Ushindi wa Lema, aibu kwa Clouds FM

Ushindi wa Lema, aibu kwa Clouds FM

Tokea hii redio imekuwepo haijawahi kusifia CDM hata siku moja. Wale gamba origino

Wana kipindi chao huwa kinaitwa ala za roho. hiki kazi yake ni kumsifia Zitto Kabwe tu. Mnyika walimjaribu akawatolea mbavuni
 
Clouds mbona wanajulikana tangu siku nyingi! Fuatilia hata waandishi wao hawana taaluma ya uandishi wamekaa kihunihuni tuu!
Ukiona vipindi vinaendeshwa na MC badala ya watangazaji wenye taaluma zao ujue udaku na kujipendekeza kwa wakubwa lazima ku overshadow kila kitu. Wangekuwa akina Mabonde ni wananawake wangeshapewa viti maaalum ila basi ana bahati mbaya hakuna viti maalum vya wanaume
 
Sidhani hata kama wakiisifia CHADEMA inahalalisha kuwa wakifanyacho ni sawa.SI SAWA. Kuna maadili ya mwanahabari. Tatizo baadhi ya waandishi, watangazaji huwa wanaongea kana kwamba "maoni yao ni maoni ya watanzania"..wanaenda mbali zaidi kuonyesha/kusisitiza aliyekinyume na kile wanachokiamini (wao) hayuko sahihi!

Kwa mtu yeyote makini akiona jambo hili hasa likijirudia rudia kwa baadhi ya wanahabari, hutaka kujua undani wa mwanahabari..mf. elimu, uzoefu wa kazi na hata credibility ya kazi yake.

Swadakta!
Hatutaki isifiwe Chadema; kama issue ni kusoma vichwa vya habari vya magazeti wasome tu na kuendelea na mambo mengine.
 
Hii radio naiona imekaa kuburudisha zaidi na sio kuelimisha au kuhabarisha, binafsi nilikuwa naisikiliza enzi ya kipanya na fina Mango na pia jahazi enzi ya Habash, angalau ndio vipindi nilivyokuwa naweza kusikiliza, munaowashauri waache ushabiki wa siasa munapoteza muda wenu bure, wanaweza kuacha lakini sio sasa kipindi hiki cha mh J.K kwani si mnaona hata sherehe za kuzaliwa kwa mheshimiwa wanaandaa wao, tayari ruge keshapewa ile studio ya wasanii sasa hapo kushabikia magamba wataachaje wakati wananufaika?

Kama ambavyo mafisadi hawawezi kuhama CCM ndivyo ambavyo na CLOUDS wasivyoweza kuacha ushabiki kwa CCM wote wanapata faida ati na wala hawaangalii madhara yake ni nini.
 
Hawana maana,Gerald Hando nina wasiwasi sana na kiwango chake cha elimu,kwa PJ sina tatizo nae,yeye ni mweledi.

Mweledi Gani anshabikia "UHURU KONGWE LA CHAMA CHA MAPINDUZI" na "JAMBOLEO"
 
Hawa ni aina ya waandishi tulionao tz wanaosubilia huruma za watawala ili wafike huko wanakotaka kwenda. Waandishi wasiojiamini kama wanaweza kusimama wenyewe.
clouds ovyooo! Na huenda wakawa wanafagilia ccm mafisadi!

Sio hili tu kunakipindi tena walishawahi kumkejeli kiongozi mmoja wa serikali! Mkomeee!
 
Hawa hawana maana hadi leo mchana mmoja wao kajichangala kuwa Lema kashindwa.
 
Ukiona vipindi vinaendeshwa na MC badala ya watangazaji wenye taaluma zao ujue udaku na kujipendekeza kwa wakubwa lazima ku overshadow kila kitu. Wangekuwa akina Mabonde ni wananawake wangeshapewa viti maaalum ila basi ana bahati mbaya hakuna viti maalum vya wanaume

Na hilo neno mkuu!
 
Tunajua , bila kujikomba watapata wapi kazi za kuandaa matamasha na mikutano ya ccm ? Kila mmoja wetu ana haki ya kuwa mfuasi au hata kuwa mwanachama wa ccm au hata chama chochote lakini media lazima ziwe fair , labda wajinasibu kwamba redio yao ni media ya ccm .
 
Wafanyakazi / watangazaji wa namna hii ni JANGA LA KITAIFA!
 
Tunajua , bila kujikomba watapata wapi kazi za kuandaa matamasha na mikutano ya ccm ? Kila mmoja wetu ana haki ya kuwa mfuasi au hata kuwa mwanachama wa ccm au hata chama chochote lakini media lazima ziwe fair , labda wajinasibu kwamba redio yao ni media ya ccm .[/QUOTE]

Kama ni hivyo - si waweke mambo wazi! ?
 
Hivi inakuwaje kila siku humu watu mara hiyo redio imekufa, mara hatuisikilizi na bado kila siku mnaianzishia topic, kwa mwenye akili timamu aliyesikiliza hicho kipindi leo atakubaliana na mm kwamba waliongea ukweli ambao wengi humu hamtaki kuukubali,
wao walikataa kuiita hukumu ya leo ya kuwa ya hadhi ya juu kwakuwa tayari kuna hukumu za kutengua ubunge na kurudisha ubunge nyingi zimetolewa, na hawakusema kwamba Lema atashinda au atashindwa, acheni ushabiki...
 
Boss wao J. Kusaga amewasikia. Atawakanya wasirudie tena kujiingiza ktk ushabiki wa politiki
 
wanashangaa wa2 kusafiri kutoka mbali kuja kusikiliza hukumu hawashangai watu kusafiri kutoka mikoa mingine kuja kumuangalia RICK ROSS au KOFFII hao watangazaji ni wakuda nazi kabisa
 
Dawa ya cloud FM 2015 tutakapo shika hatamu ni kiufungilia mbali tu! au waungane na TBC fm na UHURU kama Redio za CCM
 
tumia busara kutamka maneno kebehe na utani kwa jamii ya sasa havikubaliki kinachofuata utadharauliwa na redio yako kukosa mvuto kwa watu wenye akili

Mkuu, unadhani wao wanajali hilo?..wenye akili, uelekeo mzuri ndio wasema kama wewe.Wao kushabikiwa kwa matamasha mbalimbali na vijiweni wanadhani ni muda wote. Kwani ni mara ngapi wamekosolewa(constructively)? Wamebadilika hata mara moja?..

Inawezekana ni policy ya mmiliki wa Radio station lakini kuna maadili ya kazi, utu. Mtu mzima unajichekesha chekesha kama punguwani/taahira unategemea nini? Mf. Habari ya msingi katika magazeti inaweza isiongelewe, ikajadiliwa habari ya kipuuzi, na wakati mwingine ni aibu hata ku_Tune Clouds FM ukiwa na mwanao, wanaongea upuuzi upuuzi. Then hivi vipindi vya jioni ndio kwaaanza unaweza hata tune to Radio Tanzania, maana inakuwa habari/majadiliano ya kujisifia/majigambo na kosefu wa staha.

Sio kwamba hawatambui, wanajua..tatizo wakati mwingine wao kuongelewa(wether ni vizuri au vibaya) wanaona ni kuwa maarufu.
 
Kuna lipi clouds wasilolijua? Angalia kila habari itakayoandikwa katika gazeti ama wataikosoa au kuijadili, iwe ya gesi, umeme, mali asili, elimu, mahakama,polisi,machangudoa, walevi, wabakaji, iwe Kenya, Uganda, Mali, Marekani, wao wanajua yooote! Aibu jamani!
 
Nimewasikia sana hasa yule Gerald Hando amekandia sana habari iliyoandikwa Tz daima, hukumu ya kihistoria kusomwa leo,nataka na kesho niwasikie watasemaje.aibu yao magamba hao

Njaa mbaya ndugu yangu we acha tu, watu kwa kujipendekeza hawajambo, wakawasaidie magamba wenzao sasa gharama za kesi
 
Back
Top Bottom