kuna njia moja tu inaweza kukuponya maisha yako yote, na utarudi hapa kutoa ushuhuda kama utafuata masharti yake. Unaweza kuwa umeshajaribu sana njia nyingi na pengine hii pia ila bila kufuata masharti vizuri. na kwasababu umekamatika, hauna jinsi ila kutafuta kina namna ili upone na maisha yako yarudi kama awali. Maadamu u mzima, unaweza kuongea, unaweza hata kuandika jf, BADO LIPO TUMAINI, unayo nafasi ya kupona kabisa na ukawa ushuhuda mwingine kwa watu.
sikiliza. Njia hii, ni njia ya wokovu kwa njia ya Yesu Kristo. Mungu ameweka njia hiyo tu kwamba wanadamu wooote wenye dhambi, wenye matatizo wapitie hiyo wakaitue mizigo yao yote, wakatue magonjwa yao yote, na yeye atakubebea, wewe utabaki kuwa huru.
unachotakika (masharti), Umkiri Yesu Kristo kuwa Bwana na Mwokozi wa maisha yako, na kuamini moyoni kwamba Mungu alimfufua katika wafu, kwamba alikufa na kufufuka kwa kufanyika kafara la ukombozi wa maisha yako. Yesu Kristo ni Mwokozi, mponyaji na ndiye njia kweli na uzima.
sijui dini yako, sijui ulikopitiapitia. ila nikuambiacho, ukimkiri Yesu Kristo kwa kinywa chako na kuamua awe Mwokozi wa maisha yako, utaokoka roho, mwili na nafsi, na mali zako zote, na kazi, na watoto, na familia n.i. ila, lazima ujitoe maisha yote. You must surrender toka ndani ya moyo wako, Imani yako kwa Mungu through Yesu Kristo iwe kipaumbele cha kwanza na vingine vyote ni secondary. mwanadamu hawezi kumwona Mungu hadi asalende maisha yake yote, fikra zake, kila kitu akijenge kwenye misingi ya Imani ndani ya Yesu Kristo, hapo ndipo Mungu hufanya makao maishani mwetu, atakupigania kwa watesi wako, atawafukuza wachawi, mashetani n.k, na anao uwezo kurudisha miaka yako yoote iliyoliwa na matatizo. MUNGU ANAWEZA.
pia, anza kusoma Neno la Mungu, Biblia. nikiri kwamba, sio kwamba nabagua dini au la, ila kwa ushuhuda wa maisha yangu, hicho tu ndicho kitabu kilichobadilisha maisha yangu.
Mimi nilishapitia maisha kama hayo ya kwako, lakini amini usiamini, it takes no longer than a day Mungu kubadilisha maisha yako kama akiamua, na mazingira gani yatamfanya aamue? pale utakaposalenda maisha yako kwake ili awe Mungu wako, na ukijua kwamba hapa duniani tunaishi tu ila bila Mungu shetani anaweza kufanya lolote dhidi yetu. hatuna nguvu za kumshinda shetani bila Mungu. shukuru Mungu bado mzima.
ulifanya kosa sana kutoamini kama wachawi wapo. mimi hata watoto wangu huwa nawafundisha kwamba wachawi wapo, hivyo maisha yao wawe wanamtumaini Mungu ndiye atakayewalinda na wachawi. nasema hivyo kwasababu nilishawahi kulogwa na kufanywa fukara wa kutupa. huwa naamini kwamba kati ya watu waliowahi kupitia maisha magumu duniani wakiwa na elimu ya Masters, ni mimi na mke wangu. tulifika kipindi kila tunachofanya hakifanikiwi, kila mlango umefungwa, wale tuliowasaidia wanatucheka kwamba tumekwisha wakati sisi ndio tuliwasaidia kufika walipo, kila mtu alitukimbia, tukabaki sisi na Mungu. tulichoamua ni kuanza kumtafuta Mungu na kumuomba Mungu kwa bidii. tulitfuta uso wa Mungu, ikafika majira ambayo Mungu aliamua kushuka kututetea, IMEKUWA HISTORIA. kila kitu kilikuwa kinakuja dabodabo. siongei kishabiki, ni hakika, mafanikio yalianza kutufuata tu ni kama milango imefunguka.
wachawi wapo, ni maajenti wa shetani, na wengine huwa wanakuwa watu wako wa karibu mno. ishi ukijua kuwa kama kuna Mungu basi na shetani na maajenti wake wapo, na hizo ndio falme zinazoshindana/adui siku zote. ukiamua kuwa upande wa Mungu jua kabisa kuwa upande wa shetani ni adui zako, na ukiamua kuwa upande wa shetani jua upande wa Mungu sio watu wako. ukiamua kuwa wa shetani utapata vya shetani ila kuna siku atakuteketeza na kukufedhehesha, utalipia ulivyokula, ila ukiwa kwa Mungu gharama pekee utakayolipa ni kujitoa kwa Mungu na kufuata sheria zake tu na gharama zingine zote Mungu ameshalipa kwa Damu ya Yesu Kristo.
Mungu akusaidie.