Ushauri: Nifanyeje juu ya hali hii ya maisha yangu?

mbilitanotano

Member
Mar 8, 2022
61
32
Wakubwa kwangu shikamoni, wadogo kwangu habari zenu ?

Hongereni kwa majukumu na afya njema, poleni mnaoumwa Mungu akawajaalie mpone.

Ndugu, Nilizaliwa miaka 31 iliyopita. nilipenda sana kuwa mwanajeshi wa jeshi la wananchi, sikufanikiwa kutokana na umri wangu kupita ule unaotakiwa, kukosa fani zinazotakiwa huko, na kutokuwa na mtu wa kunishika mkono kuingia huko. Nina shahada ya sayansi.

Kuna mahala serikalini nimejitolea kwa miaka minne sasa, walivyotoa ajira kupitia utumishi nimebwagwa kwenye usahili nikashindwa ! wakaajiriwa vijana wengine ambao hawakuwa wakijitolea pale. Nimefanya saili nyingi za kuomba kazi utumishi na kwingineko lakini sijafanikiwa kupata kazi.

Hapo Kibaruani wanatoa sh. 15000 kwa siku mtu atakayofanya kazi, (300,000 na kidogo kwa mwezi maana ijumaa pili hatufanyi kazi) hicho kiasi cha fedha kwa mkoa wa Dar es salaam kinaishia kulipa kodi, nauli za kwenda kibaruani, kununua umeme, kula kwa mama ntilie (2000 msosi mmoja), kulipia taka, kulipia ulinzi mtaani, sadaka kanisani, VOCHA na matumizi mengine; sijafanikiwa kuweza kuweka akiba. Sina mchumba, mke wala mtoto maana sina hela za kuniwezesha kuwahudumia, Ukinunua napo magonjwa lukuki .... ila homoni za mwili zenyewe zinafanya kazi yake hazielewi hali yako kiuchumi kwa hiyo ni shida tupu.

Huwa ninatamani sana kwenda jeshini lakini umri, fani na konekisheni ni changamoto

Ninatamani kuoa lakini sina kazi, nikifikiria kurudi kijijini kulima, sawa lakini mtaji wa kulimia na mashamba sina. Nafikiria kusoma 'post graduate diploma in education' ili niwe na taaluma ya ualimu badae niombe kazi serikalini kama mwalimu wa fizikia n.k lakini hela ya kulipia ada (milioni mbili) sina. Huwa ninapenda pia kufanya biashara ya stationery lakini mtaji nao sina !

Ninawaza kurudi chuo kusoma kozi za afya kwa diploma, ada sina ! Nipo njia panda ndugu ninaombeni mnishauri nifanyeje ili kupata hela, niache kujitolea niende chuoni kusoma, niajiriwe serikalini au taasisi binafsi au nifanye miradi hiyo, n.k maisha mengine yaendelee.

Ninatanguliza shukrani kwa ushauri wenu, ninawatakia mda mwema.
 
Hakuna maisha rahisi Tanzania ndugu yangu kwa sasa,watu wanabebana

Nakushauri oa hiyo laki tatu inatosha

Chagua mwanamke mwenye kujua maisha mkapange uswekeni na yeye mpe nradi wa kupika vitumbua awe anauza nyumbani apo
Kidogo kidogo utaona
 
Unapata laki 3 kwa mwezi kuoa unaogopa??

kuna watu wanafanya kazi viwandani kwa siku 6000 na wana familia.

itakuwa una malengo makubwa sana. Ndio maana ukijitazama unaona kuoa bado.
Pambana mkuu hapo kwanza ni kuwa na uhakika wa mahitaji ya msingi. Uwe na hata chanzo mbadla kidogo cha mapato.

piga ua kwa siku unauwezo wa kujibana ukatumia kiasi kisichozidi 10,000
hiyo 5000 weka malengo uwe unaisevu na uzuri ndio kwanza january hii.
mpka December tayari utakuwa na kiasi kisichopingua mil 1.5

katika kipindi cha hii miezi 11 unasevu huku unatafuta kitu mbadala chankuwekeza hiyo mil 1.5

mengine tumuachie Mungu. Jitahada hazizidi bahati na kudra.

Usinywe pombe, usicheze kamari punguza misaada na huruma zisizo na lazima. Acha uzinzi.
 
Watu wanaishi kwa mishahara ya laki na nusu wewe unalalamika laki 3 ? wewe shida yako ipo kwenye matumizi na hata ukipata laki 6 huenda isikutoshe. Swali lako inabidi liwe jinsi ya kuishi Dar kwa laki 3 na sio kulalamika pesa haitoshi

Una miaka 31 hapo, hayo mawazo ya kwenda kusoma chuo fyekelea mbali kabisa, wenye umri kama wako wanaoenda vyuoni huwa tayari wana ajira au biashara wanaenda kujiongeza tu huku wanaendelea kulipwa mishahara ama kupata faida, sio kusema kwamba wategemee vyeti viwape ajira, vyuo vinaanza mwezi wa kumi mwaka huu utamaliza 2026 mda huo tayari upo umri wa mwisho katika vigezo vya kuomba ajira,yani utakuwa umebakiza mwaka moja kupata ajira, nenda kama una connection ila kama utafata utaratibu wa kawaida hio ada bora ufanyie mambo mengin.... .

