Utajiri wa gesi umepotelea wapi?

Utajiri wa gesi umepotelea wapi?

sir longo GAS YA MSIMBATI NI YA MUDA MREFU? UTAJIRI AMBAO ULIZUNGUMZWA NI WA GAS YA MSIMBATI NA NDIYO ULILETA VURUGU KULE MTWARA NA NDIYO UNAOZUNGUMZWA NA MLETA THREAD, NAHS WEWE NDYO HUFATILII MAMBO.
 
Hadi sasa ripoti zinaonesha 57 trillion cubic feet ambayo ni takribani 1.6 TRILLION Cubic Meters!

1. Gas sio story but it's real... ninachoona ni mitazamo tofauti kati ya JK na JPM. Wakati JK aliamini katika uchumi wa gas, JPM anaonekana kuamini katika uchumi wa madini (achana na porojo za viwanda).

2. Kwamba Gas imechukuliwa na Wachina ni propaganda tu za kisiasa! Kilichofanyika hadi sasa ni exploration tu... uchimbaji wa gas hujafanyika kabisa.

Na katika kufanya exploration, ni makampuni ya mafuta ya Ulaya na America ndiyo yalifanya hiyo kazi kwa pesa zao wenyewe.

There's no way mtu anaweza kutumia mabilioni ya shilingi kufanya exploration halafu agundue gas kisha ampe Mchina.

3. Uchimbaji wa gas, hususani inayopatikana kina kirefu ni very expensive! Industry ya oil na gas kwa ujumla wake ni very expensive! Angalia tu kile kiwanda ambacho kilikuwa ndio kiwe gas processing plant... kilikadiriwa kufikia gharama ya $30 Billion.

So, kwa mazingira ya sasa ambayo serikali haitabiriki itakuja na jambo gani, ni kama limefanya investors wanarudi nyuma kusikilizia! Na wala sioni kama ni top priority ya JPM ukilinganisha na anavyohangaika na madini!
Umaekula like yangu mkuu, bila kujali ukweli wa takwimu ulizonazo,umeandika kiadilifu bila ushabiki wala povu..
 
yawezekana hufuatilii masuala ya nchi yako, ila umeendekeza siasa. gesi haijaanza kuchimbwa, ila mchakato unaendelea na sasa mazungumzo ya kujenga NLG plant mkoani lindi kwa makampun washirika na serikali unaendelea. mchakato wa gesi is not an overnight event, it is a process, inapitia procedures mbalimbali. ges inayotumika sasa ni ya mda mrefu kutoka msimbati na songosongo, na ndio inayosafirishwa kwa bomba hadi dar es salaam. kama hujui jambo ni vema ukatafuta taarifa sahihi kuliko kubwabwaja tu mitandaoni
Hahaha yani wewe hukuona swali kwenye kichwa cha habari yake au umeamua tu kutoliona ili umshutumu?! Yeye nimeona ameuliza swali tena liko bolded.
 
Serikali laghai huwa hazina mipango madhubuti inayoeleweka zaidi ya blah blah zenye kulaghai wananchi wake kwenye majukwaa ya kisiasa
Word. Wamakonde walimwagiwa sana maji ya kuwasha na kupigwa mabomu na risasi, kisa wasizuie uwekezaji wa wazungu. Leo kimyaaaaa. Na mgao wa umeme uko pale pale, ilhali tuliambiwa gesi ikiingia nchini basi mgao wa umeme ungekua historia.
 
Miaka kadhaa iliyopita tulipewa taarifa ya ugunduzi wa ma million cubic ya ujazo ya gesi asilia, na moja kwa moja viongozi wa nchi wakatuambia sasa umasikini ndo bye bye. Wimbo maarufu ulikua uchumi wa gesi, huku mahubiri ya kisiasa yakichagizwa na matumaini kwa watanzania kuwa wakati wetu wa kuuaga umasikini umewadia.

Nani asiyemkumbuka Prof. Muhongo alivyosimamia mahubiri haya, lakini pia serikali ya CCM ilivyofikia hadi hatua ya kupeleka Polisi na Jeshi kudhibiti watu kule Kusini ili uchimbaji wa gesi ufanikiwe. Ziara zikafanyika nchini Algeria na Urusi ili kupata uzoefu wa kuendesha uchumi wa gesi.

Cha kushangaza, hakuna tena anayeongelea kuhusu uchumi wa gesi wala kuuaga umasikini kupitia uchumi wa gesi.

Huu utajiri wa gesi umepotelea wapi hivi?
Hilo nalo lilipita kama la Dr. shika
 
Extraction ya hiyo gas si mchezo. Inataka technolojia ya kueleweka
 
gesi ya msimbati ni ya kitambo, lkn manufaa ya kuisafirisha kwa bomba had dar, yameanza kuonekana, kwa sasa asilimia kubwa ya umeme ktk grid ya taifa ni wa maji na gas. tumeshaanza kuachana na umeme wa mafuta(iptl...) ambao ni ghali zaidi. ila gas iligunduliwa miaka ya 2005 ambayo iliyo nyingi ipo onshore. mikakati ya kuichimba na kujenga NLG plant inaendelea. maendeleo ni process ndugu zangu.
 
Mleta uzi anasahau mswaada ulipitishwa usiku wa manane, wapinzani hawahawa wakiwa wamefukuzwa ukumbini na spika. Ile ilikuwa kuiuza gas hiyo kwa mikataba sawa na ya madini mengine. WaTz hatuna wa kumlaumu tujilaumu wenyewe kwa kuendekeza uongozi huu wa CCM.
Halafu unakuta spika huyo huyo naye anaunda tume kuchunguza madini ya almasi mwadui,nchi hii haiishi maigizo.
 
Miaka kadhaa iliyopita tulipewa taarifa ya ugunduzi wa ma million cubic ya ujazo ya gesi asilia, na moja kwa moja viongozi wa nchi wakatuambia sasa umasikini ndo bye bye. Wimbo maarufu ulikua uchumi wa gesi, huku mahubiri ya kisiasa yakichagizwa na matumaini kwa watanzania kuwa wakati wetu wa kuuaga umasikini umewadia.

Nani asiyemkumbuka Prof. Muhongo alivyosimamia mahubiri haya, lakini pia serikali ya CCM ilivyofikia hadi hatua ya kupeleka Polisi na Jeshi kudhibiti watu kule Kusini ili uchimbaji wa gesi ufanikiwe. Ziara zikafanyika nchini Algeria na Urusi ili kupata uzoefu wa kuendesha uchumi wa gesi.

Cha kushangaza, hakuna tena anayeongelea kuhusu uchumi wa gesi wala kuuaga umasikini kupitia uchumi wa gesi.

Huu utajiri wa gesi umepotelea wapi hivi?
Ndio uelewe kwa nini tunaitwa Wadanganyika.
 
yawezekana hufuatilii masuala ya nchi yako, ila umeendekeza siasa. gesi haijaanza kuchimbwa, ila mchakato unaendelea na sasa mazungumzo ya kujenga NLG plant mkoani lindi kwa makampun washirika na serikali unaendelea. mchakato wa gesi is not an overnight event, it is a process, inapitia procedures mbalimbali. ges inayotumika sasa ni ya mda mrefu kutoka msimbati na songosongo, na ndio inayosafirishwa kwa bomba hadi dar es salaam. kama hujui jambo ni vema ukatafuta taarifa sahihi kuliko kubwabwaja tu mitandaoni
Lakini si nyie ndio mlikuja kwa mbwembwe zote sasa povu la nini unatoa?
 
Mkuu hao wapinzani wataongelea wapi wakati mikutano ya siasa imepigwa ban?
Serikali ya viwanda ndo yunakomaa nayo. Acheni siasa ati..

Kuna nafasi kwenye huu uchaguzi, pia kwenye vipindi mbalimbali vya TV nk.Na huku kwenye mitandao ya kijamii ndio unajimwaga upendavyo. Najua sio rahisi lakini inawezekana.
 
Achana na mambo ya ajabu ajabu ya uchumi wa gesi...kwa sasa tuko kwenye uchumi wa viwanda...mambo ya gesi yashakuwa zilipendwa.
Umenichekesha sana. Kwa kweli watu wanajua kucheza na vichwa vya Watanzania.
 
sir longo GAS YA MSIMBATI NI YA MUDA MREFU? UTAJIRI AMBAO ULIZUNGUMZWA NI WA GAS YA MSIMBATI NA NDIYO ULILETA VURUGU KULE MTWARA NA NDIYO UNAOZUNGUMZWA NA MLETA THREAD, NAHS WEWE NDYO HUFATILII MAMBO.
NI kweli, gas ambayo ilileta vurugu kule Mtwara ni gas ya Msimbati. HATA HIVYO, utajiri wa gas inayozungumzwa sio gas ya Msimbati! Gas ya Msimbati ni ya kawaida sana.

Gas ambayo Muhongo alikuwa anataka kutoana macho na akina Mengi ipo deep sea na kiasi kikubwa kimegundulika mkoani Lindi.
 
Hilo nalo lilipita kama la Dr. shika
Extraction sio tatizo kwa sababu makampuni yenye uzoefu na hizo shughuli ndiyo yalikuwa yanafana na imeshafanyika kwa kiasi kikubwa.

Issue ni kwamba, inaonekana gas sio kipaumbele cha JPM kama ilivyokuwa kwa JK.
 
Nakumbuka tuliambiwa uneme kukatika itakua mwiko! Dah ni bora kufikiri kwa nn kwa namna yoyote ukimrusha juu paka mkubwa lazima atatua chini kwa miguu kuliko kukumbuka ahadi kama hzo
 
Back
Top Bottom