Utajiri wa nchi ni akili za Watu sio rasilimali kama madini na nyinginezo

Robert Heriel Mtibeli

JF-Expert Member
Mar 24, 2018
21,341
51,907
UTAJIRI WA NCHI NI AKILI ZA WATU, SIO RASILIMALI KAMA MADINI N.K.

Anaandika, Robert Heriel.

Huwaga namshangaa mtu anayesema nchi yetu ni Tajiri. Kwa kweli sio tuu anachekesha Bali pia anaonyesha jinsi alivyokuwa mjinga na asiyeweza kufikiri sawia.

Kama nikiulizwa hivi leo sababu gani inatufanya Waafrika ikiwemo nchi yetu kuwa Masikini, basi jibu litakuwa ni kuwa Sisi tunaakili ndogo Kama sio kuwa hatuna Kabisa.

Taifa ili kiwe Tajiri linahitaji watu wenye akili zaidi kuliko Rasilimali. Utajiri ni Akili na sio wingi wa Rasilimali.
Kuna msemo usemao, penye miti hapana wajenzi.

Akili ndio inaweza kufanya madini kuwa Rasilimali Kwa kuipa Value. Madini kama madini hayajui kama yenyewe ni yathamani, Ila wenye akili ndio wanajua thamani ya madini hayo kutokana na matumizi waliyoyabuni kwayo.

Kidunia Bara la Afrika ndilo bara lenye malighafi nyingi kuliko bara lolote lile. Lakini watu wake wameshindwa kuzigeuza malighafi hizo kuwa Rasilimali Kwa kuzipa thamani.

Ukisikia mtu anakuambia Yeye ni Tajiri Kwa sababu nchi yake inamadini, maziwa na Mito, Ardhi yenye Rutuba, wanyama wa kuvutia, na mambo mengine lakini watu wake ni Hali zao za maisha ni duni jua mtu huyo hajui kufikiri vizuri, na pengine akawa mwendawazimu.

Nchi haiwezi kuwa Tajiri Kama ndani yake inawatu wajinga wengi. Watu wasio na akili wakiwa wengi ndivyo nchi inavyozidi kuwa Masikini.

Mtu asiye na akili Hana tofauti na mnyama wa porini, ni Sawa na tumbili au ngedere anayeishi msituni ananyeshewa mvua na kuchomwa na Jua lakini anashindwa kujenga nyumba hata ya mbao Kwa sababu ya upeo mdogo wa Akili.

Wazungu walivyotuita Waafrika manyani kuna watu walifikiri walimaanisha maumbile yetu yanafanana na nyani😀😀 Kama nawe ulifikiri hivyo basi nawe upo kundi la watu wajinga.

Wazungu walituita manyani mbali na ubaguzi wao lakini walituona akili zetu hazijaachana Sana na tumbili na nduguye ngedere.

Nyani au ngedere ukimpelekea Dhahabu au Almasi wala hataiona inatofauti na jiwe jingine. Kutokana na upeo mdogo wa Akili.

Sisi Watanzania wengi wetu tunaakili ndogo mno na hiyo ndio sababu Sisi sio matajiri. Na tutaendelea kuwa Vivi hivi Kwa Karne kadhaa zijazo.

Watanzania wengi ni Kama wanyama Kwa mambo mengi, kama unavyomuona ng'ombe basi ndivyo wengi wetu tulivyo.

Sio ajabu ukakuta watu kwenye makazi Yao kuna mavi au maji machafu waliyoyasababisha yamewazunguka, yananuka na nzi wamejaa lakini wao hawaoni Shida. Wanalala, wanakula hapohapo, na wanakunya na kukojoa hapohapo.

Hapo ati wanasubiri kiongozi aje awaambie wawe wasafi tena wengine ifikie hatua ya kupelekwa serikali za mitaa kisa anaambiwa asizibue chemba za mavi yake na familia yake, come on!

Sio ajabu jitu linakunya chooni labda cha umma alafu hali-flash uchafu wake. Hivi mtu huyo anatofauti ipi na Mnyama?

Mtu anajua kabisa ili aishi anatakiwa awe na chakula cha kutosha kinachomtosha yeye na familia yake, badala awe na ghala la kuhifadhi chakula kinachomtosha yeye na watoto wake angalau Kwa miaka miwili kulingana na Hali ya hewa.

