Usaliti na Unafiki unavyoangamiza Taifa - Lema

Usaliti na Unafiki unavyoangamiza Taifa - Lema

Status
Not open for further replies.
Mmmmmmm! hoja kama hoja ina ukweli kwa mustakabali wa taifa kwa ujumla wake. kwa kuwa kuwa na msaliti katika taifa ni hatari kwa taifa hilo.
Inapokuja kwenye vyama vya siasa ni kweli usaliti ni sumu mbaya sana. Na kiukweli kuwabaini wanasiasa ambayo hawana chembe ya usaliti ni kitu kigumu sana haswa huku kwetu Africa. Kwa watu wenye akili zao ukiona mtu mwenye tabia ya kuhama hama vyama huo ni wa kuogopa sana kwani ukimfuata mtu wa namna hiyo hutajua kesho atakupeleka wapi. Kwa wenzetu wao wanasimamia wanachokiamini katika sera na imani za vyama.
Huku kwetu wengi wanaangalia upepo unakwenda upande gani. Wanasiasa wanaofuata upepo hao ndiyo watu wakuogopa sana katika ujenzi wa demokrasia ya vyama vingi. Uhuni wa namna hiyo uko kenya kwa kuwa wao huangalia maslahi yao wenyewe ndo maana walipofika bungeni walianza kudai kuongezewa mishahara watu wakaandamana wakapeleka hata nguruwe maeneo ya bunge.

Viongozi wenye tabia ya usaliti huua ndoto za wafuasi wao. Na zaidi sana huwafanya wafuasi wao wakate tamaa. Ndiyo sababu viongozi makini kama kina Wales wa Scotland walikua tayari kuuawa kuliko kuomba rehema kwa mfalme wa Uingereza akijua akifanya hivyo morali ya watu wa Scotland kudai nchi yao na uhuru wao utafifia na vita yao itakuwa ni bure.

Ni watu wangapi wamepoteza maisha yao kwa kuwa tu wanaamini kuwa CDM itakomboa nchi hii toka kwenye mikono ya CCM ambayo imepoteza dira na kuwa genge la wanyang'anyi? Kile chama kilichodai bidanadamu wote ni sawa na Afrika ni Moja na kuwa sitapokea wala kutoa rushwa kwa kuwa rushwa ni adui wahaki? Kilichojipambanua kuwa ni chama cha wakulima na wafanyakazi? ambapo wakulima wakilima wanapigwa marufuku kuuza mazao yao nje ya nchi? na ambacho kinasimamia mbuge apate posho ya siku inayolingana na mshahara wa mwezi wa mfanyakazi?

Msaliti wa juhudi za vijana wa kitanzania na wapenda maendeleo ya nchi hii wanaotaka kujikomboa kutoka kwenye kongwa la kifungo cha CCM huyo ni mtu mbaya afadhali mtu huyo asingelizaliwa katika nchi hii. Ni kwasababu anasaliti juhidi na kazi inayofanywa ya kuliomboa taifa hili.

Atakayesaliti juhudi hizo alaaniwe yeye na uzao wake. Kwa kuwa juhidi hizi zimegharimu maisha ya watu kama akina Mwangosi na wengineo.
 
unajuaachokifanya huyo unaemtetea ndani ya chama chetu, uliwahi kukaachini na kuhesabu watu wangapi kasha sababisha kufukuzwa ndani ya chama? mkuu ni wakati wa kungia mizizi siyo matawi..

Mtajipambanua kama chama cha kikanda
 
Yes...na wanamuogopa mno
mpaka Lema nae sasa ni attack dog ya Mbowe...
wanatamani kumfukuza but hawajui wanachama watasemaje so
kinachofanyika ni kushawishi watu kama hivi...

Umenisononesha, najuta kukufahamu
 
mkuu unaejua niambie...lazima tukubali kutokubaliana ndipo tusonge mbele, siasa za visasi na kukamiana hazijengi zaidi ya kuongeza ufa kama taifa.

kwa post hii....hivi unafikiri Lema na Zito wanaweza kukaa pamoja na kujadili mambo ya msingi kwa maslai ya chama na Taifa.?

