Nafikiri ili tuelewane mimi na wewe unatakiwa uweke vipaumbele ambavyo nchi inatakiwa kuwa navyo ambavyo ni tofauti na kuhamia Dodoma.
Mimi nafikiri kuhamia Dodoma ni jambo zuri sababu nchi imekuwa na muunganiko mzuri wa kimaendeleo pia itarahisisha utekelezaji wa mipango ya kimaendeleo katika eneo la usimamiaji utekelezaji wa mipango ya maendeleo ya nchi katika mikoa mbali mbali ukizingatia Dodoma ni kati Kati ya nchi.
Pia nafikiri watu mmekalili sentensi kuhamia Dodoma kama ni jambo lililogharimu Pesa nyingi, lakini kiuhalisia sijaona jambo kubwa lililofanyika Dodoma ambalo limegharimu Pesa kiasi kikubwa sababu kama Ikulu ya Chamwino, Bunge, ofisi ya waziri mkuu vyote vipo miaka mingi Kabla Magufuli ajawa Raisi ila jambo liligharimu Pesa ni la kuhamisha wizara zote, lakini kama umefika mji wa Kiserikali Dodoma uliopo eneo la Mtumba kwa Aina ya ramani ya zile Wizara na aina ya ujenzi uliofanyika utaamini ni Pesa kidogo sana imetumika katika ule ujenzi na ukizingatia wizara zote Zina Ramani inayofanana kila kitu ukitoa wizara ya Tamisemi yenye Jengo tofauti.
Ikumbukwe wizara zimejengwa na wanajeshi
Sent using
Jamii Forums mobile app
Ni hivi, mini siongelei kuhamia Dodoma kama mtu ninayekusoma magazetini.
Nimeona bajeti zikipitishwa na kuliwa miaka nenda rudi. Nineona namba zikibadilishwa.
Walioongoza CDA ni watu nawajua kwa karibu sana. Nikiingea nao wananipa malalamiko yao.
Hapa sijui hata kama watu wanajua CDA ni nini.
Nchi zinazoendelea zinatakiwa kuwa na uchaguzi mzuri sana wa vipaumbele. Ili, zianze na miradi inayozalisha kwanza, ili pesa chache za kigeni kabla ya kuwekezwa kwenye projects zisizo na uzalishaji kama kuhamisha mji mkuu, ziwe zimezunguka kwenye uzalishaji.
Kuhamisha mji mkuu hakuna uzalishaji. Ni straight expenditure tu.
Tuanze na vitu vyenye Return On Investment. Kuhamisha mji mkuu hakuna ROI.
Serikali imeingilia biashara ya korosho, imeangusha mapato ya exports za agriculture kwa asilimia 55, kwa mwaka mmoja tu, halafu tunahamisha mji mkuu?
Unasema kuhamisha mji mkuu hakuna gharama, hao watu wanaotoka Dar kwenda Dodoma wanapaa kwa ungo?
Serikali inatakiwa kuweka mazingira mazuri ya biashara, kukusanya kodi, kusambaza huduma za jamii, kuhakikisha usalama wa raia na mali zao.
Serikali inadaiwa madeni kibao, haijalipa wastaafu, haina social benefit network ya kueleweka, haija exploit agri ultural potential to even half, haya yote yangewe,a kufanyika vizuri sana kwa hizi fedha zinazounguzwa kwa ujinga wa kuhamisha mji mkuu.
Mji mkuu ulikuwepo tayari Dar, ume develop kwa biashara, naturally.
Tumeamua kushindana na mji ulioibuka naturally, kwa sisi kutaka gharama nyingi za kujenga mji mkuu tofauti.
Bila ya sababu ya kueleweka.
Na watu wanafurahia.
Unasema kuhamia Dodoma hakujagharimu kwa sababu Bunge na Ikulu vipo Dodoma miaka mingi, hata huelewi kwamba mimi nakosoa hilo jengo la Bunge na Ikulu kujengwa Dodoma.
Hivi unaelewa ninachijadili hapa?
Au unarukia kuhamia Dodoma ndani ya awamu ya Magufuli tu?
Mimi naongelea idea nzima tangu enzi ya Nyerere ilikuwa ujinga mtupu!
Sasa utasemaje Ikulu na Bunge tayaribyapo Dodima? Kwani mwaka 1961 kulikuwa na Ikulu na Bunge Dodoma?
Watu ambao kodi zao zinatumika ku homa mafuta safari za Dodoma, kujenga majengo ambayo tayari yapo Dar.
Ni umasikini wa mawazo. Wa kujitakia.
Sent using
Jamii Forums mobile app