GE2010 Utafiti wa TCIB: Dk. Slaa aongoza

GE2010 Utafiti wa TCIB: Dk. Slaa aongoza

Mitandao yote ya internet inaonesha Dr Slaa mshindi mpaka ile ya serikali na CCM, na huu pia ambao sio wa internet, sasa REDET na Synovate ndio wanatoa picha halisi ya upepo wa ushindi wa JK kweli?
 
MS naye atakuja na tamko.

Lakini sasa sijui watasema nini kwa maana hizi sasa siyo za mtandao tena!!
 
Angalau, matokeo haya yanakaribia na ukweli na hali halisi ya kisiasa. Hata kama kutakuwa na tofauti haitakuwa zaidi ya 5%
 
Alafu Makamba anamfananisha Dr genuine na Mrema wa enzi zile.
Tafiti na polls zinatupa amajibu
 
Jamani, hebu hii taarifa ingesomwa wananchi wakasikia, kwani hao wengine ni pganda tupu
 
Kazi ipo.
Kila taasisi inakuja na utafiti wake
 
habari njema kwa wanademokrasia kakini!......ccm walishafulia kila mtu anajua
+
 
Sikiliza taarifa za leo; maana jamaa kaongea na waandishi wa habari labda habari zichakachuliwe na News house.

My Take: Wasomi wa kitanzania tuwe na aina mbali mbali za utafiki kuondoa gap hili ambalolina madhara sana; matokeo yake tunamtegemea mchumia tumbo Rwekaza
 
naiona hii kuwa ya ukweli zaidi,ila kwenye kutangaza matokeo watakosea na kumtangaza JK
 
At least kuna wanaoweza kutoa tafiti za kuaminika. Hali halisi inajionyesha every body is tired of CCM and JK.
 
Habari mbaya sana kwa kikwete na mafisadi wake..........hapo ccm na mafisadi watafungulia mihela ya epa kununua watu....tumejiandaa kuwadhibiti....jamani mijihela chukueni ila kura km kawa kwa chadema na dr.slaa
 
haya ule wakati uliokuwa ukisubiriwa ndo huu, people powerrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrr
 
Mkuu,

Hapo umepewa tu kwa ufupi. Riport kama hizi huwa ni ndefu sana kwani wanaweka wastani kwa wato wote kwanza na hapo wanakuja kuanza kuweka wastani katika makundi madogomadogo kwa mfano:

1. CCM watakaomchagua Slaa.
2. Akina mama wote au makundi yake.
3. Wastani kwa watu wote wanaoweza kupiga kura.
4. Wastani kwa watoto chini ya umri wa kupiga kura (hapa zaidi utajua Wazazi wako upande gani).
5. Wastani kwa Wasomi na wasiosoma, Wakulima na wafanyakazi / Wanafunzi, Wamjini na wavijijini nk.

Itakuwa heri kufanya subira ili kuuona riport nzima maana sidhani hao watoto wa chini ya darasa la saba nao watakuwa wamehesabiwa kwenye idadi ya mwisho ya Wapiga kura. Nyingine zipo zaidi ili kujua mwenendo wa kisiasa kwa watoto (inaleta picha halisi kujua wazazi wako upande gani maana mara nyingi wazazi wanawa-influence watoto).

hapo kwenye red kuna tatizo. ni vyema utafiti ufanywe kwa wale watakaopiga kura na si kuchanganya na watoto wa shule za msingi

na inaonekana hiyo sio random sampling
 
REDET na SYNOVATE walishaamua kutofanya tafiti this tyme ili wasimuangushe jamaa yao. lakini nahisi waliposikia kuwa TCIB wanafanya tafiti. basi jamaa wakakurupuka na kuanza kuembaras umma kwa tafiti yao isiyofanyika na kumbe TCIB wamekuja na majibu ya hali halisi.

Sasa tuwasubiri akina rwekaza wakiikandia ripoti hii ya TCIB maana yao ilikandwa na wasomi kama wao.

Jamaa wa TCIB wametumia vigezo murua ktk kutafiti na kuwakilisha.

Nilichofurahi ni kuona kwa mara ya kwanza wanaCHADEMA KIMSINGI WANAKUBALI matokeo ya tafiti japokuwa idadi ya washirikishwa ni 3047. Hii ni tofauti ya watu 1000 tu ukilinganisha na tafiti za REDET na SYNOVATE.

Sasa kumbe kuuliza watu 3000 katika tafiti za uchaguzi huu nu RUKSA. Basi tafiti zijazo REDET na SYNOVATE watauliza watu 4000.
 
Namsikitikia sana huyu dokata wa mezani or dr jakaya)(aka mzee yusufu wa mipasho),yaani kachoka natamani leo hii election ifanyike tuone hao REDET na SYOVET watasemea media ganikwenye huo utafiti wao wamechoka hao,eh mungu muumba wa mbingu na nchi,vinavyoonekana na visivyoonekana tunakuomba umjalie dr slaa wa ukweli (phd) umpe utukufu wako km ulivyompa Abraham kwa uzao wake aijaze dunia km nyota angani,dr slaa ndie rais wetu atakaye tukomboa wanyonge kutupa maendeleo mengi km nyota angani.
 
na hapa bado hawajataja Mwanza, Kagera na Mara. Yote hiyo iko kwenye column ya Dr. Slaa
 
Poor sampling mechanism. Tanzania ina mikoa 26... Matokeo ya mikoa 15 tu haitoshi kukupa picha kamili ya nani anapendwa, nani hapendwi Tanzania.
Aidha Dr. Vicent Leyaro amesema washiriki katika kura hii ya maoni ni 3047 wenye wasifu wa aina mbalimbali ikiwa ni pamoja na watoto chini ya darasa la saba, elimu ya sekondari na elimu iliyo juu ya sekondari ambapo katika utafiti huo silimia kubwa ya vijana wamonekana kuunga mkono mgombea urais wa CHADEMA Wllbrod Slaa na asilimia kubwa ya wazee wameonyesha kumuunga mkono mgombea urais wa CCM Jakaya Kikwete.

Siku nyingine wafanye utafiti kwa watu wenye sifa ya kupiga kura tu. Ukisema nani anapendwa hapa hata kwa watoto wa chekechea pia watakwambia watu wao. Wapiga kura ni wale wenye umri zaidi ya miaka 18 tu. Primary... kindergaten... chekechea... vidudu... sijui nini.. hawatakiwi ktk kura.

Utafiti huo sio realistic...

Nawakilisha Oktoba 31
 
Back
Top Bottom