CDM wameishiwa, wako hoi sasa hivi, wameanza kuparanganyika ...
CDM hawajatambua mihimili ya utawala wa CCM na kuishughulikia kikamilifu: baadhi ya misingi hiyo ni (1) mfumo wa uteuzi (hii ndo alfa na omega ya utawala wa CCM. Je, CDM imetumia mchakato wa katiba mpya kufumua mfumo huu? let us wait and see); na (2) rushwa (hapa angalau wamejitahidi kupambana, japo kwa mtizamo wangu naona wanaemlenga siye kwa upande wa wananchi. CDM wanalenga rushwa kubwa za wanansiasa wa CCM. HAPANA. Rushwa inamuathiri zaidi mwananchi ni ndogo2 ya POLISI, hospitali, kwa WEOs na VEO, MAHAKAMANI nk).
CDM hawaibui hoja mpya na zenye mashiko, kwani wanabinya mawazo yenye changamoto
CDM wametoka kwenye siasa za hoja na kuingia siasa za watu: oo ZITTO kafanya hivi, oo SLAA anatisha; oo oo ...
Badala ya kujadili kwa kina mapungufu ya utekelezaji wa CCM wa ILANI ya CCM ya uchaguzi, CDM wameng'ang'ania ufisadi tu. SAWA ufisadi ni hatari, lakini pekee hautoshi, na pia CDM wameshindwa kumuonyeha mwananchi wa kawaida hajaonyeshwa kwa jinsi gani RICHMOND ilivyoathiri maisha yake...
CDM wameshindwa kuthibitishia wananchi, wakipewa ridhaa watakuja na kitu gani ambacho CCM hawakifanyi au wanakifanya ndivyo sivyo ... yaani ampungufu ya CCM ni yapi na wao watayashughulikiaje
USHAURI wangu washughulikie MIHIMILI YA UTAWALA wa CCM ili kuibomoa, CDM wajifunze kwa RAILA alivyosambaratisha mifumo ya utawala wa kimabavu wa KENYA, KENYA sasa imenyooka japo kuna vimasalia vya hapa na pale. Vinginevyo, CDM inaota kuingia ikulu ...
IKUMBUKWE mimi mwananchi ni mteja kwenye duka la siasa la CDM, CCM, CUF nk; na ninachotaka ni huduma bora, ziwe zinatolewa na CCM, CUF au CDM kwangu si hoja... hivyo mjadala wa watu, kwamba huyu yuko hivi, vile nk au chama hiki kiko hivi hausaidii _ ninachotaka ni huduma, wewe niambie ukiniongoza ntafaidika hivi, vile na ntakuunga mkono. KILA LA KHERI wanasiasa ...