali...”
“Na huyo kijana amesemaje? Atamuoa?”
“Hilo ndilo tunalizungumzia, ila kama tukifanikisha kukifuata kile tunachokifuata nchini China, atamuoa tu,” alisikika Bwana James.
“Kitu gani hicho?”
“Usiwe na hofu mke wangu! Nitakujulisha tu,” alisema Bwana James na kukata simu.
Kitendo cha kuambiwa na mume wake kwamba kulikuwa na kitu ambacho hakutakiwa kukifahamu, kilimfanya kuwa na wasiwasi mkubwa, akakosa amani kwa kuona kwamba kulikuwa na kitu kibaya ambacho mumewe hakutaka akifahamu. Hilo hakujali, hakumwambia binti yake, akabaki nalo moyoni na siku kuendelea mbele.
Upande wa pili, tayari mzee huyo wa dawa za mitishamba akaanza kufanya mambo yake, alihakikisha anamchunguza kwa umakini kujua tatizo lilikuwa nini kwani hakutakiwa kufanya kazi hiyo pasipo kujua historia fupi ya mgonjwa.
“Mtoto wako alianza lini hili tatizo?” aliuliza mzee huyo kupitia mkalimani, tena mbele ya Dylan mwenyewe.
“Alizaliwa nalo.”
“Na ilikuwaje katika kipindi chake cha utotoni? Nataka nipate historia kidogo kutoka kwako mzazi,” alisema mzee yule.
“Huyu si mtoto wangu, ni rafiki yangu!”
“Siyo mtoto wako?”
“Ndiyo!”
“Mmh! Mbona mmefanana hivyo?”
“Hutokea tu, ila ni rafiki yangu!”
Si mzee yule aliyeshangaa bali hata mkalimani naye akapigwa na mshangao. Kila alipowaangalia watu hao, walionekana kuwa kama mapacha, walifanana kwa asilimia kubwa sasa kitendo cha kuambiwa kwamba watu hao hawakuwa ndugu, kiliwashangaza wote.
“Basi ni lazima mama yake au baba aje hapa, ninataka kujua historia yake kwanza juu ya afya yake,” alisema mzee huyo.
“Hakuna tatizo! Atafika ndani ya siku mbili!”
Hilo wala halikuwa tatizo, walichokifanya ni kuwasiliana na bi Leticia na kumhitaji nchini China. Bwana James ndiye alisimamia kila kitu, akawasiliana na watu wake nchini Marekani na kuwaambia kile alichokitaka.
Kutafuta hati ya kusafiria wala halikuwa tatizo kwani kila mtu alimfahamu na aliheshimika sana. Baada ya siku mbili, Bi Leticia alikuwa ndani ya ndege akielekea nchini China.
Yeye mwenyewe hakuelewa ni kitu gani kilichokuwa kikiendelea, aliposikia kwamba anahitajika na mzee huyo bilionea, moyo wake ukawa na wasiwasi mno kwa kuhisi inawezekana kulikuwa na kitu kibaya kilichokuwa kimetokea ambacho kilimtia hatihani kijana wake.
Baada ya zaidi ya saa ishirini, alikuwa akiingia katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Beijing ambapo akateremka na kupokelewa na watu ambao waliandaliwa na kumchukua na kumpeleka ndani ya gari moja na safari ya kuelekea kijijini kuanza.
Walichukua saa nne ndipo wakaingia ndani ya kijiji hicho. Wakapokelewa vizuri na kupelekwa ndani ambapo Bi Leticia akakutana na kijana wake, kitu cha kwanza kabisa kilikuwa ni kumkumbatia.
“Umefanya nini Dylan mtoto wangu?” aliuliza Bi Leticia huku akimwangalia Dylan usoni, machozi yalikuwa yakimbubujika.
“Sijafanya kitu mama!”
“Sasa kwa nini upo huku?”
“Huyu mzee anataka kushughulikia tatizo langu,” alijibu Dylan.
Miongoni mwa watu walioshtuka, hata Bi Leticia naye alishtuka, alipomuona Bwana James, jinsi alivyofanana na kijana wake alibaki akishangaa. Kipindi cha nyuma aliwasikia baadhi ya vijana wakisema kwamba kijana wake alifanana sana na bilionea huyo, alibisha lakini siku hiyo ndipo akakutana naye, walifanana kwa kiasi kubwa sana na ilikuwa rahisi kusema kwamba ni mapacha.
Hapohapo mzee wa tiba akawaita, wote watatu wakaingia ndani ya chumba kimoja ambapo huko akamtaka Bi Leticia kusimulia historia fupi kuhusu Dylan na jinsi hali ilivyokuwa ikiendelea katika ukuaji wake.
“Wewe kama mzazi utakuwa unafahamu vingi, tatizo lake uliligundua kipindi gani?” aliuliza mzee huyo.
“Kipindi fulani, alipokuwa na miaka kumi na nne...” alijibu.
“Ulimzaa huyu mtoto akiwa mzima wa afya?”
“Hapana!”
“Unamaanisha alikuwa akiumwa? Alikuwa akiumwa nini?” aliuliza mzee huyo, Dylan na Bwana James walikuwa kimya wakimsikiliza.
“Sikumzaa mimi!” alisema bi Leticia huku akiangalia chini, alijisikia uchungu sana kuzungumza maneno hayo kwani katika maisha yake yote mpaka kipindi hicho, Dylana aliamini kwamba huyo alikuwa mama yake wa kumzaa.
“Hukumzaa wewe?”
“Ndiyo!”
“Kwa hiyo wewe si mama yake?”
“Ndiyo!”
Mapigo ya moyo wa Dylan yalikuwa juu, hakuamini kile alichokisikia kutoka kwa mwanamke huyo kwamba hakuwa mama yake. Katika kipindi chote cha maisha yake alifahamu kwamba huyo alikuwa mama yake, sasa ilikuwaje tena aseme kwamba yeye hakuwa mama yake, na kama yeye si mama yake, mama yake alikuwa nani na kwa nini alimficha kwa kipindi chote hicho.
“Naomba unisamehe Dylan, sikutaka ulijue hili,” alisema bi Leticia huku akianza kububujikwa na machozi.
“Sijaelewa mama...”
“Sikukuzaa....”
“Hukunizaa?”
“Ndiyo! Mimi si mama yako!”
“Wewe si mama yangu?” aliuliza Dylan.
Bi Leticia hakujibu swali hilo, tayari machozi yaliongezeka na kuanza kulia kilio cha kwikwi, hakukuwa na mtu aliyechanganyikiwa kama Dylan, kila alipomwangalia mwanamke huyo na maneno aliyokuwa akiyasema, hakuamini, wakati mwingine aliona kama anadanganywa.
Huo ulikuwa ni wakati wa Dylan kufahamu ukweli juu ya kile kilichokuwa kimetokea, Bi Leticia hakutaka kuficha, akaanza kuwahadithia kuanza siku ya kwanza walipokuwa kanisani, tsunami ilipopiga, ilipoliharibu Jiji la New Orleans kwa kujaa maji mpaka baadaye kumuokota mtoto Dylan akiwa kwenye friji.
Alipofikia hapo tu, Bwana James akapigwa na butwaa, akasimama kutoka alipokuwa, akamwangalia Dylan mara mbilimbili, hakuamini kabisa kile alichokisikia. Kila mtu aliyekuwa mahali hapo alibaki akimwangalia mzee huyo ambaye alionyesha wazi kwamba alichanganyikiwa kwa furaha.
“Dylan ni mtoto wangu!” alisema Bwana James huku akionekana kutokuamini.
Kila mtu akabaki akimwangalia mzee huyo, bado hawakufahamu ni kitu gani kilimtokea mpaka kupagawa kiasi hicho. Bwana James akainama na kumshika Dylan, hapohapo akamkumbatia, akamng’ang’ania kama mtu ambaye hakutaka kutoka mikononi mwake.
Si Bi Leticia aliyeshangaa, kila mtu aliyekuwa ndani ya chumba hicho alishangaa mpaka mkalimani mwenyewe. Bwana James alikuwa akibubujikwa na machozi, hakuamini kama kuna siku angekutana na mtu huyo, mtoto wake ambaye alimuhifadhi ndani ya friji na hatimaye mpenzi wake, Catherine kufariki miaka mingi iliyopita.

Je, nini kitaendelea?
Hii part ni very emotional yani nimesisimka
 
UTAJIRI WENYE UCHUNGU
0718069269

Sehemu ya Ishirini na Mbili.

Muda wote Dylan na mkewe walionekana kuwa na furaha tele, hawakuamini kilichokuwa kikiendelea kwamba mwanamke huyo alishika ujauzito ambao kadiri siku zilivyokuwa zikizidi kwenda mbele, tumbo lake likaanza kuonekana.,

Dylan hakuamini kama mwisho wa kila kitu, mkewe angepata ujauzito na hivyo yeye kuitwa mwanaume kamili kama ilivyokuwa wengine. Kila alipopita, mikono yake aliitanua, ofisini kwake, kila wakati alikuwa akiwaambia wafanyakazi wenzake ni jinsi gani alikuwa na furaha na jinsi alivyohangaika kumfanya mke wake kushika ujauzito huo.

Hakumfikiria mwanaume ambaye alizitoa mbegu zake kwa ajili ya mke wake, alichokifikiria kwa wakati huo ni mkewe tu, tena kwa kujitapa kwamba watoto walikuwa wake.

Kwa Katty, muda wote alikuwa na furaha hakutaka kutoka nyumbani kwake, kila siku alibaki ndani, alihisi kwamba anaweza kupata ajali na kufariki, alijichunga na kadiri siku zilivyokuwa zikienda mbele, Marekani nzima wakajua kwamba mke wa bilionea Dylan alikuwa mjauzito.

“Mimi kidume Christina, nilikwambia, ukabisha,” Dylan alimwambia ndugu yake wakati wakiongea kwenye simu.

“Safi sana, umefanya kazi kubwa, tunahitaji kupata watoto wetu sasa,” alisema Christina huku kwa sauti yake tu, ilionyesha ni jinsi gani alikuwa na furaha.

Siku zikaendelea kukatika, Dylan akashindwa kuvumilia, alichokifanya ni kumnunulia mkewe zawadi ya gari la thamani aina ya Buggati ambalo hilo alitaka alitumie kipindi alichokuwa akienda hospitalini.

“Nashukuru sana mume wangu! Unanifanya nijisikie kupendwa sana,” alisema Katty pasipo kufahamu kilichotokea nyuma ya pazia.

Mimba tu ikaanza kuwaweka pamoja na kwa ukaribu mkubwa. Dylan akawa mtu wa kuwahi kurudi nyumbani, kuliona tumbo la mkewe, ilimpa furaha kubwa.

“Daktari amesemaje?” aliuliza Dylan.

“Amesema nina mapacha! Wa kike na wa kiume.”
“Unasemaje?”
“Nina mapacha mume wangu!”

Dylan hakuamini, hapohapo akamkumbatia mkewe, akashindwa kuvumilia, machozi ya furaha yakaanza kumtiririka mashavuni mwake. Shukrani zake zote zilikuwa kwa Dk. Fabian ambaye ndiye aliyefanikisha suala zima la upachikaji wa mbegu katika yai la mkewe.

“Nashukuru kwa kila kitu!”

“Asante na wewe pia! Hakika najisikia faraja sana kuona zoezi langu limefanikiwa,” alisema Dk. Fabian huku akiwa na furaha mno.

Baada ya miezi tisa, Katty akaanza kujisikia uchungu wa kuzaa. Siku hiyo, Dylan alikuwa nyumbani kwake, ilikuwa ni saa sita usiku. Wakati mkewe akilalamikia uchungu, tayari gari lilikuwa tayari nje kwani alijua kwamba kitu kama hicho kingetokea kutokana na muda kufika.

Alichokifanya ni kumbeba na kumpeleka ndani ya gari na safari ya kuelekea hospitalini kuanza. Njiani, alikuwa na furaha tele. Hawakuchukua dakika nyingi, wakafika ambapo manesi wakaleta machela na yeye kuanza kuifuata kule manesi walipokuwa wakiisukumia, walipofika katika chumba kilichoandikwa ‘Labour’ akatakiwa kusubiri kwenye viti vilivyokuwa nje ya chumba hicho.

Huku nje, alikuwa na presha kubwa, muda wote alikuwa amesimama, alitembea huku na kule, alitaka kusikia watoto wakilia ndani ya chumba hicho. Watu wote waliokuwa katika eneo hilo walibaki wakimwangalia, walimfahamu, alikuwa bilionea mkubwa Marekani, utajiri ambao aliachiwa na baba yake aliyekuwa amezeeka na hivyo kuhitaji msimamizi.

Baada ya dakika arobaini na tano, akajikuta akianza kurukaruka kwa furaha, hakuamini hata kidogo kile alichokisikia ndani ya chumba hicho. Sauti za watoto zikaanza kusikika. Akajikuta akitoka mbio na kuwakumbatia madaktari waliokuwa mahali hapo, tena kwa zamu. Kile kilichotokea, kilidhihirisha kwamba yeye naye alikuwa mwanaume rijali.

****

Walibaki wakiangaliana, macho yao tu yalionyesha kila kitu kilichokuwa kikiendelea mioyoni mwao. Watu wengine walibaki wakiwaangalia Mike na msichana Aisha, hawakuonekana kuwa mahali hapo, mawazo yao yalikuwa yamehama na yalikwenda sehemu nyingine kabisa.

Mwenyekiti wa mkutano huo akajikoholesha kama njia mojawapo ya kuwaambia watu hao kwamba walitakiwa kuacha kile kilichokuwa kikitokea kwao na wamsikilize yeye.

Hiyo ilisaidia, Mike akamgeukia mwenyekiti huyo lakini muda wote macho yake yalikuwa kwa msichana huyo. Siku hiyo, tena kwenye kikao hicho kazi ilikuwa ni kuangaliana kwa zamu tu.

Mapenzi mazito yakawaingia wote wawili, hawakuamini kama ingechukua muda mfupi kiasi hicho mpaka macho yao kuzoeana. Mkutano uliendelea, ulipomalizika, Mike akashindwa kuvumilia, akamfuata msichana huyo.

“Unaniangalia sana....” alisema Aisha.

“Kwa sababu u mzuri sana, siamini kama duniani kungekuwa na msichana mrembo kama wewe,” alisema Mike, macho yake tu yalionyesha ni kwa kiasi gani alikubaliana na uzuri wa msichana huyo.

“Kweli?”
“Ndiyo!”

“Asante!”

Aisha hakutaka kukaa sana kuzungumza na Mike, alizijua sheria za nchi hiyo, haukutakiwa kupendana na kuishia njiani, kama kweli mlipendana basi ilikuwa ni lazima kuoana na si kuchezeana, sheria nyingine ni kwamba hamkutakiwa kufanya ngono mpaka pale mtakapoona, vinginevyo, mkigundulika mnapigwa mawe hadharani mpaka kufa.

“Aisha...” aliita Mike. Aisha akageuka.

“Unasemaje?”
“Una macho mazuri sana, naomba unitafute...” alisema Mike, akampa kikaratasi kilichokuwa na namba yake na kisha kila mmoja kuondoka.

Hotelini, bado Mike alikuwa amechanganyikiwa. Sura ya mtoto wa Kiarabu ilimchanganya mno, hakuamini kama kweli angekutana na msichana huyo nchini Kuwait.

Usiku hakulala, alibaki akimfikiria msichana huyo mrembo kiasi kwamba akajisahau kabisa na mawazo kuhusu ndoa yakaanza kumuandama. Kwa sababu alimpa namba ya simu, alichokuwa akikisikilizia kipindi hicho ni kupigiwa simu tu.

Ilipofika saa tatu usiku, simu yake ikaanza kuita, hakuamini, namba ilikuwa ngeni hivyo harakaharaka akaichukua na kuipokea.

“Aisha...” alijikuta akiita baada ya kupokea.

“Umejuaje?”
“Hakuna mwenye namba yangu ambaye anaweza kupiga muda huu zaidi yako mrembo,” alisema Mike huku akiachia tabasamu pana kana kwamba msichana huyo alikuwa mbele yake.

“Mmmh! Aya! Niambie unataka kuniambia nini?” aliuliza Aisha.

“Nataka twende sehemu, tukakae na kuzungumza,” alijibu Mike.

“Sehemu gani?”
“Yoyote ile ya siri! Tukutane kisiri na tuzungumze...” alisema Mike.

“Mmh! Si Marekani hapa, ni Kuwait, hilo jambo haliwezekani,” alisema msichana Aisha.

“Kwa hiyo inakuwaje?”

“Labda tukutane sehemu nyingine.”
“Wapi?”
“Dubai! Huko kidogo sheria hazibani!” alijibu msichana huyo.

“Hakuna tatizo! Nataka twende kesho!”
“Ila si kuna mkutano mwingine!”
“Achana nao! Wewe ni muhimu kuliko hata huo mkutano!” alisema Mike. Aisha akacheka kidogo, wakakubaliana na simu kukatwa.

Kilichofuata ni Mike kuwa na presha kubwa ya kukutana na msichana huyo huku akijua kwamba watakapofika Dubai, hakuna sehemu yoyote ambayo wangekutania zaidi ya hotelini ambapo huko angemaliza kila kitu.

“Lazima...lazima, sijawahi kumpata Mwarabu...lazima,” alijisemea huku akivua nguo zake kwa ajili ya kulala. Hata usingizi haukumpata kwa wakati, kila wakati alimfikiria Aisha tu.

*****

Dylan hakuamini kama mke wake alikuwa amejifungua watoto mapacha, pale nje alipokuwa alikuwa akirukaruka kwa furaha huku akimkumbatia kila mtu aliyepita mbele yake.

Alibaki mahali hapo kwa dakika zaidi ya arobaini na ndipo baadaye mkewe alipotolewa na kupelekwa katika chumba cha mapumziko ambapo huko kulikuwa na wanawake wengi waliokuwa na watoto wao.

Hakutaka mke wake awe huko, alikuwa bilionea mkubwa hivyo alichokitaka ni mke wake kupelekwa katika chumba kingine cha peke yake, na hicho ndicho kilichofanyika haraka sana.

Dylan alibaki akimwangalia mkewe, alionekana kuwa na furaha muda wote, hakuamini kama kweli leo hii alikuwa akiitwa baba. Alichukua simu yake na kumpigia baba yake na kumpa taarifa hizo, baba yake alifurahi kwa kupata wajukuu.

Hakuishia hapo tu bali alichokifanya ni kuwapigia marafiki zake wengine akiwemo Catherine na kumwambia kile kilichokuwa kimetokea, msichana huyo hakutaka kubaki nyumbani, japokuwa ilikuwa ni usiku wa manane, akaamka na kuelekea hospitalini.

“Wa kiume ataitwa Patrick, na wa kike ataitwa Patricia,” alisema Dylan huku uso wake ukiwa kwenye tabasamu pana.

Kitu cha kwanza alichokifanya ni kumshukuru mke wake kwa zawadi nzuri aliyompa ambayo hakuweza kuifikiria kabla. Kila alipomwangalia, kwa furaha aliyokuwa nayo, machozi yakaanza kumbubujika mashavuni mwake.

“Nashukuru sana mke wangu,” alisema Dylan huku akimwangalia Katty usoni.

“Asante kwa kushukuru...nililia sana kwa ajili ya hawa watoto,” alisema Katty.

Wala haikuchukua muda mwingi, Catherine akaingia ndani ya chumba hicho, kitu cha kwanza kabisa kilikuwa ni kuwafuata watoto wale, akawaangalia, moyo wake ukaridhika, furaha ya ajabu ikampata moyoni mwake.

Huo ndiyo ulikuwa mwanzo wa furaha ya familia hiyo. Dylan akajipa likizo ya mwezi mzima, hakutaka kutoka ndani ya nyumba yake, alibaki huko huku muda wote akiwa pembeni ya watoto wake.

Japokuwa usiku walikuwa wakilia sana, hakujali, kelele zao zilikuwa ni furaha tele kwake. Yeye ndiye aliyekuwa na jukumu la kuwabadilisha nguo, yeye ndiye alikuwa na jukumu la kuzifua nguo zao kwani hakutaka kabisa wafanyakazi wafanye kitu chochote kwa ajili ya watoto wake.

Mwezi ulipokatika, hapo ndipo alipoanza kwenda kazini. Huko, hakuwa mkaaji sana, ilikuwa ni lazima arudi nyumbani mapema mno. Kila mtu aliyekuwa akimtazama, alionekana dhahiri kuwa na furaha kubwa moyoni mwake, alimsalimia kila mtu na kila aliporudi nyumbani, ilikuwa ni lazima awe na mfuko uliojaa nguo kwa ajili ya watoto wake.

“Nitahakikisha nawapa kila kitu,” alimwambia mke wake.

“Kweli?”

“Ndiyo! Nimekuwa na furaha mno, maisha yangu yamebadilika, wameniletea kitu moyoni mwangu ambacho sikuwa nikikifikiria kabla,” alisema Dylan huku akiwa na Patricia mikononi mwake.

Siku ziliendelea kukatika, miezi ikaenda mbele mpaka mwaka ulipokatika, bado biashara yake ilikwenda vizuri, mafanikio yaliendelea kumiminika. Mwaka wa pili ukaingia, wa tatu mpaka wa nne ambapo mapacha hao wakaanza kusoma chekechea.

Jukumu la kuwapeleka shuleni lilikuwa lake, hakutaka mtu yeyote achukue jukumu hilo. Watoto hao walikuwa wazuri wa sura, walifanana mno. Patricia ambaye ndiye alikuwa Kulwa, sura yake iliwachanganya watu wengi, urembo wake uliwafanya watu kuona kwamba mtoto huyo angekuwa msichana mrembo mno siku za usoni.

Shule waliyokuwa wakisoma ilikuwa ni St. Pius International School, hiyo ilikuwa miongoni mwa shule za matajiri, watoto waliokuwa wakisoma shuleni hapo, wazazi wao walikuwa matajiri au viongozi wa serikali kama mawaziri.

Mbali na utajiri, pia serikali iliwasomesha watoto waliokuwa na uwezo kiakili shuleni hapo. Ilikuwa ni shule ya vipaji lakini upande wa pili ilikuwa ni shule ya matajiri.

Kila siku ilikuwa ni lazima kwa Dylan kuwapeleka shule watoto wake na kuwarudisha nyumbani. Hayo ndiyo yalikuwa maisha yake ya kila siku, hakutaka kuona wakipata tabu yoyote ile, kwake, watoto wake ndiyo walikuwa kila kitu.

Miaka haikumsubirii mtu yeyote ile, baada ya kufikisha miaka nane, uzuri wa Patricia ukazidi kuongezeka, vijana wengi shuleni hapo wakamtolea macho, japokuwa alionekana kuwa mtoto lakini umbo lake lilikuwa kubwa, vijana wengi wakaanza kuweka mazoea na kijana wa kwanza kabisa kuwa karibu naye aliitwa Tenny Andrew.

Huyu alikuwa mtoto wa waziri mstaafu nchini Marekani, Bwana Carthbert Andrew. Alikuwa miongoni mwa watoto waliokuwa na akili nyingi shuleni hapo. Kila mmoja alitamani kuwa karibu na kijana huyo ambaye kama ingekuwa Tanzania, basi tungesema kwamba kijana huyo alikuwa darasa la saba huku Patricia akiwa darasa la tano.

Ukaribu wao ulianza taratibu, watu wengi wakaanza kuhisi kwamba nyuma ya pazia kulikuwa na kitu kinaendelea. Walimu hawakutaka kukaa kimya, walichokifanya ni kumuita Tenny na kuzungumza naye, walimwambia kabisa kwamba ukaribu wake na msichana Patricia uliwatia shaka lakini yeye mwenyewe hakutaka kukubaliana nao.

“There is nothing is going on, trust me,” (hakuna kinachoendelea, niamini) alisema Tenny.

Huku nyumbani, Bwana Dylan hakutaka kuvuruga ratiba yake. Kila siku ilikuwa ni lazima kuwapeleka watoto wake shuleni na kisha kuwarudisha kila ilipofika mchana.

Siku ziliendelea kukatika mpaka pale ambapo Bwana Dylan alipotaka kuwafanyia sapraizi watoto wake kwa ajili ya siku yao ya kuzaliwa.

Siku hiyo hakutaka kuwapeleka shuleni, alipotoka ofisini mapema sana, akapitia supamaketi ambapo akawanunulia keki kubwa, zawadi nyingine na kisha kurudi nyumbani.

Alipofika huko, akamuita mke wake na kumwambia kile alichotaka kukifanya. Kilionekana kuwa kitu kizuri sana. Ili kitu kile kikamilike, ilikuwa ni lazima dereva ndiye awafuate shuleni huko siku hiyo.

Akawasiliana na dereva na hivyo kwenda kuwachukua. Yeye na mkewe walibaki nyumbani, waliandaa mazingira mazuri, wakawaita watu wengine kwa ajili ya kusherehekea nao.

Muda ukaanza kwenda, ulikwenda na kwenda, kitu ambacho kiliwashangaza na kuwashtua ni kwamba watoto hao hawakufika nyumbani. Haikuwa kawaida, shule haikuwa mbali na nyumbani hapo, wakampigia simu dereva ili kumuuliza walikuwa wapi na kitu gani kilikuwa kikiendele, kilichowatisha, simu ya dereva huyo haikuwa ikipatikana.

“I can’t reach him on the phone,” (Simpati kwenye simu) alisema Bwana Dylan.

“What?” (Nini?) aliuliza mkewe.

“I can’t reach him,” (Simpati)

Kila mmoja alichanganyikiwa, kile walichokisikia hakikuaminika kabisa, walichokifanya ni kuondoka nyumbani hapo, seherehe ile iliyoandaliwa, ikavurugika kwa muda. Bwana Dylan akaingia ndani ya gari, aliendesha gari yeye mwenyewe na tena kwa kasi kubwa.

Wakafika shuleni, hakukuwa na mwanafunzi yeyote yule, wakaelekea mpaka katika ofisi ya walimu na kuwauliza kama dereva alifika shuleni hapo. Wakaambiwa kwamba alifika, aliwachukua watoto hao na kuondoka nao.

“Kwani nyumbani hawakufika?” aliuliza mwalimu mmoja.

“Hawakufika! Aliwachukua muda gani?”

“Kama saa moja lililopita!”

“Watakuwa wapi?”

“Hata sisi tunashangaa...”

Kweli walichanganyikiwa, hawakujua ni kitu gani kilikuwa kimetokea, walichokifanya ni kujaribu tena kumpigia simu dereva, kama kawaida majibu yalikuwa yaleyale, simu haikupatikana. Walichanganyikiwa, dakika ziliendelea kusonga mbele, waliogopa hivyo walichokifanya ni kuwasiliana na polisi.

“Hatujui walipo...”

Hivyo ndivyo walivyosema, polisi wakaanza kuwatafuta. Waliwatafuta kwa kuanzia kamera zao za barabarani, hawakupatikana. Walichanganyikiwa, hawakujua watoto hao walipelekwa wapi na dereva huyo.

Muda wote Katty alikuwa akilia tu, hakuwa akiamini kilichokuwa kikiendelea, Dylan, japokuwa yeye mwenyewe alikuwa na uchungu lakini hakutaka kuuonyesha waziwazi, hivyo akajitahidi kumliwaza mke wake. Mpaka inafika saa mbili usiku, polisi hawakumpata dereva wala watoto. Wakazidi kuchanganyikiwa.

Je, nini kitaendelea?

Tukutane Jumapili.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom