Ushauri: Diamond na Wasafi FM zingatieni haya

G.Man

JF-Expert Member
Feb 9, 2014
1,008
2,002
Salam wakuu

Nimepata nafasi ya kusikiliza Wasafi FM kwa siku kama mbili sasa baada ya kuwashwa kwenye mkoa niliopo, na nimeweza kusikiliza vipindi vya asubuhi kabisa(goodmorning) na cha jioni(mgahawa). Kwasababu natamani mfanye vizuri zaidi, binafsi nimeona dosari Kadhaa zinazotakiwa kushughulikiwa kama ifuatavyo:

Ethics za utangazaji
Watangazaji wengi wanakosa `Swags` za kutangaza, wanaongea kama wanapiga story tu kijiweni, kupishana kwenye Mic(kuongea) kwakwel naona ndo changamoto kubwa zaidi, watu hawapeani nafasi kuna wakati kelele zinakuwa nyingi utasema mnabishana, japo sio wakati wote ila ni mara nyingi

Usomaji wa matangazo na Habari
Hii ni changamoto nyingine kubwa kabisa, matangazo naona wanasimulia tu wakati mwingine wanapotelea kwenye story mpaka unaweza fikiri tangazo lilishaisha kumbe bado. Kwenye Habari kwakweli bado, hamna utulivu hasa sound track kwa mbali cjui kwanini inawekwa wakati mtu anasoma habari kamili

Segment nyingi sana ndogo ndogo kwenye kipindi kimoja
Ambavyo huwa naona ni kwamba segment hasa zinagawanya panapo badilishwa wadhamini au kuingiza kitu kipya kwenye kipindi, mfano labda muda wa magazeti, lakini naona wasafi kuna segment nyingi alaf unakuta wanaongelea kitu almost kilekile cha mwanzo(simaanishi break)

Kum-refer Diamond bila hoja ya msingi!
Kuna wakati unaweza tafsiri kama watu wanajipendekeza kwa boss wao, ni sawa. Lakini kidogo sioni kama kuna haja ya kuleta story kumuhusu ili tu uonekane mna mahusiano ya ziada nyuma ya kioo, yule ni Boss wenu hata wasikilizaji tuna expect mtakuwa na mahusiano mazuri tu nje ya kazi. Mjue tu Diamond ana kofia tofauti, sio kila msikilizaji wenu basi ni shabiki wake na haitakuwa ni jambo jema kwa media ikiwa ndivyo, Kikawaida naona watu wengi hukerwa na mtu anaesifia sana vitu vyake hata kama haiwahusu

Mrundikano wa watangazaji kwenye kipindi
Kama watangazaji wakiwa wengi alafu wakashindwa kuongea kiutaratibu inakuwa ni kero,pia kuna ambao sio wabishani basi unaweza hata usijue kama wapo kwenye kipindi.

Hayo ni baadhi tu ya nliyoweza kuyaona japo yako mengi zaidi. Nitaendelea na maoni yangu na ushauri...
 
N nd watu waliofngiwa n kukaa wiki moja kw mafunz zaidi (wasafi village),jpo vpo walvyboresh lkn bado kun hvjkaa sawa haswa hyo mgahwan
 
Nipongeze tu uongozi mzima wa media, mnaonekana mna nia ya dhati ya kuifikisha Redio yenu mbali. Binafsi napenda kuwashauri kulingana na kero nlizozisema mwanzo

