Ushauri tafadhali kuhusu wakwe kuongea kilugha

Ushauri tafadhali kuhusu wakwe kuongea kilugha

Habari zenu wana jf
Kuna rafiki yangu ameolewa katika familia kabila ni tofauti na lake..

Sasa linapokuja swala la vikao ukweni hata wakwe wakija nyumbani kwake ni kilugha kinacharazwa... alijaribu kumueleza mumewe akamwambia atalifanyia kazi lakini holaa mambo yaleyale..

Kwa upande wake anajiskia vibaya na ukizingatia yeye ni wa kwanza kuolewa wengine ni wanawake na wameolewa anajiona sio sehem ya hiyo familia anaogopa kuwaambia wakwe..

Je Afanyeje?
Hawa watakuwa wasukuma au wahaya!
 
" nitalifanyia kazi " Siasa imetuharibu Sana.
Wazee Na lugha zao, mwambie azoee
 
kwan lazma ujue kila lugha,we tulizana na aliyekuweka ndan basiii.mengine ziada sana.
 
Yaan Kuna Wanawake huwa wanatafuta sababu ya mifarakano tu.
Umeolewa, Unaishi vizuri na mume wako bado unaanza Habari ya kilugha ambacho walianza kuongea hata Kabla hujazaliwa.
 
Aiseee kuna watu wanamind vitu vidogo vidogo yani mie wangeongea weee hata wakeshe nisingekuwa na time nao
 
Jamaa anahofu kama kuna dili linachongwa ili kumzunguka. Kwa ustaarabu haipendezi kama mmekaa sebuleni au sehemu yoyote halafu ghafla jamaa wanabadilisha chaneli na kuongea kikwao wakati wewe upo. Lazima ujihisi kusemwa vibaya
 
Ajifunze tu kama ana mashaka...

Ila wazee wanapenda kilugha na haimaanishi kwamba wanamsema wala.
 
Ubinafsi wanaficha nn? WanTaka kufanya nn cha Siri? Sio watu walio starabika
 
Umeongea vizuri hapo pekundu. Kama unampenda mume wako basi utajifunza hiyo lugha.

Usiniambie kuwa kuna umri fulani ubongo wako unaganda na hauwezi kujifunza lugha (kukumbuka maneno na matumizi yake). Ni umri gani huo? Katika umri huo unaoufikiria, kama ukihamia mji mpya kabisa hivi hutajifunza na kuzikumbuka njia za hapo mjini na za kurudia nyumbani?

Kama ulivyosema kujifunza lugha mpya ni matakwa yako tu na hayahusiani hata kidogo na umri.

Hutaamini nikikuambia umri wangu lakini kwa sasa ninajifunza Kiarabu (chanzo cha maneno mengi ya Kiswahili) na Kilingala (nina collection kubwa sana ya nyimbo za bolingo). Sasa hivi ninapwaga vizuri tu na hizi lugha mbili (kwa wakati mmoja). Hii inawezekana kwa sababu mimi mwenyewe nimependa kujifunza. Ukinilazimisha nijifunze lugha nisioipenda (au kutaka kuijua) basi sitaijua (sitaweza kujifunza) hata kama ningekua na miaka 16.

YES - tunaweza kulinganisha kujifunza lugha na kujifunza kupika.
Usilete sababu zisizokuwa na msingi. Wewe sema hutaki kujifunza hiyo lugha tu na sio kuwa huwezi kujifunza.
Ulisoma kombi gani kama ulibahatika kusoma advance?waliosoma masomo ya lugha watakusaidia kuhusu ujifunzikaji
 
Back
Top Bottom