Ushuhuda wenye kuumiza mno

Ushuhuda wenye kuumiza mno

Mungu mwenye uwezo wote kashindwaje kubadilisha io fate wanae wapendwa wasiteketee na moto?

Wewe kwanini unataka auzie wakati viumbe wake wanarejea kwake ?

Mola muumba ana vitu vitatu kwa waja wake kwa kuzingatia ufanyaji wa matendo,navyo ni :

1. Mashi'a (Wills) 2. Iraadah (Wants) 3. Mahabah (Love)

Ukivielewa vitatu hivi hutapata shida kamwe juu ya haya yanayotokea ulimwenguni.
 
Na usisahau kwamba dereva wa lori alikua anamkwepa boda boda asimgonge na yeye yamemkuta
 
Tukio la kuokoa na wewe kifa imetokea mara nne katika maisha yangu ya kivuvi ila imetokea tena mara nne wakuokolewa anapona na muokoaji anakufa kisiwani kerebe. Hadi ilifika sehemu mwaka huu watu tukaogopa kusaidiana kwenye majanga. Ila wote tuko sekta moja
 
Kifo chake ni faida kivipi ?
Angalau abiria wa bodaboda amekutwa na kifo wakati wa kutenda mema. Kufa kwake ni faida...maandiko yanasema.

Wengine sijui tutakutwa na vifo vyetu katika mazingira gani!
 
Kwani amewaacha wateketee bila sababu ? Hujajiuliza swali hili ?

Pili, yeye ndio ametaka wateketee sababu kifo ni haki na muda ukifikia Mola huwa hacheleweshi hata sekunde.

Tatu,upendo wa Mola wetu ni upendo kamili ambao una ambatana na mambo kadha wa kadha,kama kutupa akili ya kujua lipi jema na lipi zuri,na kutupa muda wa kujirekebisha na mfano wake.
[emoji115][emoji115][emoji123][emoji120][emoji109]
 
Jamaa amekufa kifo kimoja cha kishujaa sana, amepigana vyema vita yake na as long as maisha ni safari, atakuwa na mwanzo mwema after-life! Japo inakuwa vigumu binadamu kukubaliana na ukweli, death is just the beggining of another journey! Death is not a mess na haijawahi kuwa mess! Swali ni kwamba, tutakufaje? Get prepared, tommorow isn't promised!
 
Jamaa amekufa kifo kimoja cha kishujaa sana, amepigana vyema vita yake na as long as maisha ni safari, atakuwa na mwanzo mwema after-life! Japo inakuwa vigumu binadamu kukubaliana na ukweli, death is just the beggining of another journey! Death is not a mess na haijawahi kuwa mess! Swali ni kwamba, tutakufaje? Get prepared, tommorow isn't promised!
 
Unapotoa msaada ,usiangalie wengine wanatoa au hawatoi.
As long as unafanya Jambo jema,wewe fanya tu..bila kujali Ni wangapi hawajafanya..na kila mmoja atatoa hesabu zake kwa nafasi yake aliyopewa.
umenielewa vibaya Anne.

Kwenye mazingira ya hatari ambayo unajua kutakua na mlipuko mda wowote, huna budi kuwepo hapo.

Mkishakua wengi sehemu yenye mafuta yaliyozagaa vile, unawaanije wenzako kwamba hawatasababisha ajali ya moto mfe??

Kwahiyo, nililenga kusema yangekuwepo mazingira kwamba kuna uwezekano mdogo wa mlipuko, kwamba wote tuliopo hapo timejikita kuokoa wengine na hakuna anayevuta fegi, kuchakachua betri n.k hapo ningeweza kutoa msaada wangu.
 
Hii ni simulizi ya dereva wa boda boda aliyenusurika kifo cha kuteketea na moto kwenye ajali ya Moro
Anasumulia kwamba asubuhi ile alipata abiria wa kumpeleka Nane nane... Walipofika eneo la ajali ndio kwanza ajali ilkuwa imetokea na hakuna aliyeshunghulika na majeruhi kwenye cabin ya gari... Hivyo yule abiria alimuomba dereva wa boda boda watoe msaada... Wakapanda kwenye cabin na kukuta abiria mmoja mwanamke na dereva ambao wote walikuwa wamevunjika miguu ila walikuwa hai bado
Walipojaribu kuwanasua wakakuta wamebanwa na mikanda (safety belts) hivyo yule abiria wa boda boda akamuomba bodaboda wakatafute kisu ili waje wakate ile mikanda wawatoe majeruhi... Boda boda akataka kugoma lakini yule abiria wake akamsihi wakatafute kisu wawasaidie wale majeruhi kwakuwa hata yeye boda boda hajui atakuja kusaidiwa na nani maishani...

Maneno yale yalimuingia bodaboda na kukubali huku wengine wakiendelea na harakati za kuchota mafuta yanayomwagika.... Basi ni wakati wanaiendea boda boda yao, ndipo moto ulipolipuka
Dereva wa bodaboda alinusurika ila bodaboda yake iliteketea palepale pamoja na yule abiria wake aliyetaka kutoa msaada
Maisha ni kitu gani? Maisha yamebeba siri gani? Kusudi la Mungu ninini?
Abiria mpita njia aliyekuta ajali na kutaka kutoa msaada anapoteza maisha kwenye harakati za kusaidia... Boda boda ambaye hakuwa tayari kutoa msaada pengine akuwaza muda atakaopoteza pale.. Ananusurika...!!!
Abiria yule angepita na zake pengine yasingemkuta yaliyomkuta... Utu wema wake ndio umekuwa kiama chake

Dereva wa Lori na abiria wake nao waliteketea ndani ya ile cabin... Pengine moto usingewaka wangenusurika..... Lakini anayeacha simanzi ni yule aliyejitoa kuwasaidia hawa majeruhi naye anaishia kuungua mpaka kufa.... Maisha ni kitu gani?

Kwa imani rahabu yule kahaba alinusulika kwa yule mtenda wema atalipwa kutokana na iman yak na moyo wake mungu atampa fadhila uko aendako really sad moment
 
Kifo chake ni faida kivipi ?
Kwa sababu ya nia yake njema ya kumsaidia mwenzake na kitendo kile kitaongeza katika uzani wa mambo yale mema,kwahiyo atalipwa kwa kitendohicho ama kujua hatima yake ya kuwa ni wa motoni au peponi hilo anajua yeue mwenyewe Muumba.
 
Kwa imani rahabu yule kahaba alinusulika kwa yule mtenda wema atalipwa kutokana na iman yak na moyo wake mungu atampa fadhila uko aendako really sad moment
[emoji848][emoji848][emoji144][emoji144][emoji144][emoji25][emoji25][emoji25][emoji25]
 
Hilo
umenielewa vibaya Anne.

Kwenye mazingira ya hatari ambayo unajua kutakua na mlipuko mda wowote, huna budi kuwepo hapo.

Mkishakua wengi sehemu yenye mafuta yaliyozagaa vile, unawaanije wenzako kwamba hawatasababisha ajali ya moto mfe??

Kwahiyo, nililenga kusema yangekuwepo mazingira kwamba kuna uwezekano mdogo wa mlipuko, kwamba wote tuliopo hapo timejikita kuokoa wengine na hakuna anayevuta fegi, kuchakachua betri n.k hapo ningeweza kutoa msaada wangu.
Pengine Hilo wazo halikuwepo
 
Wewe kwanini unataka auzie wakati viumbe wake wanarejea kwake ?

Mola muumba ana vitu vitatu kwa waja wake kwa kuzingatia ufanyaji wa matendo,navyo ni :

1. Mashi'a (Wills) 2. Iraadah (Wants) 3. Mahabah (Love)

Ukivielewa vitatu hivi hutapata shida kamwe juu ya haya yanayotokea ulimwenguni.
Viumbe vyake vinajerea kwake kwa mateso??
Wewe unaweza kumchoma moto mtoto wato kipenzi ili arejee kwako?
 
Viumbe vyake vinajerea kwake kwa mateso??
Wewe unaweza kumchoma moto mtoto wato kipenzi ili arejee kwako?
Arejee kwangu wapi ? Unatakuwa uwe unatoa mfano wenye kuwiana na jambo husika.
 
Back
Top Bottom