Ushauri wenu wanaJF, mke wangu ana tabia za umbea

Ushauri wenu wanaJF, mke wangu ana tabia za umbea

Umeongea point kitachofuata hapo ni kugongeana wake waishie kutiliana sumu
Mbona mmejazana hapo nyumbani kwa wazazi wako?
Acha ujinga kwanza, toka hapo nyumbani, nenda kapange kwako haraka sana...
Hata sijamaliza kusoma habari yako, tatizo hapo ni huo mlundikano.... Baba mkwe, mama mkwe, mdogo mtu na mkewe, wewe na mkeo, sijui nani na nani tena....
Toka hapo upesi sana na mkeo nenda ukapange hata kama itakua ni chumba kimoja na choo cha nje, ndoa yako itakua na amani zaidi, niamini mimi brother!! Fanya hivyo kwanza haraka sana, kabla ya chochote.
malembeka18
 
tapatalk_1567924072319.jpeg
 
Nami nangojea tukaishi ktk mazingira yetu ili nijionee atakavokua kama akiwa hivi ndo nkasema nipate busara hivi ila jicho langu la tatu nimeweza kuhisi kama nikitabia ambacho kimerithiwa maana baba mkwe alishanidokeza vitu flani flani ambavyo havipendi kwa mama mkwe wangu ambvyo baadhi hata mke wangu anavyo
Mbona hata wewe mbea sasa au hapa umeandika mini?
 
Sio vizuri nyote mmeolea kwa wazazi? Hamuoni aibu kuwagegedea kwa wazazi? Ondokeni hapo msimpe pressure mama yako.mnaishi kama waarabu kah!
 
Sawa mkuu..uandishi sio fani yangu fani yangu ni biashara ndio iko ktk damu uandishi ntaajiri mtu wakuniandikia sio kila kitu lazima nikije watanisaidia wangne wanaojua kwa ujira
Wangine hatuna fani ya uandishi tunaugonjwa yakusaka pesa tu..so uandishi nimwandiko nimadhaifu yetu tutatafuta wakutusaidia kufanya kazi ya uandishi
duh, chief una maneno ka mkeo, nyie ni perfect match, hakuna kulalamika hapa.
 
Kwahiyo unataka kumuacha au? Hama hapo kwa mama yako ndo tukushauri nini cha kufanya.
Hapana mkuu kila kitu kiko poa mjengo uko mwishoni kukamilika kama miezi miwili imebaki kuisha kabisa nakuhamia na nawife anajua hilo nashangaa kwanini kawa gafla hivi
 
Mkanye, mwambie hupendi kuona jambo kama hilo tena. Inatakiwa usimame kama kiongozi.
Nshapambana atoke...ktk kipindi choote nimechokua nae nimeona mara nyingi sana kubwa kwake hata akiwa anazungumza nasimu nandugu zangu au zake kuwapa habari yajambo fulani ambalo na mim nalifahamu fika unaona anazungumza na vitu visivyokuepo vya umbea kushadadia kuongezea chumivi hali yakua ni jambo dogo sana imepeleke baada ya ndgu kuliona hilo kama ambavyo mim naliona ndo maana nkaja kwenu kupata hekma zakuishi na mtu wanamna hii nakumbadili kidgo kidgo juu tabia kama hizi
 
Hapo kwenu kuna nini mpk muishi kundi la watu hvyo?! Hapo ni pagumu sana itafika mahali utabaki mtu kati na itakubdi uchague upande mmoja. Wew miaka yote mitatu hyo kakuvumilia sana, maana mm toka mwanzo ningejua tu bdo upo kwa mama nahis hayo mahusiano yasingefika huko. Utagombana na nduguzo wote ukiendelea kung'ang'ania kwenu! Kupita kwao ni tabia tu unaweza kumueleza kuwa huipendi basi sito big deal. Ndio maana hilo eneo mnapaswa kuhama for good
Nimeupokea ushauri wako
 
kwanza kaka, kwanini bado upo kwa wazazi alafu mtu mzima kabisa na mke. je mkiata watoto maana naona hamna watoto? cha pili, mke anatabia za kiswahili sana... alafu huyo anapenda kuchat, hawezi kuongea mambo yake uso kwa uso...lazma matext... nina shauri, uwe na kwako kwanza....alafu cheki tabia zake. in the end huyo mke ataanza kukudharau. trust me. Maana imeshaanza iyo tabia kwa kutumia nja ya umbea.
 
