Ushauri: Chadema achaneni na ndoto za urais!

Ushauri: Chadema achaneni na ndoto za urais!

KIM KARDASH

JF-Expert Member
Joined
Sep 21, 2011
Posts
5,139
Reaction score
1,150
Kama kawaida yangu mimi hupenda kuzungumza yale mambo ambayo watu huwa hawapendi kuyasikia hata kama yapo.

Leo napenda kushauri chadema ama wapinzani kiujumla waachane na ndoto za urais badala yake wajikite kwenye ubunge; hii ndio njia ya mkato na strategy ya kushika serikali. Urais ni jambo dogo sana ambalo unaweza kulipata na ukawa rais picha tu ambae hana serikali.

Kwa mfano nguvu nyingi walizotumia chadema kwenye uchaguzi uliopita ili slaa awe rais urais wake usingekua na maana kwani angekua rais bila serikali jambo ambalo lisingeisadia sana chadema na wapenda mabadiliko wengine,hivyo shime sasa chadema acheni kudanganyana na ndoto za urais, nguvu kubwa ipelekeni kwenye ubunge,itengenezwe kauli mbiu "ubunge kwanza urais utakuja wenyewe baadae"

Nawasilisha.

*Angalizo wachangiaji mnatakiwa kuwa na hoja kwanza,kama huna hoja kaa pembeni,itoshe tu kuwa msomaji kuliko kuleta vioja.


"Tukosoane, Turekebishane, Tuwajibishane, ndipo Tusameheane". - Regia Mtema.
 
Kim Kardash,

..hivi unaweza kusema kwamba CDM leo hii r in worse position than they were 3 yrs ago?

..kwa mtizamo wangu Slaa aliinua sana profile ya CDM wakati wa uchaguzi mkuu na kupelekea wananchi kuwa na interest na wagombea ubunge wa CDM.

..Kwa msingi huo naamini kitendo cha Slaa kugombea Uraisi kilisaidia kuongeza idadi ya wabunge wa CDM.

..huwezi kushinda viti vingi vya ubunge bila kuwa na mkakati wa muda mrefu[endelevu] wa kukijenga chama ktk ngazi ya wilaya na kata.

..hata katika ngazi ya Uraisi kampeni zake haziishii na mgombea kufanya mkutano wa hadhara tu. kunapaswa kuwepo wanachama ktk maeneo husika ambao wataendelea kumnadi mgombea Uraisi, pamoja na chama baada ya mikutano ya hadhara ya kampeni.

..kama uli-pay attention kwenye kampeni za CCM utaona kwamba kuna maeneo alipita Kikwete, halafu akafuatia Dr.Bilal, akaja mama Salma Kikwete, zaidi walikuwepo wagombea ubunge wenye nguvu na mabavu ya incumbency, na mwisho kabisa kulikuwepo na nguvu ya mtandao wa matawi ya CCM.

..binafsi nadhani Slaa aliwasaidia CDM ku-mask mapungufu yao, pamoja na udhaifu wa chama wa kutokuwa na mtandao wa matawi huko vijijini.

..CDM wako ktk nafasi nzuri zaidi ya kugombea Uraisi na kuongeza viti vya ubunge come 2015.
 
Habari hii ungemwambia EL aachane na ndoto za urais. Chadema haina ndoto bali ina malengo na mikakati ya kufika malengo yake.

kama ni hivyo basi vizuri,ila kwa kuanzia tuanze na arumeru,kuhakikisha tunakipata kiti kingine basi tumsimamishe mtu mwenye uwezo wa kushinda kama Slaa ili nafasi hiyo tusiiweke rehani,tuachane na kauli mbiu ya kwamba slaa ni presidential material,sasa tumtumie kama material ya ubunge kwanza.
 
CHADEMA hawajawahi kumaanisha kugombea urais. Huwa wanaweka mtu ili na wao waonekane wameweka mtu.
 
Wewe sasi basi tena, ukilala CHADEMA, ukishinda CDM, ukizunguka ukirudi CDM, una matatizo gani na CDM????? Hii thread si uliisha iweka hapa ya Dr kugombea Arumeru???? Tumekataa basi kanywe sumu!!!!!!!
 
kama ni hivyo basi vizuri,ila kwa kuanzia tuanze na arumeru,kuhakikisha tunakipata kiti kingine basi tumsimamishe mtu mwenye uwezo wa kushinda kama Slaa ili nafasi hiyo tusiiweke rehani,tuachane na kauli mbiu ya kwamba slaa ni presidential material,sasa tumtumie kama material ya ubunge kwanza.

We gamba unajidai kuifahamu CDM,endelea kulipwa vijisent na Nape
 
kwa hiyo unaamini kabisa chadema watakusikiliza!? Na kufuata ushauri wako!? Unajua wewe una mawazo ya kimasikini kabisa!? Yaani ni sawa sawa na kumwambia mtu bora uwe masikini tu naona utajiri umekushinda!? Unajua mtu au mwanaume kama mwanaume inabidi uhustle au ustraggle, so chadema ni mwanaume inabidi ahustle, unajua katika kuarchive something masnitch huwa wana exist, snitch mmoja ni kama wewe, Never forgive up chadema, walianza na wabunge 5 je unajua sasa hivi wapo wangapi!? Kama wangekuwa wanafuata ushauri kama wako unadhani ingekuwaje!? Sasa hivi wameteka kanda ya ziwa,kaskazini kule kusini Mbeya na Iringa pamoja na mpanda kati je unadhani zamani ilikuwaje!? no retreat, no surrender, freedom is coming tomorrow!
 
Sorry Kim but I have to say that, a great thinker cannot defend successfully the type of opinion started in the thread. Though you are entitled to your own opinion.

In short there is positive correlation between working hard to win the top spot in politics (Presidency) and winning more posts which are thought by voters can assist the top spot in governing (Mps). I have to end here because I think you won't understand what I mean.
 
Mimi nakupongeza kwa kutumia uhuru wako wa kutoa na uhuru huo unaishia pale uhuru wetu unapoanzia kwa hiyo usituzuie kutoa maoni.

Siyo kweli kwamba wangepata uraisi wasingekuwa na serikali au unamaanisha nini unaposema hivyo, nadhani wangekuwa na serikali huenda ya mseto ambayo ingepaswa kutekeleza sera za CDM kwa manufaa ya watanzania. Uchaguzi wa mfumo wa vyama vingi umenza mwaka 1995 lakini CDM hawakugombea 1995 wala 2000 lakini impact ya kugombea uraisi 2005 na 2010 ni kubwa inaonyesha kuwa CDM wana move forward sasa kama unawatakia mema huwezi kuwaambia waache kugombea uraisi they will be backsliding.

Ok kuwa na wabunge wengi ni kitu muhimu ili kuunda serikali hata Dr Slaa alilisema hilo lakini kwa maoni yangu kwa hatua waliyofikia usiwakatishe tama tafadhali watie moyo in fact wanayo nafasi kubwa kuchukua dola next election hayo ndiyo maoni yangu mkuu
 
magam.ba spin doctor@ work, pole. Naona unahangaika sana....... Tuko macho kama popo...
 


Nawasilisha.

*Angalizo wachangiaji mnatakiwa kuwa na hoja kwanza,kama huna hoja kaa pembeni,itoshe tu kuwa msomaji kuliko kuleta vioja.


"Tukosoane, Turekebishane, Tuwajibishane, ndipo Tusameheane". - Regia Mtema.


Tuanze na hapo nilipoweka rangi: Wewe mwenyewe huna hoja unawezaje kupima hoja za wenye hoja????

Pili: Haujakatazwa wewe kuanzisha chama kisha ukatekeleza hayo mawazo yako. Milango ya kuanzisha chama iko wazi, anzisha kisha tekeleza hayo...siyo lazima cdm wafuate ya kwako!!!

