Mafuta,spare parts Subaru Forester iko juu sana,sana sana!!!!!zingatia hiyo gari ataitumia mji gani,mji kama Dar penye madereva wengi vichaa hiyo itakupasua kichwa,mf ikivunjwa taa ya nyuma bei yake 400,000/350,000,taa mbele iko bei sawa na nyuma,indicotor moja sio chini ya 200,000,bumper la mbele 1.2/1.5mil,radiotor/condensor vyote sio chini 1.6mil,(hizi ni bei za used)tuseme imepigwa bonge la mzinga kwa mbele ikulazimu kununua norse cut(kipande cha mbele kikiwa na kila kitu)hesabu yake mpaka gari irudi mtaani utaacha hapo hela ya kununua Ist au Passo mpyaaa,kwenye chassis ndo penye balaa zaidi then spare zake waeza kuwa na cash ukashindwa kuzipata unaambiwa uagize mpya hizo bei za mpya ukiwa vibaya kifedha gari utafugia kuku uwani,nisikutishe sana mkuu angalia kama mfuko wako umekaa vizuri mnunulie wife hiyo gari kweli ni nzuri but ndo hivyo,nimechangia nkiwa na xperience na hizo makitu so sijabahatisha.