Poa mkuu za weweMambo?za siku
Ila Katty nae anaonekana alikuwa anatulia sana aisee, yani akijilaza kajilaza anatulia tuliiiiii kama yule mrembo wa gwajiseeeee yani hana makeke wala mbwembwe... .. Ndomana hajaweza kulistukia dili la mkanda wa dude bandia la bwana Dylan..NYEMO CHILONGANI.
UTAJIRI WENYE UCHUNGU.
0718069269.
Sehemu ya Ishirini
Kila mmoja alionekana mwenye furaha kubwa huko Bahamas, walitembea kila sehemu, kwa siku zote walizokuwa huko, Dylan alikuwa akifanya mapenzi na mkewe, Katty usiku tu.
Hakutaka kufanya mchana, alijifanya kuwa bize mchana na hata alipoguswa hapa na pale, alikuwa mkali, ila usiku, tena huku taa zikiwa zimezimwa, alifanya kwa nguvu zote kwa kutumia kiungo cha bandia ambacho alikifunga kama mkanda fulani hivi.
Baada ya kukaa kwa mwezi mzima ndani ya kisiwa hicho huku wakiponda raha, wakaamua kurudi nchini Marekani kuendelea na shughuli zao kama kawaida. Maisha yake yakabadilika, hayakuwa kama yalivyokuwa kipindi cha nyuma.
Japokuwa alikuwa na furaha tele lakini tatizo moja ambalo lilimfanya kukosa raha katika maisha yake ni juu ya afya yake tu. Alijitahidi kuwaona wataalamu mbalimbali, hakukuwa na mtu aliyemtibu hivyo kubaki hivyohivyo.
Siku zikaendelea kukatika, miezi ikakatika, baada ya miezi sita ya ndoa, mkewe, Katty akaanza kulilia mtoto. Huo ulikuwa mtihani mkubwa kwake, kama kufanya mapenzi, walifanya, tena kwa nguvu zote, kwa nini mtoto hakupatikana?
Hali hiyo ikampa mawazo mazito Dylan, yeye alilijua tatizo lakini mkewe hakujua kitu chochote kile. Kazi yake kubwa kwa kipindi hicho ikawa ni kumfariji tu kwamba muda ukifika, Mungu atawapa mtoto, kwa kipindi hicho walitakiwa kuendelea kusubiri.
“Tatizo nini mume wangu?” aliuliza Katty.
“Hata mimi sijui mke wangu.”
“Kama vipi tukamuone daktari...” alishauri Katty.
“Unahisi tunaweza kuwa na tatizo?”
“Nahisi itakuwa hivyo...”
Hicho ndicho walichotakiwa kufanya hasa katika hali kama hiyo. Kesho yake walikuwa katika Hospitali ya Marie Stopes ambapo wakakutana na daktari wao, Fabian na kumueleza tatizo lao.
“Poleni sana, ila hali kama hiyo inawatokea watu wengi, ngoja niwafanyie vipimo,” alisema Dk. Fabian na hivyo kuanza kazi ya kuwafanyia vipimo.
Muda wote Dylan alikuwa na mawazo tele, moyo wake ulimuuma mno, hakuamini kama bilionea kama yeye ndiye aliyekuwa akipitia maisha hayo. Mbele yake aliiona aibu kubwa, kitendo cha kushindwa kumpa mimba mke wake kilimfanya kuona kwamba siku yoyote ile angeweza kugundulika kile alichokuwa akikifanya kitandani.
Baada ya daktari kuwafanyia vipimo na wiki moja iliyofuata, wakafuata matokeo ya vipimo vyao na kuonekana wote wapo vizuri, hapakuwa na mtu yeyote aliyekuwa na tatizo lolote lile.
“Unasema kweli daktari?”
“Ndiyo Dylan, hakuna mwenye tatizo kabisa,” alijibu Dk. Fabian,
Wakaondoka mahali hapo huku daktari akiwataka kufika hospitalini hapo mara kwa mara kwa ajili ya kupewa ushauri juu ya kitu walichotakiwa kufanya.
Hilo wala halikuwa tatizo, mara kwa mara walifika mahali hapo kama walivyokuwa wakiambiwa, pamoja na hali yote hiyo, matokeo hayakuweza kubadilika, hali ilikuwa ileile kwamba mimba haikupatikana.
“Sasa tatizo litakuwa nini?” aliuliza Katty.
“Hata mimi sifahamu! Au twende sehemu za maombezi..”
“Labda, inawezekana kuna tatizo.”
Wakawa watu wa kwenda kanisani, huko, wakafanyiwa maombezi lakini bado hali iliendelea kuwa vilevile. Waliishi maisha ya majonzi, muda mwingine Katty alikuwa mtu wa kulia tu.
Siku nyingine hakuwa akizungumza na mumewe, hasira zilimkaba kooni na muda mwingi alikuwa akimlaumu Mungu. Kazi yao kubwa ilikuwa ni kubadilisha hospitali, kote huko, matokeo yaliendelea kubaki vilevile lakini Dylan alifahamu nini lilikuwa tatizo.
“Hivi siku akinigundua, itakuwaje?” alijiuliza Dylan.
“Nafikiri itakuwa mwisho! Mungu wangu, nitaishi maisha haya mpaka lini? Ngoja nimuone daktari, nahisi kuna kitu natakiwa kufanya,” alisema Dylan.
Siku hiyo hakutaka kurudi nyumbani mapema, alichokifanya ni kupitia hospitalini ambapo huko akaonana na Dk. Fabian na kuanza kuzungumza naye. Hakutaka kumficha, alijiweka wazi kila kitu kilichokuwa kikiendelea katika maisha yake.
“Ooppss...” alishusha pumzi nzito daktari.
“Ndiyo hivyo! Ninahitaji msaada wako,” alisema Dylan.
“Unafikiri nitakusaidia vipi?”
“Nataka tufanye kitu kimoja...”
“Kipi hicho...”
“Tupandikize mbegu za kiume katika yai la mke wangu,” alisema Dylan.
“Mbegu zako?”
“Hapana! Za mtu mwingine...”
“Mmh!”
“Nini sasa?”
“Nahisi inaweza kuleta matatizo baadaye...”
“Matatizo gani?”
“Huyo mtu akitoa siri...!”
“Sitaki ajue hizo mbegu zinakwenda wapi, iwe siri, nitamlipa dola milioni moja,” alisema Dylan.
“Kweli?”
“Ndiyo! Haina jinsi, nataka kumuona mke wangu akiwa na furaha siku zote katika maisha yake,” alisema Dylan.
Hakuwa na jinsi, kitu pekee alichokihitaji kwa wakati huo ni kumuona mke wake akiwa na furaha. Alijua kwamba jambo alilotaka kulifanya lilikuwa na hatari lakini hakujali, alizihitaji hizo mbegu za kiume kwa gharama zozote zile.
Alichokifanya ni kumuachia jukumu hilo Dk. Fabian ambaye kazi yake kubwa ilikuwa ni kumtafuta mtu ambaye angeweza kuifanya kazi hiyo, mwanaume mwenye sura nzuri ili mtoto atakayezaliwa basi awe na sura nzuri.
Kazi hiyo ikaanza mara moja, alichokifanya Dk. Fabian ni kuwatafuta vijana ambao waliingia mtaani na kumpata Mike ambaye walizungumza naye na kumpeleka hospitali pasipo kumwambia kwamba lengo la yeye kuwa mahali hapo ni kwamba mbegu zake zilikuwa zikihitajika sana.
“Kwa hiyo ishu ni kutoa mbegu tu?” aliuliza Mike.
“Ndiyo! Utapata dola milioni moja...”
“Kweli?”
“Ndiyo!”
“Hakuna kingine?”
“Hakuna!”
Kwake, kwa umasikini aliokuwa nao wala halikuwa tatizo, lilikuwa jambo dogo sana. Kutoa mbegu hizo huku akiingiza dola milioni moja ambazo kwa fedha za Kitanzania ilikuwa ni zaidi ya bilioni mbili, ilikuwa ni bahati mno.
Alichoambiwa ni kuingia ndani ya chumba kimoja kilichokuwa na televisheni, akapewa chombo na kisha kuwashiwa televisheni hiyo na kuwekewa filamu ya utupu huku akitakiwa kujichua.
Akaanza kazi huku akiwa peke yake. Dakika tano nyingi, akafanikiwa kutoa mbegu zake ambazo zilichukuliwa na kuwekwa kwenye mashine maalumu na kutakiwa kuondoka mahali hapo huku akiambiwa kwamba kila kitu kilichoendelea, kiwe siri, asijue mtu yeyote yule. Akakubaliana nao. Ndani ya saa tatu, kiasi hicho cha fedha kaingizwa katika akaunti yake.
****
“Nimeanza kusikia kizunguzungu mpenzi,” alilalamika Katty, ilikuwa ni saa sita usiku.
“Kuna nini tena mpenzi wangu?” aliuliza Dylan huku akionekana kuwa na wasiwasi.
“Sijui! Tumbo linaniuma, nisaidie, tumbo linaniuma na nasikia kizunguzungu, nisaidie mume wangu,” alipiga kelele Katty.
Hakukuwa na kitu kingine cha kufanya zaidi ya kumchukua mkewe, Katty, akambeba na kumpeleka ndani ya gari lake na kuanza safari ya kuelekea katika Hospitali ya Marie Stoppes Medical Center.
Njiani, bado Katty alikuwa akilalamika kwa maumivu huku kile kizunguzungu kikiongezeka kadiri dakika zilivyokwenda mbele. Dylan alichanganyikiwa, aliendesha gari kwa kasi ya ajabu mpaka walipofika katika hospitali hiyo ambapo harakaharaka akawaita manesi ambao wakafika mahali hapo na kumpakiza kwenye machela na kuanza kuisukuma kuelekea nani.
Dylan alikuwa akifuatilia kwa nyuma, alionekana kuchanganyikiwa, hakujua tatizo lilikuwa nini mpaka mke wake kuwa kwenye tatizo kubwa namna ile. Machela ile ikaingizwa katika chumba kilichoandikwa Theatre kwa mlangoni na yeye kuambiwa kubaki mahali hapo.