Kwanini cdm na siyo CUF, TLP, n.k

Cdm ni chama cha siasa: moja ya malengo ni kushika serikali/dola na kuwa na wabunge wengi iwezekanvyo. Na safari hii hatuhitaji mtu wa kutusemea ambaye hayuko cdm maana malengo yetu yamesha jipanga tayari. hatuna muda wa kupoteza, na wala hatubahatishi. Waambie ccm kuwa tuko serious this time na tumejipanga na kama yupo anayedhani tunatania angojee aone yatakayompata. Tunakwenda kuisambaratisha ccm hadi hamtaamini. Miaka yetu 2 ya kuelekea 2015 ndo utaijua vizuri cdm ni kitu gani

Ila huu mti cdm yaani kila mtu anautupia mawe na magongo kuangusha matunda yake na hata hayaishi maana kila siku watu wanayapopoa kwa mawe yaanguke lakini wapi yako imara..hayaanguki....

Slaa ni marufuku kugombea Arumeru.... eeh ndo hivo.... tunajua hii ni janja ya ccm na wote wasiotutakia mema...akagombee akafanye nini bungeni? Wapo tayari akina slaa kibao kule bungeni sasa yeye naye akafanye nini tena... PASIPO MAONO WATU HUANGAMIA.... Ubunge is now a low profile for Dr wa ukweli...Slaaa
 
Tuanze na hapo nilipoweka rangi: Wewe mwenyewe huna hoja unawezaje kupima hoja za wenye hoja????

Pili: Haujakatazwa wewe kuanzisha chama kisha ukatekeleza hayo mawazo yako. Milango ya kuanzisha chama iko wazi, anzisha kisha tekeleza hayo...siyo lazima cdm wafuate ya kwako!!!

Kwanini cdm na siyo CUF, TLP, n.k

Cdm ni chama cha siasa: moja ya malengo ni kushika serikali/dola na kuwa na wabunge wengi iwezekanvyo. Na safari hii hatuhitaji mtu wa kutusemea ambaye hayuko cdm maana malengo yetu yamesha jipanga tayari. hatuna muda wa kupoteza, na wala hatubahatishi. Waambie ccm kuwa tuko serious this time na tumejipanga na kama yupo anayedhani tunatania angojee aone yatakayompata. Tunakwenda kuisambaratisha ccm hadi hamtaamini. Miaka yetu 2 ya kuelekea 2015 ndo utaijua vizuri cdm ni kitu gani

Ila huu mti cdm yaani kila mtu anautupia mawe na magongo kuangusha matunda yake na hata hayaishi maana kila siku watu wanayapopoa kwa mawe yaanguke lakini wapi yako imara..hayaanguki....

Slaa ni marufuku kugombea Arumeru.... eeh ndo hivo.... tunajua hii ni janja ya ccm na wote wasiotutakia mema...akagombee akafanye nini bungeni? Wapo tayari akina slaa kibao kule bungeni sasa yeye naye akafanye nini tena... PASIPO MAONO WATU HUANGAMIA.... Ubunge is now a low profile for Dr wa ukweli...Slaaa

Mzee hakuna chama kitafanikiwa kushika dola bila kupata sapoti ya wasio wanachama kama independent voter ambao ndi wengi,kudhani nyie cdm mtafanikiwa kwa kutumia wanachama wenu ni kujidanganya,hao ccm wenyewe wanashinda kwa kuwa wanapigiwa kura hata na wasio wanachama,mkijifungia kwenye kachumba kadogo ka chama cha wanachama mtachukua muda mrefu sana bila mafanikio.Mnahitaji kuvutia watu kama mimi pia ambao sio wanachama ili tushawishike kuwapigia kura.CHADEMA ina wanachama wangapi tanzania nzima?je kura zao pekee zinatosha kuwapa dola?amka usingizini hata kama usingizi ni mtamu kiasi gani mzee
 
Back
Top Bottom