Ushauri wa bure kwa Waislam

Ushauri wa bure kwa Waislam

Status
Not open for further replies.
Mkuu, this stuff is quite good, accurate and well reasoned.


Muslims have to come out with unqualified and doubtless justifications as to why it is unavoidable to establish Kadhi Courts under our Constititution.
 
unapotaja "waislam" uwe una specify, waislam wa dhehebu lipi? vilevile hakuna aliyewazuia waislam kuanzisha mahakama ya kadhi, hata serikali imewaruhusu ila imetaka watumie garama zao kwasababu hii ni mahakama ya kidini ambayo ni part of ibada kwenu ninyi, hivyo hamuwezi kuweka kipengele cha ibada kwenye katiba ya umma (katiba inayojumuisha waisilamu na pia wapagani na wakristo makafiri wasioamini uislam). kodi za wakristo na wapagani hazitakiwi kutumika kuendesha ibada yenu ya mahakama ya kadhi, huo utakuwa upendeleo kwa dini yenu. kwanini suala ambalo ni la imani ya mtu liwekwe kwenye katiba ya umma inayojumuisha waislam na watu wengine?how special are you among the many other Tanzanians? ninyi ni nani haswa hata katiba iwapendelee peke yenu, mbona mambo ya kikristo hayajaingizwa mle kwenye katiba, na je, mnataka tuamini kuwa uwezo wenu kifedha au kuendesha dini yenu ni mdogo hamuwezi kitu hadi kutegemea kodi zinazojumuisha wauza nguruwe na pombe ili muendeshe ibada yenu ya mahakama ya kadhi?(mmetuamia kuwa kadhi haikwepeki kwasababu ni haki ya kuabudu kwenu na kuendesha mahakama hiyo ni mojawapo ya ibada ya kiislam.).

mbona kuna waislam wenzenu wanapinga hili suala, ninyi mnaong'angania ni waislam special sana ehee, halafu UISLAM NI NDOA MIRATHI NA TALAKA TU? ukitaka kupractice uislam hapa tz utakuwa umetimilizwa kwa ndoa mirathi na talaka peke yake? masuala mengine yaliyoandikwa kwenye vitabu vyenu mtayaacha? akizini mtamwacha akahukumiwe na kafiri, akiiba aende kuhukumiwa na kafiri etc, halafu, hivi mahakimu na majaji wote Tanzania ni wakristo ehee?
Ninaposema Waislam ni wote siseme kundi fulani au wewe ulitaka niseme Waislam wa namna gani? Hebu nifundishe basi?
 
hizo jumuiya kama zitakuwa hazitambuliwi kisheria zitakuwa hazina maana.huwezi kuunda jumuiya inayo towa taraka kwa waislam pindi wakiachana kisha ukienda mahakamani unaambiwa taraka hiyo batili.

mahakama ya kadhi haiwahusu nyinyi wakristo,tunahusika sisi waislam.

Sheria ya mirathi kwa waislamu mtoto wa asie zaliwa ndani ya ndoa haruhusiwi kurisi mali ya marehem.je mahakama za serikali inalitambuwa hilo?

Wakristo kwanini mnapinga mahakama ya kadhi wakati haiwahusu?tukisema mna husda nyinyi wakristo mtabisha?

Nyinyi mnajifanya mnamjua Mwenyezi Mungu kulikowatu woote. Na mko wema daima. Mnauwezo wa kumwita mtu kafir na kumchinja kwasababu dini yake sio kiislam. Sasa kama nyinyie mko sawa na mnamjua Mungu kwanini mnaitaka hio KAdhi?

Maana kufanya kwenu mauaji na kuhalalisha mshanfanya mnamjua Mwenyezi Mungu (creator) na hamna lolote baya. Sasa mahakama kadhi ya nini??

Kikwete akiruhusu hili namshauri asikimbie nchi.








The King.
 
