Hii ni simulizi ya dereva wa boda boda aliyenusurika kifo cha kuteketea na moto kwenye ajali ya Moro
Anasumulia kwamba asubuhi ile alipata abiria wa kumpeleka Nane nane... Walipofika eneo la ajali ndio kwanza ajali ilkuwa imetokea na hakuna aliyeshunghulika na majeruhi kwenye cabin ya gari... Hivyo yule abiria alimuomba dereva wa boda boda watoe msaada... Wakapanda kwenye cabin na kukuta abiria mmoja mwanamke na dereva ambao wote walikuwa wamevunjika miguu ila walikuwa hai bado
Walipojaribu kuwanasua wakakuta wamebanwa na mikanda (safety belts) hivyo yule abiria wa boda boda akamuomba bodaboda wakatafute kisu ili waje wakate ile mikanda wawatoe majeruhi... Boda boda akataka kugoma lakini yule abiria wake akamsihi wakatafute kisu wawasaidie wale majeruhi kwakuwa hata yeye boda boda hajui atakuja kusaidiwa na nani maishani...
Maneno yale yalimuingia bodaboda na kukubali huku wengine wakiendelea na harakati za kuchota mafuta yanayomwagika.... Basi ni wakati wanaiendea boda boda yao, ndipo moto ulipolipuka
Dereva wa bodaboda alinusurika ila bodaboda yake iliteketea palepale pamoja na yule abiria wake aliyetaka kutoa msaada
Maisha ni kitu gani? Maisha yamebeba siri gani? Kusudi la Mungu ninini?
Abiria mpita njia aliyekuta ajali na kutaka kutoa msaada anapoteza maisha kwenye harakati za kusaidia... Boda boda ambaye hakuwa tayari kutoa msaada pengine akuwaza muda atakaopoteza pale.. Ananusurika...!!!
Abiria yule angepita na zake pengine yasingemkuta yaliyomkuta... Utu wema wake ndio umekuwa kiama chake
Dereva wa Lori na abiria wake nao waliteketea ndani ya ile cabin... Pengine moto usingewaka wangenusurika..... Lakini anayeacha simanzi ni yule aliyejitoa kuwasaidia hawa majeruhi naye anaishia kuungua mpaka kufa.... Maisha ni kitu gani?
Duuuh kwaiyo aliwapa hao watu mioyo migumu ili itokee kilichotokea?Turejee maandiko ya biblia wakati Musa anamuomba Farao awaruhusu wana wa Israel waondoke Misri. Mungu akaufanya moyo wa Farao kuwa mgumu.
Ndicho kilichotokea Morogoro kweli unataka kuniambia watu zaidi ya 500 walikuwa wanachota mafuta na kirandaranda eneo la tukio zaidi ya nusu saa bila kumuona na kumsaidia kumuokoa dereva? Sidhani watanzania tumekuwa na moyo mgumu hivyo
Labda yametokeo hayo ili kazi ya Mungu aliyopanga itimie.
Hata Mimi hii imenishangaza.Bado naendelea kuangalia video ya raia kuchota mafuta na kuacha kuwaokoa dereva na mwenzie.
Raia tunakuwa na roho ngumu za kutotoa msaada hatimaye maangamizi yanàtukumba.
Nina imani yule aliyetaka kumukoa dereva amerejea kwa Muumba wake salama kutokana na nia yake ya kuokoa maisha ya wenzio ila bahati mbaya kateketea pamoja na wale waliotaka kuadhibiwa kutokana na roho zao za kukosa utu na kujali vipato/mali(mafuta)
Unapotoa msaada ,usiangalie wengine wanatoa au hawatoi.Inahuzunisha ndio ila kuokoa mtu kwenye mazingira hayo sio wazo zuri kabisa.
Binafsi ningefanya hivyo kama tu pasingelikua na watu wengine pembeni.
Ndicho kilichotokea Morogoro kweli unataka kuniambia watu zaidi ya 500 walikuwa wanachota mafuta na kirandaranda eneo la tukio zaidi ya nusu saa bila kumuona na kumsaidia kumuokoa dereva?Turejee maandiko ya biblia wakati Musa anamuomba Farao awaruhusu wana wa Israel waondoke Misri. Mungu akaufanya moyo wa Farao kuwa mgumu.
Ndicho kilichotokea Morogoro kweli unataka kuniambia watu zaidi ya 500 walikuwa wanachota mafuta na kirandaranda eneo la tukio zaidi ya nusu saa bila kumuona na kumsaidia kumuokoa dereva? Sidhani watanzania tumekuwa na moyo mgumu hivyo
Labda yametokeo hayo ili kazi ya Mungu aliyopanga itimie.
Hii ni simulizi ya dereva wa boda boda aliyenusurika kifo cha kuteketea na moto kwenye ajali ya Moro
Anasumulia kwamba asubuhi ile alipata abiria wa kumpeleka Nane nane... Walipofika eneo la ajali ndio kwanza ajali ilkuwa imetokea na hakuna aliyeshunghulika na majeruhi kwenye cabin ya gari... Hivyo yule abiria alimuomba dereva wa boda boda watoe msaada... Wakapanda kwenye cabin na kukuta abiria mmoja mwanamke na dereva ambao wote walikuwa wamevunjika miguu ila walikuwa hai bado
Walipojaribu kuwanasua wakakuta wamebanwa na mikanda (safety belts) hivyo yule abiria wa boda boda akamuomba bodaboda wakatafute kisu ili waje wakate ile mikanda wawatoe majeruhi... Boda boda akataka kugoma lakini yule abiria wake akamsihi wakatafute kisu wawasaidie wale majeruhi kwakuwa hata yeye boda boda hajui atakuja kusaidiwa na nani maishani...
Maneno yale yalimuingia bodaboda na kukubali huku wengine wakiendelea na harakati za kuchota mafuta yanayomwagika.... Basi ni wakati wanaiendea boda boda yao, ndipo moto ulipolipuka
Dereva wa bodaboda alinusurika ila bodaboda yake iliteketea palepale pamoja na yule abiria wake aliyetaka kutoa msaada
Maisha ni kitu gani? Maisha yamebeba siri gani? Kusudi la Mungu ninini?
Abiria mpita njia aliyekuta ajali na kutaka kutoa msaada anapoteza maisha kwenye harakati za kusaidia... Boda boda ambaye hakuwa tayari kutoa msaada pengine akuwaza muda atakaopoteza pale.. Ananusurika...!!!
Abiria yule angepita na zake pengine yasingemkuta yaliyomkuta... Utu wema wake ndio umekuwa kiama chake
Dereva wa Lori na abiria wake nao waliteketea ndani ya ile cabin... Pengine moto usingewaka wangenusurika..... Lakini anayeacha simanzi ni yule aliyejitoa kuwasaidia hawa majeruhi naye anaishia kuungua mpaka kufa.... Maisha ni kitu gani?
[emoji120][emoji120][emoji120][emoji120][emoji120][emoji120][emoji120][emoji120][emoji120][emoji120][emoji115][emoji115][emoji115][emoji109][emoji109][emoji109][emoji120][emoji120][emoji120]Premature death, untimely death, death caused by ignorance and negligence..
Kwa kuwa tunajifanya watu wa imani basi tunamsingizia Mungu kuwa amepanga au sijui shetani ndo kafanya yake na tunasahau kuna mahali hatujatimiza wajibu.
Fikiria police wangewahi na kuweka ulinzi hakuna mtu angelazimisha kuiba mafuta, wangesimama mbali wanaangalia.
Ukiacha Hayo chukulia mgonjwa aliye wodini anamwita nurse kwa kuwa amebanwa pumzi nesi anamu ignore baada ya mda anafariki, kumbe nesi angemuwahi kwa sindano au oxygen yule mgonjwa angepona, sisi tunasema mapenzi ya Mungu.
Kufa ni lazima lakini wakati mwingine tunakufa kabla ya muda, bado hatujui kuthamini uhai...
Kwani amewaacha wateketee bila sababu ? Hujajiuliza swali hili ?Mungu mwenye upendo wote anaachaje watoto wake wanateketea?
Hili ni swali la uongo kwake,yaani umekosea kuuliza swali bila shaka kwa kutomjua Mola ana sifa gani na tabia gani.Mungu mwenye uwezo wote kashindwaje kubadilisha io fate wanae wapendwa wasiteketee na moto?