Wakusoma 12
JF-Expert Member
- Jul 3, 2017
- 5,412
- 15,449
Mmiliki wa makampuni ya teknolojia ya SpaceX na Tesla, Elon Musk, anakaribia kuweka rekodi ya kuwa trilionea ambayo wa kwanza dunia kwa kufikia utajiri wa zaidi ya dola trilioni moja.
Kwa sasa Musk anamiliki hisa zenye thamani ya takribani dola bilioni 273 kupitia kampuni ya Tesla pekee. Lakini ikiwa thamani ya kampuni yake ya SpaceX itaendelea kupanda kama ambavyo wawekezaji wengi wanatarajia, utajiri wake unaweza kuongezeka kwa mamia ya mabilioni ya dola zaidi.
Umiliki wake kwa pamoja Tesla na SpaceX unaweza kufikisha thamani inayozidi dola trilioni 1.1. Hiyo ni sawa na dola bilioni 1,100 au dola milioni milioni 1.1.
Ni kiwango cha utajiri ambacho hakijawahi kufikiwa na mtu yeyote katika historia ya dunia. Lakini dola trilioni moja ni kiasi gani hasa? Huu ni mifano 7 kuonyesha ukubwa wa fedha hizo.
Lakini dola trilioni moja ni kiasi gani hasa?
Dola trilioni moja ni sawa na dola bilioni 1,000, unaweza kuitumia miaka zaidi ya 5,000.
Njia ya pili ya kuelewa kiasi hicho ni kuigawanya kwa watu wote duniani. Kwa sasa idadi ya watu duniani inakadiriwa kufikia takribani bilioni 8.3. Kama Musk ataamua na kugawa dola trilioni 1.1 kwa kila mtu duniani mpaka watoto, basi kila mtu angepata karibu dola 133.
Hiyo ni sawa na takribani shilingi za Tanzania 350,000 kwa kila mtu au karibu shilingi za Kenya 17,000 kwa kila mtu. Kwa familia ya watu watano au 6, mgao huo ungefikia karibu shilingi milioni 2 za Tanzania au karibu shilingi 90,000 za Kenya.
Na kama kila mmoja angeamua kutumia shilingi 100,000 za Tanzania kwa siku, fedha hizo zingemtosha kwa zaidi ya siku tatu mfululizo bila kufanya kazi yoyote.
Kwa sasa Musk anamiliki hisa zenye thamani ya takribani dola bilioni 273 kupitia kampuni ya Tesla pekee. Lakini ikiwa thamani ya kampuni yake ya SpaceX itaendelea kupanda kama ambavyo wawekezaji wengi wanatarajia, utajiri wake unaweza kuongezeka kwa mamia ya mabilioni ya dola zaidi.
Umiliki wake kwa pamoja Tesla na SpaceX unaweza kufikisha thamani inayozidi dola trilioni 1.1. Hiyo ni sawa na dola bilioni 1,100 au dola milioni milioni 1.1.
Ni kiwango cha utajiri ambacho hakijawahi kufikiwa na mtu yeyote katika historia ya dunia. Lakini dola trilioni moja ni kiasi gani hasa? Huu ni mifano 7 kuonyesha ukubwa wa fedha hizo.
Lakini dola trilioni moja ni kiasi gani hasa?
Dola trilioni moja ni sawa na dola bilioni 1,000, unaweza kuitumia miaka zaidi ya 5,000.
Njia ya pili ya kuelewa kiasi hicho ni kuigawanya kwa watu wote duniani. Kwa sasa idadi ya watu duniani inakadiriwa kufikia takribani bilioni 8.3. Kama Musk ataamua na kugawa dola trilioni 1.1 kwa kila mtu duniani mpaka watoto, basi kila mtu angepata karibu dola 133.
Hiyo ni sawa na takribani shilingi za Tanzania 350,000 kwa kila mtu au karibu shilingi za Kenya 17,000 kwa kila mtu. Kwa familia ya watu watano au 6, mgao huo ungefikia karibu shilingi milioni 2 za Tanzania au karibu shilingi 90,000 za Kenya.
Na kama kila mmoja angeamua kutumia shilingi 100,000 za Tanzania kwa siku, fedha hizo zingemtosha kwa zaidi ya siku tatu mfululizo bila kufanya kazi yoyote.