Yeye anakula Kama mnyama asijue kesho atakula nini. Halafu ikifika kesho anaanza kumlalamikia mtu mwingine labda ni serikali au viongozi. Jamani hivi tunaakili kweli?

Tena wakati mwingine tunazidiwa akili hata na Wanyama.

Hakuna mnyama ambaye atazaa watoto ambao hawezi Kuwatunza. Hakuna na hajawahi kutokea. Mfano Kuku anaouwezo wa kutaga mayai hata Mia moja.

Lakini atataga mayai kumi (10-12) kulingana na uwezo wake wakuyaatamia, sio atage mayai 20 alafu wakati wa kuatamia mengine ashindwe kuyaatamia yajitokeze nje.

Kisha Kwa mayai 10-12 anaouwezo wa kuwachunga na kuwakuza watoto hao.

Halikadhalika na mbwa, ng"'ombe, mbuzi, Simba n.k.

Lakini Sisi unakuta mtu anazaa watoto nje ya uwezo wake wa Kuwatunza, labda watoto 10 alafu ananilaumu serikali kuwa gharama za Shule au hospitali ziondolewe.

Au anaomba msaada Kabisa wa kusaidiwa kulelewa watoto.

Hivi tumelogwa au ni kitu gani?

Mtu unajua kabisa miti ndio huleta hewa Safi, huleta mvua na kivuli kizuri, na Kupunguza joto la nchi. Alafu unakuta watu wamekata miti mtaa mzima ili wajenge nyumba.

Unashangaa mtaa mzima miti ipo 20 Kwa eneo la kilometa moja. Alafu muda huohuo unasikia mwehu akipiga kelele jamani joto Kali, jamani jua linawaka! Mara kiyama kinakaribia.

Kiama ya mavi. Ujinga na wehu wako ndio unaita Kiyama?

Utajiri WA nchi ni akili za watu na sio Rasilimali Kama madini.

Chakufanya;
I. Tujifunze kuwa na Akili ili tuwe nchi yetu itajirike.

Robert Heriel
Taikon wa Fasihi
Kwa sasa Dar es salaam
 
Wakikuelewa naomba uniambie

Ndio utajua umuhimu wa kuwa na mtaala bora mazingira mazuri ya kufundisha na vifaa na kuwajali walimu na kuwapa mishahara minono na marupurupu ya kutosha maana ndio wanaiandaa nchi ya kesho

Kama hawataki sawa tukae tuendelee
 
Ukisikia mtu anakuambia Yeye ni Tajiri Kwa sababu nchi yake inamadini, maziwa na Mito, Ardhi yenye Rutuba, wanyama wa kuvutia, na mambo mengine lakini watu wake ni Hali zao za maisha ni duni jua mtu huyo hajui kufikiri vizuri, na pengine akawa mwendawazimu.
Yule baba alikuwa na likichwa kubwa kama tembo, lakini ajili ndogo kama sisimizi.
 
Wakikuelewa naomba uniambie

Ndio utajua umuhimu wa kuwa na mtaala bora mazingira mazuri ya kufundisha na vifaa kiwajali walimu na kuwapa mishahara minono na marupurupu ya kutosha maana ndio wanaiandaa nchi ya kesho

Kama hawataki sawa tukae tuendelee

Kuna mambo yanashangaza Sana. TMA ishatangaza kuwa kutakuwa na uhaba wa mvua ndani ya nchi.

Wizara ya maji tangazo Hilo ingekuwa ni Alert kwao kuwa kutakuwa na upungufu wa Maji Kwa mwaka huu au miaka hii miwili mitatu. Hivyo tayari kabla tatizo la maji halijajitokeza mbele za watu wa kawaida au wachini kabisa wangetakiwa washajiandaa kukabiliana na changamoto zote za uhaba WA Maji unaotokana na uhaba wa mvua.

Yaani kuna mambo mengine ukiyatafakari unabaki kusikitika Sana.

Serikali lazima iongozwe na watu wenye AKILI.
Na Kama wenye akili sio watawala Kwa sababu ya uoga basi Wale majasiri wawe watawala alafu wawatumie wenye akili katika kuwapa mawazo na ushauri.
 
Leo dishi limekaa sawa.
Naunga hoja hii mkono kwa 100%.
Kuna mambo yanashangaza Sana. TMA ishatangaza kuwa kutakuwa na uhaba wa mvua ndani ya nchi.

