Safi sana mkuu, maelezo yako yamejitosheleza. Nimelizungumzia mara nyingi suala hili humu lakini inaonekana wengi hawana ufahamu sahihi juu ya suala la gas ya mtwara ikiwa ni kwa kutofuatilia taarifa mbalimbali zihusuzo nchi yao au wadau kutotoa elimu ya nini kinachoendelea hadi sasa kwa gas ya mtwara.
Kama ambavyo umeandika hapo juu, mkuu wa nchi inaonyesha alichotilia mkazo kwa sasa ni madini tena sana sana ni dhahabu pekee labda na tanzanite kidogo. Viwanda kiukweli bado sijaona ameweka mkazo sana. Endapo angekuwa "serious" na kuchukulia kwa "uzito" kama alivyofanya kwenye sgr, dhahabu, stieglers gorge (ingawa sijui tuta-finance vipi kwa billions of USD) basi tungeshapiga hatua fulani.
Tukirudi kwenye gas ya mtwara, kuwekeza trillions almost 70 za Tanzania si jambo la kukurupuka tu. Kuna vitu vingi lazima mwekezaji aangalie hasa kwenye kodi. Mara nyingi huwa wanapenda kupewa incentives fulani(ambazo zinaweza kuwa za kinyonyaji pia) ili warudishe haraka invested capital na kuanza tengeneza faida. Sasa nadhani wameona kwa sera za kodi za utawala huu ni bora kwanza wasubiri.
Hali hii pia ndio iliyoikumba chuma cha liganga na makaa ya mawe ya mchuchuma vitu ambavyo ni msingi mzuri wa heavy industries lakini mkuu huku ni kama vile hakuoni.