Ushauri: Biashara ipi nifanye

Ushauri: Biashara ipi nifanye

Ipi bora

  • Mtaani duka la mangi

    Votes: 0 0.0%

  • Total voters
    2

GwajiBoy

Member
Joined
Jan 7, 2025
Posts
34
Reaction score
60
Habari Mimi ni kijana wa miaka 25+ ninamtaji wa Tah 1M niko shinyanga mjini sasa naombeni ushauri wakuu,
1: Kufugua biashara ya duka la mangi mtaani. Kwa sababu ya ufinyu wa mtaji. Mzunguko mtaani ni mkubwa

2: Kufungua duka sokoni (kibanda kipo hakuna Kodi) ili niwe nachanganya baadhi ya bidhaa ziwe za jumla na zingine za reja reja (nimeambiwa naweza kuwa nachukua mzigo harafu nikiuza napeleka Hela) Mzunguko wake ni mkubwa ila una faida kidogo sana
 
Hahahaaa we jamaa afanye biashara gani sasa na huo mtaji
Yaani hapa kwanza kapata wapi Mil 1, usikute kwenye kilimo, Bora akomae uko uko.

Hizi biashara anazojifariji eti mzunguko upo kisa anawaona wenye maduka "wanapiga Hela" ataumia. Ukiingia kwenye game unakuta hali tofauti.

Sisi mshua alikua anaona daladala kila siku zinajaza abiria akajua biashara nyepesi. Akashauriana na bro wanavuta coaster. Oya game gumu sana, simple ukiwa nje.

Pia umri 25 years unataka ukae tu unasubiria wateja, serious maisha Yako yooote ukae tu. Ukizeeka je?
 
Yaani hapa kwanza kapata wapi Mil 1, usikute kwenye kilimo, Bora akomae uko uko.

Hizi biashara anazojifariji eti mzunguko upo kisa anawaona wenye maduka "wanapiga Hela" ataumia. Ukiingia kwenye game unakuta hali tofauti.

Sisi mshua alikua anaona daladala kila siku zinajaza abiria akajua biashara nyepesi. Akashauriana na bro wanavuta coaster. Oya game gumu sana, simple ukiwa nje.

Pia umri 25 years unataka ukae tu unasubiria wateja, serious maisha Ya
Dogo Achukue madini hapa
 
Achana na Biashara za bidhaa, jifunze kutoa online service iyo m1 weka kwenye Matangazo 20m hii hapa kama faida kamili
unatoa taarifa nunusu ili iweje? kama umeamua kumsaidia basi mtajie hzo online services na namna ya kuzifanya au ndo unataka aje DM?. Ukiamua kumsaidia mtu basi andika full information, kama hutaki kusaidia unapita kimya kama hawa wengne walopita kimya hakuna ataekudai.
 
1m ni pesa ndogo sana ukiingiza katika mchakato huo hata kwa duka la mangi, najaribu kuwaza tu ukinunua vitu vya chini, eg, mfuko wa sukari, dumu la mafuta, mchele, nk, hiyo pesa haitosh kabsa bora ukomae tu na hicho kilichofanya uipate hiyo pesa uisogeze sogeze!
 
Yaani hapa kwanza kapata wapi Mil 1, usikute kwenye kilimo, Bora akomae uko uko.

Hizi biashara anazojifariji eti mzunguko upo kisa anawaona wenye maduka "wanapiga Hela" ataumia. Ukiingia kwenye game unakuta hali tofauti.

Sisi mshua alikua anaona daladala kila siku zinajaza abiria akajua biashara nyepesi. Akashauriana na bro wanavuta coaster. Oya game gumu sana, simple ukiwa nje.

Pia umri 25 years unataka ukae tu unasubiria wateja, serious maisha Yako yooote ukae tu. Ukizeeka je?
Ukiwa hujanywa bia unatema cheche kishenzi 😁 safi sana
 
Ukiwa na mtaji mdogo usifanye biashara ya kuchanganya bidhaa kama ya duka la mangi. Uza kitu kimoja tu ujulikane kwa signature yako.

Uza mishikaki mizuri, au choma kuku, au choma chapati, au uza viatu, au sandals. Fanya kitu kimoja kiasi kwamba inventory ya 600,000 inanunua kitu kimoja tu au cha aina moja.

Sio 1M hiyo hiyo inunue sukari, mchele, unga, sabuni, mafuta. Utachanganyikiwa.
 
Back
Top Bottom