Nidhamu ya kazi kwa watangazaji na swags za kutangaza
Ukienda kwenye sherehe alafu wakawa wanaongea wageni waalikwa na akaongea Mc, ni rahisi kumjua Mc kwa vile anavyoongea tu . Nashauri muache kusimulia au kuelezea, Mtangaze, wale ambao wamepewa nafasi bila kusoma utangazaji ni vyema wakala kozi kidogo, nampongeza David Rweikiza anajitahidi sana kipind cha asubuhi
Usomaji taarifa ya habari na matangazo
Japo sijui utaratibu ni upi ila kama Wasafi mngepata access ya kurusha matangazo ya idhaa za Kiswahili mngekuwa mmecheza eko sana, alafu vipindi vya habari (hasa za ndani) mviingize kwenye vipindi tu vya kawaida kama mnavyochambua magazeti yani. Kuhusu matangazo ni vyema watangazaji wakayasoma kama yalivyo alafu kama kuna neno la kuongeza aongeze baada au kabla. Aliyah, Calipso na Jonijoo walikuwa wanafanya vizuri sana kuhusu matangazo kwenye Block89. Atleast the switch pia nliona wakisoma matangazo fresh
Watangazaji kwenye kipindi
Nmeona thread kuhusu Musa Hussein humu, kuwa haskiki Clouds, nafikiri ni moja kati ya watangazaji wazuri sana, kama kuna uwezekano wa kumsajili huyu jamaa ndani ya kikosi wala msisite, aingie kwenye Gud Morning, Chumvi na Ndimu kuna mda wanafurahisha japo wana fujo sana wapunguze,ila nashauri Zembwela apewe kipindi cha pekeake kabisa mida ya jioni hivi awe anaongelea matukio, kero au changamoto za watu mbalimbali nahisi atafanya vizuri sana, Kitenge asipayuke sana, pia kama hawezi kusubiri mtu amalize kuongea apewe vipindi vya siriaz kama mahojiano hivi akiwa mwenyewe pia n.k. Alafu kupunguza mazoea zaidi yule dada wa asubuhi pia aondoke(aende hata kwenye mambo ya taarabu hivi) alafu awekwe @ImCalipso kama host kwenye kipindi hicho cha asubuhi.
Kuhusu Diamond
Ifike mahali watangazaji waifanye media ionekane imesimama yenyewe, ili kuwavuta hata wasikilizaji wasiomkubali boss wenu, He is Great, lakini kila mtu ana mtazamo wake na hamuwezi kuingilia, hamna haja ya kumpa credit kupita kiasi hata kama anawapea mshahara unless iwe ni lazima. Kubalace shobo ndo kiswahili fasaha kwenye hili
Kuhusu vipindi
Nashauri muda wa baadhi ya vipindi kama mashamsham upunguzwe kidogo, mambo ya taarab tu kuongelewa masaa matatu alaf kila siku sioni kama ikoje, cjui haswa contents zao lakin naona kama parefu sana, alaf kuhusu sauti naona kama watu wanaongelea mbali na Mic, pia kuna ka base flani mngeongeza ingekaa powa, baadhi ya segment pia ziwe tu ni commercial break tu

Mwisho naomba Mungu awajalie mzidi kufanya vizuri hadi kimataifa. Msione haya pia kuiga kitu kizuri hasa kwa wapinzani wenu kama Clouds, ambao wapo kwenye game mda mrefu wanafanya kwa u professional naona hasa kipindi cha asubuhi. Najua mnaweza msiwe na experience nzuri ya maisha ya media maana mmeanzia juu sana na tuna expect high kutoka kwenu kulingana na brand yenu..
 
G.Man hiyo hoja yako ya 4 naiunga mkono kwa asilimia 💯 Binafsi inanikera kumtaja Diamond bila sababu za msingi ndio shida kubwa ya Watanzania kujipendekeza kwa boss sijui itaisha lini hata wafanyakazi wa clouds wanatabia hii ya kumtaja ruge au kusaga Sana as if wataongezewa mishahara hata pia maofisini hipo hivyo hivyo watanzania wengi wanatabia ya kujipendekeza kwa maboss wao
 
G.Man hiyo hoja yako ya 4 naiunga mkono kwa asilimia 💯 Binafsi inanikera kumtaja Diamond bila sababu za msingi ndio shida kubwa ya Watanzania kujipendekeza kwa boss sijui itaisha lini hata wafanyakazi wa clouds wanatabia hii ya kumtaja ruge au kusaga Sana as if wataongezewa mishahara hata pia maofisini hipo hivyo hivyo watanzania wengi wanatabia ya kujipendekeza kwa maboss wao
Baada ya msiba wa Ruge Clouds pia walitia fora, maana kila mtu ambae alikuwa na kastory kumuhusu basi alikuwa anataka kushare tu yani sijui ionekane walikuwa na ukaribu hivi! ila inaboa
 
Back
Top Bottom