beth
JF-Expert Member
- Aug 19, 2012
- 3,877
- 6,326
Ili kuongeza Ushiriki wa Wanawake Mtandaoni, Mkurugenzi Mkazi wa Benki ya Dunia, Nathan Belete amesisitiza umuhimu wa Mafunzo ili kuwapa Wasichana Ujuzi wa Kidigitali
Ameshauri wigo wa upatikanaji wa Intaneti uongezeke, na gharama ya Huduma hiyo iwe nafuu ili kuwafikia Wanawake wengi zaidi
Ameeleza hayo katika Kongamano la Wanawake na Teknolojia leo katika Ukumbi wa Mikutano wa JNICC Machi 07, 2023 Jijini Dar es Salaam
Kongamano hilo limeandaliwa na Taasisi ya LP Digital kwa kushirikiana na Wadau mbalimbali. Mgeni rasmi ni Waziri wa Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari, Nape Nnauye
Akizungumza katika Kongamano hilo Waziri Nape Nnauye amesema Matumizi ya TEHAMA yameongezeka duniani, lakini ushiriki wa Wanawake na Vijana bado upo chini
Amesema licha ya idadi ya Wanawake kuwa kubwa hapa Nchini kama ilivyobainika katika Sensa ya Mwaka 2022, Sekta ya Teknolojia bado ina pengo kubwa la kijinsia
Ameshauri wigo wa upatikanaji wa Intaneti uongezeke, na gharama ya Huduma hiyo iwe nafuu ili kuwafikia Wanawake wengi zaidi
Ameeleza hayo katika Kongamano la Wanawake na Teknolojia leo katika Ukumbi wa Mikutano wa JNICC Machi 07, 2023 Jijini Dar es Salaam
Kongamano hilo limeandaliwa na Taasisi ya LP Digital kwa kushirikiana na Wadau mbalimbali. Mgeni rasmi ni Waziri wa Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari, Nape Nnauye
Akizungumza katika Kongamano hilo Waziri Nape Nnauye amesema Matumizi ya TEHAMA yameongezeka duniani, lakini ushiriki wa Wanawake na Vijana bado upo chini
Amesema licha ya idadi ya Wanawake kuwa kubwa hapa Nchini kama ilivyobainika katika Sensa ya Mwaka 2022, Sekta ya Teknolojia bado ina pengo kubwa la kijinsia