Verily Verily
Senior Member
- Jan 4, 2007
- 192
- 148
Utajiri ni ile hali ya kumiliki mapesa mengi na kuwa na mali nyingi, utajiri ni mzuri kwa kuwa unakupa uwezo nguvu mamlaka sifa na umaarufu!kwa kifupi Utajiri ni kitu chema.
Watu wengi hutafuta utajiri kwa njia mbalimbali halali na haramu wao wanachotaka ni utajiri ili waweze kutimiza ndoto zao nyingi.
Sasa kuna wakati mtu hutafuta utajiri kwa njia za mkato hapa nazungumzia kwa njia za ushirikina na uchawi.
Utajiri huu ni mzuri na huja haraka lakini ukiwa na masharti mengi lakini kubwa likiwa ni kutoa kafara la damu kwa kuangamiza roho.
Unapoingia kwenye utajiri huu mwanzoni utafurahia na masharti utayaona mepesi lakini kadiri siku zinavyozidi kwenda mambo hubadilika na tabu huanzia hapo.
Mwanzoni utaambiwa toa kafara la damu ya kuku baadae itakuja mbuzi, halafu itafuatia ng'ombe na mwishowe itakuja binadamu mmoja na hatimaye kwa makundi.
Hii yote ni kutaka kulinda utajiri wako usiporomoke na ukivunja masharti kila kitu kinaharibika .
Kuna pia masharti ya kujisaidia kulala kula kuvaa na hata matumizi ya vitu mbalimbali. Mwanzoni inakuwa ni rahisi tu kwenda sambamba nayo lakini mbeleni mambo hubadilika hasa pale watu wanapoanza kuhoji hiki au kile.
Wote tunajua jamii ya watu wenye ulemavu wa ngozi inavyoteketea kutokana na waganga wa kienyeji kuwaaminisha wateja wao kuwa viungo hivyo vikichanganywa na dawa nyingine huleta utajiri bahati nguvu na uwezo! Kuna zaidi ya waganga 300 kwenye mahabusu na Magereza mbalimbali wenye kesi zinazowahusisha na mauaji ya albino.
Jamani utajiri wa masharti ya namna hii haufai na mwishowe huwa na anguko kuu tunashuhudia visa vya kila aina kuhusiana na utajiri wa namna hii lakini kila uchao watu hawakomi kuendelea kuutafuta.
Hakika dunia inaumwa.
Mshana Jr yani huu uzi wako ni kweli kabisa. Kuna tajiri fulani anamiliki mababasi ya Urio Arusha wanadai eti kapewa masharti awe analala chooni tu tena choo cha shimo. iyo ruti ya ngarenanyuki yeye ndie alikuwa anamiliki peke yake ukijifanya uingie iyo ruti utakiona. kuna jamaa alipeleka gari lake huko asubuhi akapakia akizan abiria mbele ya safari kuangalia nyuma wote walikuwa nyani wakamuambia dereva tunakusamehe kwa leo. nasikia wadau wanadai jamaa alijisahau cku moja akalala chumbani na kitandan alikula mkongoto mkali na wa haja kutoka kwa majini na mabas yake kuharibika na kupata pancha biashara ikayumba. lisemwalo lipo!
Senior Boss mila za kichaga usipofata ka ni ukoo lazma uangamie bila kupenda watu kuenda kinyume na miiko ya kikoo na familia bora hyo kuliko kutoa mikafara.
Halafu sijawahi ona albino Masai
Utajiri una madaraja na kila daraja lina kafara lake mfano
Milioni 20-50 ni tofauti na milioni 100-200 na kila daraja huhitaji kitu kikubwa zaidi au damu nyingi zaidi
Naelewa ila usijali nitajazia palipopelea ushirikina kwenye maisha yetu upo kila kona na watu wanauabudu sana wengine kwa kificho na wengine waziwazi kabisa
Aaaah bwana wewe acha ibishi bwana, wakinga wengi walipata utajiri kwa njia za majoka.... unajua nini kuhusu mwakipande
kisu kwenye mfupaumegonga mshana jr
kanda ya ziwa matajiri wengi ni shida,kuna ndugu wawili nawafahamu kabisa utajiri wao unamashaka kabisa ,kuna huyo mzee ni maarufu congo,rwanda na Burundi yote wanamtumia kwa mambo hayo.hii dhana ya utajiri wa kishirikina ipo sana watu wanajenga nyumba zao lazima wafukie vitu kibao eti kinga...watu wana mihirizi kibao kiunoni.
kisu kwenye mfupaumegonga mshana jr
kanda ya ziwa matajiri wengi ni shida,kuna ndugu wawili nawafahamu kabisa utajiri wao unamashaka kabisa ,kuna huyo mzee ni maarufu congo,rwanda na Burundi yote wanamtumia kwa mambo hayo.hii dhana ya utajiri wa kishirikina ipo sana watu wanajenga nyumba zao lazima wafukie vitu kibao eti kinga...watu wana mihirizi kibao kiunoni.
Mtaje uyo mzee na eneo analotoka nani anataka kuishi chini ya dola moko arifu
Thank you. Sijawahi ona wachagga tukifanya mila kwa nia mbaya kama ni hvyo watu wangepiga kelele sanaa.
Kuna watu nawajua wamekua wakiugua kwa muda mrefu sanaa, hangaika kote, maombi kwa sana na hospitali, toa hela kibao, wapii hamna nafuu. Wamerudi Moshi wamefanyiwa mila wamepona wanadunda mpaka kesho.
Ivi vitu watu wana dharau ila vipo. Usione mwanao anafanya vitu vya ajabu ajabu ukasema zezeta au ana kasoro flan. See beyond what u see or understand under normal circumstances.
kama hawaendeshi magari,hawali nyama,hawavai vizuri,hawendi vacation,hawa enjoy .hiyo pesa haina maana.mi nawaona ni masikini.siyo matajiri. Tajiri unaogopa kula nyama? Ha ha ha h..
Pole mkuu km ulikuwa hujui!.hakuna kitu km hicho,
Kuna utajiri wa halali na wa kishirikina
Nikweli kabisa senior boss wachaga mila ndio kila kitu na asiefata hupata shida sana
Kuna tofauti kubwa kati ya mila na uchawi. Mila za kichagga si uchawi bali ni ibada flan za Miungu ya asili.
Zina madhara kama ukoo wenu una practice alaf we uache. Kama unaacha shikilia imani yako thabiti kama uko nje ndani kwa uroho wa mbege na nyama utapata shida sanaa. Wengi hawajui asili ya nyumba zao ndio maana wanateseka na kila wanachofanya hakifanikiwi.
Mchagga anayejielewa hawezi acha kufanya mila. Not exactly kila mwisho wa mwaka but in any major event of ur life (pia si lazma kuangusha ng'ombe au mbuzi. Unaweza tumia mbege au maziwa kufanyia ibada/sala hyo na majani flan yaitwayo " Masale" au " Isale ". Inategemea)
Kuna Mti wake special (Isale) wa ukoo/familia unaoteshwa kwenye eneo maalum ya nyumba yenu ni hapo ndio mnapo fanyia sala/ibada fupi kabla ya kuchinja au kumwagia mbege/maziwa kiasi flan kwenye Ardhi nyingine mna inywa.
Binafsi nazipenda na kuziheshimu sana mila za wachaga
Kuna mfanya biashara mmoja (mchagga) mkubwa tu hapa Dar nampata...yuko makini sanaa ana utajiri wa ajabu (hayuko top 10 among the richest in Tz, maybe top 20 or 25).
Hela zake ni za mapaka live, kama una akili zilizotulia ni rahisi kumjua. Ndugu zake wengi wanakuambia jamaa sio kabisa. Washazika sana ndugu zao wakimlaumu jamaa. Kila baada ya muda flan anaanguka mtu ki utata sanaa uki connect the dots, with facts and good analysis unajua kabsa jamaa anahusika.
I'm chagga i kno my people well...Hizi issue zipo sanaaa. Nashindwaga elewa ki undani kuna mechanism gan kati ya kutoa ndugu na kupata utajiri. Whats the secret code behind ?? Ukiangalii juu juu utaona tu jamaa anajituma kwa bidii nd stuff like that. Ki uhalisia unakuta anaogopeka balaa.