Ushauri wenu, dunia naona mviringo!

Ushauri wenu, dunia naona mviringo!

Mimi si mwanachama na mchanguaji sana huku MMU, lakini hata bubu aking'atwa ataongea hata neno.
Huku kuna walimwengu wa maisha halisi ya kibantu.

Hadithi ni ndefu lakini nitaifupisha.
Nina mke na watoto, tena wakubwa tu.
Katika mishe mishe za safari mikoani huko, sitaji mkoa lakini nilikaa mwaka.

Hili na lile katika kuchapa ripoti za kazi tukaelewana sana dada mmoja, kwa kweli alikuwa mzuri na ni figure 8.

Kwa utani tu nikatongoza, hakujibu wala kukataa.
Bado nikaendelea kutongoza, mwisho baada ya miezi 3, akakakubali na akasema nikuambie kitu?
Nikastuka kidogo, ila akaniambia nitakuambia tukionana.
Kweli tukaenda outing, na tukala na kunywa.
Kwa kweli tuli enjoy.

Fukuto langu lilikuwa kujua anachotaka kuniambia.
Na wakati huo alivyo mzuri na umbo la kutia hamasa, moyo unanidunda ndi.. ndi..ndi...!

Nikamsihi aniambie.
Akaanza taratibu.
Kaka mimi nimeolewa.
Moyo wangu ukadondoka pwaa....!
Sasa itakuwaje tena kumpenda mke wa mtu?
Nikamwuliza na kujiuliza, na nikaanza kusononeka.
Yule dada aliona kusononeka kwangu, lakini akanituliza, akaniambia usijali kaka.
Akaniambia amenichunguza sana muda wote huu licha ya kuolewa, na amenipenda ndio maana ana kitu cha kunieleza.
Ha!
Nikajiuliza , kuna kingine tena ?
Nikamwuliza kuna kitu gani?

Yule dada kwa unyonge akasema nitakuwa pamoja na wewe ila nifichie siri yetu!
Nikamwambia mbona hilo si tatizo mpenzi!
Akanidakia tena, akaniambia tukisex hataki condom!
Hapo nikapigwa butwaa!

Sasa nami nikadakia, mbona sielewi?
Nikamwambia si utapata mimba?
Huku nikijzuia kumwambia magonjwa je?

Hapo ndii akanieleza taratibu, kuwa ameoana na mume wake miaka miwili na hajapata mimba.
Ikabidi waende hospitali wapimwe na ikagundulika mume wake hana uwezo wa kutengeneza mbegu za kiume.
Na kwamba wameenda hospitali tatu tofauti, majibu ni yale yale.
Akaniambia ,nami natafuta mtoto, nimekupenda.

Nilichanganyikiwa!
END OF PART I

Wadau ushauri wenu, part zingine NNE zitakuja mbele.

Hapo mkeo na watoto utawakumbuka baadae😅😅😅
 
Bona siku hizi hofu ya mungu na neno lake hamna au haiko, mtu amekwambia ni mke wa mtu, kusikia hayo tu, ungepiga STOP,ufahamu upandacho ndicho unavuna period, pale huyu mke wa mtu alikuambia hilo ungemwambia asante wa kuwa mkweli kuazia leo sisi ni marafiki tu, hakuna zaidi, haijalishi hana mtoto , mume hazai au hili au kile, ni mke wa MTU. ungempa ushauri kaa hi hivyo muadapt mtoto, yeye na mume wake au umuachie maamuzi, lakini story za awe mpenzi zingeoshia hapo.mimi hata binti akiniambia ako na boyfreand , story mimi nasimalizia hapo, bona mabinti warembo wa kutupa wamejaa, bona niende kuharibu ndoa ya mtu, na nivuje amri ya mungu, NOT ME PLS

Kwa hiyo mwamba amri ya Mungu unaijua kwa mke wa mtu tu, haukusoma kwamba hata hao mabinti unaosema wapo wengi amri inakataza? Pia usiwe vuguvugu. Kama unazotaja amri, fuata zote hauwezi kutekeleza chache tu.

Wewe sema tu nafsi yako inakusuta au hauoni vizuri kuwa na mke wa mtu, usilete mambo ya amri kabisa.
 
Nkamu em lete muendelezo; kama nakuona ulivyoifukuza amani yako na ya ndoa yako, ukaikaribisha vita.

"...Niko chini ya Mwambaa, mwamba juu yanguu...wambie adui zangu, nipo chini ya Mwambaa..."

Hadi hapo ujue tu kwamba sijakuzaa, full amani.

Hizi stress zingine hapana kabisa, najua tu aliharibu, utaona mwisho wa simulizi.
 
kila mtu abaki na necha zake.... wanawake necha zetu nyingi ni siri make pale bustanini rol modo wetu aliongea mengi na baby nyoka

Kwakweli kila mtu abakie na necha zake!
 
Wamekutana pwagu na pwaguzi. Na kila siku tunawasema singo mommas hawana misimamo; sasa sijui hao singo daddies wanaopasha viporo na wazazi wenzao ndiyo wana misimamo? Kuna watu wana allergy na amani; ngoja tusubiri hilo la Hiroshima sisi

Em ongeza kidogo volum iko chini sana, rudia kwa nguvu kidogo tafadhali.
 
We usidanganywe, hatujawahi kuwa wengi kabisaaa.

Ingekuwa heri kama ungefanya kampango ka ubuyu mpendwa.

Hayo tutaongea faragha mpendwa, kwa sasa acha kwanza tumpe ushauri jemedari. Japo kimsingi, wanaume wote tunahitaji ushauri...kinachotutofautisha ni level ya majanga tu.

Heaven Sent sijakuzaa narudia tena, mwaka bado una makaratasi mpyaaa ndio tunaufungua, sijakuzaa.
 
Kuna papuchi za kula kama tulivyokubaliana katika umoja wa wanaume


Ila hizo za wake za watu hazipo kwenye katiba japo we are polygamist in nature


kwa yeyote yule mwanachama atakayetoka nje ya ibara atajua mwenyewe siku akiliwa kiboga
 
Hayo tutaongea faragha mpendwa, kwa sasa acha kwanza tumpe ushauri jemedari. Japo kimsingi, wanaume wote tunahitaji ushauri...kinachotutofautisha ni level ya majanga tu.

Heaven Sent sijakuzaa narudia tena, mwaka bado una makaratasi mpyaaa ndio tunaufungua, sijakuzaa.
Teh una mbwembwe. Usiharibu tu ankal, maana kigugumizi kitahamia kwenye mtetemo
 
Hahaha si nakuona una amani kama zote. Mungu akuepushe na mabalaa

Tazama ya kale yamepita yamekua mapya, hauamini kama hayo ni maneno kutoka kwa Baba K na M

Hapa tu wiki hii nimevuka mitego ya hatari, kama sio tuition ya mwaka jana ingekua najutia. Sasa hivi sidanganyiki!!

Na mie kile kipindi niliiona duara kabisa yaani dunia mviringo.
 
Back
Top Bottom