Utajiri wenye uchungu

Utajiri wenye uchungu

Aiseeeee
Madame asantee
NYEMO CHILONGANI.
UTAJIRI WENYE UCHUNGU.

Sehemu ya Kumi na Sita.

Mpaka dakika kumi baadaye, Bwana James na mkewe walifika katika floo hiyo, kila mmoja alionekana kuchoka mno. Hawakuwa peke yao bali walikuwa na watu wengine ambao wote hao walibaki wakiwaangalia kwa mshangao, hawakujua ni kitu gani kilikuwa kikiendelea.
“Watoto wangu...” alisema Bwana James, akawasogelea na kuwakumbatia wote.
****
Dylan alikuwa na ndoto kubwa za kuwa mchezaji mkubwa wa mpira wa kikapu, ila ndoto zake zote zikafa kwa sababu baba yake alitaka asimamie biashara zake kwani kwa jinsi zilivyokuwa, kama angemuachia Catherine, asingeweza kabisa.
Hilo kwake wala halikuwa tatizo, akaanza kusimamia biashara hizo kama alivyoambiwa. Dylan yule kijana aliyekulia kwenye umasikini mkubwa, leo hii hakuwa masikini, alikuwa tajiri aliyekuwa akiogelea katika dimbwi la fedha za baba yake.
Hakuwa mtu wa starehe, hakuwa mtu wa kupenda wanawake kutokana na hali yake kiafya ilivyokuwa. Siku zikaendelea kukatika kama kawaida huku utajiri huo wa baba yake ukizidi kuongezeka kwani usimamizi aliokuwa akiufanya ulikuwa mkubwa na uliojaa umakini.
Kutokana na kuwa kijana mdogo, wanawake wengi walimpapatikia, kila alipopita alionekana kuwa kawaida, hakuwa mtu wa kujikweza, sifa, hayo yalikuwa mambo yaliyomfanya kupata marafiki wengi kila siku.
“Habari yako....” ilisikika sauti ya msichana mmoja, alikuwa ameingia kwenye lifti kupanda juu katika jengo la Kampuni ya Ericom aliyokuwa akimili baba yake nchini Marekani.
Dylan akageuka nyuma kwani mara alipoingia ndani ya lifti hiyo, hakuwa amemuona msichana huyo kutokana na macho yake kuwa kwenye karatasi alizokuwa amezishika. Ndani ya lifti walikuwa wawili tu.
“Salama tu, habari yako binti?” alimsalimia.
“Salama kabisa. Umependeza...” alisema msichana huyo.
“Asante sana.”
Dylan hakutaka kuzungumza neno jingine lolote, alibaki kimya huku macho yake akiyarudisha katika karatasi ile. Alionekana kuwa makini sana na hakutaka kusubiri mpaka afike ofisini kwake kwani kila siku aliokuwa mtu wa kuwa bize tu.
“Naitwa Katty....” alisema msichana huyo huku tabasamu likiwa usoni mwake.
“Nashukuru kukufahamu...”
“Nashukuru pia Dylan...”
Lifti ilipofika katika ghorofa ya saba, Dylan akateremka na kumuacha msichana yule ndani ya lifti ile huku watu wengine wakiwa wamekwishaingia. Akaondoka na kwenda ofisini kwake, kitu cha kwanza kabisa akahitaji ripoti kamili juu ya viporo vyote alivyoviacha jana yake, hivyo akaletewa.
Aliendelea kukaa ofisini, hakuwa mtu wa kutoka, aliwaamini wafanyakazi wake kwamba walikuwa watendaji na hawakuwa watu wa kumuangusha. Walifanya kazi vizuri na kwa kujitoa sana.
Wakati amemaliza kazi zake majira ya saa nane mchana, akachukua begi lake lililokuwa na laptop, akaliweka begani kwa ajili ya kutoka huku akiwa amekwishampigia simu dereva kwa ajili ya kuligeuza gari lake. Wakati anaingiza mkono mfukoni mwake, akahisi kuna kitu, alipoangalia vizuri, mkono wake ukakutana na kikaratasi, akakitoa na kuanza kukiangalia, kwani kumbukumbu zake zilimwambia kwamba kwa siku hiyo hakuwahi hata kukiingiza kikaratasi chochote mfukoni mwake.
‘Maybe, I am in love, see you soon, it’s me, Katty Perrishian...’ (Labda, nipo kwenye penzi zito, nitakuona hivi karibuni, ni mimi, Katty Perrishian...) yalisomeka maneno yaliyokuwa kwenye kikaratasi kile.
Moyo wa Dylan ukapiga paa! Akahisi kwamba aliingiziwa kikaratasi kile na yule msichana wakati wapo ndani ya ile lifti. Akashusha pumzi nzito.
****
Dylan hakumfahamu msichana huyo, hakujua alikuwa nani na alihitaji nini kutoka kwake. Moyo wake ukawa na presha kubwa, hakumkumbuka hata sura yake kwani walipokutana kwenye lifti hakuonekana kujali sana kuhusu yeye, alikuwa na mambo yake hivyo ilikuwa vigumu mno kuikumbuka sura yake.
Hakutaka kujali sana, akarudi nyumbani kwake na kutulia. Alikuwa kwenye hali ya kawaida tu, akafungulia televisheni na kuanza kuangalia mchezo wa kikapu uliokuwa ukiendelea kati ya Chicago Bulls na La Lakers. Hakutaka kumtilia maanani msichana huyo, aliamua kwa moyo mmoja kufanya mambo yake kwani alikumbuka vizuri kwamba hakuwa salama kiafya na hilo tatizo hakutaka lijulikane na mtu yeyote yule.
Ulipofika muda wa kulala, akajikuta akianza kukikumbuka kile kikaratasi kilichoandikwa ule ujumbe aliopewa. Ulikuwa ujumbe mfupi lakini wenye kusisimua sana. Kwa kipindi hicho, hakutaka kuwa na msichana yeyote yule, mawazo yake yalikuwa kwenye kazi tu. Alipoona ameshindwa kabisa kujikontroo, akachukua simu yake na kumtumia ujumbe wa maneno mdogo wake, Catherine.
“Kama utakuwa na nafasi kesho, naomba nikuone,” aliandika uumbe huo kwenye simu yake na kumtumia Catherine.
“Kuna nini?”
“Hakuna kitu cha kutisha, naomba nikuone kwanza...’
“Sawa...”
Usingizi haukumpata, alikuwa kwenye mawazo tele, alijaribu kuuvuta kwa kbimbilika huku na kule lakini hakulala mpaka ilipofika majira ya saa sita usiku ndipo akalala usingizi mzito.
Asubuhi alipoamka, kitu cha kwanza kilichokuja kichwani mwake kilikuwa ni juu ya yule msichana, bado alikisumbua kichwa chake japo kuukumbuka uso wake lakini hilo halikuwezekana.
Akaelekea bafuni, akaoga na kisha kujiandaa kwa ajili ya kuonana na Catherine kabla ya kwenda ofisini kwake. Jambo kama hilo, hasa kuhusu msichana hakutaka liwe peke yake, alimzoea Catherine, alikuwa ndugu yake na rafiki yake wa karibu ambaye mara kwa mara alikuwa naye na kushauriana mambo mbalimbali kuhusu maisha.
“Huyo msichana ni nani?” aliuliza Catherine.
“Simfahamu kabisa...”
“Na haujawahi kumuona kabla?”
“Ndiyo! Na hata pale nipomuona, sikumtilia maanani..” alijibu Dylan.
Catherine ndiye alikuwa mshauri wake lakini mpaka muda huo hakujua ni kwa namna gani alitakiwa kumshauri Dylan ambaye alionekana kutamani sana kuambiwa neno lolote lile kuhusu msichana huyo.
Hiyo ilikuwa siku ya pili, alitegemea kumuona msichana huyo siku hiyo lakini palikuwa patupu. Katika hali ya kushangaza kabisa, mawazo yakaanza kumsumba, hakuwa na furaha, muda wote alikuwa kimya ndani ya ofisi yake akimfikiria msichana huyo.
Ukimya huo haukuishia siku hiyo tu, ilikatika wiki ya kwanza, msichana huyo hakutokea, wiki ya pili ikakatika lakini bado msichana huyo hakuweza kutokea kitu kilichompa maswali mengi kwani naye kwa kipindi hicho alitamani sana kumuona msichana huyo.
Wiki ya tatu ilipoingia huku mawazo juu ya msichana huyo yakiwa yamepungua kichwani mwake ndipo sekretari wake alipompigia simu na kumwambia kwamba kulikuwa na mzigo wake na ulikuwa umeletwa na msichana fulani ambaye hakujitambulisha.
“Mzigo wa nini?” aliuliza kwenye simu.
“Maua...”
“Maua?”
“Ndiyo bosi! Nikuletee?” aliuliza sekratari.
“Niletee...”
Ndani ya sekunde kadhaa, msichana huyo akaufungua mlango na kuingia ndani, moja kwa moja akaenda katika meza aliyokuwepo bosi wake kisha kumpa maua yale.
Ndani ya sekunde kadhaa, msichana huyo akaufungua mlango na kuingia ndani, moja kwa moja akaenda katika meza aliyokuwepo bosi wake kisha kumpa maua yale.
Dylan akayachukua, kitu cha kwanza kabisa ilikuwa ni kuyanusa, yalinukia vizuri, harufu yake ilimvutia mno. Yalikuwa maua ya kila rangi, yaliyopendeza machoni mwake.
“Nashukuru,” alimwambia mfanyakazi wake na kutoka.
Alibaki akiyaangalia, kila wakati moyo wake ulihisi kitu fulani hivi ambacho wala hakupata wakati mgumu kutambua kilikuwa kitu gani, yalikuwa ni mapenzi ya dhati.
Hakutaka kabisa kitu hicho kitokee, aliufahamu moyo wake, aliifahamu afya yake ambayo ndiyo ilikuwa sababu kubwa ya kuwakataa wanawake waliokuwa wakimfuatilia, kitu ambacho kilimpa maswali ni juu ya huyu msichana ambaye wala hakumkumbuka sura, alikuwa amempenda tu kutokana na vitu alivyokuwa amemfanyia.
Maua yale yalikuja kama yalivyokuja, hakukuwa na kitu kingine kama watu wengine wanavyofanya kwamba kuna jina, namba ya simu na hata mahali yalipotoka.
Siku hiyo kazi hazikufanyika, kila wakati macho yake yalikuwa kwenye maua yale ambapo muda wa kutoka ulipofika, akayachukua, akayaingiza ndani ya gari na kisha kuondoka zake kuelekea nyumbani.
Huo ndiyo ukawa mwanzo, hakuishia kupokea maua, aliendelea kupokea zawadi mbalimbali za kimapenzi ambazo zilimchanganya. Alipagawa, hakujua Katty alikuwa wapi na alihofia nini kurudi tena katika jengo lile kwa ajili ya kumuoa.
Katika siku ambayo aliletewa boksi lililokuwa na nguo za kiume ndiyo siku ambayo alichanganyikiwa zaidi baada ya kuona anuani iliyomuenyesha kwamba mzigo huo ulitumwa kutoka nje ya nchi, tena Ulaya nchini Ufaransa.
“Duh! Hayupo Marekani tena?” alijiuliza.
Ndani ya boksi hilo kulikuwa na cd ambayo aliichukua na kuiweka kwenye kompyuta yake na kuanza kuitazama. Picha alizozikuta humo zikamfariji, akamuona msichana mwenyewe, alikuwa msichana mrembo mno na kila picha iliyokuwa ikionekana ilibeba ujumbe mzito ulioandikwa kwa lugha mbili, yaani Kiingereza na Kiitaliano.
“Te amo,” (Nakupenda) lilikuwa neno pekee la Kiitaliano ambalo alilielewa.
Uso wake ukawa kwenye tabasamu pana, moyo wake ukajisikia faraja kubwa, mapenzi yakaongezeka zaidi, kiu ya kumuona msichana huyo ikamshika zaidi.
Huo ulikuwa mwezi wa kwanza, hakukuwa na kitu alichokuwa akikitamani kama kuonana na msichana huyo. Mwezi wa pili ulipoingia, akatumiwa zawadi ya gari ambayo ilipelekwa mpaka ofisini kwake.
Japokuwa alikuwa bilionea lakini zawadi ile ya gari ambayo alipelekewa ilikuwa bab’ kubwa kwake. Hakuamini kama msichana huyo angeweza kumletea gari ya thamani kama hilo.
Akatokea kulipenda kutokana na jinsi lilivyokuwa ila pamoja na hayo yote, akalipenda zaidi kwa kuwa lilikuwa ni zawadi kutoka kwa msichana aliyehisi kwamba alikuwa na mapenzi mazito juu yake.
Pale lilipoegeshwa, kila mtu alikuwa akilishangaa, lilikuwa zuri, aina ya Porsche lenye gharama kubwa na lilikuwa la kisasa zaidi. Wengi wakahisi kwamba bosi wao Dylan ndiye alikuwa amelinunua, wengi wakampongeza pasipo kujua kwamba lile lililetwa kama zawadi kutoka kwa msichana ambaye hakuwahi kumuona uso kwa uso zaidi ya mara moja.
Miezi ikakatika, mwaka wa kwanza ukapita, bado aliendelea kupokea zawadi tu, kulikuwa na jina, ila hakukuwa na anuani yoyote, akabaki akiwa amechanganyikiwa tu. Alitamani hata kuisikia sauti yake.

Je, nini kitaendelea?
Tukutane Alhamisi hapahapa
 
NYEMO CHILONGANI.
UTAJIRI WENYE UCHUNGU.

Sehemu ya Kumi na Sita.

Mpaka dakika kumi baadaye, Bwana James na mkewe walifika katika floo hiyo, kila mmoja alionekana kuchoka mno. Hawakuwa peke yao bali walikuwa na watu wengine ambao wote hao walibaki wakiwaangalia kwa mshangao, hawakujua ni kitu gani kilikuwa kikiendelea.
“Watoto wangu...” alisema Bwana James, akawasogelea na kuwakumbatia wote.
****
Dylan alikuwa na ndoto kubwa za kuwa mchezaji mkubwa wa mpira wa kikapu, ila ndoto zake zote zikafa kwa sababu baba yake alitaka asimamie biashara zake kwani kwa jinsi zilivyokuwa, kama angemuachia Catherine, asingeweza kabisa.
Hilo kwake wala halikuwa tatizo, akaanza kusimamia biashara hizo kama alivyoambiwa. Dylan yule kijana aliyekulia kwenye umasikini mkubwa, leo hii hakuwa masikini, alikuwa tajiri aliyekuwa akiogelea katika dimbwi la fedha za baba yake.
Hakuwa mtu wa starehe, hakuwa mtu wa kupenda wanawake kutokana na hali yake kiafya ilivyokuwa. Siku zikaendelea kukatika kama kawaida huku utajiri huo wa baba yake ukizidi kuongezeka kwani usimamizi aliokuwa akiufanya ulikuwa mkubwa na uliojaa umakini.
Kutokana na kuwa kijana mdogo, wanawake wengi walimpapatikia, kila alipopita alionekana kuwa kawaida, hakuwa mtu wa kujikweza, sifa, hayo yalikuwa mambo yaliyomfanya kupata marafiki wengi kila siku.
“Habari yako....” ilisikika sauti ya msichana mmoja, alikuwa ameingia kwenye lifti kupanda juu katika jengo la Kampuni ya Ericom aliyokuwa akimili baba yake nchini Marekani.
Dylan akageuka nyuma kwani mara alipoingia ndani ya lifti hiyo, hakuwa amemuona msichana huyo kutokana na macho yake kuwa kwenye karatasi alizokuwa amezishika. Ndani ya lifti walikuwa wawili tu.
“Salama tu, habari yako binti?” alimsalimia.
“Salama kabisa. Umependeza...” alisema msichana huyo.
“Asante sana.”
Dylan hakutaka kuzungumza neno jingine lolote, alibaki kimya huku macho yake akiyarudisha katika karatasi ile. Alionekana kuwa makini sana na hakutaka kusubiri mpaka afike ofisini kwake kwani kila siku aliokuwa mtu wa kuwa bize tu.
“Naitwa Katty....” alisema msichana huyo huku tabasamu likiwa usoni mwake.
“Nashukuru kukufahamu...”
“Nashukuru pia Dylan...”
Lifti ilipofika katika ghorofa ya saba, Dylan akateremka na kumuacha msichana yule ndani ya lifti ile huku watu wengine wakiwa wamekwishaingia. Akaondoka na kwenda ofisini kwake, kitu cha kwanza kabisa akahitaji ripoti kamili juu ya viporo vyote alivyoviacha jana yake, hivyo akaletewa.
Aliendelea kukaa ofisini, hakuwa mtu wa kutoka, aliwaamini wafanyakazi wake kwamba walikuwa watendaji na hawakuwa watu wa kumuangusha. Walifanya kazi vizuri na kwa kujitoa sana.
Wakati amemaliza kazi zake majira ya saa nane mchana, akachukua begi lake lililokuwa na laptop, akaliweka begani kwa ajili ya kutoka huku akiwa amekwishampigia simu dereva kwa ajili ya kuligeuza gari lake. Wakati anaingiza mkono mfukoni mwake, akahisi kuna kitu, alipoangalia vizuri, mkono wake ukakutana na kikaratasi, akakitoa na kuanza kukiangalia, kwani kumbukumbu zake zilimwambia kwamba kwa siku hiyo hakuwahi hata kukiingiza kikaratasi chochote mfukoni mwake.
‘Maybe, I am in love, see you soon, it’s me, Katty Perrishian...’ (Labda, nipo kwenye penzi zito, nitakuona hivi karibuni, ni mimi, Katty Perrishian...) yalisomeka maneno yaliyokuwa kwenye kikaratasi kile.
Moyo wa Dylan ukapiga paa! Akahisi kwamba aliingiziwa kikaratasi kile na yule msichana wakati wapo ndani ya ile lifti. Akashusha pumzi nzito.
****
Dylan hakumfahamu msichana huyo, hakujua alikuwa nani na alihitaji nini kutoka kwake. Moyo wake ukawa na presha kubwa, hakumkumbuka hata sura yake kwani walipokutana kwenye lifti hakuonekana kujali sana kuhusu yeye, alikuwa na mambo yake hivyo ilikuwa vigumu mno kuikumbuka sura yake.
Hakutaka kujali sana, akarudi nyumbani kwake na kutulia. Alikuwa kwenye hali ya kawaida tu, akafungulia televisheni na kuanza kuangalia mchezo wa kikapu uliokuwa ukiendelea kati ya Chicago Bulls na La Lakers. Hakutaka kumtilia maanani msichana huyo, aliamua kwa moyo mmoja kufanya mambo yake kwani alikumbuka vizuri kwamba hakuwa salama kiafya na hilo tatizo hakutaka lijulikane na mtu yeyote yule.
Ulipofika muda wa kulala, akajikuta akianza kukikumbuka kile kikaratasi kilichoandikwa ule ujumbe aliopewa. Ulikuwa ujumbe mfupi lakini wenye kusisimua sana. Kwa kipindi hicho, hakutaka kuwa na msichana yeyote yule, mawazo yake yalikuwa kwenye kazi tu. Alipoona ameshindwa kabisa kujikontroo, akachukua simu yake na kumtumia ujumbe wa maneno mdogo wake, Catherine.
“Kama utakuwa na nafasi kesho, naomba nikuone,” aliandika uumbe huo kwenye simu yake na kumtumia Catherine.
“Kuna nini?”
“Hakuna kitu cha kutisha, naomba nikuone kwanza...’
“Sawa...”
Usingizi haukumpata, alikuwa kwenye mawazo tele, alijaribu kuuvuta kwa kbimbilika huku na kule lakini hakulala mpaka ilipofika majira ya saa sita usiku ndipo akalala usingizi mzito.
Asubuhi alipoamka, kitu cha kwanza kilichokuja kichwani mwake kilikuwa ni juu ya yule msichana, bado alikisumbua kichwa chake japo kuukumbuka uso wake lakini hilo halikuwezekana.
Akaelekea bafuni, akaoga na kisha kujiandaa kwa ajili ya kuonana na Catherine kabla ya kwenda ofisini kwake. Jambo kama hilo, hasa kuhusu msichana hakutaka liwe peke yake, alimzoea Catherine, alikuwa ndugu yake na rafiki yake wa karibu ambaye mara kwa mara alikuwa naye na kushauriana mambo mbalimbali kuhusu maisha.
“Huyo msichana ni nani?” aliuliza Catherine.
“Simfahamu kabisa...”
“Na haujawahi kumuona kabla?”
“Ndiyo! Na hata pale nipomuona, sikumtilia maanani..” alijibu Dylan.
Catherine ndiye alikuwa mshauri wake lakini mpaka muda huo hakujua ni kwa namna gani alitakiwa kumshauri Dylan ambaye alionekana kutamani sana kuambiwa neno lolote lile kuhusu msichana huyo.
Hiyo ilikuwa siku ya pili, alitegemea kumuona msichana huyo siku hiyo lakini palikuwa patupu. Katika hali ya kushangaza kabisa, mawazo yakaanza kumsumba, hakuwa na furaha, muda wote alikuwa kimya ndani ya ofisi yake akimfikiria msichana huyo.
Ukimya huo haukuishia siku hiyo tu, ilikatika wiki ya kwanza, msichana huyo hakutokea, wiki ya pili ikakatika lakini bado msichana huyo hakuweza kutokea kitu kilichompa maswali mengi kwani naye kwa kipindi hicho alitamani sana kumuona msichana huyo.
Wiki ya tatu ilipoingia huku mawazo juu ya msichana huyo yakiwa yamepungua kichwani mwake ndipo sekretari wake alipompigia simu na kumwambia kwamba kulikuwa na mzigo wake na ulikuwa umeletwa na msichana fulani ambaye hakujitambulisha.
“Mzigo wa nini?” aliuliza kwenye simu.
“Maua...”
“Maua?”
“Ndiyo bosi! Nikuletee?” aliuliza sekratari.
“Niletee...”
Ndani ya sekunde kadhaa, msichana huyo akaufungua mlango na kuingia ndani, moja kwa moja akaenda katika meza aliyokuwepo bosi wake kisha kumpa maua yale.
Ndani ya sekunde kadhaa, msichana huyo akaufungua mlango na kuingia ndani, moja kwa moja akaenda katika meza aliyokuwepo bosi wake kisha kumpa maua yale.
Dylan akayachukua, kitu cha kwanza kabisa ilikuwa ni kuyanusa, yalinukia vizuri, harufu yake ilimvutia mno. Yalikuwa maua ya kila rangi, yaliyopendeza machoni mwake.
“Nashukuru,” alimwambia mfanyakazi wake na kutoka.
Alibaki akiyaangalia, kila wakati moyo wake ulihisi kitu fulani hivi ambacho wala hakupata wakati mgumu kutambua kilikuwa kitu gani, yalikuwa ni mapenzi ya dhati.
Hakutaka kabisa kitu hicho kitokee, aliufahamu moyo wake, aliifahamu afya yake ambayo ndiyo ilikuwa sababu kubwa ya kuwakataa wanawake waliokuwa wakimfuatilia, kitu ambacho kilimpa maswali ni juu ya huyu msichana ambaye wala hakumkumbuka sura, alikuwa amempenda tu kutokana na vitu alivyokuwa amemfanyia.
Maua yale yalikuja kama yalivyokuja, hakukuwa na kitu kingine kama watu wengine wanavyofanya kwamba kuna jina, namba ya simu na hata mahali yalipotoka.
Siku hiyo kazi hazikufanyika, kila wakati macho yake yalikuwa kwenye maua yale ambapo muda wa kutoka ulipofika, akayachukua, akayaingiza ndani ya gari na kisha kuondoka zake kuelekea nyumbani.
Huo ndiyo ukawa mwanzo, hakuishia kupokea maua, aliendelea kupokea zawadi mbalimbali za kimapenzi ambazo zilimchanganya. Alipagawa, hakujua Katty alikuwa wapi na alihofia nini kurudi tena katika jengo lile kwa ajili ya kumuoa.
Katika siku ambayo aliletewa boksi lililokuwa na nguo za kiume ndiyo siku ambayo alichanganyikiwa zaidi baada ya kuona anuani iliyomuenyesha kwamba mzigo huo ulitumwa kutoka nje ya nchi, tena Ulaya nchini Ufaransa.
“Duh! Hayupo Marekani tena?” alijiuliza.
Ndani ya boksi hilo kulikuwa na cd ambayo aliichukua na kuiweka kwenye kompyuta yake na kuanza kuitazama. Picha alizozikuta humo zikamfariji, akamuona msichana mwenyewe, alikuwa msichana mrembo mno na kila picha iliyokuwa ikionekana ilibeba ujumbe mzito ulioandikwa kwa lugha mbili, yaani Kiingereza na Kiitaliano.
“Te amo,” (Nakupenda) lilikuwa neno pekee la Kiitaliano ambalo alilielewa.
Uso wake ukawa kwenye tabasamu pana, moyo wake ukajisikia faraja kubwa, mapenzi yakaongezeka zaidi, kiu ya kumuona msichana huyo ikamshika zaidi.
Huo ulikuwa mwezi wa kwanza, hakukuwa na kitu alichokuwa akikitamani kama kuonana na msichana huyo. Mwezi wa pili ulipoingia, akatumiwa zawadi ya gari ambayo ilipelekwa mpaka ofisini kwake.
Japokuwa alikuwa bilionea lakini zawadi ile ya gari ambayo alipelekewa ilikuwa bab’ kubwa kwake. Hakuamini kama msichana huyo angeweza kumletea gari ya thamani kama hilo.
Akatokea kulipenda kutokana na jinsi lilivyokuwa ila pamoja na hayo yote, akalipenda zaidi kwa kuwa lilikuwa ni zawadi kutoka kwa msichana aliyehisi kwamba alikuwa na mapenzi mazito juu yake.
Pale lilipoegeshwa, kila mtu alikuwa akilishangaa, lilikuwa zuri, aina ya Porsche lenye gharama kubwa na lilikuwa la kisasa zaidi. Wengi wakahisi kwamba bosi wao Dylan ndiye alikuwa amelinunua, wengi wakampongeza pasipo kujua kwamba lile lililetwa kama zawadi kutoka kwa msichana ambaye hakuwahi kumuona uso kwa uso zaidi ya mara moja.
Miezi ikakatika, mwaka wa kwanza ukapita, bado aliendelea kupokea zawadi tu, kulikuwa na jina, ila hakukuwa na anuani yoyote, akabaki akiwa amechanganyikiwa tu. Alitamani hata kuisikia sauti yake.

Je, nini kitaendelea?
Tukutane Alhamisi hapahapa
Daah ajitokeze basi namimi wakunihonga hivyo jaman
 
NYEMO CHILONGANI.
UTAJIRI WENYE UCHUNGU.

Sehemu ya Kumi na Saba.

Siku ziliendelea kukatika, bado moyo wake ulikuwa na shauku kubwa ya kumuona msichana huyo, akutane naye na kuzungumza naye kwani kuna mengi alitaka kumwambia hasa jinsi alivyokuwa akijisikia kwa kipindi hicho.
Siku hazikumsubiri, ziliendelea kukatika kama kawaida na kila wiki ilikuwa ni lazima kupokea zawadi yoyote kutoka kwa msichana huyo ambaye bila hofu yoyote ile alikuwa amempenda kwa mapenzi ya dhati.
Baada ya mwaka huo kukatika, mwezi wa sita ndipo akapokea simu. Kwanza alipokiangalia kioo, ilionyesha kwamba haikuwa simu kutoka nchini Marekani, ilitoka nje kabisa hasa kwenye nchi za Ulaya.
Kwanza hakufikiri kama mpigaji alikuwa Katty, alichojua ni kwamba mpigaji wa simu hiyo alikuwa mmoja wa wafanyabiashara wakubwa ambao alikuwa akifanya nao biashara, alichoamua ni kuipokea.
“Habari...” ilisikika sauti nzuri ya msichana.
“Salama...”
“Bila shaka naongeza na Dylan....”
“Ndiyo! Wewe nani tafadhali?”
“Naitwa Katty, sijui unanifahamu?”
Aliposikia jina hilo tu, moyo wake ukapiga paa, hakuamini kama baada ya kusubiri kwa muda wa mwaka mmoja na nusu hatimaye msichana huyo alimpigia simu na kuzungumza naye.
Alichokifanya ni kuangalia tena kioo cha simu yake, furaha aliyokuwa nayo kipindi hicho haikuweza kuelezeka hata mara moja.
“Mbona unanitesa namna hii?” aliuliza Dylan.
“Nakutesa? Kivipi?” aliuliza msichana huyo.
“Kwa nini unanitumia zawadi?”
“Kwa sababu nakupenda!”
“Sasa huoni kama zawadi hizo zinaweza kubadilisha moyo wangu na mimi kukupenda?” aliuliza Dylan kwa sauti ya chini.
“Kwa hiyo nimefanikiwa?”
“Kufanikiwa nini?”
“Kuuteka moyo wako?”
“Tena sana tu...”
Walikuwa wakizungumza kwenye simu huku kila mmoja akionekana kumpenda mwenzake, walizungumza mengi na hata simu ilipokatwa, bado waliendelea kuwasiliana kila siku.
Msichana Katty hakuwa mtu wa kutulia, alikuwa ni wa kwenda huku na kule. Kama ilivyokuwa kwa Dylan kuwa mtoto wa bilionea, hata Katty naye alikuwa hivyohivyo huku baba yake ndiye akiwa mwanzilishi wa kampuni ya magari ya Ferrari.
Kitu alichokitamani Dylan ni kumuona tena msichana huyo ana kwa ana, japokuwa alikuwa akitumiwa video za msichana huyo lakini hilo wala hakuridhika nalo hata kidogo, kitu alichokitaka ni kumuona tu.
Siku zikaendelea kukatika, kila wiki ilikuwa ni Katty kusema kwamba angerudi siku fulani, siku hiyo ilipokuwa ikifika, ilikuwa kimya hivyo kupanga siku nyingine.
Dylan alichanganyikiwa, kama kupenda, muda huo moyo wake ulikuwa kwenye hatua za mwisho kabisa. Hakutaka kusikia la mtu yeyote yule, alichokuwa akikitaka ni Katty tu.
Baada ya mwaka wa pili kuingia, akajikuta akianza kuingia kwenye urafiki wa karibu na binti mwingine ambaye alikuwa akifika sana ofisini kwake kwa ajili ya kuweka mpangilio mzuri wa ofisi (office designing), binti huyo mrembo aliitwa Pauline Mendez.
Msichana huyu alikuwa mrembo hasa, baba yake alikuwa masikini aliyekuwa na asili ya Mexico huku mama yake akiwa Mmarekani mweusi. Alikulia katika maisha ya kimasikini na mama yake aliyekuwa akisumbuliwa na kansa ya titi.
Alipambana sana katika maisha yake, alitafuta fedha kwa ajili ya kumtibu mama yake. Siku zote alikuwa mtu mwenye huzuni kubwa, alitafuta sana kazi, alipopata, nusu ya mshahara wake ulikwenda kwa mama yake.
Baba yake ambaye alikuwa akiishi nchini Mexico naye alikuwa masikini wa kutupwa, alifilisika baada ya kuendekeza sana mchezo wa kamari. Kwa sababu alikuwa na utaalamu wa kutengeneza ofisi ziwe na muonekano mzuri, akaajiliwa na kampuni moja.
Kila siku ilikuwa ni lazima kufika katika jengo la kampuni hiyo aliyokuwa akiisimamia Dylan. Kila mtu aliyemuona Pauline, alimpenda kwani sura yake ya kipole ilimpagawisha kila mtu.
Jinsi ya kumuingia Pauline ilikuwa kazi ngumu, muda mwingi alionekana kuwa bize na mambo yake, hakuwa mtu wa kujichanganya na kila alipoingia katika ofisi hiyo, alikuwa mkimya, haongei mpaka alipoongeleshwa.
“Yule dada amefika bosi...” alisema sekratari wa Dylan kwenye simu.
“Yupi?”
“Yule wa kupamba ofisi...”
“Mwambie aingie...”
Dylan alikuwa bize na mambo yake, japokuwa kila siku msichana huyo alikuwa akifika hapo lakini hakuwa amepata muda wa kumuona zaidi ya kuona ofisi zikipendeza lakini mpendezeshaji hakumfahamu.
Baada ya sekunde kadhaa, msichana Pauline akaingia ndani ya ofisi yake, akamkaribisha, akakifuata kiti na kutulia. Alimwangalia, sura yake tu ilionyesha ni jinsi gani alikuwa mpole, ila kwa sababu kichwa chake kilikuwa na uwezo mkubwa, akagundua kwamba msichana huyo hakuwa sawa, alikuwa na maumivu makubwa moyoni mwake.
“Unaitwa nani?”
“Pauline Mendez...”
“Samahani! Wewe ndiye mbunifu wa ofisi zetu?” aliuliza Dylan.
“Ndiyo!”
“Hongera sana, unajitahidi sana kufanya kazi, ila naruhusiwa kukuuliza swali?” aliuliza Dylan.
“Niulize tu...”
“Kuna nini kinakusumbua moyoni mwako?”
“Hakuna kitu..”
“Hapana Pauline, haupo sawa, unaonekana kama mtu aliyekata tamaa, aliyepoteza matumaini, mwenye huzuni kubwa, tatizo ni nini?” aliuliza Dylan huku akimwangalia msichana huyo usoni.
Pauline hakujibu kitu, alinyamaza, akakiinamisha kichwa chake chini, alipokiinua, machozi yalikuwa yakimtoka. Alichokisema Dylan kilikuwa kweli kabisa, moyo wake ulikuwa kwenye maumivu makali kwa sababu ya mama yake aliyekuwa mgonjwa.
Hakujua kama ilikuwa sahihi kumwambia Dylan au la. Alichokifanya Dylan ni kusimama na kuanza kumfuata msichana huyo. Alipomfikia, akaupeleka mkono wake begani kwa msichana huyo, akamuinamia, akakitoa kitambaa chake, akaanza kumfuta machozi.
*****
Machozi hayakutoka hivihivi, kitu alichohisi Dylan ni kwamba kulikuwa na kitu kikubwa sana kilichokuwa kikimsumbua msichana Pauline na ndiyo maana akaamua kumsogelea na kumfuta machozi yake.
“Kuna nini?” aliuliza Dylan kwa sauti ya chini.
“Inaniuma...”
“Nini tatizo?”
Pauline hakujibu swali hilo, alibaki kimya huku akiugumia kwa kwikwi mfululizo. Moyoni mwake, picha ya mama yake akiwa kitandani ikamjia, alikuwa kwenye mateso makubwa, alikosa msaada kwa kuwa hakuwa na fedha za kutosha.
“Mama yangu ni mgonjwa,” alisema msichana huyo.
“Anaumwa nini?
Hapo ndipo Pauline alipoanza kumuhadithia Dylan kile kilichokuwa kikiendelea kwa mama yake. Historia yake ilimuumiza mno Dylan na kitu pekee kilichomgusa kuliko vyote ni jinsi alivyokuwa akitumia zaidi ya nusu ya mshahara wake kwa ajili ya mama yake.
Huruma nyingi ikazidi kumuingia Dylan, maumivu aliyokuwa nayo msichana yule aliamini kwamba angeweza kuyaondoa kwani hata kiasi ambacho kilihitajika hospitalini, kwake kilikuwa kidogo mno.
Alichomwambia ni kwamba angemfanyia mambo yote likiwemo hilo la kumtibu mama yake mpaka kuhakikisha anapona au kama si kupona basi kuwa na nafuu. Kwa Pauline maneno hayo kwake yalikuwa kama ndoto, hakuwahi kuamini kama kuna siku kungetokea mtu ambaye angekuwa tayari kumsaidia mama yake kwa ule ugonjwa aliokuwa akiugua na kumlaza kitandani.
Siku hiyo, alichokifanya Dylan ni kumchukua Pauline na kuondoka naye kuelekea huko nyumbani. Kwa kumwangalia, alikuwa msichana mrembo, aliyevutia mno lakini nyumba aliyokuwa akiishi na mama yake haikuendana na urembo wake kabisa.
Wakaingia ndani, moja kwa moja Dylan akapelekwa katika chumba alicholazwa mwanamke huyo. Chumba kilikuwa ni cha hadhi ya chini na mwanamke huyo alikuwa kwenye hali mbaya mno.
Dylan akashindwa kujizuia, hapohapo machozi ya uchungu yakaanza kububujika mashavuni mwake, hali aliyoikuta kwa mwanamke huyo hakika ilimuumiza mno. Akapiga hatua kumsogelea, alipomfikia, akamshika mkono.
“Pole sana mama...” alijikuta akimwambia.
“Asante sana...koh...koh...koh...” aliitikia na kukohoa.
Hakuwa na cha kufanya zaidi ya kumsaidia katika matibabu, kitu cha kwanza kabisa alichokifanya kwao ni kuwatafutia nyumba nyingine ambayo ilipatikana siku hiyohiyo, tena ilikuwa na kila kitu ndani.
Hakuishia hapo tu bali alimpeleka mwanamke yule katika hospitali kubwa ya Herieth Medical Center hapo New York kwa ajili kufanyiwa matibabu ambayo yangegharimu dola elfu hamsini ambazo ni zaidi ya shilingi milioni mia moja.
Fedha kwake halikuwa tatizo lolote, kitu alichokuwa akikitamani wakati huo ni kumuona mwanamke huyo akipona na kuwa mzima kabisa. Siku zikaendelea kukatika, hakuacha kumtembelea hapo hospitalini.
Kwa Pauline, kila kitu kilichoendelea kwake kilionekana kuwa kama ndoto, hakuamini kama katika dunia hii kungekuwa na mtu aliyekuwa na roho nzuri kama alivyokuwa Dylan.
Kupitia msaada huo, akajikuta akianza kumpenda kijana huyo, mara kwa mara alikuwa akimfikiria kichwani mwake. Moyo wake ukawa na hamu ya kuwa naye, kila alipojilaza kitandani, hakumfikiria mtu yeyote zaidi ya Dylan tu.
Kile alichofanyiwa, akatamani kukilipa kwa kulala naye tu na ikiwezekana kumpa mapenzi yake yote. Hakuwa na fedha hivyo malipo ambayo kwake aliyaona kufaa ni kumpa penzi zito ambalo asingeweza kusahau katika maisha yake yote.
Hata kabla ya kumwambia kile alichojisikia moyoni mwake akaanza kumfuatilia mwanaume huyo kama alikuwa na mpenzi au la! Kama asingekuwa karibu naye lingekuwa suala gumu sana kumchunguza hivyo alichokifanya ni kuomba kazi katika kampuni ya Dylan kitu ambacho kilikubaliwa haraka sana pasipo kujua lengo la msichana huyo.
Kila siku ilikuwa ni lazima kuonana naye, wanazungumza kisha kuendelea na ishu nyingine. Kwa Dylan, hakuweza kugundua kitu chochote kile, kwake, msichana huyo alionekana kuwa wa kawaida sana hivyo kumchukulia kama rafiki yake jambo ambalo halikukubalika kabisa kichwani mwa msichana huyo.
“Nina shida...” alimwambia Dylan.
“Ipi?”
“Ninataka kutoka mtoko wa usiku na wewe,” alimwambia.
“Na mimi?”
“Ndiyo! Ninaomba...” alimwambia kwa upole mwingi.
“Hapana Pauline, siwezi kufanya hivyo!”
“Kwa nini?”
“Nina mambo mengi sana, labda mwezi ujao...”
“Una uhakika itawezekana bosi?”
“Napo tutaangalia pia...”
Jibu hilo hakulipenda, lilimuumiza moyoni mwake lakini hakuwa na jinsi, alifahamu kwamba Dylan alikuwa tajiri, mtu ambaye hakutaka kabisa kuonekana na watu wengi na ndiyo maana muda mwingi alishinda ofisni kwake ila pamoja na hayo yote, aliona kuna kila sababu ya kutoka mtoko wa usiku na mwanaume huyo.
Hakukuwa na kingine alichokifanya zaidi ya kuwa na subira, kwa sababu aliambiwa kwamba mwezi mmoja, basi akaona litakuwa suala la busara na linalohitaji uvumilivu kama tu angesubiri.
Siku ziliendelea kukatika, hakuacha kumwambia Dylan kuhusu ahadi yao na bado mwanaume huyo alimwambia kwamba wangekwenda tu. Baada ya mwezi kukatika, msichana huyo akamfuata Dylan ofisini kwake na kumuuliza kama alikuwa tayari.
“Tufanye Jumamosi...” alisema, siku hiyo ilikuwa Jumatatu.
Kwa Pauline hakuamini, kwake, alikuwa na furaha mno na muda wote uso wake ulikuwa ni wenye kutabasamu tu. Siku zikakatika na ilipofika Ijumaa, akapata taarifa kwamba usiku wa siku hiyo Dylan alikuwa akipanda ndege kuondoka kuelekea Qatar kwani kuna wafanyabiashara wa mafuta alitaka kuzungumza nao.
Moyo wake uliumia mno, hakuamini kama kweli ilishindikana kwake kuonana na mwanaume huyo na hatimaye amchukue na kutoka naye mtoko wa usiku. Usiku wa siku hiyo alishindwa kulala, alibaki akilia tu kwani kilichotokea kilimuumiza mno.
Mama yake alimshangaa, alimfahamu vilivyo binti yake, kila alipokuwa na furaha, alijua hilo na hata alipokuwa na huzuni, alilijua hilo. Usiku wa siku hiyo alipoingia chumbani kwake, binti yake hakuwa kama alivyokuwa, macho yake yalikuwa mekundu na ilionyesha kwamba alikuwa na huzuni sana tofauti na kipindi kilichopita.
“Kuna nini?” aliuliza mama yake kwa sauti ya chini, tena huku akiwa karibu naye kabisa.
“Inaniuma mama...”
“Inakuuma nini?”
“Dylan mama...”
“Amefanya nini?”
“Ameondoka kwenda Qatar.”
“Sasa ndiyo uumie?” aliuliza mama yake, Pauline hakujibu swali hilo, kilio kikaanza upyaaaa.

Je, nini kitaendelea?
Tukutane Ijumaa hapahapa
 
thanks babe
NYEMO CHILONGANI.
UTAJIRI WENYE UCHUNGU.

Sehemu ya Kumi na Saba.

Siku ziliendelea kukatika, bado moyo wake ulikuwa na shauku kubwa ya kumuona msichana huyo, akutane naye na kuzungumza naye kwani kuna mengi alitaka kumwambia hasa jinsi alivyokuwa akijisikia kwa kipindi hicho.
Siku hazikumsubiri, ziliendelea kukatika kama kawaida na kila wiki ilikuwa ni lazima kupokea zawadi yoyote kutoka kwa msichana huyo ambaye bila hofu yoyote ile alikuwa amempenda kwa mapenzi ya dhati.
Baada ya mwaka huo kukatika, mwezi wa sita ndipo akapokea simu. Kwanza alipokiangalia kioo, ilionyesha kwamba haikuwa simu kutoka nchini Marekani, ilitoka nje kabisa hasa kwenye nchi za Ulaya.
Kwanza hakufikiri kama mpigaji alikuwa Katty, alichojua ni kwamba mpigaji wa simu hiyo alikuwa mmoja wa wafanyabiashara wakubwa ambao alikuwa akifanya nao biashara, alichoamua ni kuipokea.
“Habari...” ilisikika sauti nzuri ya msichana.
“Salama...”
“Bila shaka naongeza na Dylan....”
“Ndiyo! Wewe nani tafadhali?”
“Naitwa Katty, sijui unanifahamu?”
Aliposikia jina hilo tu, moyo wake ukapiga paa, hakuamini kama baada ya kusubiri kwa muda wa mwaka mmoja na nusu hatimaye msichana huyo alimpigia simu na kuzungumza naye.
Alichokifanya ni kuangalia tena kioo cha simu yake, furaha aliyokuwa nayo kipindi hicho haikuweza kuelezeka hata mara moja.
“Mbona unanitesa namna hii?” aliuliza Dylan.
“Nakutesa? Kivipi?” aliuliza msichana huyo.
“Kwa nini unanitumia zawadi?”
“Kwa sababu nakupenda!”
“Sasa huoni kama zawadi hizo zinaweza kubadilisha moyo wangu na mimi kukupenda?” aliuliza Dylan kwa sauti ya chini.
“Kwa hiyo nimefanikiwa?”
“Kufanikiwa nini?”
“Kuuteka moyo wako?”
“Tena sana tu...”
Walikuwa wakizungumza kwenye simu huku kila mmoja akionekana kumpenda mwenzake, walizungumza mengi na hata simu ilipokatwa, bado waliendelea kuwasiliana kila siku.
Msichana Katty hakuwa mtu wa kutulia, alikuwa ni wa kwenda huku na kule. Kama ilivyokuwa kwa Dylan kuwa mtoto wa bilionea, hata Katty naye alikuwa hivyohivyo huku baba yake ndiye akiwa mwanzilishi wa kampuni ya magari ya Ferrari.
Kitu alichokitamani Dylan ni kumuona tena msichana huyo ana kwa ana, japokuwa alikuwa akitumiwa video za msichana huyo lakini hilo wala hakuridhika nalo hata kidogo, kitu alichokitaka ni kumuona tu.
Siku zikaendelea kukatika, kila wiki ilikuwa ni Katty kusema kwamba angerudi siku fulani, siku hiyo ilipokuwa ikifika, ilikuwa kimya hivyo kupanga siku nyingine.
Dylan alichanganyikiwa, kama kupenda, muda huo moyo wake ulikuwa kwenye hatua za mwisho kabisa. Hakutaka kusikia la mtu yeyote yule, alichokuwa akikitaka ni Katty tu.
Baada ya mwaka wa pili kuingia, akajikuta akianza kuingia kwenye urafiki wa karibu na binti mwingine ambaye alikuwa akifika sana ofisini kwake kwa ajili ya kuweka mpangilio mzuri wa ofisi (office designing), binti huyo mrembo aliitwa Pauline Mendez.
Msichana huyu alikuwa mrembo hasa, baba yake alikuwa masikini aliyekuwa na asili ya Mexico huku mama yake akiwa Mmarekani mweusi. Alikulia katika maisha ya kimasikini na mama yake aliyekuwa akisumbuliwa na kansa ya titi.
Alipambana sana katika maisha yake, alitafuta fedha kwa ajili ya kumtibu mama yake. Siku zote alikuwa mtu mwenye huzuni kubwa, alitafuta sana kazi, alipopata, nusu ya mshahara wake ulikwenda kwa mama yake.
Baba yake ambaye alikuwa akiishi nchini Mexico naye alikuwa masikini wa kutupwa, alifilisika baada ya kuendekeza sana mchezo wa kamari. Kwa sababu alikuwa na utaalamu wa kutengeneza ofisi ziwe na muonekano mzuri, akaajiliwa na kampuni moja.
Kila siku ilikuwa ni lazima kufika katika jengo la kampuni hiyo aliyokuwa akiisimamia Dylan. Kila mtu aliyemuona Pauline, alimpenda kwani sura yake ya kipole ilimpagawisha kila mtu.
Jinsi ya kumuingia Pauline ilikuwa kazi ngumu, muda mwingi alionekana kuwa bize na mambo yake, hakuwa mtu wa kujichanganya na kila alipoingia katika ofisi hiyo, alikuwa mkimya, haongei mpaka alipoongeleshwa.
“Yule dada amefika bosi...” alisema sekratari wa Dylan kwenye simu.
“Yupi?”
“Yule wa kupamba ofisi...”
“Mwambie aingie...”
Dylan alikuwa bize na mambo yake, japokuwa kila siku msichana huyo alikuwa akifika hapo lakini hakuwa amepata muda wa kumuona zaidi ya kuona ofisi zikipendeza lakini mpendezeshaji hakumfahamu.
Baada ya sekunde kadhaa, msichana Pauline akaingia ndani ya ofisi yake, akamkaribisha, akakifuata kiti na kutulia. Alimwangalia, sura yake tu ilionyesha ni jinsi gani alikuwa mpole, ila kwa sababu kichwa chake kilikuwa na uwezo mkubwa, akagundua kwamba msichana huyo hakuwa sawa, alikuwa na maumivu makubwa moyoni mwake.
“Unaitwa nani?”
“Pauline Mendez...”
“Samahani! Wewe ndiye mbunifu wa ofisi zetu?” aliuliza Dylan.
“Ndiyo!”
“Hongera sana, unajitahidi sana kufanya kazi, ila naruhusiwa kukuuliza swali?” aliuliza Dylan.
“Niulize tu...”
“Kuna nini kinakusumbua moyoni mwako?”
“Hakuna kitu..”
“Hapana Pauline, haupo sawa, unaonekana kama mtu aliyekata tamaa, aliyepoteza matumaini, mwenye huzuni kubwa, tatizo ni nini?” aliuliza Dylan huku akimwangalia msichana huyo usoni.
Pauline hakujibu kitu, alinyamaza, akakiinamisha kichwa chake chini, alipokiinua, machozi yalikuwa yakimtoka. Alichokisema Dylan kilikuwa kweli kabisa, moyo wake ulikuwa kwenye maumivu makali kwa sababu ya mama yake aliyekuwa mgonjwa.
Hakujua kama ilikuwa sahihi kumwambia Dylan au la. Alichokifanya Dylan ni kusimama na kuanza kumfuata msichana huyo. Alipomfikia, akaupeleka mkono wake begani kwa msichana huyo, akamuinamia, akakitoa kitambaa chake, akaanza kumfuta machozi.
*****
Machozi hayakutoka hivihivi, kitu alichohisi Dylan ni kwamba kulikuwa na kitu kikubwa sana kilichokuwa kikimsumbua msichana Pauline na ndiyo maana akaamua kumsogelea na kumfuta machozi yake.
“Kuna nini?” aliuliza Dylan kwa sauti ya chini.
“Inaniuma...”
“Nini tatizo?”
Pauline hakujibu swali hilo, alibaki kimya huku akiugumia kwa kwikwi mfululizo. Moyoni mwake, picha ya mama yake akiwa kitandani ikamjia, alikuwa kwenye mateso makubwa, alikosa msaada kwa kuwa hakuwa na fedha za kutosha.
“Mama yangu ni mgonjwa,” alisema msichana huyo.
“Anaumwa nini?
Hapo ndipo Pauline alipoanza kumuhadithia Dylan kile kilichokuwa kikiendelea kwa mama yake. Historia yake ilimuumiza mno Dylan na kitu pekee kilichomgusa kuliko vyote ni jinsi alivyokuwa akitumia zaidi ya nusu ya mshahara wake kwa ajili ya mama yake.
Huruma nyingi ikazidi kumuingia Dylan, maumivu aliyokuwa nayo msichana yule aliamini kwamba angeweza kuyaondoa kwani hata kiasi ambacho kilihitajika hospitalini, kwake kilikuwa kidogo mno.
Alichomwambia ni kwamba angemfanyia mambo yote likiwemo hilo la kumtibu mama yake mpaka kuhakikisha anapona au kama si kupona basi kuwa na nafuu. Kwa Pauline maneno hayo kwake yalikuwa kama ndoto, hakuwahi kuamini kama kuna siku kungetokea mtu ambaye angekuwa tayari kumsaidia mama yake kwa ule ugonjwa aliokuwa akiugua na kumlaza kitandani.
Siku hiyo, alichokifanya Dylan ni kumchukua Pauline na kuondoka naye kuelekea huko nyumbani. Kwa kumwangalia, alikuwa msichana mrembo, aliyevutia mno lakini nyumba aliyokuwa akiishi na mama yake haikuendana na urembo wake kabisa.
Wakaingia ndani, moja kwa moja Dylan akapelekwa katika chumba alicholazwa mwanamke huyo. Chumba kilikuwa ni cha hadhi ya chini na mwanamke huyo alikuwa kwenye hali mbaya mno.
Dylan akashindwa kujizuia, hapohapo machozi ya uchungu yakaanza kububujika mashavuni mwake, hali aliyoikuta kwa mwanamke huyo hakika ilimuumiza mno. Akapiga hatua kumsogelea, alipomfikia, akamshika mkono.
“Pole sana mama...” alijikuta akimwambia.
“Asante sana...koh...koh...koh...” aliitikia na kukohoa.
Hakuwa na cha kufanya zaidi ya kumsaidia katika matibabu, kitu cha kwanza kabisa alichokifanya kwao ni kuwatafutia nyumba nyingine ambayo ilipatikana siku hiyohiyo, tena ilikuwa na kila kitu ndani.
Hakuishia hapo tu bali alimpeleka mwanamke yule katika hospitali kubwa ya Herieth Medical Center hapo New York kwa ajili kufanyiwa matibabu ambayo yangegharimu dola elfu hamsini ambazo ni zaidi ya shilingi milioni mia moja.
Fedha kwake halikuwa tatizo lolote, kitu alichokuwa akikitamani wakati huo ni kumuona mwanamke huyo akipona na kuwa mzima kabisa. Siku zikaendelea kukatika, hakuacha kumtembelea hapo hospitalini.
Kwa Pauline, kila kitu kilichoendelea kwake kilionekana kuwa kama ndoto, hakuamini kama katika dunia hii kungekuwa na mtu aliyekuwa na roho nzuri kama alivyokuwa Dylan.
Kupitia msaada huo, akajikuta akianza kumpenda kijana huyo, mara kwa mara alikuwa akimfikiria kichwani mwake. Moyo wake ukawa na hamu ya kuwa naye, kila alipojilaza kitandani, hakumfikiria mtu yeyote zaidi ya Dylan tu.
Kile alichofanyiwa, akatamani kukilipa kwa kulala naye tu na ikiwezekana kumpa mapenzi yake yote. Hakuwa na fedha hivyo malipo ambayo kwake aliyaona kufaa ni kumpa penzi zito ambalo asingeweza kusahau katika maisha yake yote.
Hata kabla ya kumwambia kile alichojisikia moyoni mwake akaanza kumfuatilia mwanaume huyo kama alikuwa na mpenzi au la! Kama asingekuwa karibu naye lingekuwa suala gumu sana kumchunguza hivyo alichokifanya ni kuomba kazi katika kampuni ya Dylan kitu ambacho kilikubaliwa haraka sana pasipo kujua lengo la msichana huyo.
Kila siku ilikuwa ni lazima kuonana naye, wanazungumza kisha kuendelea na ishu nyingine. Kwa Dylan, hakuweza kugundua kitu chochote kile, kwake, msichana huyo alionekana kuwa wa kawaida sana hivyo kumchukulia kama rafiki yake jambo ambalo halikukubalika kabisa kichwani mwa msichana huyo.
“Nina shida...” alimwambia Dylan.
“Ipi?”
“Ninataka kutoka mtoko wa usiku na wewe,” alimwambia.
“Na mimi?”
“Ndiyo! Ninaomba...” alimwambia kwa upole mwingi.
“Hapana Pauline, siwezi kufanya hivyo!”
“Kwa nini?”
“Nina mambo mengi sana, labda mwezi ujao...”
“Una uhakika itawezekana bosi?”
“Napo tutaangalia pia...”
Jibu hilo hakulipenda, lilimuumiza moyoni mwake lakini hakuwa na jinsi, alifahamu kwamba Dylan alikuwa tajiri, mtu ambaye hakutaka kabisa kuonekana na watu wengi na ndiyo maana muda mwingi alishinda ofisni kwake ila pamoja na hayo yote, aliona kuna kila sababu ya kutoka mtoko wa usiku na mwanaume huyo.
Hakukuwa na kingine alichokifanya zaidi ya kuwa na subira, kwa sababu aliambiwa kwamba mwezi mmoja, basi akaona litakuwa suala la busara na linalohitaji uvumilivu kama tu angesubiri.
Siku ziliendelea kukatika, hakuacha kumwambia Dylan kuhusu ahadi yao na bado mwanaume huyo alimwambia kwamba wangekwenda tu. Baada ya mwezi kukatika, msichana huyo akamfuata Dylan ofisini kwake na kumuuliza kama alikuwa tayari.
“Tufanye Jumamosi...” alisema, siku hiyo ilikuwa Jumatatu.
Kwa Pauline hakuamini, kwake, alikuwa na furaha mno na muda wote uso wake ulikuwa ni wenye kutabasamu tu. Siku zikakatika na ilipofika Ijumaa, akapata taarifa kwamba usiku wa siku hiyo Dylan alikuwa akipanda ndege kuondoka kuelekea Qatar kwani kuna wafanyabiashara wa mafuta alitaka kuzungumza nao.
Moyo wake uliumia mno, hakuamini kama kweli ilishindikana kwake kuonana na mwanaume huyo na hatimaye amchukue na kutoka naye mtoko wa usiku. Usiku wa siku hiyo alishindwa kulala, alibaki akilia tu kwani kilichotokea kilimuumiza mno.
Mama yake alimshangaa, alimfahamu vilivyo binti yake, kila alipokuwa na furaha, alijua hilo na hata alipokuwa na huzuni, alilijua hilo. Usiku wa siku hiyo alipoingia chumbani kwake, binti yake hakuwa kama alivyokuwa, macho yake yalikuwa mekundu na ilionyesha kwamba alikuwa na huzuni sana tofauti na kipindi kilichopita.
“Kuna nini?” aliuliza mama yake kwa sauti ya chini, tena huku akiwa karibu naye kabisa.
“Inaniuma mama...”
“Inakuuma nini?”
“Dylan mama...”
“Amefanya nini?”
“Ameondoka kwenda Qatar.”
“Sasa ndiyo uumie?” aliuliza mama yake, Pauline hakujibu swali hilo, kilio kikaanza upyaaaa.

Je, nini kitaendelea?
Tukutane Ijumaa hapahapa
 
CHILONGANI.
UTAJIRI WENYE UCHUNGU.
0718068269.

Sehemu ya Kumi na Nane.

“Dylan mama...”
“Amefanya nini?”
“Ameondoka kwenda Qatar.”
“Sasa ndiyo uumie?” aliuliza mama yake, Pauline hakujibu swali hilo, kilio kikaanza upyaaaa.
*****
Mama yake alijitahidi kumbembeleza lakini msichana huyo haikuwa rahisi kunyamaza, moyoni mwake kulikuwa na maumivu makali, mapenzi yaliyokuwa yalikuwa makubwa mno, hakutaka kuona Dylan akifanya kitu chochote kile ambacho hakutaka kukifanya, yaani kama alimwambia ni lazima kwenda mtoko wa usiku, basi watoke.
Mpaka mama yake anaondoka chumbani humo, hakurudi katika hali yake ya kawaida, bado alikuwa na huzuni tele huku muda mwingine akilia kama kawaida yake.
Alijuta kuuruhusu moyo wake kumpenda mtu ambaye wala hakuwa na habari naye, alishindwa kuelewa ni kitu gani kingetokea kama tu angepata taarifa kwamba Dylan alikuwa na mwanamke mwingine.
Alihisi angekufa kama angesikia hivyo, na kama si kufa basi angeweza kuathirika kiafya kwani tayari akili yake ilichanganyikiwa kwa mapenzi mazito aliyokuwa nayo kwa mwanaume huyo.
Hakuacha kuwasiliana naye, hakuacha kuzifikisha hisia zake kwamba mwanaume huyo aliondoka katika siku ambayo alimhitaji sana, hakuacha kumwambia kuhusu huzuni yake, yote hayo, alimwambia wazi ili afahamu.
“Utanisamehe, ilikuwa ni ghafla sana, nilihisi angekwenda baba au Catherine, matokeo yake nimekuja mimi,” alisema Dylan kwenye simu, kwanza kitendo cha kuombwa msamaha tu, kikaonyesha ni jinsi gani alikuwa na thamani kubwa kwa mwanaume huyo.
“Na unarudi lini?” aliuliza Pauline.
“Sijajua, ila ningependa nirudi Jumatatu...”
“Nitafurahi sana kukuona..”
“Usijali, na mama naye anaendeleaje?”
“Anaendelea vizuri tu, anaendelea kutibiwa, asante sana kwa msaada wako...”
“Usijali! Nipo kwa ajili ya kukusaidia kama rafiki yangu...” alisema Dylan.
Walikuwa wakiongea maneno mengi, wakati Dylan akifikiria kwamba msichana huyo alikuwa rafiki yake wa kawaida tu, kwa Pauline hali ilikuwa tofauti kabisa, kwake alimuona mwanaume huyo kuwa mpenzi wake, hivyo hata alipoambiwa kwamba yeye alikuwa rafiki tu, moyo wake ulimuuma mno.
****
Hakukuwa na msichana aliyekuwa akimfikiria kichwani mwake kama alivyokuwa Katty, huyo alikuwa msichana pekee ambaye kwa kipindi hicho alitamani sana kumuona.
Mwaka wa pili ulikuwa umekatika lakini hakuweza kukutana na msichana huyo. Katika kipindi ambacho alikuwa Qatar, aliwasiliana naye na kumwambia kwamba anataka kuonana naye kwa mara nyingine.
Kwa kuwa Katty alimwambia kuwa katika kipindi hicho alikuwa mjini Dubai, hivyo akamuahidi kwamba ilikuwa ni lazima amfuate na kuonana naye kwani kutoka Dubai mpaka Qatar hapakuwa mbali, ilikuwa ni kama kilometa elfu moja tu kwani zote hizo zilikuwa katika muunganiko wa nchi za Kiarabu, Emirates.
“Unataka nije lini?” aliuliza Katty.
“Siku yoyote, ukishindwa, hata mimi naweza kuja.”
“Sawa! Naomba tufanye kesho, nitakuja mara moja kisha nitarudi...”
“Hakuna tatizo!”
Moyo wake ulikuwa kwenye presha kubwa, tangu aanze ukaribu na msichana huyo hakuwa ameonana naye tena kitu kilichomuumiza na kumpa mawazo mno. Miaka miwili ilikuwa mingi sana kwake, hakutaka kuvumilia, hakutaka kuona mwaka huo unakatika pasipo kuonana naye.
Kitendo cha kuambiwa kwamba kesho angeonana na Katty kilimpagawisha mno, hakuamini, akajiandaa vilivyo ila tatizo lililokuja lilikuwa ni afya yake tu.
Hicho ndicho kilichomtia uchungu, alikuwa tajiri, lakini kuwa tajiri pasipo jogoo wake kuwika, utajiri ukawa mchungu mno kwake. Kitu alichokuwa akikifikiria kipindi hicho ni namna gani angeweza kulala na msichana huyo pasipo kugundua kama kiungo chake hakikuwa kikifanya kazi.
Alichokifanya ni kuondoka na kuelekea katika duka linalouza dawa za kuongeza nguvu na hata midoli ya kufanyia mapenzi. Aliingia ndani ya duka hilo kisiri, hakutaka mtu yeyote yule afahamu, alivalia kofia kubwa na miwani.
Alipoingia, akanunua kifaa alichokihitaji na kisha kuondoka zake huku akimsubiri msichana Katty afike Qatar na kuzungumza naye, ikiwezekana usiku mzima walale wote.
Ilipofika saa moja usiku, akapigiwa simu na Katty na kuambiwa kwamba tayari msichana huyo alikwishafika katika uwanja wa ndege hivyo amuelekeze hoteli aliyofikia amfuate.
Ndani ya dakika kadhaa, msichana Katty alikuwa mapokezi. Dylan alipopigiwa simu na kuambiwa kwamba kulikuwa na mgeni wake, hakutaka kumwambia dada wa mapokezi amruhusu aende huko bali alitoka na kuelekea chini, alitaka kumpokea yeye mwenyewe.
Alipofika, kitu cha kwanza baada ya kumuona ni kumkimbilia na kumkumbatia huku kila mmoja akionekana kuwa na furaha kubwa. Watu waliokuwa mahali hapo, wakabaki wakiwashangaa tu, mapokeo waliyopokeana watu hao ilikuwa tofauti kabisa na watu wengine.
Hawakutaka kubaki mahali hapo, walichokifanya ni kuifuata lifti huku wakiwa wameshikana kimahaba, walipoingia ndani, wakaanza kupanda juu huku wakishikana hapa na pale.
“Ninakuhitaji usiku wa leo,” alisema Katty, yeye mwenyewe hakufikiria kama siku hiyo angekuwa namna hiyo kwani hata kuzungumza na Dylan kwa kipindi kirefu tangu afike, hawakuzungumza.
“Nitafanya lolote utakalo, mpaka utaridhika...”
“Kweli?”
“Niamini mpenzi!”
Walipofika katika floo waliyokuwa wakienda, wakateremka, wakashikana kimahaba mpaka ndani ya chumba walichochukua, kuingia ndani, hawakutaka hata kuzungumza chochote kile, wakaelekea kitandani.
“Naomba...naomba, nataka unipe,” alisema Katty huku akilalamika kimahaba.
“Nakupa, nakupa mpenzi...”
Wakati Dylan akisema maneno hayo, hakukuwa na mabadiliko yoyote yale mwilini mwake, alikuwa kama mtu aliyekuwa akila chakula huku akiwa na mawazo tele.
Wakati Katty akiendelea na utundu wake mwilini mwake ndipo akakumbuka kwamba alikuwa na kifaa chake katika droo na ilikuwa ni lazima kitumike usiku huo.
Akili yake ilicheza kwa haraka sana, akasimama na kuifuata taa, akaizima na kurudi kitandani. Katty alikuwa hoi, hakujiweza, alichokuwa akisubiri ni kuanza kwa mechi tu.
Kwa siri sana akaupeleka mkono wake kwenye droo ya kitanda na kutoa kifaa alichotakiwa kukitumia na kujiweka tayari, macho yakawa yakimwangalia Katty ambaye alifumba macho kwa hisia kali.
“Upo tayari?” aliuliza huku akiwa amevaa, tena kwa kufunga kamba kiunoni.
“N..ip..o tay..ar..i...” alijibu Katty huku akitoa pumzi nzito kimahaba.
Kilichofuatia baada ya hapo ni miguno ya mahaba kutoka kwa wote wawili, kitanda kililia sana, kila mmoja alikuwa akihema kwa nguvu, Katty, kwa jinsi alivyokuwa na hamu na Dylan, muda wote alikuwa akimvuta kwake, alimng’ang’ania sana huku aking’atang’ata sikio na shingo ya Dylan.
****
Baada ya dakika kadhaa, kila mmoja alikuwa hoi, kwa haraka sana hata kabla Katty hajagundua, Dylan akasimama na kuelekea chooni. Katty hakushtukia kitu chochote kile, kwa kuwa kulikuwa na giza hata kumuona vizuri hakumuona, ndiyo kwanza akageukia upande wa pili na kulala.
Kule chooni, Dylan akakitoa kile kiungo cha bandia, akakisafisha na kisha kuanza kurudi nacho chumbani ambapo akafungua droo ya kitanda na kukihifadhi, tena kwa kukifichaficha chini ya makaratasi na yeye kulala.
Asubuhi ya siku iliyofuata, wote wakaamka, wakanywa chai, wakatoka mahali hapo na kuelekea katika bwawa la kuogelea ambapo waliogelea mpaka mida ya saa tano wakatoka na kwenda kunywa chai.
Katika kipindi chote hicho, wote wawili walionekana kuwa na furaha tele, kila mmoja hakuamini kama mwisho wa siku wangekuwa hivyo wawili. Walipiga stori, walipomaliza wakaelekea chumbani ambapo muda wote Katty alikuwa akililia kurudiwa kwa mchezo.
“Nataka tena....” alisema Katty huku akianza kumvua nguo Dylan.
“Subiri kwanza....”
“Nina kiu mpenzi, nimekumisi, nimeyamisi mambo yako,” alisema msichana huyo huku akimbembeleza.
Japokuwa alimuonea huruma msichana huyo lakini hakuwa na jinsi, asingeweza kumsaidia kwa sababu haikuwa usiku na kama angefanya naye ilikuwa ni lazima msichana huyo agundue kwamba kiungo kilichokuwa kikitumika hakikuwa halisi bali kilikuwa bandia.
Alishikwa hapa na pale, alinyonywa huku na kule lakini mwili wake haukubadilika hata kidogo, ulikuwa vilevile pasipo mabadiliko yoyote yale. Katty hakuacha, aliamini kwamba angeweza kumbadilisha mwanaume huyo na kumpa ashki ya kufanya mapenzi lakini pamoja na jitihada zote hizo, majibu yalikuwa bila-bila.
“Kwa hiyo hutaki?” aliuliza Katty huku macho yake yakianza kuwa mekundu.
“Mpenzi! Ninasikia uchovu, nahisi naumwa...”
“Tatizo nini?”
“Sijajua, ila naumwa, sijisikii vizuri...”
Katty alikasirika, mwili wake uliwaka moto, hakutaka kusikia kitu chochote kile, alichokuwa akikitaka ni kufanya mapenzi na mpenzi wake mpya, kuambiwa kwamba hakuwa akijisikia vizuri, roho yake ilimuuma mno. Hakuendelea kumshikashika tena, alichokifanya ni kujilaza pembeni na kutulia zake.
Dylan alikaa siku kadhaa huko Dubai, akaagana na mpenzi wake ambaye alirudi Qatar na yeye Marekani. Njiani, kila mmoja alikuwa na majonzi tele, walizoeana sana, Katty alimpenda mno Dylan, kwake, alikuwa mwanaume mwenye ndoto naye ambaye alijitolea maisha yake kwa ajili yake.
Hata kwa Dylan, hakukuwa na msichana ambaye alikuwa na mapenzi ya dhati kama aliyokuwa nayo kwa Katty. Walitumiana picha huku wakiwa kwenye mapozi mbalimbali, waliwasiliana wakiwa njiani huku ishara nyingi za kimapenzi zikionekana kati yao.
Alipofika nchini Marekani, miongoni mwa watu waliofika mahali hapo kwa ajili ya kumpokea alikuwa msichana Pauline. Dylan alishangaa, hakutaka msichana huyo afike hapo, taarifa aliipa familia yake na watu wengine wa karibu, cha kushangaza, msichana huyo naye alifika kwa ajili ya kumpokea.
“Nimekukumbuka sana Dylan...” alisema msichana Pauline wakati alipokuwa akimkumbatia.
“Nimekukumbuka pia...”
Hakumkumbuka Pauline hata kidogo lakini kwa kuwa aliambiwa hivyo, akaona si tatizo kama naye atamwambia hivyohivyo. Wakaondoka hapo uwanja wa ndege na kuelekea nyumbani, muda wote huo msichana huyo alikuwa karibu naye mno kitu kilichowapa maswali mengi ndugu zake, hasa Catherine.
“Huyu ndiye yule msichana uliyeniambia?” aliuliza Catherine.
“Yupi?”
“Yule Katty!”
“Hapana!”
“Na huyu naye nani?”
“Ni mfanyakazi wangu!”
“Mfanyakazi wako au mpenzi wako?”
“Mfanyakazi!”
“Sasa mbona yupo hivyo, yaani beneti kana kwamba mpenzi wako?”
“Hata mimi mwenyewe nashangaa...” alijibu Dylan.
Muda huo walikuwa nyumbani, walitulia huku wakila na kunywa, ukaribu ule bado uliendelea kuwatia maswali wengine lakini Dylan hakutaka kujali kwani tayari alihisi kwamba kulikuwa na kitu kilichokuwa kikiendelea moyoni mwa Pauline.
Alikuwa msichana mrembo mno, hata naye moyo wake alihisi kama kulikuwa na kitu kilianza kuingia ila hakutaka kujiweka kirahisi, hakutaka kuona akimsaliti msichana Katty kwa sababu ya Pauline.
Siku hiyo walikaa nyumbani hapo mpaka usiku, tena kwa Dylan kumng’ang’aniza kuondoka kwani bila kufanya hivyo, tayari Pauline alitaka alale nyumbani hapo.
“Naomba nikueleze kitu Dylan...” alisema Pauline huku wakiwa njiani kuelekea nyumbani.
“Kitu gani?”
“Unahisi nini kuhusu mimi?” aliuliza.
“Sihisi chochote...kuna nini kwani?” aliuliza Dylan, wakati huo alikuwa akiendesha gari.
“Haujahisi kwamba nakupenda?”
“Kunipenda?”
“Ndiyo! Ninakupenda, nimekuwa nikitamani kukwambia hili kwa kipindi kirefu sana...” alisema msichana huyo.
“Kunipenda mimi?”
“Ndiyo!”
“Mbona umechelewa sana?”
“Nimechelewa? Hapana! Sijachelewa, nimekuwa nikikufuatilia kwa kipindi kirefu, ukiniambia kwamba una mpenzi, sitokubaliana nawe,” alisema msichana huyo kwa sauti ya upole.
“Nina mpenzi Pauline, na hata nilipokwenda Dubai, nilionana naye, anaitwa Katty!” alisema Dylan.
Kwa Pauline, hakutaka kukubali hata kidogo, alimfahamu Dylan, tangu awe naye, hakukuwa hata na siku moja ambayo alimuona mwanaume huyo akiwa na msichana. Si kumuona tu hata kusikia tetesi kwamba alikuwa na mwanamke yeyote, hakuwahi kusikia.
Kitendo cha Dylan kumwambia kwamba alikuwa na msichana, kilimuumiza na kuona kwamba mwanaume huyo hakutaka tu kuwa naye. Hiyo ilimuumiza mno, alikosa furaha, akajikuta macho yakianza kuwa mekundu na hapohapo machozi kuanza kumtoka.
“Dylan...unanidanganya...kwa nini hutaki kuniambia ukweli?” aliuliza Pauline huku akilia.
“Ndiyo ukweli huo?”
“Unanidanganya, huo ni uongo...unaniumiza Dylan...” alisema msichana huyo huku sauti ya kilio chake ikizidi kuwa kubwa.
“Ndiy...” alisema Dylan lakini hata kabla hajamaliza sentensi yake, tena huku gari likiwa kwenye mwendokasi wa 80, hapohapo msichana huyo akaufungua mlango, kilichotokea, akajirusha barabarani. Dylan macho yakamtoka.
****
Dylan akafunga breki, hakuamini kilichotokea, alichanganyikiwa, harakaharaka akateremka kutoka garini mwake na kuelekea kule msichana Pauline alipojirusha.
Kitu ambacho alimshukuru sana Mungu ni kwamba nyuma hakukuwa na gari lolote lile. Pauline alikuwa amebimbirika mpaka pembeni ya barabara, Dylan alipomfikia na kumwangalia, alikuwa amechubuka mno, mikononi, miguuni na hata mgongoni.
Moyo wa Dylan uliumia mno, hakutaka kuchelewa, hapohapo akambeba na kuanza kuondoka naye huku hata yeye mwenyewe machozi yakianza kumtoka kwani hakuamini kama msichana huyo angefanya hivyo.
“Pauline! What have you done?” (Umefanya nini Pauline?) alimuuliza huku akiwa mikononi mwake.
Alipomfikisha garini, hakutaka kubaki mahali hapo, akaondoka na breki yake ya kwanza ilikuwa ni kwenye Hospitali ya St. Angel Medical Center iliyokuwa hapohapo New York.
Kitendo cha kufika hapo huku akiwaita manesi, tayari machela ikafikishwa, akaufungua mlango na kumtoa msichana huyo. Manesi walipomuona Pauline, hawakuamini, msichana yule alichubuka sana, kabla ya kuuliza chochote kile, wakaisukuma machela ile kuelekea ndani ya jengo la hospitali hiyo.
Walipofika katika chumba kilichoandikwa theatre kwa nje, akaambiwa asubiri kwani humo ndipo ambapo msichana huyo alitakiwa kufanyiwa matibabu kutokana na hali yake kuwa mbaya namna ile.
Dylan alibaki nje, bado alikuwa haamini kilichotokea, kwake, aliendelea kumshangaa msichana huyo, alionekana kuwa mtu wa ajabu na hakufikiria kabisa kama msichana huyo angeweza kufanya jambo hilo.
Akampigia simu Catherine na kumwambia kile kilichotokea. Hakutaka kumwambia mtu yeyote yule kwani msichana huyo, mbali na undugu waliokuwa nao, walikuwa marafiki wa karibu mno.
“Yaani amejirusha kutoka garini?” alisikika Catherine akiuliza.
“Ndiyo!”
“Ilikuwaje?”
“Yaani wewe acha tu...”
“Wewe niambie ilikuwaje!”
“Njoo kwanza..”
“Nakuja!”
Dylan hakutaka kumwambia katika simu, alitaka kuonana naye na kumwambia kile kilichotokea. Baada ya dakika kadhaa, msichana huyo akafika hospitalini hapo na moja kwa moja kuanza kuzungumza naye.
“Kwa hiyo unamaanisha alivyokutaka, ukamkataa?” aliuliza msichana huyo.
“Nilimwambia kwamba nina mtu...”
“Na kweli unaye?”
“Ndiyo!”
“Mbona hukuniambia?”
“Ndiyo nilitaka kukwambia, ni yule Katty ambaye nilionana naye Dubai,” alijibu Dylan.
“Kwa hiyo itakuwaje kwa huyu msichana?”
“Yaani hapa nimechanganyikiwa! Anaweza kujiua huyu!” alisema Dylan.
Waliendelea kusubiri hospitalini hapo mpaka pale ambapo madaktari walipomaliza na kuwataka kumjulia hali mgonjwa wao. Wakaingia ndani ya chumba kile, Pauline alikuwa kimya kitandani, bandeji zilifungwa katika sehemu kubwa ya mwili wake.
Dylan alipomwangalia msichana huyo, moyo wake ulimuuma mno, alimuona jasiri ambaye alikuwa tayari kufanya lolote kwa ajili ya moyo wake. Japokuwa msichana huyo alikuwa na mapenzi ya dhati kwake lakini Dylan hakutaka kujihusisha naye kabisa.
“Ila ni msichana mrembo sana Dylan...” alisema Catherine.
“Nakubaliana na wewe...ila nina msichana tayari...”
“Kwa hiyo itakuwaje kuhusu huyu?”
“Sijajua kwani hata ndoto za kumuacha Katty, sina...”
Wakati wakizungumza hayo, Pauline alikuwa kimya kitandani pale. Alibaki kwenye hali hiyo kwa saa moja, akayafumbua macho yake, watu wa kwanza kukutana nao walikuwa ni Dylan na Catherine.
“Dylan....” aliita msichana huyo kwa sauti ya chini.
“Nipo hapa...” alijibu Dylan huku akimsogelea msichana huyo.
“Niambie kitu kimoja....”
“Kitu gani?”
“Unanipenda?” aliuliza msichana huyo akimwangalia Dylan usoni, Catherine alikuwa pembeni akiangalia kinachoendelea.
“Sikiliza Pauline....ni laz...”
“Niambie moja, unanipenda?” aliuliza msichana huyo.
Jibu ni kwamba hakumpenda, hakuhisi hisia zozote za mapenzi moyoni mwake lakini kumwambia ukweli kwamba hakuwa akimpenda, alihisi kungeibua tatizo jingine kabisa.
Alibaki akimwangalia msichana huyo, hata kama angesema anampenda, ingekuwa ni kumwambia kwa sababu tu hakutaka apate tatizo lolote lile. Pauline aliendelea kumwangalia Dylan, kitu alichotaka kusikia ni jibu kutoka kwa mwanaume huyo.
“Ninakupenda....” alisema Dylan, hata kuongea kwake ilikuwa ni kujilazimisha tu.
“Una uhakika?”
“Ndiyo! Ninakupenda Pauline...” alisema Dylan.
Msichana huyo akatoa tabasamu pana, hakuamini alichokisikia. Kwa kipindi kirefu alitaka kusikia mwanaume huyo akimwambia anampenda hivyo kuambiwa hivyo, kwake ilikuwa faraja tele.
Akajitahidi kuinuka kitandani pale na kisha kumkumbatia Dylan. Muda wote huyo, Catherine alibaki akiwaangalia tu. Msichana aliyekuwa mbele yake, hata kwa kumwangalia tu, alionekana kuwa na mapenzi ya dhati kwa kaka yake.
“Nataka unioe...” alisema Pauline kwa sauti ya chini kabisa, karibu na sikio la Dylan.
“Nikuoe?”
“Ndiyo!” alijibu msichana huyo.
“Lakini Pauline!”
“Nakuomba Dylan...ninakupenda sana...” alisema msichana huyo.
Hata kabla Dylan hajatoa jibu lolote kuhusu suala la Pauline kutaka kuolewa, hapohapo akasikia simu yake ikianza kuita. Harakaharaka akaitoa kutoka mfukoni mwake, hisia zake zilimwambia kwamba mpigaji alikuwa baba yake tu ambaye angemuuliza mahali alipokuwa.
Pauline alifuatilia, naye mwenyewe alitaka kumfahamu mpigaji. Dylan alipoitoa simu ile na kuangalia kioo, jina la Katty lilionekana vizuri, moyo wake ukapiga paaa......Pauline akanyong’onyea, akajikuta akianza kuishiwa nguvu.

Je, nini kitaendelea
 
Back
Top Bottom