Utajiri wa kishirikina unavyotesa wengi

Utajiri wa kishirikina unavyotesa wengi

Ukianza kujihusisha na waganga wa kienyeji ujue hutoacha kuwategemea.... hutojitambua kuwa umefikia hatua mbaya......kibaya zaidi tunaingiza familia zetu matatani sasa au hata baadae kutokana na maagano yako kwa waganga kwa kujua au kutojua.

Utajiri au ulinzi wa kiganga mwisho wake ni mbaya na majuto shetani akiwa ameshahakikisha kakumaliza ndio akili zitakurudia na kuanza kuhaha kwa wachungaji kusubiri huruma ya Mungu ambayo anaitoa kwa mapenzi yake.
Tuwe makini na tupigane na maisha tukimtegemea Mungu pekee. Tuache tamaa zilizopitiliza hadi kugeuka kuwa chukizo kwa muumba wetu.
 
Duh,pori likivamiwa nawewe unahama mh,sasa mshana ile madayetu mbona haikuendelea(kunawatu hufa malambili))

Twende kule dagii naendelea mdogo mdogo
 
Last edited by a moderator:
Inawahusu hasa wale wenzetu wa kutoka wilaya ya Makete. Yaani Wakinga. Full mazingaombwe

Ila wangetoka kaskazini ndo matajiri halali wakitoka kusini sio halali toa evidence ya uchawi kwa Wakinga
 
Kiyoya hili jambo la kutafuta utajiri wa haraka limeitafuna jamii vibaya sana asilimia kubwa sana ya wafanyabiashara wanafanya haya mambo
Kuna hili kundi lingine ambalo watu hawalijui lakini nalo linafanya uchafu mwingi sana kwa maagizo ya waganga MAMA NTILIE NA WAUZA VYAKULA watu wanalishwa uchafu mwingi sana kwenye hii sekta epuka sana chakula cha mamantilie ambaye kamwe hali alichopika mwenyewe
Biashara ndogo nyingi kama saluni maduka ya nguo mafundi mbalimbali na hata kwenye mabar wote hawa ni mabingwa wa kwenda kwa waganga kusaka utajiri!tusivae miwani ya mbao wakati haya mambo yapo live kabisa kwenye jamii yetu
Kaka usisahau maofisini- tulia angalia mienendo ya watumishi walio wengi yaani ni ushirikina tupu tupu
 
Haswaaa lakini umeniacha na kiu ya kuendelea kufuatilia maelezo, umekatisha mada kwa mtazamo wangu.
 
Haswaaa lakini umeniacha na kiu ya kuendelea kufuatilia maelezo, umekatisha mada kwa mtazamo wangu.

Naelewa ila usijali nitajazia palipopelea ushirikina kwenye maisha yetu upo kila kona na watu wanauabudu sana wengine kwa kificho na wengine waziwazi kabisa
 
Kaka usisahau maofisini- tulia angalia mienendo ya watumishi walio wengi yaani ni ushirikina tupu tupu
Kiyoya hii kitu ni kila mahali mpaka kwenye ndoa na mahusiano hata kwenye dini zetu huwezi amini watu wanaroga sana tu,ila niliamua kuanza na kipengele kimoja kwanza cha utajiri .nitakuja na kingine cha dini ambacho najua nitapata upinzani mkubwa sana
 
Last edited by a moderator:
boss hiyo ni imani yako tu.
wakinga wanatafuta hela mahali popote na wanaishi maisha ya kujibana ndio maana wanakuwa na mali pale wanapozipata.
matumizi mabaya ya kile kidogo unachopata yanakufanya usifanikiwe hata kidogo.

mkinga asubuhi anakunywa chai nyumbani, mchana analetewa chakula kutoka nyumbani, jioni anaenda kula nyumbani kwa nini asiwe na hela?
dukani kwake yupo yeye na mkewe ndio wauzaji akiweka msaidizi basi ni ndugu yake.
kwani wangapi wameenda kwa waganga na bado biashara zikagoma/kuanguka?
siku zote hata kwa anayetegemea mshahara, matumizi mazuri ya anachopata ndio mafanikio yake.
sio mtu kila siku asubuhi anaamkia supu ya kuku, mchana nyama choma na jioni kitimoto na bia juu.
huyu hawezi kufanikiwa.

Aaaah bwana wewe acha ibishi bwana, wakinga wengi walipata utajiri kwa njia za majoka.... unajua nini kuhusu mwakipande
 
Mkuu nimeanza kuelewa kuna kitu unacho ila unakitoa taratiibu, bado naikumbuka ile mada yako ya juzi ya milango ya kuzimu ...anyway, i like it.
 
Utajiri una madaraja na kila daraja lina kafara lake mfano
Milioni 20-50 ni tofauti na milioni 100-200 na kila daraja huhitaji kitu kikubwa zaidi au damu nyingi zaidi

Mkuu mshana nielekeze niende huko nikaukwae huo utajiri
 
Ukianza kujihusisha na waganga wa kienyeji ujue hutoacha kuwategemea.... hutojitambua kuwa umefikia hatua mbaya......kibaya zaidi tunaingiza familia zetu matatani sasa au hata baadae kutokana na maagano yako kwa waganga kwa kujua au kutojua.

Utajiri au ulinzi wa kiganga mwisho wake ni mbaya na majuto shetani akiwa ameshahakikisha kakumaliza ndio akili zitakurudia na kuanza kuhaha kwa wachungaji kusubiri huruma ya Mungu ambayo anaitoa kwa mapenzi yake.
Tuwe makini na tupigane na maisha tukimtegemea Mungu pekee. Tuache tamaa zilizopitiliza hadi kugeuka kuwa chukizo kwa muumba wetu.

Hapo unapo yaandika haya una bonge la hirizi kwenye walleti
 
Back
Top Bottom