“Nataka niende na mke wangu,” alisema Dylan.
“Hapana...unatakiwa kubaki hapa,” alisema nesi.
“Nesi...nesi, ninampenda mke wangu, ninataka kuwa karibu naye...” aliendelea kusema Dylan huku akionekana kuchanganyikiwa mno, ugonjwa wa ghafla wa mkewe ulimuweka katika hali mbaya mno.
Hakuruhusiwa kuingia ndani ya chumba hicho, alitakiwa kubaki mahali hapo huku manesi wale wakienda na Katty ndani ya chumba kile. Huku nje, Dylan alibaki akiwa ametulia, muda wote alionekana kuwa na mawazo. Manesi walipokuwa wakitoka nje, aliwang’ang’ania na kutaka kujua ni kitu gani kilikuwa kikiendelea.
“Kuna nini? Nini kimemtokea mke wangu?” aliuliza Dylan huku akionekana kuchanganyikiwa.
“Hakuna kitu, subiri, daktari atakwambia kila kitu,” alisema nesi.
“Atapona?”
“Utaambiwa, subiri hapo,” alisema nesi huyo, hakutaka kubaki mahali hapo kwa kuogopa maswali mengi, huyo akaondoka zake.
Dylan alibaki mahali hapo huku akiwa na mawazo tele, alijiinamia chini, alionekana kuwa na wasiwasi mno, wala haukupita muda mrefu, mlango ukafunguliwa na nesi mwingine kutoka, akasimama na kumdaka na kumuuliza maswali mengine lakini nesi huyo hakutaka kujibu swali lolote lile.
Baada ya dakika chache, Dk. Fabian akatokea mahali hapo huku akiwa kwenye mwendo wa kasi, Dylan alipoyainua macho yake, wakagonganisha macho na daktari huyo kumkonyeza, akaachia tabasamu kisha kuingia ndani ya chumba kile.
Huo ndiyo ulikuwa mpango waliotaka kufanya, Dylan hakutaka kukosea, alijua siku za hatari za mke wake kushika mimba hivyo alihakikisha siku hiyo anafanya kitu kimoja kikubwa.
Kwanza akamuwekea madawa ya usingizi ambayo yangemfanya kusikia maumivu ya tumbo kwa mbali na kuhisi kizunguzungu na mwisho wa siku kupoteza fahamu. Hilo ndilo lililofanyika, wakati amejisikia kizunguzungu, akapoteza fahamu ili Dk. Fabian afanye kazi yake ya kupandikiza mbegu za kiume katika mwili wa Katty.
Hilo lilifanyika kwa siri, ni Dk. Fabian na daktari mwenzake, Dk. Alexander ndiyo waliojua mchezo huo. Mara moja, tena kwa haraka sana kazi ikaanza kufanyika ndani ya chumba hicho.
Dylan alikaa nje ya chumba kile, alijiona kuwa na mafanikio makubwa, alimshukuru Mungu kwa kufanikisha mpango huo, kazi kubwa ilibaki kwa madaktari hao ambao walimuongezea nusu kaputi kitandani pale.
Baada ya saa moja, kila kitu kikawa tayari, madaktari hao wawili wakatoka, kitu cha kwanza baada ya kuonana na Dylan nje ya chumba hicho ni kuanza kumpongeza na kumwambia ainge ndani ya chumba kile.
“Tumefanikiwa...” alisema Dk. Fabian.
“Kweli?”
“Asilimia mia moja, tumefanikiwa!”
“Asante Mungu, siamini!”
“Amini sasa, imekuwa kazi nyepesi mno!”
Wakapongezena, baada ya saa mbili, Katty akarudiwa na fahamu, mtu wa kwanza kabisa kumuona ndani ya chumba hicho alikuwa mume wake. Japokuwa ilikuwa ni saa nane usiku lakini mwanaume huyo hakulala, alipomuona mkewe amefumbua macho, uso wake ukaonyesha tabasamu pana.
“Mume wangu! Nini kilitokea?” aliuliza Katty huku akimwangalia Dylan usoni.
“Sijui! Ila madaktari wamekupima wamegundua kwamba kizunguzungu kimesababishwa na akili yako kuchoka, umefanya kazi mfululizo,” alijibu Dylan bila kupepesa macho pembeni, alitaka kuaminika zaidi.
Hata madaktari walipoingia, majibu yao yalikuwa yaleyale kwamba alifanya kazi kwa kipindi kirefu hivyo alichoka sana hali iliyompelekea kusikia kizunguzungu.
Saa tisa usiku, akaruhusiwa na kurudi nyumbani.
Usiku wa siku hiyo, ulikuwa ni wa mahaba mazito, Dylan hakutaka kuichezea nafasi hiyo, akaanza kumpapasa mkewe kitandani na mwisho wa siku wakajikuta wakiwa kwenye dimbwi la mahaba na hatimaye kuanza kuvuana nguo, kilichofuatia ni sauti za mahaba huku Dylan akiwa makini sana katika kucheza na kifaa kile cha bandia.
