Ushawahi Kupendwa Mpaka Ukawa Unahisi Kero?

Ushawahi Kupendwa Mpaka Ukawa Unahisi Kero?

Wakuu
Katika maisha ya mahusiano tunapitia mengi,unaweza ukapendwa sana mpaka ukawa unahisi ni kero sasa

Mtu kila saa anakutafuta,anakutumia text,anakupigia,ukimjibu au ukichelewa kumjibu anakulaumu na "mbona kimya" zinakuwa nyingi

Hali hii mimi binafsi huwa siipendi na ikitokea mwanamke wa namna hii basi nampiga chini haraka sana,siwezi kuwa saa niko na simu tu nachati au naongea na wewe kama nimekosa kazi ya kufanya.

Nimeachana na first11 ya wanawake dizaini hii.

Usawahi kudate na mdada au mwanaume wa namna hii? Hali ilikuwaje,ulikabiliana nae vipi na mahusiano yako bado yapo?
Cc Binti Sayuni03
Ukabiliane nae tena?

Pendeka wewe,mpe kampani Mrembo,acha ujinga

Au mueleze kwa upole akuelewe kua ukimaliza majukumu yako unamtafuta
 
Huelewi.

Yeye ndiye anafunga, halafu jioni analalia kifua.

Huelewi wapi?
Ulikua unamtemdesha dhambi kubwa sana binti wa watu .
Dhambi ambayo mpaka leo huko alipo anajutia alichofanya..

Astaghaffillah astaghaffillah astaghaffillah
 
Ulikua unamtemdesha dhambi kubwa sana binti wa watu .
Dhambi ambayo mpaka leo huko alipo anajutia alichofanya..

Astaghaffillah astaghaffillah astaghaffillah
Mimi sikumtendesha dhambi, actually mimi nilikuwa nakataa kukutana naye mwezi huo. Miaka miwili nimekataa, mwaka wa tatu kanililia.

Ndiyo nikamkubalia.

Kwani kulalia kifua ni dhambi mkuu?
 
Mimi sikumtendesha dhambi, actually mimi nilikuwa nakataa kukutana naye mwezi huo. Miaka miwili nimekataa, mwaka wa tatu kanililia.

Ndiyo nikamkubalia.

Kwani kulalia kifua ni dhambi mkuu?
Yaa taqurub zinaaa...
Tusikaribie zinaa

Sasa nyie mlichofanya ni kukaribia zinaa.
Pili huyo mdada nae alikua hana mikazo yaani kiufup mikazo zero
 
Wakuu
Katika maisha ya mahusiano tunapitia mengi,unaweza ukapendwa sana mpaka ukawa unahisi ni kero sasa

Mtu kila saa anakutafuta,anakutumia text,anakupigia,ukimjibu au ukichelewa kumjibu anakulaumu na "mbona kimya" zinakuwa nyingi

Hali hii mimi binafsi huwa siipendi na ikitokea mwanamke wa namna hii basi nampiga chini haraka sana,siwezi kuwa saa niko na simu tu nachati au naongea na wewe kama nimekosa kazi ya kufanya.

Nimeachana na first11 ya wanawake dizaini hii.

Usawahi kudate na mdada au mwanaume wa namna hii? Hali ilikuwaje,ulikabiliana nae vipi na mahusiano yako bado yapo?
Cc Binti Sayuni03
Mkuu kwa maelezo yako yameonesha jinsi ulivyo mdhaifu wa mahusiano.

Pili ni kuwa hao unaowamwaga kwa sababu ya kukushobokea, huwa wamekupenda zaidi ya ulivyowapenda wewe, mizani huwa imeegemea kwako.

Udhaifu wako ninaousema hapa ni kwamba, hao wapenzi wako hushindwa kuwapa ratiba zako sahihi za mawasiliano namna unavyotaka yawe, badala yake unakuja kufungukia huku Jf kuwa huwa unapata kero, ambapo wao wanakuwa hawajui lolote!

Ungeliwaweka wazi wala wasingelijisumbua kufanya kihere here cha kukutafuta kila saa.

Wanaume kama nyinyi, siyo strong sana kwenye mahusiano ya kimapenzi pamwe ndoa.

