Ushauri tafadhali kuhusu wakwe kuongea kilugha

Ushauri tafadhali kuhusu wakwe kuongea kilugha

Wazazi wetu wengi wamekulia huko vijijin na Lugha inayotumika huko si kiswahili ni kinyumbani..Na wanasema akiongea kiswahili anahisi kinamchelewesha na bila yeye kujua anajikuta keshakubadilshia gia hewan toka kiswahili karudi lugha ya hme na wengi hawana maana mbaya ya kusema mtu ila ni mazoea tu...Hapo ndiyo busara inahitajika kidogo kama mke keshamtonya Mume kwamba hajihisi salama wanapoongea kilugha Mume ilitakiwa ajaribu kujibu kiswahili atleast wife atapata picha ya hayo mazungumzo na atakuwa na amani..
ajifunze yeye lugha yao hakuna namna!
 
Kwani wakiongea kilugha yeye anachunika ngozi???

Pyeeee mbona kuna binadamu wanapenda kukompliketi maisha???
 
Ukiwa na msimamo mkali kama huo basi utaanza kusikia maneno kutoka ukweni wakisema

Wazee:
"yaani huyu mtoto kaolewa huku kwetu miaka nenda miaka miaka rudi hata kusalimia kilugha tu hawezi? Hawezi au hataki? Au anatudharau? Kajifunzaje Kiingereza na Kifaransa leo iweje kashindwa kujifunza kilugha chetu rahisi kama hiki?

Mawifi:
Dawa yake ndogo huyu. Ni kumtafutia kaka yetu msichana bomba wa kabila letu - basi hata kama ni kimada tu. Ataisoma namba huyu.

Wewe:
Huna hili wala lile unajikuta umeachika, au amani inakuwa ndogo katika familia.

Jifunze lugha ya wakwe zako - hata kama utaivunjavunja unapoizungumza. Wakwe zako (na muhimu zaidi, mume wako) watafurahia sana kuwa unajitahidi uijue.

Ushauri wa bure huu.
Mtu akimuacha mkewe kwa sababu ya lugha ujue hakumpenda tu aisee......
 
This is too much asee, wanajua mie kabila lingine wanaongea lugha all the time afu nianze tena kuulizia cha kufanya mmh ngumu, sasa hapo kwenye kumtafutia kaka yao dem itabidi hao dada ndo wawe madem zake ili waelewane lugha.....
Kuna lugha za kujifunza kirahisi, namie ni mwepesi sana kujifunza lugha (sio lugha ya queen Eliza ha ha ha) Ila kuna lugha zingine mmh kama kiiraq(mbulu) hiki kimenishinda zaidi ya salamu siambulii kitu na hii ndo lugha ya ukweni kwangu
Rahisi tu hiyo,mwezi tu watosha. Ayi laway,baba laway,a i doma,... Hâta JPM anaimanya
 
Rahisi tu hiyo,mwezi tu watosha. Ayi laway,baba laway,a i doma,... Hâta JPM anaimanya
Nshaisikiliza sana sielewi, nimekaa na wanyiramba miezi Sita tu nikajua kinyiramba, hicho kimenishinda
 
Ishue happ unajaribu kutumia bsara kwa kuwa huelwi means wamekuengua mazungunzo...tafuta playstation portable wao wakiogea we cheza mortalkombat au resident evil
 
wanawake msijifanye hakuna mnachojifunza na kung'ang'ania kujifunza kupaka rangi kucha tu. wewe kujifunza lugha ya ukweni inakushinda nini?? mbona ukiwa na wa kwenu unaongea cha kwenu??
 
unapokubali kuchanganya kabila haya mambo hayakwepeki.
mimi huwezi ukanifanya nianze kumtesa mama yangu kuongea kiswahili wakati hakijui. kuna vitu ni vyepesi tu. jifunze hata cha kuombea maji
 
Mtu akimuacha mkewe kwa sababu ya lugha ujue hakumpenda tu aisee......
Ngoja nikupe mfano huu:

Mume kaoa msichana mzuri tu lakini kila ndugu zake (wazee, mawifi na mashemeji) wakija kuwatembelea anakuwa kanuna au hawachangamkii. Hili sio kosa la kumuacha mke lakini litafanya hii ndoa isiwe na amani kwa sababu mume hatajisikia raha ndugu zake wakija kuwatembelea.

Vile vile, kama mke hataonesha ukaribu na vitu anavyopenda mume wake (marafiki, michezo, starehe za jioni, au kuzungumza kilugha na ndugu) haisababishii kuachwa bali itamfanya mume asiwe karibu (kihisia) na mkewe.

Kujifunza lugha ya ukweni sio utumwa au udhalilishaji, bali unamuashiria mumeo kuwa ungependa kushiriki mazungumzo anapoongea na ndugu zake. Hivyo hivyo mume nae ajitahidi kujua lugha ya ukweni kama nao wanapenda kukiongea kilugha chao wanapokutana.

Hiki sio kitendo cha ukandamizaji bali ni kitendo cha mapenzi/mahaba. Ni sawa na mke kujifunza kucheza pool (billiards) ili acheze na mumewe asubuhi - siku ya kazi (hii nimechapia tu).
 
Ukiwa na msimamo mkali kama huo basi utaanza kusikia maneno kutoka ukweni wakisema

Wazee:
"yaani huyu mtoto kaolewa huku kwetu miaka nenda miaka miaka rudi hata kusalimia kilugha tu hawezi? Hawezi au hataki? Au anatudharau? Kajifunzaje Kiingereza na Kifaransa leo iweje kashindwa kujifunza kilugha chetu rahisi kama hiki?

Mawifi:
Dawa yake ndogo huyu. Ni kumtafutia kaka yetu msichana bomba wa kabila letu - basi hata kama ni kimada tu. Ataisoma namba huyu.

Wewe:
Huna hili wala lile unajikuta umeachika, au amani inakuwa ndogo katika familia.

Jifunze lugha ya wakwe zako - hata kama utaivunjavunja unapoizungumza. Wakwe zako (na muhimu zaidi, mume wako) watafurahia sana kuwa unajitahidi uijue.

Ushauri wa bure huu.
Sio lazima kujifunza lugha ya mtu,hata mimi yangu hajui nitafutiwe mume kwetu?
 
This is too much asee, wanajua mie kabila lingine wanaongea lugha all the time afu nianze tena kuulizia cha kufanya mmh ngumu, sasa hapo kwenye kumtafutia kaka yao dem itabidi hao dada ndo wawe madem zake ili waelewane lugha.....
Kuna lugha za kujifunza kirahisi, namie ni mwepesi sana kujifunza lugha (sio lugha ya queen Eliza ha ha ha) Ila kuna lugha zingine mmh kama kiiraq(mbulu) hiki kimenishinda zaidi ya salamu siambulii kitu na hii ndo lugha ya ukweni kwangu
Ewe ka salt hujui kujifunza lugha ya wakwe ni kama umekubalika? Akikoroge tu akivunje vunje tu ila mme wake naye ndo bomu kwanini asimlazimishe tuition week moja kabla ya kuja ili wakifika ana kianzio?
 
Sio lazima kujifunza lugha ya mtu,hata mimi yangu hajui nitafutiwe mume kwetu?
Kujifunza lugha ya mpenzi wako ni kitendo cha mahaba na sio ukandamizaji. Nyie watu hamjui hata hizi romance za vijijini jamani? Mkoje nyie?

Hujui ni kiasi gani mume wako anavyokunwa anapokuona unaongea na kucheeeka na mama yake. Huyo mume hata kama alikuwa ameficha mgao wake wa Escrow mtungini atautoa tu akupeleke Dubai. Muwe na vijiujanja ujanja kidogo wakina dada. Hee! Lugha tu ndiyo unayogangamalia hivi? Wengine wanasema "MWE!"
 
Kujifunza lugha ya mpenzi wako ni kitendo cha mahaba na sio ukandamizaji. Nyie watu hamjui hata hizi romance za vijijini jamani? Mkoje nyie?

Hujui ni kiasi gani mume wako anavyokunwa anapokuona unaongea na kucheeeka na mama yake. Huyo mume hata kama alikuwa ameficha mgao wake wa Escrow mtungini atautoa tu akupeleke Dubai. Muwe na vijiujanja ujanja kidogo wakina dada. Hee! Lugha tu ndiyo unayogangamalia hivi? Wengine wanasema "MWE!"
Sasa mbona inaongelewa kama lazim?nisinge react hivi.kama ni hiyari.ntajifunza nikitaka lakini sio itumike kama fimbo,ungeoa dada zako wanaijua vizuri tu
 
Sasa mbona inaongelewa kama lazim?nisinge react hivi.kama ni hiyari.ntajifunza nikitaka lakini sio itumike kama fimbo,ungeoa dada zako wanaijua vizuri tu
Huyu bwana alipokuja kukuoa wewe aliwapita wengi tu wa kabila lake. Hii ina maana amekupenda wewe zaidi. Tunachozungumzia hapa ni njia ipi ya kumfanya mke awe karibu na watu wa ukweni (hasa kama wanapenda kuongea kilugha).

Mfano rahisi.
Sio lazima kila mke ajue kupika.

Kutojua kupika (chakula alichopenda mumeo wakati anakua - comfort foods) sio kosa lakini kutotaka kujua kupika anachopenda mumeo ni kosa. Sio kosa la kuachika bali usilalamike mnapotembelea kwao ukamuona na shamra shamra anapokula chakula kilichopikwa na mama yake.

Ushauri - Jifunze kupika chakula anachokichekelea mumeo wakati kikipikwa na mama yake (mama mkwe wako).

Lugha haiko mbali sana na chakula katika mfano huu.
 
Mimi wakiongea lugha yao mbele yangu najua hayanihusu. Wakitaka kunihusisha wataongea lugha ninayoelewa.
Najua salamu
 
Mbona anajipa stress zisizo za lazima au hajiamini? tena ashukuru mungu yani ningekua mie wakiongea lugha yao mie nakua
chumbani na tv nawasha au naingia JF kwa raha zangu,akiuliza why umekaa huku namwambia "Habibi unajua napenda
nikupe nafasi uonge na Mama huenda ana mengi yatakayo tusaidia sasa kwasababu mimi sielewi lugha nakupa nafasi
wewe umsikilize halafu utakuja kinielezea halafu una mpa bonge la Kiss,bila kukasirika as if umependa alivyofanya..
lakini ukiuliza kasemaje mbona hasemi nikaelewa sometimes wakwe wanafanya visa hasa kwa watoto wao wa kiume..
Nimekupima sana we mwanamke unaonekana una mahaba sana,
 
Hiyo lugha wanayoongea inamkera nini rafiki yako?

Kule kwetu mimi peke yangu ndio nimebahatika kujua japo kiswahili.
 
Back
Top Bottom