Je nini kitaendelea?
Tukutane Junapili
Anaogopa kupoteza kabisa.. ..Aisee
Huyu Dylan bora angekuwa tu mkweli kwa mkewe jamani
Madame santee
Ukweli unamuweka mtu huruAnaogopa kupoteza kabisa.. ..
Kweli aisee.Ukweli unamuweka mtu huru
Pamoja kuwa angeumia
Dear kule kwa Wapemba umetugaya nitumie PM basNYEMO CHILONGANI.
UTAJIRI WENYE UCHUNGU.
0718069269.
Sehemu ya Ishirini
Kila mmoja alionekana mwenye furaha kubwa huko Bahamas, walitembea kila sehemu, kwa siku zote walizokuwa huko, Dylan alikuwa akifanya mapenzi na mkewe, Katty usiku tu.
Hakutaka kufanya mchana, alijifanya kuwa bize mchana na hata alipoguswa hapa na pale, alikuwa mkali, ila usiku, tena huku taa zikiwa zimezimwa, alifanya kwa nguvu zote kwa kutumia kiungo cha bandia ambacho alikifunga kama mkanda fulani hivi.
Baada ya kukaa kwa mwezi mzima ndani ya kisiwa hicho huku wakiponda raha, wakaamua kurudi nchini Marekani kuendelea na shughuli zao kama kawaida. Maisha yake yakabadilika, hayakuwa kama yalivyokuwa kipindi cha nyuma.
Japokuwa alikuwa na furaha tele lakini tatizo moja ambalo lilimfanya kukosa raha katika maisha yake ni juu ya afya yake tu. Alijitahidi kuwaona wataalamu mbalimbali, hakukuwa na mtu aliyemtibu hivyo kubaki hivyohivyo.
Siku zikaendelea kukatika, miezi ikakatika, baada ya miezi sita ya ndoa, mkewe, Katty akaanza kulilia mtoto. Huo ulikuwa mtihani mkubwa kwake, kama kufanya mapenzi, walifanya, tena kwa nguvu zote, kwa nini mtoto hakupatikana?
Hali hiyo ikampa mawazo mazito Dylan, yeye alilijua tatizo lakini mkewe hakujua kitu chochote kile. Kazi yake kubwa kwa kipindi hicho ikawa ni kumfariji tu kwamba muda ukifika, Mungu atawapa mtoto, kwa kipindi hicho walitakiwa kuendelea kusubiri.
“Tatizo nini mume wangu?” aliuliza Katty.
“Hata mimi sijui mke wangu.”
“Kama vipi tukamuone daktari...” alishauri Katty.
“Unahisi tunaweza kuwa na tatizo?”
“Nahisi itakuwa hivyo...”
Hicho ndicho walichotakiwa kufanya hasa katika hali kama hiyo. Kesho yake walikuwa katika Hospitali ya Marie Stopes ambapo wakakutana na daktari wao, Fabian na kumueleza tatizo lao.
“Poleni sana, ila hali kama hiyo inawatokea watu wengi, ngoja niwafanyie vipimo,” alisema Dk. Fabian na hivyo kuanza kazi ya kuwafanyia vipimo.
Muda wote Dylan alikuwa na mawazo tele, moyo wake ulimuuma mno, hakuamini kama bilionea kama yeye ndiye aliyekuwa akipitia maisha hayo. Mbele yake aliiona aibu kubwa, kitendo cha kushindwa kumpa mimba mke wake kilimfanya kuona kwamba siku yoyote ile angeweza kugundulika kile alichokuwa akikifanya kitandani.
Baada ya daktari kuwafanyia vipimo na wiki moja iliyofuata, wakafuata matokeo ya vipimo vyao na kuonekana wote wapo vizuri, hapakuwa na mtu yeyote aliyekuwa na tatizo lolote lile.
“Unasema kweli daktari?”
“Ndiyo Dylan, hakuna mwenye tatizo kabisa,” alijibu Dk. Fabian,
Wakaondoka mahali hapo huku daktari akiwataka kufika hospitalini hapo mara kwa mara kwa ajili ya kupewa ushauri juu ya kitu walichotakiwa kufanya.
Hilo wala halikuwa tatizo, mara kwa mara walifika mahali hapo kama walivyokuwa wakiambiwa, pamoja na hali yote hiyo, matokeo hayakuweza kubadilika, hali ilikuwa ileile kwamba mimba haikupatikana.
“Sasa tatizo litakuwa nini?” aliuliza Katty.
“Hata mimi sifahamu! Au twende sehemu za maombezi..”
“Labda, inawezekana kuna tatizo.”
Wakawa watu wa kwenda kanisani, huko, wakafanyiwa maombezi lakini bado hali iliendelea kuwa vilevile. Waliishi maisha ya majonzi, muda mwingine Katty alikuwa mtu wa kulia tu.
Siku nyingine hakuwa akizungumza na mumewe, hasira zilimkaba kooni na muda mwingi alikuwa akimlaumu Mungu. Kazi yao kubwa ilikuwa ni kubadilisha hospitali, kote huko, matokeo yaliendelea kubaki vilevile lakini Dylan alifahamu nini lilikuwa tatizo.
