Je, Tanzania ni miongoni mwa nchi zenye laana ya rasilimali?

Yoda

JF-Expert Member
Jul 22, 2018
37,660
46,338
Laana ya rasilimali "resource curse" ni ile hali ya nchi zenye kuwa na rasilimali nyingi kuwa na maendeleo duni, ufisadi mkubwa, migogoro na demokrasia hafifu kutokana na wingi wa rasilimali ilizo nazo.Yani rasilimali walizo nazo inakuwa ndio kikwazo cha maendeleo yao kiuchumi na kisiasa.

Inasemekana katika baadhi ya maeneo ya dunia nchi ikishakuwa na rasilimali nyingi, raia wanakuwa wavivu kufanya maendeleo ya teknolojia yenye kutumia nguvu kubwa za akili, wanapenda kuagiza zaidi bidhaa za uchuuzi kuliko kutengeneza nchini mwao, wanaopenda kuishi kwa rushwa na urasimu wanakuwa wengi na pia migogoro ya aina mbalimbali inaongezeka sana hali inayodidimiza maendeleo.

Chukulia mfano wa nchi yetu
Ardhi, Tanzania ni nchi yenye ardhi kubwa sana lakini kila kona ya nchi kuna migogoro watu wanagombania ardhi.

Uchumi wa bidhaa, fremu na uchuuzi, Sehemu kubwa ya uchumi wetu ni biashara za kuchuuza bidhaa malighafi za kilimo, madini na za kutoka nje huko China. Sekta za teknolojia na viwanda ni duni sana.

Rushwa na ufisadi hilo wala halina ubishi, ni wimbo wa kila siku. Urasimu uliopitiliza nao ni tatizo kubwa kila mahali.
 
Uzuri wa biashara za uchuuzi nyingi huwazimeshalipiwa kodi huko awali, kuanzia zinapoingia nchini, "" quadro-taxation"", inaumiza sana wafanyabiashara wadogo!
-Rasilimali zilipaswa zipunguze mzigo wa kikodi kwa mtanzania huyu wa chini asiyetakiwa anyanyuke!
 
Tanzania ni nchi yenye rasilimali nyingi kama DRC,

Tofauti yetu na wao... Ni kwamba wao wanatumia Bunduki kupora Mali...

Sisi wanatumia tafsida...eti "mama anaupiga mwingi"(kumjaza kichwa) huku wakiendelea kuvuna rasilimali! Indirect
 
• Kwamba tumelaaniwa na wazungu, au tumelaaniwa na Waarabu 🤒🤒?
 
Tanzania ni nchi yenye rasilimali nyingi kama DRC,

Tofauti yetu na wao... Ni kwamba wao wanatumia Bunduki kupora Mali...

Sisi wanatumia tafsida...eti "mama anaupiga mwingi"(kumjaza kichwa) huku wakiendelea kuvuna rasilimali! Indirect
Hebu tutajieni hizo Rasilimali basi...Orodhosheni hata 7 tu, na wingi wake...
 
Tanzania ni nchi yenye rasilimali nyingi kama DRC,

Tofauti yetu na wao... Ni kwamba wao wanatumia Bunduki kupora Mali...

Sisi wanatumia tafsida...eti "mama anaupiga mwingi"(kumjaza kichwa) huku wakiendelea kuvuna rasilimali! Indirect
Kama D.R.C,,story za vijiweni au una ushahidi wa kuweka hapa...?
 
Hebu tupe orodha ya hizo Rasilimali...
Zitaje angalau 7.
Ndiyo mjadala utanoga.
NIGERIA, MSUMBIJI, ANGOLA, UGANDA, DRC, SUDAN, ETHIOPIA, EQUATORIAL GUINEA,SIERRA LEONE, ECUADOR, VENEZUELA,
 
Tunavyozidi kuwaacha walioshindwa kuzisimamia rasilimali zetu waendelee kuzisimamia, ndivyo tunavyozidi kujichimbia kaburi.
 
Tunavyozidi kuwaacha walioshindwa kuzisimamia rasilimali zetu waendelee kuzisimamia, ndivyo tunavyozidi kujichimbia kaburi.
Hiyo ndio sehemu ya laana yenyewe ya rasilimali inayozungumziwa, kwamba raia wa nchi wanakuwa hawawezi kufanya mambo yanayohitaji teknolojia na innovations badala yake wanajikita katika kuvuna na kutumia rasilimali zinazopatikana bila kuumiza sana kichwa, kwa hapo kwetu utaona raia wengi wanajikita shambani, kwenye utalii na madini, mabasi ya abiria n.k
 
Ardhi nzuri,
Madini
Mbuga za wanyama,
Bahari na bandari,
Mito na maziwa
Misitu,
Gesi,
1.Ardhi-Nchi nyingi wanayo hiyo.
2.Madini-madini yapi haswa?
3.Mbuga za wanyama:Kila nchi ina mbuga za wanyama.
4.Bahari-85% ya nchi ni zina hiyo
5.Mito na maziwa:Ni arabuni na Antarctica ndipo kuna ufinyu wa hivyo vitu.
6.Misitu - Angalia kidunia tupo nafasi ya ngapi..?
7.Gesi - Unajua kidunia hata 20 bora kwenye gesi hatumo...
 
Laana ya rasilimali "resource curse" ni ile hali ya nchi zenye kuwa na rasilimali nyingi kuwa na maendeleo duni, ufisadi mkubwa, migogoro na demokrasia hafifu kutokana na wingi wa rasilimali ilizo nazo.Yani rasilimali walizo nazo inakuwa ndio kikwazo cha maendeleo yao kiuchumi na kisiasa.

Inasemekana katika baadhi ya maeneo ya dunia nchi ikishakuwa na rasilimali nyingi, raia wanakuwa wavivu kufanya maendeleo ya teknolojia yenye kutumia nguvu kubwa za akili, wanapenda kuagiza zaidi bidhaa za uchuuzi kuliko kutengeneza nchini mwao, wanaopenda kuishi kwa rushwa na urasimu wanakuwa wengi na pia migogoro ya aina mbalimbali inaongezeka sana hali inayodidimiza maendeleo.

Chukulia mfano wa nchi yetu
Ardhi, Tanzania ni nchi yenye ardhi kubwa sana lakini kila kona ya nchi kuna migogoro watu wanagombania ardhi.

Uchumi wa bidhaa, fremu na uchuuzi, Sehemu kubwa ya uchumi wetu ni biashara za kuchuuza bidhaa malighafi za kilimo, madini na za kutoka nje huko China. Sekta za teknolojia na viwanda ni duni sana.

Rushwa na ufisadi hilo wala halina ubishi, ni wimbo wa kila siku. Urasimu uliopitiliza nao ni tatizo kubwa kila mahali.
Tanzania ni nchi iliyolaaniwa kwa kila kitu sio kilarasimali tu mkuu.
 
wenye laana kubwa ni ccm
Sisi wananchi ndiyo tuna laana. Tumekalia kwenye ushabiki wa mpira, dini na muziki wakati nchi inateketea. CCM ni mchwa wenye lengo la kula kila kilicho mbele yao. Mchwa wakishambilia nyumba yako, na wewe ukakaa kimya basi wewe ndiyo ulaumiwe. Wananchi tukiamua leo Ijumaa kuwa tunataka Jumatatu ijayo Samia na CCM wasiwepo tena madarakani tunaweza.
 
A.Ufaransa
1.Calanques National Park
2.Cévennes National Park
3.Guadeloupe National Park
4.Mercantour National Park
5.Pyrénées National Park
15% ya ardhi ni mbuga

B.Ujerumani
1.Schleswig-Holstein Wadden Sea National Park
2.Lower Saxon Wadden Sea National Park
3.Lower Oder Valley National Park
4.Saxon Switzerland National Park
5.Berchtesgaden National Park
-25% ya ardhi ni mbuga

C.U.K
1.Peak District
2.Snowdonia
3.Peak District
4.Dartmoor
5.New Forest

Hizo nchi tatu zinapokea watalii wengi kuliko nchi zote Afrika
-Hata nao wana wanyama ambao nasi hatuna
 
1.Ardhi-Nchi nyingi wanayo hiyo.
2.Madini-madini yapi haswa?
3.Mbuga za wanyama:Kila nchi ina mbuga za wanyama.
4.Bahari-85% ya nchi ni zina hiyo
5.Mito na maziwa:Ni arabuni na Antarctica ndipo kuna ufinyu wa hivyo vitu.
6.Misitu - Angalia kidunia tupo nafasi ya ngapi..?
7.Gesi - Unajua kidunia hata 20 bora kwenye gesi hatumo...
Dingilay Tanzania ina natural resources za kufa mtu. Hoja yako ya kwamba kila nchi ina hizo resources haina mashiko maana hoja ya mleta mada ni kuhusu "resouce curse".

Ipo mifano ya nchi nyingi ziliyopigwa na resource curse ikiwemo Tanzania.

Lakini pia zipo nchi nyingi zilizopiga hatua kwa kutumia hizo rasilimali za asili mfano Australia, Canada....

Ajabu ni kwamba zipo nchi zilizopiga hatua bila kuwepo na rasilimali za kutosha, Singapore, Japan....

Pia hauhitaji kuwa na rasilimali zaidi ya moja kupiga hatua za kimaendeleo. Mfano Tanzania kwenye uzalishaji wa Gold ni kati ya nchi za juu lakini hatujawahi kunufaika na hiyo gold wala tanzanite.

Kwa hivyo tatizo letu hasa ni uongozi usiojali maslahi ya wananchi. Fikiria kuhusu utajiri wa viongozi wetu! Waliopita na wa sasa.... Utakuta kiongozi ana mabilioni ya shilingi! Ameyatoa wapi? Kutumia rasilimali za nchi kwa maslahi binafsi.
 
Back
Top Bottom