Bw mdogo wangu alikuwa na maneno kama ya kwako hayo, ...'ooh mi siwezi pandwa kichwani na mwanamke'!...

Siku moja nikafumania anafulishwa nguo na mke wake, huku shemeji kakaa kwenye sofa akichati raha mustarehe.

Nikaona kumbe hawa wanaojigamba sana kwenye mahusiano ndiyo watu dhaifu na dhalili sana wakipatiwa 'angle' ya kuwekwa sawa!

Sasa na wewe ipo siku utajakwamishwa na sehemu ambayo kila mtu atakushangaa, msg ama simu kutoka kwake utakuwa unaziona kama dhahabu, ni nzuri sana, tamu hata ikiwa na herufi mbili tu za 'hi', zisizokuwa na maana yoyote na hautapenda kuzifuta na kuzipoteza haraka haraka.

Mkuu omba sana siku zote chaguo lako liegemee kupendwa tu, lakini ikija kutokea na wewe ukapenda, utakuja kunyanyasika sana kisaikolojia kwa sababu ulishazoea kunyanyasa na kukandamiza wapenzi zako.

Wanakwambia 'Karma is real' ama 'muosha huoshwa'.

Hayanaga sifa wala formula hayo.
 
Ukaribu kama huo.unaweza sababisha kuingiliana kimaumbile na ukizingatia ni mwezi mtukufu.
Hajafunga ndoa .

Zinaa inakatazwa kwa sababu ina hasara NYingi kuliko faida
Kwa hiyo mwezi mtukufu ndiyo vibaya kufanya hivyo, miezi mingine poa?

Unafiki huu mwisho mwezi huu tu ?

Mtu unamkaza kila siku halafu mwezi huu unajibaraguza mwezi mtukufu?

Huu si unafiki kweli?
 
Wakuu
Katika maisha ya mahusiano tunapitia mengi,unaweza ukapendwa sana mpaka ukawa unahisi ni kero sasa

Mtu kila saa anakutafuta,anakutumia text,anakupigia,ukimjibu au ukichelewa kumjibu anakulaumu na "mbona kimya" zinakuwa nyingi

Hali hii mimi binafsi huwa siipendi na ikitokea mwanamke wa namna hii basi nampiga chini haraka sana,siwezi kuwa saa niko na simu tu nachati au naongea na wewe kama nimekosa kazi ya kufanya.

Nimeachana na first11 ya wanawake dizaini hii.

Usawahi kudate na mdada au mwanaume wa namna hii? Hali ilikuwaje,ulikabiliana nae vipi na mahusiano yako bado yapo?
Cc Binti Sayuni03
WANAIGIZA SANA
 
Kwa hiyo mwezi mtukufu ndiyo vibaya kufanya hivyo, miezi mingine poa?

Unafiki huu mwisho mwezi huu tu ?

Mtu unamkaza kila siku halafu mwezi huu unajibaraguza mwezi mtukufu?

Huu si unafiki kweli?
Mtu kutaka ligi na wewe ni kuhatarisha imani yake..
Mkuu naomba tuishie hapa..
Ila huu ni mwezi ambao kufanya madhambi ujie wewe ni moja kw moja motoni tena daraja la chini kabisa la moto mkuu
 
Mshangazi aliona huyu kijana ni jau, akafunga vioo.
Alikukomesha, 😂😂😂😂😂
😂😂😂😂😂😂 Yule maza jau...
Juzi aliniita nikafuturu nikamwambia naijua hiyo..
ila asikwambie mtu kublokiwa inauma sana sis hasa kwa mtu ambaye unajua ana sapport mambo yako
 
😂😂😂😂😂😂 Yule maza jau...
Juzi aliniita nikafuturu nikamwambia naijua hiyo..
ila asikwambie mtu kublokiwa inauma sana sis hasa kwa mtu ambaye unajua ana sapport mambo yako
Uache kutegemea mishangazi ikuweke town, utakua na mwisho mbayaa.
Anza kujitafuta kivyako na ujipate, ufaidi life.

Acha kulelewa. Lol 😂😂😂😂😂
 
Back
Top Bottom