Utajiri wa gesi umepotelea wapi?

Utajiri wa gesi umepotelea wapi?

miaka kadhaa iliyopita tulipewa taarifa ya ugunduzi wa ma million cubic ya ujazo ya GAS asilia, na moja kwa moja viongozi wa nchi wakatwambia sasa umaskini ndo bye bye. Wimbo maarufu ulikua UCHUMI WA GAS, huku mahubiri ya kisiasa yakichagizwa na matumaini kwa watanzania kuwa wakati wetu wa kuuaga umaskini umewadia.

Nani asiyemkumbuka Prof Muhongo alivyosimamia mahubiri haya, lakini pia serikali ya CCM ilivyofikia hadi hatua ya kupeleka POLIS na JESHI kudhibiti watu kule kusini ili uchimbaji wa GAS ufanikiwe. Ziara zikafanyika nchini Algeria na URUSI ili kupata uzoefu wa kuendesha uchumi wa gas

CHA KUSHANGAZA, hakuna tena anayeongelea kuhusu UCHUMI WA GAS wala kuuaga umaskini kupitia UCHUMI WA GAS.
HUU UTAJILI WA GAS umepotelea wapi hivi??
Bei za dunia za mafuta na gesi kwa sasa haziruhusu uwekezaji mkubwa
 
Uchumi wa gesi,umepotea kama makinikia,ni mwendelezo tu,wa madudu kibao ya ccm.
Mkukuta,mkurabita,memkwa,kilimo kwanza,
Watuambie tangu gesi imeanza kuvunwa,tumepata Tirioni ngapi,sekta gani imepata nafuu,
Somesheni basi hata wadogo zetu vyuoni,bodi ya mikopo IPO hoi,kazi kuvamia ofisi za watu kama majembe auction mart,
Mwaka Jana,walipokea michango ya malipo ya mkopo,Leo wanafika,kampuni,inawafanyakazi watatu,wanauliza,wanaambiwa,tumewapunguzwa,wanatoa macho
 
Mleta Uzi Asante kwa kuwakumbusha watanganyika ndo maana Nkapa aliwaita watu malofa mtu kipindi yupi madarakani ameuza Nchi na bado anadaunda anawaita watu malofa turudi kwenye Gas nachokijua viongozi wa Tanzania hawajawai kuwaeshimu wananchi na wanachi Wa Tanzania wajinga
 
Kabla ya gesi walisema pia mkonge wa mawasiliano ukishakamilia,gharama za mawasiliano zitakuwa ndogo......leo hii mkonge ulikamilika na gharama bado ni kubwa

Umesahau pia analogy to digital television, tuliambiwa itakuwa cheep, free 5 channels, but what happened, lazima utoe pesa kwa kila channel.
 
Mkuu hizi ndio hoja wapinzani wanapaswa kupanda nazo majukwaani kuonyesha umma kwamba wanahadaiwa. Hili la uchumi wa gas likipata mtu mzuri wakati wa hizi kampeni dakika 5 tu kila mkutano litawafanya ccm kupanda jukwaani kujitetea na sio kuuzia wananchi maendeleo Kiduchu/hewa. Akipatikana mpinzani mwingine, anasifia kidogo ujenzi wa SGR ili kuchota akili za wananchi, kisha anakandamiza maelezo ya kina yatolewe kwanini reli zilizoko zimedondoka mpaka kufanya chini ya ufanisi, na matatizo hayo hayatoikumba reli hii mpya? Kuna mambo mengi wapinzani wanaweza kuifanyia damage serekali ya ccm bila kuingia kwenye mikwaruzano isiyo na sababu.

Awamu hii hata ukizungumzia Gas utaitwa mchochezi unawachonganisha wananchi na serikali hila uchochezi mkubwa amabao serikali aijuona kukamata wapinzani kuwafungulia kesi na kuwanyima dhamana siku wanachi wakisema inatosha
 
Wenye maujuzi ya hayo mambo sasa tunafugia kuku tuu tulisha kosea maisha ‍♂️‍♂️
 
miaka kadhaa iliyopita tulipewa taarifa ya ugunduzi wa ma million cubic ya ujazo ya GAS asilia, na moja kwa moja viongozi wa nchi wakatwambia sasa umaskini ndo bye bye. Wimbo maarufu ulikua UCHUMI WA GAS, huku mahubiri ya kisiasa yakichagizwa na matumaini kwa watanzania kuwa wakati wetu wa kuuaga umaskini umewadia.

Nani asiyemkumbuka Prof Muhongo alivyosimamia mahubiri haya, lakini pia serikali ya CCM ilivyofikia hadi hatua ya kupeleka POLIS na JESHI kudhibiti watu kule kusini ili uchimbaji wa GAS ufanikiwe. Ziara zikafanyika nchini Algeria na URUSI ili kupata uzoefu wa kuendesha uchumi wa gas

CHA KUSHANGAZA, hakuna tena anayeongelea kuhusu UCHUMI WA GAS wala kuuaga umaskini kupitia UCHUMI WA GAS.
HUU UTAJILI WA GAS umepotelea wapi hivi??
NIVYEMA KUULIZA .. KWELI GAS GESI GESI ... KIMYAAAA. WHY? TUNGEPENDA KUJUA TUMEFIKIA WAPI NA PIA KUHUSU MAKAA YA MAWE.. AHSANTE WAHUSIKA
 
Nahisi waliotaka kuwekeza kwenye gesi wameshutukia sharia na sera sizizo rafiki kwao wenye mapesa katika uwekezaji wa aina hiyo nchini TZ.
 
Tatizo ni ujuaji uchwara wa hao waliojifanya washauri kumbe hawakuwahi hata kufanya kazi za uchimbaji wa gesi na mafuta.Walifikiri its business as usual kumbe wamepanda mwamba.
Sasa wamekwama kwa sababu hawana exposure wamegeuka bubu.
Hawajui kufanya speculation ya kitaalamu bali wanafikiri ukubwa wa ofisi zao ndio ukubwa wa akili.Pole sana hadi hapo ita SOS.
 
Tatizo ni ujuaji uchwara wa hao waliojifanya washauri kumbe hawakuwahi hata kufanya kazi za uchimbaji wa gesi na mafuta.Walifikiri its business as usual kumbe wamepanda mwamba.
Sasa wamekwama kwa sababu hawana exposure wamegeuka bubu.
Hawajui kufanya speculation ya kitaalamu bali wanafikiri ukubwa wa ofisi zao ndio ukubwa wa akili.Pole sana hadi hapo ita SOS.
Unapiga domo apa wakati ndani kwako kuna vimitungi vya gesi acheni lawama kachimbeni nyie basi.
 
Back
Top Bottom