Walioweka Suala la Mahakama ya kadhi ndani ya Katiba ni Serikali ya CCM ndio wa

kulaumiwa Sio wa kulaumiwa Waislam. Waislam wameomba kuwa na Mahakama yao ya kadhi na hiyo Mahakama ya kadhi kazi yake ni mambo ya

ndoa, talaka na mambo ya mirathi. Waislam wanacho kitabu chao Quran amabacho hakibadilishwi na mtu yoyote tangu alipo kiacha


Mtume Muhammad S.A.W. sasa ni wajibu kukifuata kitabu chao wao wafuasi wa Dini ya Kiislam Serikali haiwahusu sasa Serikali ndio imeamuwa

kuweka Suala la Mahakama ya kadhi ndani ya katiba yao ambayo kila baada ya miaka Katiba inarekekbishwa wakati Kitabu cha Waislam

Quran ndani yake kuna Sheria za Mwenyeezi Mungu hazibadilishwi kamwe. Tuwaachie Waislam na Mahakama yao ya Kadhi.

Mambo ya Ngoswe Muachie Ngoswe Mwenyewe.
Naomba nijifunze kutoka kwako mkuu.
Tunafahamu kwamba hakuna maelewano mazuri kati baina Tanaka mbili zaislam hapa tz yaani Suni na Shia, sasa Je tutahitaji mahakama ya kadhi ya washia na mahakama ya kadhi ya wasuni?
Vipi tutahitaji magereza za waislam?
Samahani naomba nisikukwaze lengo nikujifunza mkuu.
 
Naomba nijifunze kutoka kwako mkuu.
Tunafahamu kwamba hakuna maelewano mazuri kati baina Tanaka mbili zaislam hapa tz yaani Suni na Shia, sasa Je tutahitaji mahakama ya kadhi ya washia na mahakama ya kadhi ya wasuni?
Vipi tutahitaji magereza za waislam?
Samahani naomba nisikukwaze lengo nikujifunza mkuu.
Dhehebu kubwa hapo Tanzania la Waislam ni lipi? Ninakuuliza wewe? ukisha nijibu hapo ndio hao wanaotaka Mahakama ya Kadhi.
 
Critical Reasoning. MP's OF CA ARE GOING ASTRAY WITHOUT CONSIDERING MAJORITY INTEREST.
 
Saalaam ndugu zangu. Kwakuanza we mgaratia unaonekana mvunjifu wa amani vpi ushtuke kuchangia mahakama ya kadhi wakati waisilam wamechangia ruzuku ya makanisa kwa zaidi ya miaka 30 . Je inakuwaje mahakama ya usuluhisho nyingine na ya kugawa nyingine? Na kwa faida yako anaetoa taraka si mahakama mume ndo anatoa taraka
 
Wakristo kwanini mnapinga mahakama ya kadhi wakati haiwahusu?tukisema mna husda nyinyi wakristo mtabisha?
Kama haiwahusu Wakristu, kwa nini mnataka uendeshaji wake ugharamiwe na serikali ambayo ina kila aina ya wananchi wenye kuamini dini na wasio amini?
 
Watu badala ya kuzungumza mambo muhimu ya nchi kama Muungano wa Tanganyika na Zanzibar, Kuundwa kwa Katiba ya Jamhuri ya Muungano, Uchumi wa nchi yetu, Umasikini, Maradhi Sugu , njaa, Ukosefu wa Ajira na Mafisadi wa nchi yetu.Badala ya haya kuzungumza ni muhimu kwa Taifa letu lilio masikini nyinyi munaacha shughuli zenu na kuwazungumzia Eti kwanini Waislam wanataka Mahakama ya Kadhi? Wa-Tanzania sisi ni watu wajinga sana kielimu tutakuwa kila siku tuko nyuma kimaisha hatutaendelea kabisa. Tuamkeni tuache yasiyotuhus tushughulike na mambo yanayoleta maendeleo ya nchi yetu jamani Wabongo amkeni tuko nyuma tena tuko shimoni hatutaweza kutoka ndani ya shimo pasipo na kufanya juhudi zetu sisi wenyewe. Miafrika Bwana ndivyo ilivyo.@screentouch
 
Kama haiwahusu Wakristu, kwa nini mnataka uendeshaji wake ugharamiwe na serikali ambayo ina kila aina ya wananchi wenye kuamini dini na wasio amini?
Wewe ndugu Idimi Msikilize Baba wa Taifa Mwalimu Nyerere anavyosema .

