Na hili ndo tatizo la wafuasi wa Chadema ambao sasa nchi nzima saivi imeshuhudia mlivo misukule wa ajabu.
Kipanya ni mwandishi huru anayetoa habari zake kupitia katuni. Kuna haki zinalindwa na katiba ikiwemo uhuru wa kutoa habari, uhuru wa mawazo na kujieleza, Kipanya amesimama kwenye misingi hii bila kuvunja sheria yeyote ile, labda ninachokiona ni kuwa amewakamata kisawa sawa wafuasi wa Chadema na Lowassa kiasi ambacho mnashindwa mumzuie kivipi.
Kama mlishindwa kumuhonga ili achore katuni zinazowasifia kwa kula matapishi yenu basi kaeni mtulie sindano iwaingie vizuri.
Hongera sana Kipanya, Kusema kweli unaitendea haki tasnia hii ambayo kazi kubwa si tu kuhabarisha bali kuelimisha.
Namshauri Jakaya kabla hajamaliza muda wake atoe Nishani kwa wanamichezo,wanahabari na wasanii na katika hao Masoud Kipanya awepo.
Kipanya ni hazina katika taifa hili kwa upande wa tasnia ya habari na katuni.