Viongozi waache ujinga wanatukatisha tamaa wananchi , na hatime kuifanya ccm itawale kwa muda mrefu zaidi

Mkuu idawa, kwa hili alilofanya Lema, ccm wanatucheka sana sana , na kiukweli tunajiumiza wenyewe. Sioni kwanini hata tunaanza kushambuliana humu jf kwa sababu ya ujinga aliofanya Lema. Chadema inapaswa kujifunza kwa waliopanda na kuporomoka, walianza hivihivi, mara huyu anamsema yule, mara fulani yuko kwa fulani na ccm wanapenyezea hapohapo. We have to be careful, otherwise tutasuffer na siasa hizi. Wito wangu kwa mwenyekiti ni kwamba yeye ndiyo mwenye dhamana ya chama. Akiruhusu upuuzi huu ukaendelea, tutashindwa kumwelewa. Narudia, chama ni mali ya wanachama, siyo ya mtu!!!!!!!
 
Uropokaji.Leta kanuni,miongozo na katiba ya CHADEMA iliyovunjwa.

Wewe chizi,ulipewa adhabu kwa kosa la kulipuana kwenye mitandao na wajinga wenzio kina shonza,leo unamtetea lema? Rejea mada yangu,'viongozi hawa chadema ni tatizo',ulijifanya unatetea utaratibu wa kutumia vikao halali kutatua migogoro,leo umegeuka? We mtoto sio.
 
Hii Mihemko ya hawa watoto wa CHADEMA ishachokwa na jamii, siasa za kitoto, zisizo na tija kutoka kwa MBOWE, LEMA , SLAA na wapambe wao zifike mwisho sasa.
 
Ndugu LEMA ninakubaliana na wewe kwa %100 na mm nina amini kama chama wataendelea kumngangania zitto kabwe ikulu watazidi kuiona kwenye tv na kuisikia kwenye radio

Inaonekana unafikiria kwa kutumia tumbo wewe.
We una mchango gani mkubwa kwa Taifa hili na chama hata ujilinganishe na Zitto hata utake afukuzwe ubaki wewe??

Malizeni Agenda ya madai ya Posho kwanza ndo mhamie agenda nyingine.
 
Leo mtatukana matusi yote maana hamna uwezo wa kujenga hoja zaidi ya ujanja ujanja na unafiki tu.Turudi kwenye hoja.

Je wanafiki na wasaliti sio kikwazo cha Mabadiliko?

Je Lema kuwasema Wasaliti amekosea wapi?Ni kanuni au sheria zipi amekiuka?

Punguza hasira tujadiliane!
mkuu kamanda Ben, binafsi nakuheshimu sana,lakini kitendo cha kamanda lema sio sahihi hata kidogo, lema ni kiongozi hakupaswa kuleta kwenye media kuhusu kuwalaumu wasaliti ndani ya chama. Angetumia vikao, huo ndo ukweli. Tukitaka chama chetu kisonge mbele, lazima tuepuke double standard katika maamuzi.
 
we are not interested in these cheap F4F , internal wranglings za CHADEMA.
Leteni mambo ya kitaifa hapa,

Mambo ya kitaifa kwa Chadomo ?

Ukitaka thamani yako iwe juu ndani ya chadomo basi weka chama mbele utaifa baadae kama anavyofanya Lema.

Na kama utaweka taifa mbele chama baadae basi utafanyiwa mizengwe na kuitwa majina ya kila aina kama msaliti.
 
na kweli itawakwaza wengi maana kazi ya kutembea na sumu kutaka kumuua kamanda wetu zzk hakuna atakaeifurahia.

unamdekeza huyo msukule! Ukitaka kuua nyoka piga kichwani mara nying. Hatakiw kujibiwa kistaarabu!
 
lema ni mnafiki tu,kaamia juz juz tu CDM anajifanya yeye anauchungu sana na CDM,anakivuruga CHAMA,sisi kama CCM tunataka upinzani Madhubuti sio Dhaifu kama huu wa sasa,CHADEMA rudini katika mstari,nani msemaji wa CDM,haya maandishi ya Lema angeandika Mwanachama mwingine angeonekana Msaliti"CHADEMA inavurugwa na wakuja kama LEMA"walitaka Mwigamba azungumze katika vikao,inakuaje mbunge awe na nguvu kuliko mwenyekiti wa mkoa,sijawai hona hii kitu katika vyama vingine,majimbo mengi yenye wabunge wa CDM yatakuwa na ugomvi wa wenyewe kwa wenyewe kisa Ubunge.Lema anakataza watu kutokua waoga,anataka watanzania wasiwe waoga kwa serikali halali ya Tanzania,ila wawe waoga kwa viongozi wa Chadema katika kusema Ukweli,ikitokea bahati mbaya CDM ikashika dola,si mtafunga jera kila anaewapinga,Lema afukuzwe CDM
 
Last edited by a moderator:
Zaidi ya hapa JF kutujibu sisi utakuwa na nini kingine? labda uwe na ile "special assignment" (ampules).

Unafikiri unalipwa bure na Josephine?

hivi mada ni kumjadili ben...bibi jikite kwenye mada acha porojo za sido..
 
Last edited by a moderator:
lema ni mnafiki tu,kaamia juz juz tu CDM anajifanya yeye anauchungu sana na CDM,anakivuruga CHAMA,sisi kama CCM tunataka upinzani Madhubuti sio Dhaifu kama huu wa sasa,CHADEMA rudini katika mstari,nani msemaji wa CDM,haya maandishi ya Lema angeandika Mwanachama mwingine angeonekana Msaliti"CHADEMA inavurugwa na wakuja kama LEMA"walitaka Mwigamba azungumze katika vikao,inakuaje mbunge awe na nguvu kuliko mwenyekiti wa mkoa,sijawai hona hii kitu katika vyama vingine,majimbo mengi yenye wabunge wa CDM yatakuwa na ugomvi wa wenyewe kwa wenyewe kisa Ubunge.Lema anakataza watu kutokua waoga,anataka watanzania wasiwe waoga kwa serikali halali ya Tanzania,ila wawe waoga kwa viongozi wa Chadema katika kusema Ukweli,ikitokea bahati mbaya CDM ikashika dola,si mtafunga jera kila anaewapinga,Lema afukuzwe CDM
mbona Lema hakutaja mtu
 
Last edited by a moderator:
Wewe chizi,ulipewa adhabu kwa kosa la kulipuana kwenye mitandao na wajinga wenzio kina shonza,leo unamtetea lema? Rejea mada yangu,'viongozi hawa chadema ni tatizo',ulijifanya unatetea utaratibu wa kutumia vikao halali kutatua migogoro,leo umegeuka? We mtoto sio.
Mkuu haka kajamaa kanafiki sana sijui kwann mpaka sasa bado kapo kwenye chama cha makamanda
 
lema ni mnafiki tu,kaamia juz juz tu CDM anajifanya yeye anauchungu sana na CDM,anakivuruga CHAMA,sisi kama CCM tunataka upinzani Madhubuti sio Dhaifu kama huu wa sasa,CHADEMA rudini katika mstari,nani msemaji wa CDM,haya maandishi ya Lema angeandika Mwanachama mwingine angeonekana Msaliti"CHADEMA inavurugwa na wakuja kama LEMA"walitaka Mwigamba azungumze katika vikao,inakuaje mbunge awe na nguvu kuliko mwenyekiti wa mkoa,sijawai hona hii kitu katika vyama vingine,majimbo mengi yenye wabunge wa CDM yatakuwa na ugomvi wa wenyewe kwa wenyewe kisa Ubunge.Lema anakataza watu kutokua waoga,anataka watanzania wasiwe waoga kwa serikali halali ya Tanzania,ila wawe waoga kwa viongozi wa Chadema katika kusema Ukweli,ikitokea bahati mbaya CDM ikashika dola,si mtafunga jera kila anaewapinga,Lema afukuzwe CDM

ukishakuwa mwanachama wa chadema mnakuwa na haki sawa hata kama unamiaka hamsini tujadiri juu ya wasariti kuwangoa..
 
Last edited by a moderator:
Kwa nini watu wanafikiri ni Zitto wakati Lema katoa tu hisia na ukweli anaouamini
 
Safari yetu ya kubadilisha utawala inaonekana kufika ukingoni na nifuraha ya kila Mtu mwenye hisia ya ukweli katika maisha na ninapotazama mbali sana ninaona jinsi ambavyo Usaliti na Unafiki unavyoangamiza Taifa ni bahati mbaya sana uwezi kuwaepuka katika harakati hizi lakini tukiwa makini tunaweza kuwathibiti .

Kama Chadema leo itashindwa kuwachukulia hatua wasaliti wa wazi wa kazi hii njema ni vipi Chadema itaweza kuitaka Serikali na Rais iwajibishe Viongozi wake katika ufisadi na wizi wa mamilioni ? Na Wananchi lazima wajue lengo kubwa na muhimu la Chadema kwanza liwe kubadilisha fikra na mitazamo na kuupa UMMA elimu na mamlaka na nguvu ya kusimamia Taifa lao katika kuhoji ,kudadisi na kukemea , kwani UMMA usipojua wajibu wake katika kusimamia rasilimali na Taifa lao , ukweli utabaki kuwa Nchi itabadilishwa na kufanikishwa na Jamii iliyoamua kuishi matendo dhahiri ya ukweli na haki na sio unafiki na usaliti .

Viongozi wote wa Siasa wanatokana na Jamii kwa hiyo jamii Thabiti inayo furahia UTU ni Nchi bora tutakayoijenga lakini Jamii yenye woga na hofu na Sifa itazaa Taifa lenye usaliti na Wanafiki . Usaliti na Unafiki unaliangamiza Taifa sana . Maombi na Dua za Watu wengi kuelekea 2015ni kutaka kuona Chadema inachukua Nchi , lakini Dua na Sala hizi zina Imani kubwa na Viongozi wa Chadema na sio rangi ya Chadema , hivyo ni muhimu Chadema kuchukua hatua sasa ya kusafisha Chama na kama hatua hiyo muhimu ya kuondoa Watu wenye rangi mbili italeta madhara katika Uchaguzi Mkuu wa 2015 kwamba tunaweza tusishinde dola basi madhara hayo ni muhimu kwani lengo letu lisiwe tu kwenda Ikulu bali kubadilisha fikra ya utawala katika kutenda na kuamua .

“ Ni bora Simba wakali mia moja walioko Nje kuliko nyoka mdogo mmoja aliye ndani “ Chadema lazima ifanye maamuzi sasa ya kusafisha Nyumba yake la sivyo itakuja kujuta katika siku za mwisho , wasaliti wote waondolewe hasa yule Kiongozi wao kwani hakuna genge la usaliti lisilokuwa na Kiongozi , kuna Watu wengi Vijana wamekuwa wahanga na ndoto zao kupotea katika Siasa kwa sababu waliongozwa vibaya na Kiongozi mkubwa anayeratibu usaliti ndani ya Chama .

Mtu huyu wote tunamjua ni matumaini yangu Usaliti wake sasa utafika kikomo kama Chama kitaamua kuwa na busara za kutosha katika kujenga siku njema zinazokuja . Mtu huyu amefanya mambo mengi mabaya katika Chama yanayohusu usaliti na amewaponza Vijana wengi na kuangamiza ndoto zao kwa sababu ya mambo yake binafsi .

“ To me, the thing that is worse than death is betrayal. You see, I could conceive death, but I could not conceive betrayal.” Malcolm X



Lema Godbless - Mp

Usaliti uko wa namna nyingi, hata ule wa kusubiri ulipwe zaidi ndipo uhudumie na kutetea maslahi ya waliokuweka (maslahi ya wananchi) hapo ulipo. Rejea kauli yako Mhe. kwa mujibu wa ulivyonukuliwa kwenye vyombo vya habari.

“Nilisema huwezi kuzuia taasisi moja
kupewa maslahi bora eti tu kwa sababu
watumishi wengine hawalipwi vizuri, ni
haki wabunge kulipwa vizuri na wakati
huo wapiganie maslahi ya watumishi
wengine,” alisema Lema na kuongeza.
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom