Utajiri wa kishirikina unavyotesa wengi

Utajiri wa kishirikina unavyotesa wengi

mshana jr

Mimi nachojiulizaga hizo kafara huwa zina uhusiano gani na utajiri? yani ni process gani inafanya mtu apate hayo mahela baada ya kumuua ndugu/jamaa yake.
 
Last edited by a moderator:
Naona wasengenyaji mko kwenye kikao....hii dhana ni kazi sana kuiprove,inafanya watu wawe wavivu
Haya yote ni maneno ya mkosaji
 
Duu hili swala la utajiri usiokuwa na manufaa baadae huleta shida..
 
Naona wasengenyaji mko kwenye kikao....hii dhana ni kazi sana kuiprove,inafanya watu wawe wavivu
Haya yote ni maneno ya mkosaji

Think big mutisya mutambu hebu niambie hawa waganga zaidi ya 300 waliokamatwa yale waliyoyaongea unataka kuniambia walifundishwa? Au hamfuatilii habari kama hizi? Na wale ambao huwa mambo yakiwazidi huamua kusema yote nao ni waongo?
Mbona hizi habari zipo sana tu kwenye jamii? Kwanini tujilimit ufahamu wetu kwa kutojadili kitu kinachosemwa sana? Tena kikisemwa na baadhi ya wahanga wenyewe?
Huwa kuna shida ya watu kusoma kitu kwa papara na juu juu heading iko wazi kabisa inazungumzia utajiri wa kishirikina na si utajiri katika ujumla wake
 
Last edited by a moderator:
Najua kuna msalaba na tasbihi sasa huku kuvaa Mabangili,mapete makubwa sometimes mikono yote tena yenye tochi,namba 1111111(chale) ya nini kama sio ushirikina
Kiyoya hili jambo la kutafuta utajiri wa haraka limeitafuna jamii vibaya sana asilimia kubwa sana ya wafanyabiashara wanafanya haya mambo
Kuna hili kundi lingine ambalo watu hawalijui lakini nalo linafanya uchafu mwingi sana kwa maagizo ya waganga MAMA NTILIE NA WAUZA VYAKULA watu wanalishwa uchafu mwingi sana kwenye hii sekta epuka sana chakula cha mamantilie ambaye kamwe hali alichopika mwenyewe
Biashara ndogo nyingi kama saluni maduka ya nguo mafundi mbalimbali na hata kwenye mabar wote hawa ni mabingwa wa kwenda kwa waganga kusaka utajiri!tusivae miwani ya mbao wakati haya mambo yapo live kabisa kwenye jamii yetu
 
Last edited by a moderator:
Hayo mashart yakujisaidia naomba niyafaham mkuu
 
boss hiyo ni imani yako tu.
wakinga wanatafuta hela mahali popote na wanaishi maisha ya kujibana ndio maana wanakuwa na mali pale wanapozipata.
matumizi mabaya ya kile kidogo unachopata yanakufanya usifanikiwe hata kidogo.

mkinga asubuhi anakunywa chai nyumbani, mchana analetewa chakula kutoka nyumbani, jioni anaenda kula nyumbani kwa nini asiwe na hela?
dukani kwake yupo yeye na mkewe ndio wauzaji akiweka msaidizi basi ni ndugu yake.
kwani wangapi wameenda kwa waganga na bado biashara zikagoma/kuanguka?
siku zote hata kwa anayetegemea mshahara, matumizi mazuri ya anachopata ndio mafanikio yake.
sio mtu kila siku asubuhi anaamkia supu ya kuku, mchana nyama choma na jioni kitimoto na bia juu.
huyu hawezi kufanikiwa.

Pamoja na hayo lakn wakinga ni nouma nawajua vilivyo
 
Utajiri ni mmoja tu ndugu,hakuna wa ushirikina wala wa nini...umeshafatilia maaharti mengine wanayopewa hao watafuta utajiri kwa waganga,mwisho utakuta masharti hayo yanawarudisha kulekule kwenye kufanya kazi kwa bidii na si kwenda kulala miguu juu kusubiri hela zitoke hewani...waganga ni wajanja..hutakiwi kuamini wanachosema hata waseme wangapi
 
Utajiri ni mmoja tu ndugu,hakuna wa ushirikina wala wa nini...umeshafatilia maaharti mengine wanayopewa hao watafuta utajiri kwa waganga,mwisho utakuta masharti hayo yanawarudisha kulekule kwenye kufanya kazi kwa bidii na si kwenda kulala miguu juu kusubiri hela zitoke hewani...waganga ni wajanja..hutakiwi kuamini wanachosema hata waseme wangapi

Hapo tunaenda sawa sasa lakini kumbuka haya mambo yanaendelea sana tu kwenye jamii yetu
 
Duh,pori likivamiwa nawewe unahama mh,sasa mshana ile madayetu mbona haikuendelea(kunawatu hufa malambili))
 
Back
Top Bottom