“Hivi siku akinigundua, itakuwaje?” alijiuliza Dylan.
“Nafikiri itakuwa mwisho! Mungu wangu, nitaishi maisha haya mpaka lini? Ngoja nimuone daktari, nahisi kuna kitu natakiwa kufanya,” alisema Dylan.
Siku hiyo hakutaka kurudi nyumbani mapema, alichokifanya ni kupitia hospitalini ambapo huko akaonana na Dk. Fabian na kuanza kuzungumza naye. Hakutaka kumficha, alijiweka wazi kila kitu kilichokuwa kikiendelea katika maisha yake.
“Ooppss...” alishusha pumzi nzito daktari.
“Ndiyo hivyo! Ninahitaji msaada wako,” alisema Dylan.
“Unafikiri nitakusaidia vipi?”
“Nataka tufanye kitu kimoja...”
“Kipi hicho...”
“Tupandikize mbegu za kiume katika yai la mke wangu,” alisema Dylan.
“Mbegu zako?”
“Hapana! Za mtu mwingine...”
“Mmh!”
“Nini sasa?”
“Nahisi inaweza kuleta matatizo baadaye...”
“Matatizo gani?”
“Huyo mtu akitoa siri...!”
“Sitaki ajue hizo mbegu zinakwenda wapi, iwe siri, nitamlipa dola milioni moja,” alisema Dylan.
“Kweli?”
“Ndiyo! Haina jinsi, nataka kumuona mke wangu akiwa na furaha siku zote katika maisha yake,” alisema Dylan.
Hakuwa na jinsi, kitu pekee alichokihitaji kwa wakati huo ni kumuona mke wake akiwa na furaha. Alijua kwamba jambo alilotaka kulifanya lilikuwa na hatari lakini hakujali, alizihitaji hizo mbegu za kiume kwa gharama zozote zile.
Alichokifanya ni kumuachia jukumu hilo Dk. Fabian ambaye kazi yake kubwa ilikuwa ni kumtafuta mtu ambaye angeweza kuifanya kazi hiyo, mwanaume mwenye sura nzuri ili mtoto atakayezaliwa basi awe na sura nzuri.
Kazi hiyo ikaanza mara moja, alichokifanya Dk. Fabian ni kuwatafuta vijana ambao waliingia mtaani na kumpata Mike ambaye walizungumza naye na kumpeleka hospitali pasipo kumwambia kwamba lengo la yeye kuwa mahali hapo ni kwamba mbegu zake zilikuwa zikihitajika sana.
“Kwa hiyo ishu ni kutoa mbegu tu?” aliuliza Mike.
“Ndiyo! Utapata dola milioni moja...”
“Kweli?”
“Ndiyo!”
“Hakuna kingine?”
“Hakuna!”
Kwake, kwa umasikini aliokuwa nao wala halikuwa tatizo, lilikuwa jambo dogo sana. Kutoa mbegu hizo huku akiingiza dola milioni moja ambazo kwa fedha za Kitanzania ilikuwa ni zaidi ya bilioni mbili, ilikuwa ni bahati mno.
Alichoambiwa ni kuingia ndani ya chumba kimoja kilichokuwa na televisheni, akapewa chombo na kisha kuwashiwa televisheni hiyo na kuwekewa filamu ya utupu huku akitakiwa kujichua.
Akaanza kazi huku akiwa peke yake. Dakika tano nyingi, akafanikiwa kutoa mbegu zake ambazo zilichukuliwa na kuwekwa kwenye mashine maalumu na kutakiwa kuondoka mahali hapo huku akiambiwa kwamba kila kitu kilichoendelea, kiwe siri, asijue mtu yeyote yule. Akakubaliana nao. Ndani ya saa tatu, kiasi hicho cha fedha kaingizwa katika akaunti yake.
****
“Nimeanza kusikia kizunguzungu mpenzi,” alilalamika Katty, ilikuwa ni saa sita usiku.
“Kuna nini tena mpenzi wangu?” aliuliza Dylan huku akionekana kuwa na wasiwasi.
“Sijui! Tumbo linaniuma, nisaidie, tumbo linaniuma na nasikia kizunguzungu, nisaidie mume wangu,” alipiga kelele Katty.
Hakukuwa na kitu kingine cha kufanya zaidi ya kumchukua mkewe, Katty, akambeba na kumpeleka ndani ya gari lake na kuanza safari ya kuelekea katika Hospitali ya Marie Stoppes Medical Center.
Njiani, bado Katty alikuwa akilalamika kwa maumivu huku kile kizunguzungu kikiongezeka kadiri dakika zilivyokwenda mbele. Dylan alichanganyikiwa, aliendesha gari kwa kasi ya ajabu mpaka walipofika katika hospitali hiyo ambapo harakaharaka akawaita manesi ambao wakafika mahali hapo na kumpakiza kwenye machela na kuanza kuisukuma kuelekea nani.
Dylan alikuwa akifuatilia kwa nyuma, alionekana kuchanganyikiwa, hakujua tatizo lilikuwa nini mpaka mke wake kuwa kwenye tatizo kubwa namna ile. Machela ile ikaingizwa katika chumba kilichoandikwa Theatre kwa mlangoni na yeye kuambiwa kubaki mahali hapo.
“Nataka niende na mke wangu,” alisema Dylan.
“Hapana...unatakiwa kubaki hapa,” alisema nesi.
“Nesi...nesi, ninampenda mke wangu, ninataka kuwa karibu naye...” aliendelea kusema Dylan huku akionekana kuchanganyikiwa mno, ugonjwa wa ghafla wa mkewe ulimuweka katika hali mbaya mno.
Hakuruhusiwa kuingia ndani ya chumba hicho, alitakiwa kubaki mahali hapo huku manesi wale wakienda na Katty ndani ya chumba kile. Huku nje, Dylan alibaki akiwa ametulia, muda wote alionekana kuwa na mawazo. Manesi walipokuwa wakitoka nje, aliwang’ang’ania na kutaka kujua ni kitu gani kilikuwa kikiendelea.
“Kuna nini? Nini kimemtokea mke wangu?” aliuliza Dylan huku akionekana kuchanganyikiwa.
“Hakuna kitu, subiri, daktari atakwambia kila kitu,” alisema nesi.
“Atapona?”
“Utaambiwa, subiri hapo,” alisema nesi huyo, hakutaka kubaki mahali hapo kwa kuogopa maswali mengi, huyo akaondoka zake.
Dylan alibaki mahali hapo huku akiwa na mawazo tele, alijiinamia chini, alionekana kuwa na wasiwasi mno, wala haukupita muda mrefu, mlango ukafunguliwa na nesi mwingine kutoka, akasimama na kumdaka na kumuuliza maswali mengine lakini nesi huyo hakutaka kujibu swali lolote lile.
Baada ya dakika chache, Dk. Fabian akatokea mahali hapo huku akiwa kwenye mwendo wa kasi, Dylan alipoyainua macho yake, wakagonganisha macho na daktari huyo kumkonyeza, akaachia tabasamu kisha kuingia ndani ya chumba kile.
Huo ndiyo ulikuwa mpango waliotaka kufanya, Dylan hakutaka kukosea, alijua siku za hatari za mke wake kushika mimba hivyo alihakikisha siku hiyo anafanya kitu kimoja kikubwa.
Kwanza akamuwekea madawa ya usingizi ambayo yangemfanya kusikia maumivu ya tumbo kwa mbali na kuhisi kizunguzungu na mwisho wa siku kupoteza fahamu. Hilo ndilo lililofanyika, wakati amejisikia kizunguzungu, akapoteza fahamu ili Dk. Fabian afanye kazi yake ya kupandikiza mbegu za kiume katika mwili wa Katty.
Hilo lilifanyika kwa siri, ni Dk. Fabian na daktari mwenzake, Dk. Alexander ndiyo waliojua mchezo huo. Mara moja, tena kwa haraka sana kazi ikaanza kufanyika ndani ya chumba hicho.
Dylan alikaa nje ya chumba kile, alijiona kuwa na mafanikio makubwa, alimshukuru Mungu kwa kufanikisha mpango huo, kazi kubwa ilibaki kwa madaktari hao ambao walimuongezea nusu kaputi kitandani pale.
Baada ya saa moja, kila kitu kikawa tayari, madaktari hao wawili wakatoka, kitu cha kwanza baada ya kuonana na Dylan nje ya chumba hicho ni kuanza kumpongeza na kumwambia ainge ndani ya chumba kile.
“Tumefanikiwa...” alisema Dk. Fabian.
“Kweli?”
“Asilimia mia moja, tumefanikiwa!”
“Asante Mungu, siamini!”
“Amini sasa, imekuwa kazi nyepesi mno!”
Wakapongezena, baada ya saa mbili, Katty akarudiwa na fahamu, mtu wa kwanza kabisa kumuona ndani ya chumba hicho alikuwa mume wake. Japokuwa ilikuwa ni saa nane usiku lakini mwanaume huyo hakulala, alipomuona mkewe amefumbua macho, uso wake ukaonyesha tabasamu pana.
“Mume wangu! Nini kilitokea?” aliuliza Katty huku akimwangalia Dylan usoni.
“Sijui! Ila madaktari wamekupima wamegundua kwamba kizunguzungu kimesababishwa na akili yako kuchoka, umefanya kazi mfululizo,” alijibu Dylan bila kupepesa macho pembeni, alitaka kuaminika zaidi.
Hata madaktari walipoingia, majibu yao yalikuwa yaleyale kwamba alifanya kazi kwa kipindi kirefu hivyo alichoka sana hali iliyompelekea kusikia kizunguzungu.
Saa tisa usiku, akaruhusiwa na kurudi nyumbani.
Usiku wa siku hiyo, ulikuwa ni wa mahaba mazito, Dylan hakutaka kuichezea nafasi hiyo, akaanza kumpapasa mkewe kitandani na mwisho wa siku wakajikuta wakiwa kwenye dimbwi la mahaba na hatimaye kuanza kuvuana nguo, kilichofuatia ni sauti za mahaba huku Dylan akiwa makini sana katika kucheza na kifaa kile cha bandia.
Je nini kitaendelea?
Tukutane Junapili
Nakubalituko pamoja
Hii part ni very emotional yani nimesisimkaNYEMO CHILONGANI.
UTAJIRI WENYE UCHUNGU.
Sehemu ya Kumi na Nne.
Nyumbani hawakutulia, kila wakati Catherine alikuwa akipiga simu kwa baba yake kujua walifikia wapi, kama Dylan alikubali au alikataa. Moyo wake haukuwa na amani hata kidogo, hakutulia, alijifikiria kuhusu mvulana huyo, alimpenda mpaka hatua ya mwisho kabisa ambapo akipenda zaidi ya hapo angechanganyikiwa na kuwa kichaa.
Saa zikaendelea kukatika, kila alipomuuliza baba yake waliishia wapi, alimwambia asubiri kwani bado kulikuwa na vitu vichache vya kufanya. Catherine akatulia, akajipa moyo kwamba iwe isiwe ilikuwa ni lazima baba yake akamilishe kile kitu, hivyo akatulia.
Siku hiyo ilipokatika, Bwana James akawapigia simu na kuwaambia kwamba ni lazima waondoke waelekee nchini China kwani kulikuwa na kitu hakikukaa sawa. Hilo liliwachanganya Catherine na mama yake, hawakuelewa ni kitu gani kilichokuwa kikiendelea kwani hata safari hiyo ilikuwa ya ghafla sana.
“Kuna nini?” aliuliza bi Claire.
“Kuna kitu mke wangu!”
“Ni salama lakini?”
“Ndiyo! Wala msijali...”
“Na huyo kijana amesemaje? Atamuoa?”
“Hilo ndilo tunalizungumzia, ila kama tukifanikisha kukifuata kile tunachokifuata nchini China, atamuoa tu,” alisikika Bwana James.
“Kitu gani hicho?”
“Usiwe na hofu mke wangu! Nitakujulisha tu,” alisema Bwana James na kukata simu.
Kitendo cha kuambiwa na mume wake kwamba kulikuwa na kitu ambacho hakutakiwa kukifahamu, kilimfanya kuwa na wasiwasi mkubwa, akakosa amani kwa kuona kwamba kulikuwa na kitu kibaya ambacho mumewe hakutaka akifahamu. Hilo hakujali, hakumwambia binti yake, akabaki nalo moyoni na siku kuendelea mbele.
Upande wa pili, tayari mzee huyo wa dawa za mitishamba akaanza kufanya mambo yake, alihakikisha anamchunguza kwa umakini kujua tatizo lilikuwa nini kwani hakutakiwa kufanya kazi hiyo pasipo kujua historia fupi ya mgonjwa.
“Mtoto wako alianza lini hili tatizo?” aliuliza mzee huyo kupitia mkalimani, tena mbele ya Dylan mwenyewe.
“Alizaliwa nalo.”
“Na ilikuwaje katika kipindi chake cha utotoni? Nataka nipate historia kidogo kutoka kwako mzazi,” alisema mzee yule.
“Huyu si mtoto wangu, ni rafiki yangu!”
“Siyo mtoto wako?”
“Ndiyo!”
“Mmh! Mbona mmefanana hivyo?”
“Hutokea tu, ila ni rafiki yangu!”
Si mzee yule aliyeshangaa bali hata mkalimani naye akapigwa na mshangao. Kila alipowaangalia watu hao, walionekana kuwa kama mapacha, walifanana kwa asilimia kubwa sasa kitendo cha kuambiwa kwamba watu hao hawakuwa ndugu, kiliwashangaza wote.
“Basi ni lazima mama yake au baba aje hapa, ninataka kujua historia yake kwanza juu ya afya yake,” alisema mzee huyo.
“Hakuna tatizo! Atafika ndani ya siku mbili!”
Hilo wala halikuwa tatizo, walichokifanya ni kuwasiliana na bi Leticia na kumhitaji nchini China. Bwana James ndiye alisimamia kila kitu, akawasiliana na watu wake nchini Marekani na kuwaambia kile alichokitaka.
Kutafuta hati ya kusafiria wala halikuwa tatizo kwani kila mtu alimfahamu na aliheshimika sana. Baada ya siku mbili, Bi Leticia alikuwa ndani ya ndege akielekea nchini China.
Yeye mwenyewe hakuelewa ni kitu gani kilichokuwa kikiendelea, aliposikia kwamba anahitajika na mzee huyo bilionea, moyo wake ukawa na wasiwasi mno kwa kuhisi inawezekana kulikuwa na kitu kibaya kilichokuwa kimetokea ambacho kilimtia hatihani kijana wake.
Baada ya zaidi ya saa ishirini, alikuwa akiingia katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Beijing ambapo akateremka na kupokelewa na watu ambao waliandaliwa na kumchukua na kumpeleka ndani ya gari moja na safari ya kuelekea kijijini kuanza.
Walichukua saa nne ndipo wakaingia ndani ya kijiji hicho. Wakapokelewa vizuri na kupelekwa ndani ambapo Bi Leticia akakutana na kijana wake, kitu cha kwanza kabisa kilikuwa ni kumkumbatia.
“Umefanya nini Dylan mtoto wangu?” aliuliza Bi Leticia huku akimwangalia Dylan usoni, machozi yalikuwa yakimbubujika.
“Sijafanya kitu mama!”
“Sasa kwa nini upo huku?”
“Huyu mzee anataka kushughulikia tatizo langu,” alijibu Dylan.
Miongoni mwa watu walioshtuka, hata Bi Leticia naye alishtuka, alipomuona Bwana James, jinsi alivyofanana na kijana wake alibaki akishangaa. Kipindi cha nyuma aliwasikia baadhi ya vijana wakisema kwamba kijana wake alifanana sana na bilionea huyo, alibisha lakini siku hiyo ndipo akakutana naye, walifanana kwa kiasi kubwa sana na ilikuwa rahisi kusema kwamba ni mapacha.
Hapohapo mzee wa tiba akawaita, wote watatu wakaingia ndani ya chumba kimoja ambapo huko akamtaka Bi Leticia kusimulia historia fupi kuhusu Dylan na jinsi hali ilivyokuwa ikiendelea katika ukuaji wake.
“Wewe kama mzazi utakuwa unafahamu vingi, tatizo lake uliligundua kipindi gani?” aliuliza mzee huyo.
“Kipindi fulani, alipokuwa na miaka kumi na nne...” alijibu.
“Ulimzaa huyu mtoto akiwa mzima wa afya?”
“Hapana!”
“Unamaanisha alikuwa akiumwa? Alikuwa akiumwa nini?” aliuliza mzee huyo, Dylan na Bwana James walikuwa kimya wakimsikiliza.
“Sikumzaa mimi!” alisema bi Leticia huku akiangalia chini, alijisikia uchungu sana kuzungumza maneno hayo kwani katika maisha yake yote mpaka kipindi hicho, Dylana aliamini kwamba huyo alikuwa mama yake wa kumzaa.
“Hukumzaa wewe?”
“Ndiyo!”
“Kwa hiyo wewe si mama yake?”
“Ndiyo!”
Mapigo ya moyo wa Dylan yalikuwa juu, hakuamini kile alichokisikia kutoka kwa mwanamke huyo kwamba hakuwa mama yake. Katika kipindi chote cha maisha yake alifahamu kwamba huyo alikuwa mama yake, sasa ilikuwaje tena aseme kwamba yeye hakuwa mama yake, na kama yeye si mama yake, mama yake alikuwa nani na kwa nini alimficha kwa kipindi chote hicho.
“Naomba unisamehe Dylan, sikutaka ulijue hili,” alisema bi Leticia huku akianza kububujikwa na machozi.
“Sijaelewa mama...”
“Sikukuzaa....”
“Hukunizaa?”
“Ndiyo! Mimi si mama yako!”
“Wewe si mama yangu?” aliuliza Dylan.
Bi Leticia hakujibu swali hilo, tayari machozi yaliongezeka na kuanza kulia kilio cha kwikwi, hakukuwa na mtu aliyechanganyikiwa kama Dylan, kila alipomwangalia mwanamke huyo na maneno aliyokuwa akiyasema, hakuamini, wakati mwingine aliona kama anadanganywa.
Huo ulikuwa ni wakati wa Dylan kufahamu ukweli juu ya kile kilichokuwa kimetokea, Bi Leticia hakutaka kuficha, akaanza kuwahadithia kuanza siku ya kwanza walipokuwa kanisani, tsunami ilipopiga, ilipoliharibu Jiji la New Orleans kwa kujaa maji mpaka baadaye kumuokota mtoto Dylan akiwa kwenye friji.
Alipofikia hapo tu, Bwana James akapigwa na butwaa, akasimama kutoka alipokuwa, akamwangalia Dylan mara mbilimbili, hakuamini kabisa kile alichokisikia. Kila mtu aliyekuwa mahali hapo alibaki akimwangalia mzee huyo ambaye alionyesha wazi kwamba alichanganyikiwa kwa furaha.
“Dylan ni mtoto wangu!” alisema Bwana James huku akionekana kutokuamini.
Kila mtu akabaki akimwangalia mzee huyo, bado hawakufahamu ni kitu gani kilimtokea mpaka kupagawa kiasi hicho. Bwana James akainama na kumshika Dylan, hapohapo akamkumbatia, akamng’ang’ania kama mtu ambaye hakutaka kutoka mikononi mwake.
Si Bi Leticia aliyeshangaa, kila mtu aliyekuwa ndani ya chumba hicho alishangaa mpaka mkalimani mwenyewe. Bwana James alikuwa akibubujikwa na machozi, hakuamini kama kuna siku angekutana na mtu huyo, mtoto wake ambaye alimuhifadhi ndani ya friji na hatimaye mpenzi wake, Catherine kufariki miaka mingi iliyopita.
Je, nini kitaendelea?