Wizara ya maji tangazo Hilo ingekuwa ni Alert kwao kuwa kutakuwa na upungufu wa Maji Kwa mwaka huu au miaka hii miwili mitatu. Hivyo tayari kabla tatizo la maji halijajitokeza mbele za watu wa kawaida au wachini kabisa wangetakiwa washajiandaa kukabiliana na changamoto zote za uhaba WA Maji unaotokana na uhaba wa mvua.

Yaani kuna mambo mengine ukiyatafakari unabaki kusikitika Sana.

Serikali lazima iongozwe na watu wenye AKILI.
Na Kama wenye akili sio watawala Kwa sababu ya uoga basi Wale majasiri wawe watawala alafu wawatumie wenye akili katika kuwapa mawazo na ushauri.
 
UTAJIRI WA NCHI NI AKILI ZA WATU, SIO RASILIMALI KAMA MADINI N.K.

Anaandika, Robert Heriel.

Huwaga namshangaa mtu anayesema nchi yetu ni Tajiri. Kwa kweli sio tuu anachekesha Bali pia anaonyesha jinsi alivyokuwa mjinga na asiyeweza kufikiri sawia...
Hili jibu ni kweli
 
UTAJIRI WA NCHI NI AKILI ZA WATU, SIO RASILIMALI KAMA MADINI N.K.

Anaandika, Robert Heriel.

Huwaga namshangaa mtu anayesema nchi yetu ni Tajiri. Kwa kweli sio tuu anachekesha Bali pia anaonyesha jinsi alivyokuwa mjinga na asiyeweza kufikiri sawia.
Kama nikiulizwa hivi leo sababu gani inatufanya Waafrika ikiwemo nchi yetu kuwa Masikini, basi jibu litakuwa ni kuwa Sisi tunaakili ndogo Kama sio kuwa hatuna Kabisa.

Taifa ili kiwe Tajiri linahitaji watu wenye akili zaidi kuliko Rasilimali. Utajiri ni Akili na sio wingi wa Rasilimali.
Kuna msemo usemao, penye miti hapana wajenzi.

Akili ndio inaweza kufanya madini kuwa Rasilimali Kwa kuipa Value. Madini kama madini hayajui kama yenyewe ni yathamani, Ila wenye akili ndio wanajua thamani ya madini hayo kutokana na matumizi waliyoyabuni kwayo.

Kidunia Bara la Afrika ndilo bara lenye malighafi nyingi kuliko bara lolote lile. Lakini watu wake wameshindwa kuzigeuza malighafi hizo kuwa Rasilimali Kwa kuzipa thamani.

Ukisikia mtu anakuambia Yeye ni Tajiri Kwa sababu nchi yake inamadini, maziwa na Mito, Ardhi yenye Rutuba, wanyama wa kuvutia, na mambo mengine lakini watu wake ni Hali zao za maisha ni duni jua mtu huyo hajui kufikiri vizuri, na pengine akawa mwendawazimu.

Nchi haiwezi kuwa Tajiri Kama ndani yake inawatu wajinga wengi. Watu wasio na akili wakiwa wengi ndivyo nchi inavyozidi kuwa Masikini.

Mtu asiye na akili Hana tofauti na mnyama wa porini, ni Sawa na tumbili au ngedere anayeishi msituni ananyeshewa mvua na kuchomwa na Jua lakini anashindwa kujenga nyumba hata ya mbao Kwa sababu ya upeo mdogo wa Akili.

Wazungu walivyotuita Waafrika manyani kuna watu walifikiri walimaanisha maumbile yetu yanafanana na nyani Kama nawe ulifikiri hivyo basi nawe upo kundi la watu wajinga.
Wazungu walituita manyani mbali na ubaguzi wao lakini walituona akili zetu hazijaachana Sana na tumbili na nduguye ngedere.

Nyani au ngedere ukimpelekea Dhahabu au Almasi wala hataiona inatofauti na jiwe jingine. Kutokana na upeo mdogo wa Akili.

Sisi Watanzania wengi wetu tunaakili ndogo mno na hiyo ndio sababu Sisi sio matajiri. Na tutaendelea kuwa Vivi hivi Kwa Karne kadhaa zijazo.

Watanzania wengi ni Kama wanyama Kwa mambo mengi, kama unavyomuona ng'ombe basi ndivyo wengi wetu tulivyo.
Sio ajabu ukakuta watu kwenye makazi Yao kuna mavi au maji machafu waliyoyasababisha yamewazunguka, yananuka na nzi wamejaa lakini wao hawaoni Shida. Wanalala, wanakula hapohapo, na wanakunya na kukojoa hapohapo.
Hapo ati wanasubiri kiongozi aje awaambie wawe wasafi tena wengine ifikie hatua ya kupelekwa serikali za mitaa kisa anaambiwa asizibue chemba za mavi yake na familia yake, come on!

Sio ajabu jitu linakunya chooni labda cha umma alafu hali-flash uchafu wake. Hivi mtu huyo anatofauti ipi na Mnyama?

Mtu anajua kabisa ili aishi anatakiwa awe na chakula cha kutosha kinachomtosha yeye na familia yake, badala awe na ghala la kuhifadhi chakula kinachomtosha yeye na watoto wake angalau Kwa miaka miwili kulingana na Hali ya hewa.
Yeye anakula Kama mnyama asijue kesho atakula nini.
Alafu ikifika kesho anaanza kumlalamikia mtu mwingine labda ni serikali au viongozi. Jamani hivi tunaakili kweli?

Tena wakati mwingine tunazidiwa akili hata na Wanyama.
Hakuna mnyama ambaye atazaa watoto ambao hawezi Kuwatunza. Hakuna na hajawahi kutokea. Mfano Kuku anaouwezo wa kutaga mayai hata Mia moja.
Lakini atataga mayai kumi (10-12) kulingana na uwezo wake wakuyaatamia, sio atage mayai 20 alafu wakati wa kuatamia mengine ashindwe kuyaatamia yajitokeze nje.
Kisha Kwa mayai 10-12 anaouwezo wa kuwachunga na kuwakuza watoto hao
Halikadhalika na mbwa, ng"'ombe, mbuzi, Simba n.k.
Lakini Sisi unakuta mtu anazaa watoto nje ya uwezo wake wa Kuwatunza, labda watoto 10 alafu ananilaumu serikali kuwa gharama za Shule au hospitali ziondolewe.
Au anaomba msaada Kabisa wa kusaidiwa kulelewa watoto.
Hivi tumelogwa au ni kitu gani?

Mtu unajua kabisa miti ndio huleta hewa Safi, huleta mvua na kivuli kizuri, na Kupunguza joto la nchi. Alafu unakuta watu wamekata miti mtaa mzima ili wajenge nyumba.
Unashangaa mtaa mzima miti ipo 20 Kwa eneo la kilometa moja. Alafu muda huohuo unasikia mwehu akipiga kelele jamani joto Kali, jamani jua linawaka! Mara kiyama kinakaribia.
Kiama ya mavi. Ujinga na wehu wako ndio unaita Kiyama?

Utajiri WA nchi ni akili za watu na sio Rasilimali Kama madini.

Chakufanya;
I. Tujifunze kuwa na Akili ili tuwe nchi yetu itajirike.

Robert Heriel
Taikon wa Fasihi
Kwa sasa Dar es salaam
Pole sana Robert Heriel. Tulianza kutoka huko kielimu, kifikra na kiutendaji. Pia tukawa na wasomi maarufu duniani hata kwenye kiwango cha Chuo Kikuu waliokuwa wanatuelekeza namna ya kutoka huko ambako leo umeamua kusimilia. Tunarudi nyuma sababu uongozi umefutika! Shule mpaka kwenye ngazi ya Chuo Kikuu nchini ndiyo haipo ya kutosha. Cha kuanza nacho ni uongozi, mawazo, elimu na utendaji utakaotutoa Watanzania wengi kwenye hiyo tabia uliyoeleza. Suala siyo kwamba hakuna akili hapa Tanzania. Ila ni suala lile la mwana falsafa Socrates, je wenye akili wanaruhusiwa kuongoza, wako radhi kuongoza au wasio na akili ambao ni wengi wanaona wana akili kwa hiyo hawahitaji wenye akili? Tatizo ni huo mfumo unaolea tabia hiyo. Hapo ndipo tatizo lilipo. Pole sana naona umeandika kwa hasira. Lakini siyo peke yako na wala hii hoja yako haihusu Chama cho chote. Inahusu future ya Taifa letu. Tanzania iliongoza Afrika kwa fikra, sasa hata majirani tu wanatupiku!!! Lakini ukitusikia bado tunajisifuu!!!
 
Pole sana Robert Heriel. Tulianza kutoka huko kielimu, kifikra na kiutendaji. Pia tukawa na wasomi maarufu duniani hata kwenye kiwango cha Chuo Kikuu waliokuwa wanatuelekeza namna ya kutoka huko ambako leo umeamua kusimilia. Tunarudi nyuma sababu uongozi umefutika! Shule mpaka kwenye ngazi ya Chuo Kikuu nchini ndiyo haipo ya kutosha. Cha kuanza nacho ni uongozi, mawazo, elimu na utendaji utakaotutoa Watanzania wengi kwenye hiyo tabia uliyoeleza. Suala siyo kwamba hakuna akili hapa Tanzania. Ila ni suala lile la mwana falsafa Socrates, je wenye akili wanaruhusiwa kuongoza, wako radhi kuongoza au wasio na akili ambao ni wengi wanaona wana akili kwa hiyo hawahitaji wenye akili? Tatizo ni huo mfumo unaolea tabia hiyo. Hapo ndipo tatizo lilipo. Pole sana naona umeandika kwa hasira. Lakini siyo peke yako na wala hii hoja yako haihusu Chama cho chote. Inahusu future ya Taifa letu. Tanzania iliongoza Afrika kwa fikra, sasa hata majirani tu wanatupiku!!! Lakini ukitusikia bado tunajisifuu!!!

Mpaka sasa tumeshapigwa. Vita tumepoteza
 
Ukisikia mtu anakuambia Yeye ni Tajiri Kwa sababu nchi yake inamadini, maziwa na Mito, Ardhi yenye Rutuba, wanyama wa kuvutia, na mambo mengine lakini watu wake ni Hali zao za maisha ni duni jua mtu huyo hajui kufikiri vizuri, na pengine akawa mwendawazimu.

Maneno mazito haya yaliyokuwa yanarudiwa rudiwa ktk awamu ya tano ya uongozi wa CCM na kwenda mbali kuwa SISI NI NCHI TAJIRI


Huku nchi zingine wanatumia makaa ya mawe kupata nishati ya umeme au kugeuza jiwe la Mchuchuma kuwa engine ya motokari au mitambo ya kiwanda n.k sisi tunayaangalia mawe hayo au makaa ya mawe sana sana tukijitahidi tunapeleka malighafi hiyo nje ya nchi ili wenye akili wayageuze kuwa kitu kingine cha thamani au nishati.
 
Maneno mazito haya yaliyokuwa yanarudiwa rudiwa ktk awamu ya tano ya uongozi wa CCM na kwenda mbali kuwa SISI NI NCHI TAJIRI


Huku nchi zingine wanatumia makaa ya mawe kupata nishati ya umeme au kujeuza jiwe la Mchuchuma kuwa engine ya motokari au kiwanda sisi tunayaangalia mawe hayo au makaa ya mawe sana sana tukijitahidi tunapeleka malighafi hiyo nje ya nchi ili wenye akili wayageuze kuwa kitu kingine cha thamani au nishati.

Nchi yetu haikupaswa kuwa na changamoto za nishati Kama umeme maana vyanzo vyake kama Maji, upepo, jua, makao ya Mawe vyote yapo.

Hatukupaswa kuwa na shida ya maji. Yaani kila nyumba ilipaswa iwe na maji.
Barabara zote zilitakiwa zipambwe na Miti na maua mazuri huku maji yakitiririka kama urembo.

Mifumo ya umwagiliaji, Kwa wakulima ilikuwa muhimu kabla ya ununuzi WA madege yaliyogharimu mapesa mengi huku return yake ikiwa ni ndogo.

Angalau Jpm alipopatia ni miundombinu ya barabara na Reli pamoja na vituo vya usafiri,
Pamoja na Hospitali.

Uchumi wetu ili ukue itapasa serikali imulike sekta nyeti zinazogusa Raia wengi Kama kilimo, umeme na Maji.
 
Kwangu mimi tanzania ni Tajiri (rasilimali), lakini watanzania ni masikini. Hapa swali ni tufanyeje ili ku geuza utajiri wa nchi kuwa utajiri wa wananchi. Hapa ndio akili inapoingia.
Lakini pia hata kama ni masikini wa rasilimali ukiwa na akili unaweza ukajenga utajiri wa wananchi wako.
Hivyo cha msingi ni akili lakini utajiri wa rasilimali ukiwa na utajiri wa akili hukupaisha.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom