Miaka michache iliyopita, kulikuwa na mdada mmoja mtaani kwetu alikuwa ananipenda kweli na alijuwa kabisa mimi ni mume wa mtu, alijitahidi mpaka akaja kujuwa nafanya kazi wapi. Katika yote haya mimi nilikuwa sijuwi kama ananipenda kwani nilikuwa sina mazoea naye kivile kwani kila nikimsalimia alikuwa ananiangalia tu na kunijibu pale anapojisikia, awali nilidhani ana dharau ila sikumtilia maanani na wala sikumjali. Nilishangaa siku ya siku nipo kazini naitwa na mlinzi, ananiambia una mgeni ghorofa ya chini anakusubiri, kumuuliza ni nani kwani nilikuwa sipendi watu waje kunitembele kazini, akaniambia tu kuna mwanamama anadai ni shangazi yako. Nilipanic mno na kwenda chini, ile nashuka tu nakutana na huyo mdada jirani yangu kapendeza kama vile anatoka kwenye interview ya kazi. Namsogelea kujuwa kulikoni, nashangaa ananikumbatia na kunibusu shavuni as if tunajuana kinoma....kwa kweli nilishangaa sana na kuanza kuona haibu kwani nilikuwa sina mazoea naye.
Tukaenda sehemu ya wageni, tukakaa pale na mdada akaanza kujinadi na kumwaga sera zake za uchaguzi kwangu. Anaongea huku anatetemeka, nikamuelewa na kumpa masharti yangu akayakubali so tukayajenga. Kesho yake nikaanza kuvamia jimbo lake na kuanza kula mzigo kama mpiga kura wake halali na akawa anataka kila siku kabla ya kurudi nyumbani nipitie kwake nimle kisha niende nyumbani na wakati mwingine alikuwa anataka nilale kwake mpaka nikawa nahisi anataka kunivunjia ndoa yangu. Nilipoanza sasa kupunguza kumla kwa fujo akawa ananiwinda na mpaka akaja nyumbani na kuanza urafiki na mke wangu. Sikupendelewa na hili kwani mke wangu naye alishangaa huyu mdada kunijuwa kinoma. Nikampiga marufuku huyu mdada kuja nyumbani, hakupendezwa na hili so akawa ananifuata kazini na kudai atanisubiri mpaka kazi iishe tukakulane na alikuwa ananiambia kabisa hawezi kulała bila kumpa chakula cha roho. Basi hiki chakula cha roho kilikuja kumchanganya akili huyu mdada mpaka akawa sasa anamtambia mke wangu huko mitaani kuwa yeye (hawara) ndiye mke halali kwangu na mke wangu ni suala la muda tu eti nina mpango wa kumwacha.
Aliaminisha watu mtaani mpaka kina Mama wengine walikuwa wakiniona walikuwa wananiambia nimuonee huruma mke wangu na wakawa wanasema mbona mnapendana na mnaendana iweje nimwache mke wangu kwa jailli ya changudoa kama yule? Baada ya kuuliza kulikoni ndipo nikaambiwa kuwa yule mdada anatangazia watu kuwa nina mpango wa kumwacha mke wangu kwa ajili yake. Pale mtaani karibia kila mtu alikuwa anajuwa mimi namla yule mdada japo sijamtangazia mtu yeyote.
Nikakaa kama siku mbili hivi bila kuwasiliana na yule mdada maana nilikuwa na hasira naye na kazini alikuwa haji kwani nilishamkatazaga. Cha kushangaza bwana, siku moja tupo nyumbani tunaangalia Champions League na mke wangu na baadhi ya mashemeji zangu, nashangaa saa tano usiku mtu anabonyeza kengele getini, ile nafungulia mbwa na kwenda kuangalia ni nani namkuta yeye, wacha aangushe varangati pale pale getini. Nilimzaba vibao ili anyamaze lakini wapi kwani alipiga mayowe eti nabakwa jamani naomba msaada, huyu mtu ananibaka. Ndani ya dakika 10 watu walijazana mno pale getini, basi yule mdada akamwaga mboga na kusimulia watu kila kitu juu ya uhusiano wetu. Yaani nilikoma jamani ila naishia hapa kwa sasa kwani bado nina mdachungu na yule demu.