Hyo nyumba mbona imejaa kama kama baraza la madiwani
 
Kwanini usifanye mpango wa kupata sehemu yako ya kuishi kuliko kuendelea kujibana hapo kwa wazazi. Tena unaoa ukiwa hapo hapo , kibongo bongo hiyo haipo njema.
 
kwanza kaka, kwanini bado upo kwa wazazi alafu mtu mzima kabisa na mke. je mkiata watoto maana naona hamna watoto? cha pili, mke anatabia za kiswahili sana... alafu huyo anapenda kuchat, hawezi kuongea mambo yake uso kwa uso...lazma matext... nina shauri, uwe na kwako kwanza....alafu cheki tabia zake. in the end huyo mke ataanza kukudharau. trust me. Maana imeshaanza iyo tabia kwa kutumia nja ya umbea.
Asante kwa ushauri
 
Mimi nimeoa takribana miaka3.9 sasa mimi na mke wangu tunaishi nyumbani kwa wazazi wangu kwa miaka yote hii tangu tuone hadi hii leo kilichonileta kwenu JF hivi.

Wiki tatu zilizopita mdogo wangu alikuwa anaoa na baada ya kuoa tunaishi nae hapa nyumbani yeye na mke wake mdogo waliolea mkoa mwingne hivo basi wakati wa harusi biharusi alisindikizwa na somo yake kwa hiyo nae somo tulikuwa nae ktk nyumba hii sasa baada ya kumtawisha kesho yake somo akahitaji kwenda kumnunulia vitu sokoni biharus ikabid mama yngu mzazi amwambie mke wangu msindikize sokoni sasa kwa maelezo ya somo wakati wanaenda sokoni mke wangu akawa anamuelezea somo mambo ya nyumba hii kuhusu wakwe akawa anamwambia kuwa hawa wakwe ni wabaya wanaroho mbaya wananinyanyasa sjui kama ndgu yenu ataweza kuishi humu ndani basi somo anasema hakuongea chochote.

Baada ya somo kuondoka kurudi kwao somo alimfuata mshenga wetu waharusi ambae alikua anatuwakilisha huko akamuelezea yoote alioambiwa na mke wangu kuhusu wakwe zake.

Yule mshenga ambae ni ndgu ikabid ampigie sim kumuelezea hizo habari mke wangu,mke wangu akakataa katakata kuongea akabaki analia tu nakuna maneno mke wangi akamwambia mshenga hakuyapenda hiyo alimwabilia kwa sms ikabid mshenga akawaelezea wazazi yoote alioambiwa na somo ikabid tuweke kikao ambacho skua najua nicha nini ila wazazi tayar inaonekana walikua washakaa wenyewe wameonge ila kikao ikawa nikufahamishana mambi ya ndani yasiwe yanatoka nje wala nje yasiwe yanaingia ndani

Sasa baada yakikao mke wangu akawa mnyonge sana akawa najitenga na mama mkwe wake na pia akawa anjitenga na mke mpya wa mdogo wangu hivyo ikapelekea wazazi kuona mabadiliko yake hayo yoote yanatokea hakuwahi kukaka au kuwaomba wazazi wangu wakae waongee nae kuhusu hizo habari zikoje koje lakini mke wangu walaa hana habar wakuwaza kukaa.

Mambo yakawa yanaendelea kumbe nje akienda kuhemea sokoni mke wangu anawahadhia wamama wasokoni kuwa amezushiwa mambo kwamba amewasemea wakwe zake kwa watu kuwa wa roho mbaya wanamtesa hayo mambo kumbe wale wanohadithiwa nao wanayaleta wanaambia ndgu zangu na hata baadhi wanamwambia mama yangu juu ya hayo maneno kuwa wanamtesa wanaroho mbaya na siku akihama kwenda kwake atafanya sherehe

Ikawa sasa mke wangu anajitenga nawazazi wangu na pia anajitenga na mke mpya wa mdogo mim binafsi hali hiyo niliiona nkawa nambembeleza sana kwa upendo anambie lakini katakata kagoma kunambia kulikoni zaid anakua nikulia mda wote analia tu.

Baada ya siku tatu hivi tena akiwa anatokea sokoni mke wangu akiwa kashika kitu mkononi akakutana namama yangu,mama akamuuliza hiko nin mke akasema kitenge cha harus ya jirani mama akamwambia kwa hiyo utakua unashona sare kila harusi utakayo alikwa maisha hayako hivo mwanangu usiwafurahishe watu kwani ukihudhuria nakutoa mchango utapungukiwa nini maana harus yetu haijapita wiki mbili tumeshona majuzi hapa kwa jirani umevaa sare na leo unaenda tena kushona sare ya hiyi harus ya mtaa wa tatu sasa maneno yakamwingia mke wangu hakupenda hakufutahishwa na hiyo nasaaa..kumbe baada ya masaa matatu nyumbani walikuepo bado wapo wageni wakike waupande wa baba yngu waliokuja kwenye harusi ambao mke wangu alikua nao karibu sanaa akafika anawahadithia kimafumbo kuwa kuna watu hawapendi hela zao kuliwa wanuchungu na hela zao kumbe mama alikua chooni anaskia kutoka nje baadae akawauliza wale ndgu kuwa mlikua mnaongea nini wakamuhadhithi yote baadae mama kumuliiza akasema nikweli niliyasema baada ya sku tatu tena mke wangu akaenda kumwambia shangazi yangu tunaishi nae jirani akamwambia kazushiwa mambo juu ya wakwe zake hapo hali yakua mke wangu hata hajakaa na wazazi wangu kuwaelezea ikoje ikoje hiyo kitu zaid anayapeleka nje kwa watu

Sasa wakati kabla ya harus ya mdogo wangu kulikua na sakata zito sana linalomuhusu mdogo wangu na hawala ambae alimpelekea mdogo wangu kfanya ubadhilifu mwingi sana wahela sasa mdgo wangu alikua anataka amuoe huyo mtu sasa sisi tukaona hamfai nayuko kimaslahi kumbe ktk vikao vyoote tuanavyokaa mke wangu kumbe anayatoa nje tunayaskia kwa watu ambao nimashoga zake na baaadhi ya watu amekuoa nao karibu ukifuatilia kiundani unakuta yanakweli kabisa maana vikao tulikua watu wachache muhimu nayeye akiwemo

Ikabidi mimi nianze uchunguzi wangu ktk uchunguzi wangu kuna sku nlimuomba sm yake nipige picha document nkasema ngoja niperuzi nikakutana na sms nyingi sana ambazo alikuwa anachati na huyo hawala wa mdgo wangu ambae familia nzima tunampiga vita kumbe mke wangu yeye akawa anamuhadhia yoote na sms nying akawa anampa ushauri nahata kudoza mambo au tabia za wazazi wangu kwahuyo mwanamke.

Nkajiuliza huyu vip mtu amabae sis tunampiga vita alafu ndo achati nae mda wote siku nkakaa nae nakamuelezea kuwa ww huwa unamwasiliano na mtu flani maana anatangaza habari zote za humu ndani anazipata lakini mke wangu alikataa katakata wakat minajua fika wanawasiliana

Vile vile ktkt vikao vya sisi wandani tu tulivyokua tunakaa nae akiwemo kujadili harus mamabo tunayojadili baada ya muda utayaskia nje ukiyaangalia unakuta anahio tabia

Pia lingine nimemchunguza kwa kina amekua simchungu sana wahela anatumia sana kuvaa hakuna hata siku ananishauri mambo ya msingi kimaendeleo zaid yakuzungumiza habari za watu

Pia maekua natabia yakupita kwao mara kwa mara maana kwao nimtaa watatu kutoka tunapoishi yaani hata awe anaenda sehemu ya juu napalipo kwao lazima atapitia kwao pabila sababu yoyote hakuna anaeumwa kwao na sm zipo.

Tangu masakata yoote haya amekua mtu wakunilazimisha kuhama hali yakua nimemuelezea hali halisi.

Jingine kubwa tangu tuoanae hajawahi kukaaa na mim kunielezea matatizo yake anayoyapitia zaid huwa nikiondoka tu atatuma sms nyingi sana zakulaumu lakini nkirudi nkimbembeleza tuongeee hakubali katakata ye amekua nimtu wakunambia mlalamiko yake kwa sms nasi kwamazungumzo yamdomo anakwa ana mim nayeye
Niishie hapo wanajamiiforum naombeni mawazo yenu katika hili
sasa unataka tukupe ushauri gani zaidi ya kumtimua
 
Mkuu nshajiongeza kuhusu hilo nanyumba yangu iko mwishoni kabisa kuisha nawife anaijua hiyo hali nashangaa amekua niwavitimbi sana kwavitu ambavyo anajua anamda mfupi tu wakukaa ukweni
Hamia haraka kwenye hilo Pagale utamalizia mambo mengine ukiwa humo ndani....
 
we mwenyewe mmbea......unapaswa kumlinda mkeo..........halafu unaishije hapo kwa wazazi wako na mkeo....we ni pumbafu sana.....wacha awaseme tuu.....
 
Back
Top Bottom