Nachoweza kukushauri hakunaga kizuri cha halali kinakuja bila jasho, fanya kujibana huu mwaka mzima uwe unatumia laki 2 tu na inayobaki laki 1 unaitunza, hadi mwaka unaisha unaweza ukawa umekusanya milioni 1 ambayo inaweza kuwa mtaji wa biashara hata ya chakula ama kwenda kulima huko kijijini kwenu.
 
Wakubwa kwangu shikamoni, wadogo kwangu habari zenu ?

Hongereni kwa majukumu na afya njema, poleni mnaoumwa Mungu akawajaalie mpone.

Ndugu, Nilizaliwa miaka 31 iliyopita. nilipenda sana kuwa mwanajeshi wa jeshi la wananchi, sikufanikiwa kutokana na umri wangu kupita ule unaotakiwa, kukosa fani zinazotakiwa huko, na kutokuwa na mtu wa kunishika mkono kuingia huko. Nina shahada ya sayansi.

Kuna mahala serikalini nimejitolea kwa miaka minne sasa, walivyotoa ajira kupitia utumishi nimebwagwa kwenye usahili nikashindwa ! wakaajiriwa vijana wengine ambao hawakuwa wakijitolea pale. Nimefanya saili nyingi za kuomba kazi utumishi na kwingineko lakini sijafanikiwa kupata kazi.

Hapo Kibaruani wanatoa sh. 15000 kwa siku mtu atakayofanya kazi, (300,000 na kidogo kwa mwezi maana ijumaa pili hatufanyi kazi) hicho kiasi cha fedha kwa mkoa wa Dar es salaam kinaishia kulipa kodi, nauli za kwenda kibaruani, kununua umeme, kula kwa mama ntilie (2000 msosi mmoja), kulipia taka, kulipia ulinzi mtaani, sadaka kanisani, VOCHA na matumizi mengine; sijafanikiwa kuweza kuweka akiba. Sina mchumba, mke wala mtoto maana sina hela za kuniwezesha kuwahudumia, Ukinunua napo magonjwa lukuki .... ila homoni za mwili zenyewe zinafanya kazi yake hazielewi hali yako kiuchumi kwa hiyo ni shida tupu.

Huwa ninatamani sana kwenda jeshini lakini umri, fani na konekisheni ni changamoto

Ninatamani kuoa lakini sina kazi, nikifikiria kurudi kijijini kulima, sawa lakini mtaji wa kulimia na mashamba sina. Nafikiria kusoma 'post graduate diploma in education' ili niwe na taaluma ya ualimu badae niombe kazi serikalini kama mwalimu wa fizikia n.k lakini hela ya kulipia ada (milioni mbili) sina. Huwa ninapenda pia kufanya biashara ya stationery lakini mtaji nao sina !

Ninawaza kurudi chuo kusoma kozi za afya kwa diploma, ada sina ! Nipo njia panda ndugu ninaombeni mnishauri nifanyeje ili kupata hela, niache kujitolea niende chuoni kusoma, niajiriwe serikalini au taasisi binafsi au nifanye miradi hiyo, n.k maisha mengine yaendelee.

Ninatanguliza shukrani kwa ushauri wenu, ninawatakia mda mwema.
Unalalamika pesa huna then ukipata unakwenda kugawa kanisani ,aisee utakuwa na matatizo ya akili si bure.
 
Hapa nmeona unawaza kurudi shule tu as if hyo ndo solution pekee.
In life kuna vitu 2, ukiona jambo flan halifanikiwi kwa muda mref kuna vitu 2 vya kujiuliza, its either unaambiwa utemane nalo au unaambiwa ukaze zaidi kulifanikisha. Hapi n masuala ya imani. N juu yako.
Kuhus laki 3, kwanza shukuru hata unaipata, wengi watakwambia u save zaid n.k, lkn kichwa chako inabd ubadilishe mindset uanze kuwaza utafanyaje kuiongeza rather than kuisave. Hapo ndo ideas utaanza kuziona.
Wewe n mwalim mpka hapa, hapo unapofanya wizarani si uongee na maboss wako wenye watoto hata uwe unawapiga tuisheni?
Uko dar mji wenye fursa kibao, unaeza hata anza ka biashar uchwara humo humo wizarani kwa hao staff wenzako ili uraise capital.
Smtyms ukingoja sana ajira utaishia kua dissapointed.
Kuhusu kuoa, ng'ombe hazeeki maini, its either uweke ultimatum lets ssay ukifika 35 lazma uoe, au uoe yoyote anaepita mbele yako anaeweza kuvumilia hali yako lakn just knw siku ukishika chambi huyo dem utamtosa na hapo n kujilaanisha full suit
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom