Utachukua uamuzi gani ukigundua watoto uliowalea na kuamini ni wako kumbe sio wako?

watoto wenyewe ni kaka zake au dada zake na mtoto wako uliyezaa na mwanamke huyo. hilo nalo ni la kuzingatia. mimi watoto wa mama tulionyonya ziwa moja hata kama wasingekuwa wa baba yangu, sioni tofauti yeyote, ni wenzangu na nisingependa mtu yeyote hata baba awatose. connection hiyo ipo, anayewanyanyasa au kuwatosa ananikwaza na mimi pia.
Umeoa?
 
ndoa yangu muda si mrefu itatimiza 20
Mwenzio ana miaka 12 analea mapacha wasio wake huku mkewe akijua na kala buyu hii Mfalme baada ya kuingia nyumba ya mtumishi wake ambae alikuwa vitani na mwanamke akashika mimba na daud akataka atengeneze kama huu yaan mume atoke vitani aje alale na mkewe ili mimba ihesabike na ya mume lkn bado Mungu alimuua mtoto yule
basi kwa kuwa liko kwa njitap tuliache hivyo hivyo.
 
Mwenzio ana miaka 12 analea mapacha wasio wake huku mkewe akijua na kala buyu hii Mfalme baada ya kuingia nyumba ya mtumishi wake ambae alikuwa vitani na mwanamke akashika mimba na daud akataka atengeneze kama huu yaan mume atoke vitani aje alale na mkewe ili mimba ihesabike na ya mume lkn bado Mungu alimuua mtoto yule
basi kwa kuwa liko kwa njitap tuliache hivyo hivyo.
kwa huyu ni tofauti, mwanamke wake huyu alikuwa na ndoa yake, kwake alikuja akiwa ameachika kwa bwanake, na kuna uwezekano kama ni hivyo alikuwa anamwacha mume asiye na pesa aje kwa huyu mwenye pesa. huko alikotoka alikuwa analala kitanda kimoja na ex wake, ndio wewe ukamwambia aje. unategemea atakuja bila mbegu ya ex wake? kwa akili ya kawaida tu? ukipora mke wa mtu mfano tu, akaja kuzaa mtoto wa yule uliyempora, utamlaumu mwanamke? kuna wanaume wengine huwa wanakubaliana hata kulea mimba ya mwingine huko alikotoka as long as anampata huyo mwanamke. yeye hakuona wanawake woote hadi achukue aliyeachika? au kwasababu miaka 12 iliyopita alikuwa mzuri sana? that was something at his own risk.
 
Kwanini Mungu asisamehe tu kwa kuwa si mwingi wa hasira ana upendo mwingi?
Mungu aliandaa Jehanum kwa ajili ya kwenda kuwaunguza shetani na 1/3 ya malaika walioasi, lakini shetani kwa kuona hapendi kwenda peke yake, akaamua kuwashawishi wanadamu ambao Mungu aliwaumba wamwabudu ili nao waasi, wakaungue nao moto. hivyo wanadamu wote watakaofuata mambo ya sheteni, wameasi Mungu na wataadhibiwa pamoja na shetani jehanum.

1YOHANA 3 INASEMA:
1 Tazameni, ni pendo la namna gani alilotupa Baba, kwamba tuitwe wana wa Mungu; na ndivyo tulivyo. Kwa sababu hii ulimwengu haututambui, kwa kuwa haukumtambua yeye. 2 Wapenzi, sasa tu wana wa Mungu, wala haijadhihirika bado tutakavyokuwa; lakini twajua ya kuwa atakapodhihirishwa, tutafanana naye; kwa maana tutamwona kama alivyo. 3 Na kila mwenye matumaini haya katika yeye hujitakasa, kama yeye alivyo mtakatifu. 4 Kila atendaye dhambi, afanya uasi; kwa kuwa dhambi ni uasi.

5 Nanyi mnajua ya kuwa yeye alidhihirishwa, ili aziondoe dhambi; na dhambi haimo ndani yake. 6 Kila akaaye ndani yake hatendi dhambi; kila atendaye dhambi hakumwona yeye, wala hakumtambua. 7 Watoto wadogo, mtu na asiwadanganye; atendaye haki yuna haki, kama yeye alivyo na haki; 8 atendaye dhambi ni wa Ibilisi; kwa kuwa Ibilisi hutenda dhambi tangu mwanzo. Kwa kusudi hili Mwana wa Mungu alidhihirishwa, ili azivunje kazi za Ibilisi. 9 Kila mtu aliyezaliwa na Mungu hatendi dhambi, kwa sababu uzao wake wakaa ndani yake; wala hawezi kutenda dhambi kwa sababu amezaliwa kutokana na Mungu. 10 Katika hili watoto wa Mungu ni dhahiri, na watoto wa Ibilisi nao. Mtu ye yote asiyetenda haki hatokani na Mungu, wala yeye asiyempenda ndugu yake.

NIMEPENDA HAPO MWISHONI, anaposema watoto wa Mungu ni dhahidi, na wale wa ibilisi ni dhahidi. huhitaji kuuliza. yule anayehubiri kuua wasio wa dini yake hampendi ndugu yake, mweke wewe mwenyewe kwenye kundi analostahili. ila jueni dhambi ni uasi. na waasi wataenda kweney moto alioandaliwa muasi ibilisi shetani.
 
Kwanini Mungu asisamehe tu kwa kuwa si mwingi wa hasira ana upendo mwingi?
Mungu anasamehe wanadamu, na alikuja kwa njia ya mwili ili atoe kafara la damu ya kimwili kabisa, Damu ya Yesu Kristo. hiyo ilikuwa baada ya kuona shetani amefanay wanadamu wameasi, Mungu hataki wanadamu waende jehanum, akaweka njia, ya kwamba wote waliotenda dhambi wakitubu kwa njia ya kafara la Damu ya Yesu Kristo, kwa kumaanisha kuacha dhambi (sio kufanya masihara) Mungu atawasamehe na kufuta kabisa dhambi zao na hawataenda motoni.

unachotakiwa kuelewa ni kwamba, shetani amekwisha kuhukumiwa, hawezi kutubu tena kwasababu ameshaandaliwa na adhabu kabisa, mwanadamu hajahukumiwa, bado ana nafasi ya kutubu na kutengeneza mambo yake na Mungu. ipo siku ambayo Mungu ameiweka kwa ajili ya kuihukumu dunia ili wenye dhambi waende wakaungane na shetani motoni na watakatifu waende uzima wa milele. matatizo yote haya ameyalesa shetani, kuharibu uzao wa Mungu, na Mungu ametoa neema bure, kutubu tu, hakuna kulipa garama yeyote, hakuna kulipa garama ya ngo'ombe au chochote, ni kupiga magoti na kutubu na kuamua kukabidhi maisha yako kwa Yesu (kuokoka) ili akuongoze, unakuwa salama, ama la utaenda kuungana na shetani.
 
Hii ndio ile hatua wenzetu wa geita, rukwa na iringa huchukua na mara ingine tunaona kama hawapo sawa,

Ukitaka kuona ni zito fanya kama limekutokea afu jipige kifua uamue uone kama utaamua unavyowaamuliaga watu wakitolewa na hilo tukio
Ingekuwa ni Geita, Njombe, Kigoma, Arumeru au Rukwa mbona mapema sana habari ingesikika, mume amkata mapanga mke na kutenganisha kichwa na kiwiliwili chanzo ikadaiwa mgogoro wa ndoa...

Hii mikoa hawalazi damu kwenye ishu kama hizi.
 
Kuna kitu hakipo sawa kwenye kizazi hiki na serikali inakosea sana kukipromote. Kupima DNA.

Mi ni Baba wa watoto 4, sithubutu kwa namna yoyote ile kupima DNA. Mtoto aliyezaliwa kwenye Boma langu ni wa kwangu hata asifanane na mimi. Huu ukisasa wa kutaka kupima DNA ni chanzo cha migogoro, misongo ya mawazo na mauaji kwenye familia nyingi. Msijiumize bila sababu. Toka enzi za wazee wetu, familia nyingi zina mchanganyiko wa damu ila wazee walinyamaza.
 
Hodari sana wewe.

Nahisi kwenye jina lako ungetowa hiyo "e" ukaweka "u" ingependeza zaidi.
Hahaaaa nimecheka kama mazuri. Bibi unanitukana wakati wa mfungo ustaadhati wangu. Leo umeharibu Swaumu yako bureπŸ˜€πŸ˜ƒπŸ˜„πŸ˜πŸ˜†πŸ˜…. Tulikumiss, karibu tena JF mkongwe. Tunakuheshimu na kukujali ndio maana tulikumiss tukajua upo Gaza maana ulipotea.
 
Ingekuwa ni Geita, Njombe, Kigoma, Arumeru au Rukwa mbona mapema sana habari ingesikika, mume amkata mapanga mke na kutenganisha kichwa na kiwiliwili chanzo ikadaiwa mgogoro wa ndoa...

Hii mikoa hawalazi damu kwenye ishu kama hizi.
Ni hatari sana hilo usiombe
 
Back
Top Bottom