Watanzania tuamke, viongozi wanatudharau

Kiranja wa jamii

JF-Expert Member
Jan 2, 2023
222
528
Kuna mjadala wa kuletewa msaada wa mchele na nchi ya Marekani na walengwa ni vijana wetu walioko mashuleni.

Kwa bahati mbaya kizazi hiki hakina uwezo wa kuhoji na wazazi wao wamekuwa machawa wanaosifia kila kitu kinachofanywa na mabwana wakubwa bila kujali madhara ya kitu chenyewe.

Wazazi na wanafunzi wa shule hizo wanahaki ya kufahamu kama;

1.Shule hizo zilikuwa hatarini kiasi gani kufungwa sababu ya uhaba wa chakula?

2. Wakuu wa shule hizo waliandika barua wizarani kuomba msaada wa dharula wa kupatiwa chakula? Kama hawakuandika, serikali imejuaje kama wanahitaji msaada?

3. Wazazi walihusishwa kwenye majaribio ya project hiyo ya GMO? (Walijaza consent form?) ya kukubali msaada huo wa chakula? Kitu cha kupewa bila kuomba unayo haki ya kupokea au kukataa na kisheria watoto maamuzi yao hufanywa na wazazi

Kama wazazi na uongozi wa shule walishirikishwa hatua kwa hatua na wakakubali wenyewe, basi sasa ni zamu yetu kuhoji kwasababu hatukuwa na taarifa na ni haki yetu kufahamu pale maslahi ya kiafya ya watanzania wenzetu yanapokuwa mashakani.

Hata kama yote hayo yalifanyika, yatupasa kufahamu kwamba wakulima wa mchele "originale" huko mashambani wanalanguliwa na madalali mchele wao mzuri kwa bei rahisi sana na mchele wao kusafirishwa nchi za nje kwa bei ya super normal profit, halafu watoto wao wanafanyiwa majaribio kwa kulishwa mfano wa mchele uliotengenezwa maabara na viongozi wao wanachekelea mbele ya camera

Tutambue kwamba hayo mazao ya GMO ni project ya muda mrefu yenye malengo maalumu ambayo ki uhalisia wanaofahamu ni wao wenyewe.

Ni jambo la ajabu sana kuruhusu wafanye majaribio ya miradi yao kwa watoto wetu. Huu ni wenda wazimu

Kama zamani, watoto hawa walitakiwa wagome kula na waandamane kudai haki yao ya kula chakula kizuri.

Wazazi nao huku mtaani walitakiwa waifundishe serikali kwamba hawajashindwa kuwapa watoto wao chakula kizuri. Wazazi wafungashe viroba vya mchele kutoka Kyela na Kilombero na madumu ya mafuta ya alizeti kutoka Singida wawapelekee watoto wao shuleni kama ishara ya kuonyesha kwamba Tanzania hatujafikia hatua ya kupewa msaada wa chakula.

Kwanini chakula hicho kipelekwe kwa vijana? Watanzania tuamke
 
Hivi,kwanza vyombo husika kweli walithibitisha unafaa kuliwa?
Je,kwa nini marekani haiwagawii raia wake wanaolala na kushinda njaa au kula vya jararani! Kwa nini basi haiuzi na kuwasaidia hata makazi!!! Mtanzania anaelala kwenye chumba cha kawaida chenye bati,na mmarekani anaelala nje kwenye box,yupi bora!!! Bora Kim Jong Un kuliko huyo Biden. Japo kosa ni la walioomba
 
Hivi,kwanza hao TFDA kweli wanathibitisha unafaa kuliwa?
Je,kwa nini marekani haiwagawii raia wake wanaolala na kushinda njaa au kula vya jararani! Kwa nini basi haiuzi na kuwasaidia hata makazi!!! Mtanzania anaelala kwenye chumba cha kawaida chenye bati,na mmarekani anaelala nje kwenye box,yupi bora!!! Bora Kim Jong Un kuliko huyo Biden. Japo kosa ni la walioomba
Wewe ndo hopeless kabisa. Nchi hii kuna taasisi inaitwa TFDA? Food standards and safety ipo chini ya TBS wewe TFDA umeitoa wapi?
 
Yani Kuna upumbavu unaendelea humu..kwamba Mchele unakufanya uwe shoga? Serikali yenu ndio iliyoomba msaada..
 
Kuna mjadala wa kuletewa msaada wa mchele na nchi ya Marekani na walengwa ni vijana wetu walioko mashuleni.

Kwa bahati mbaya kizazi hiki hakina uwezo wa kuhoji na wazazi wao wamekuwa machawa wanaosifia kila kitu kinachofanywa na mabwana wakubwa bila kujali madhara ya kitu chenyewe.

Wazazi na wanafunzi wa shule hizo wanahaki ya kufahamu kama;

1.Shule hizo zilikuwa hatarini kiasi gani kufungwa sababu ya uhaba wa chakula?

2. Wakuu wa shule hizo waliandika barua wizarani kuomba msaada wa dharula wa kupatiwa chakula? Kama hawakuandika, serikali imejuaje kama wanahitaji msaada?

3. Wazazi walihusishwa kwenye majaribio ya project hiyo ya GMO? (Walijaza consent form?) ya kukubali msaada huo wa chakula? Kitu cha kupewa bila kuomba unayo haki ya kupokea au kukataa na kisheria watoto maamuzi yao hufanywa na wazazi

Kama wazazi na uongozi wa shule walishirikishwa hatua kwa hatua na wakakubali wenyewe, basi sasa ni zamu yetu kuhoji kwasababu hatukuwa na taarifa na ni haki yetu kufahamu pale maslahi ya kiafya ya watanzania wenzetu yanapokuwa mashakani.

Hata kama yote hayo yalifanyika, yatupasa kufahamu kwamba wakulima wa mchele "originale" huko mashambani wanalanguliwa na madalali mchele wao mzuri kwa bei rahisi sana na mchele wao kusafirishwa nchi za nje kwa bei ya super normal profit, halafu watoto wao wanafanyiwa majaribio kwa kulishwa mfano wa mchele uliotengenezwa maabara na viongozi wao wanachekelea mbele ya camera

Tutambue kwamba hayo mazao ya GMO ni project ya muda mrefu yenye malengo maalumu ambayo ki uhalisia wanaofahamu ni wao wenyewe.

Ni jambo la ajabu sana kuruhusu wafanye majaribio ya miradi yao kwa watoto wetu. Huu ni wenda wazimu

Kama zamani, watoto hawa walitakiwa wagome kula na waandamane kudai haki yao ya kula chakula kizuri.

Wazazi nao huku mtaani walitakiwa waifundishe serikali kwamba hawajashindwa kuwapa watoto wao chakula kizuri. Wazazi wafungashe viroba vya mchele kutoka Kyela na Kilombero na madumu ya mafuta ya alizeti kutoka Singida wawapelekee watoto wao shuleni kama ishara ya kuonyesha kwamba Tanzania hatujafikia hatua ya kupewa msaada wa chakula.

Kwanini chakula hicho kipelekwe kwa vijana? Watanzania tuamke
Kwakweli kwa hili tujitafakari,
 
Ndizi, viazi na maharage. Mimi wa Kyela niliyelowea daslama😜
Afu new I’d....em niambie I’d yako ya zamani ili nichat nawe kwa kujiachia hapa....maana nipo na muda ndiyo niende kulambalala🤓
 
Back
Top Bottom