 
Last edited by a moderator:
Napenda kujua jambo moja, "wosia" wa marehemu unatambulika vipi katika suala hili la mirathi? Je mtu hana kauli juu ya kugawa mali zake kwa mtu yeyote amtakaye? Wakati wa kufanya zinaa hamuoni kama wakosaji ni wazazi na si mtoto anayezalwa? Kosa la motto ni lipi hata asipate sehemu katika mali za wazazi waliomleta duniani? Haki ya Mungu iko wapi hapa?
 
Kitu ambacho mimi sielewi ni kwanini hawa makafiri huwa wanaoongelea hii kitu?
Kwani inawahusu nini? Je wameambiwa ipo siku watashtakiwa humu?
Watuache bwana..wakiona nawao dini yao inahitaji mahakama basi waombe nawala sio kujifanya ni wasemaji wa dini nyingine....kila kukicha wakianzisha mada ni hii hii tu...Badilikeni bwana mnakera!

...kweli wewe kunguni wa ulaya
 
Kama haiwahusu Wakristu, kwa nini mnataka uendeshaji wake ugharamiwe na serikali ambayo ina kila aina ya wananchi wenye kuamini dini na wasio amini?

Napenda kujua jambo moja, "wosia" wa marehemu unatambulika vipi katika suala hili la mirathi? Je mtu hana kauli juu ya kugawa mali zake kwa mtu yeyote amtakaye? Wakati wa kufanya zinaa hamuoni kama wakosaji ni wazazi na si mtoto anayezalwa? Kosa la motto ni lipi hata asipate sehemu katika mali za wazazi waliomleta duniani? Haki ya Mungu iko wapi hapa?
Muulize huyo Idimi kaleta Topic ya Ukristo ndani ya Thread ya Mahakam ya kadhi imehusu nini hapo? Kwani suala la Mahakam ya Kadhi Wakristo linawahus kitu gani? Kwani Serikali ya Tanzania inafuata Dini gani?
 
Napenda kujua jambo moja, "wosia" wa marehemu unatambulika vipi katika suala hili la mirathi? Je mtu hana kauli juu ya kugawa mali zake kwa mtu yeyote amtakaye? Wakati wa kufanya zinaa hamuoni kama wakosaji ni wazazi na si mtoto anayezalwa? Kosa la motto ni lipi hata asipate sehemu katika mali za wazazi waliomleta duniani? Haki ya Mungu iko wapi hapa?

Muislam ana hak ya kuandika wosia na ikithibitisha kama kwel ni wosia utaheshimika hata kama katika wosia huo ataingizwa mtu nje ya familia ila kama marehem alikufa kabla hajaacha wosia hapo itabid wafungue mirath. Kuhusu mtoto huyu mtoto ni wa dhinaa na uislam umekataza dhinaa kukumkubali huyu mtoto ni sawa na kuikubal dhinaa na kwa adhabu hii watu wasingezaa nje ya ndoa kwa kuogopa kuwatesa watoto wao .so tungedhibit swala la watoto wa nje ya ndoa .hii maanake mtoto umleavyo ndivyo akuavyo
 
Nikiwa kama muislamu naunga mkono mahakama ya kadhi iwepo kwa mujibu wa sheria. Lakini suala la kuiendesha kwa kodi ya jumla ndio siungi mkono, naona itapelekea kuendeshwa na pesa chafu za wauza pombe na nguruwe.
Mimi mawazo yangu ni kuunda kitengo maalumu ndani ya TRA ambacho kazi yake itakuwa kukusanya kodi ya kuendeshea mahakama ya kadhi tu. Kitengo hiki kiwe na kitu kama fomu hivi ambayo walipa kodi wakiislamu wenye TIN wata declare kwa hiyari yao kuongezewa percent ndogo kwenye kodi wanazolipa kuendeshea mahakama ya kadhi. Naamini waislamu ni walipa kodi wazuri na wanaipenda dini yao, hawawezi kupinga utaratibu kama huu.

Ukishaweka TRA tayari inahusisha serikali,kwa kifupi tafuteni pesa au undeni taasisi ya kukusanya ata hizo pesa
 
kweli mdau kapotosha, lakini hilo la kusema eti uislamu umependelea mwanamke? hapo hapana, nchi za kiislamu zipo kibao Saudi, Iran, Iraq, Afghanistan, pakistani, somalia, northern nigeria etc, tunaona jinsi wanawake wanavyopendelewa huko ambako serikali inafuata FULL SHARIA not just KADHI COURTS!

taja sababu ya kutokwenda kuomba uraia huko kwenye gurantee kuishi kiislamu in all aspects...na ung`ang`anie hapa kwenye vikwazi vya kila namna...
 
Ndugu Ishamael naona unatokea sana na povu. Suala la Rasimu sasa limehamia mambo ya Mahakama ya Kadhi na mambo ya Serikali3 kusahaulika. Naona hoja imehama ghafla. Nami nichangie kidogo tu :

Kwenye andiko lako hoja 1 na 2 tunasema HAIKUHUSU kabisa, povu la nini? Huruma hii umeitoa wapi? So its non of your business!

Namba 3 ni kuwa Mahakama itashughulikia mambo ya ndoa na mirathi. Yamefafanuliwa vizuri ndani ya Quran. Mtu kama hataridhishwa anaruhusiwa kukata rufaa.

Namba4! Unaogopa kivuli wakati kitu siyo halisi. Nchini Uganda Mahakama hii ipo na hamna shida yoyote hakuna cha Sunni wala Shia amelalama ila wewe Ishmael unalalama wakati haikuhusu kabisa huruma hii ya ghafla inatoka wapi? Wakati wa mfumo wa vyama vingi tuliogopeshwa kuwa utaleta vita lakini huu ni mwaka wa 22 hamna vita wala nini. Hata hii ya Serikali3 zitavunja Muungano na au gharama linafanana na hili kwamba mtu unatokwa na povu kwa hisia tu na maslahi binafsi

Namba 5 ni hisia tu. Si kweli. Haki za akina mama ziko waz kabisa. Atakaeona hajatendewa haki anaruhusiwa kukata rufaa na au kwenda Mahakama za kawaida

Concern zako:

.Msingi halali na mahsusi upo
.Yule atakae ona Waislam wanafaidi aanzishe ya kwake na atueleze yeye atashughulikia mambo gani na atutajie mifano ya nchi zilizowahi kufanya hicho anachokianzisha
.Kipengele c kwa nini?
.Hamna kitu kama hicho. Mambo ya ndoa yako sawa sawa.
.Huo mkanganyiko unaousema ni upi au ni hisia zilezile?
.Namba f huo ni uongo wa kutunga tu
.Ina maana wewe umetumwa na hao wanawake wa Kiislam? Yule ambae hataridhika ataruhusiwa kukata rufaa

Recommendations zako:

Kwa muktadha wa andishi lote inaonekana ni hisia tu na wakati mwingine chuki tu. Hii ni historia iliyopo duniani kwamba jambo dogo tu wakianzisha Waislam kwa kuwa upande wa pili halipo basi maneno maneno hujitikeza kwa chuki tu.

Hivyo namalizia kusema kuwa kwa kuwa msingi wa hoja za andiko lako na hizo concern zako zimejaa hisia ambazo katu hazireflect uhalisia, nahitimisha kwa kusema kuwa Hoja zako zote ni VOID, na hivyo ni BASELESS, zinatupiliwa mbali!
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom