Us Green Card Lottery




Ogah na wengine wote mlioshauri na kuchangia kwenye thread hii nawashukuru sana kwa ushauri na mafunzo niliyoyapata kwenu. Kwa kupitia links ulizozitoa hapa kwenye post hii, nilifanya application yangu mwaka jana 2007 November. Nafurahi kuwajulisha kwamba leo asubuhi nimepokea barua kutoka Kentucky Consular Centre kwamba nipo kati ya wale waliochaguliwa kupata Green card mwaka huu!!!

Nashukuru sana na nahitaji tena muongozo wenu zaidi na zaidi ili niweze kufanikiwa kupata hiyo VISA. Nilijiandikisha na watoto wadogo wawili na sijui kama wote watapata pamoja na mama yao ambaye sikuwa na picha yake wakati huo kwa hiyo hajakuwepo kwenye entry.

Naomba mnisaidie whats next?? and I will be contacting you now and then muweze kunisaidia nisiipoteze nafasi hii wakuu wangu
 

nilifanya application yangu mwaka jana 2007 November. Nafurahi kuwajulisha kwamba leo asubuhi nimepokea barua kutoka Kentucky Consular Centre kwamba nipo kati ya wale waliochaguliwa kupata Green card mwaka huu!!!


Mbona walisema majibu yangetoka kati ya May na June mwaka huu!?


Waliweka masharti kuwa asiyeyatimiza, ikiwa ni pamoja na kuambatanisha picha, application yake itakuwa batili. Km, kweli umefanikiwa kupata, basi wataangalia case yako kwa mtazamo maalum khs wewe na familia yako.
 


Aise Mzuzu HONGERA sana ndugu yangu! Its a dream come true, Iam sure uliweka bidii na umefanikiwa. Kama wanavyosema waungwana humu, this world is full of resources ni unafiki na uchoyo wetu tuu. Watanzania jamani huko mliko tusaidiane! Sasa JF is one of the best board kwa watanzania..ukipata nafasi ibandike humu..au sema watu waku-PM.. Kuna nafasi nyingi sana kwenye mashirika especially International.as long as mtu ana qualifications and he/she can do the job, please recommend him! Msaada SIYO pesa tuu, bali katika age ya leo, msaada wa mawazo ni mkubwa na maridadi sana.

Ambao mliapply mkakosa, please give it another shot! Huwezi jua bahati yako itakuwa wapi. Ila wewe ukichoka, kuna yule wa Nigeria anajitayarisha kutuma applications mara ya saba! maskini hachoki..akichoka, ameshapata!

Mzuzu nikutakie kila lakheri katika maandalizi yako na please have plan B usiende kubweteka tuu, you have to know why you applied for your Green Card and use it for the betterment of yourself and your compatriots back home.Unaweza kufikiria kuinvest, hata kuwasomesha wadogo zako (kama wewe ni mtoto wa mkulima kama mimi) nk!

Najua wengi tuna mtizamo tofauti wa kwenda nje, ila huko nje ni sehemu ya kujifunza na kuwa na mikakati ya kujikomboa na kuikomboa nchi yako! Wachina wakipata chansi kama hizo wao ni kuiba technology (hata ya Nuklia) na kuipeleka kwao..liwalo na liwe..sikushauri uibe..ila jitahidi kuitumia hiyo nafasi vyema!

All the best na Mungu akusaidie. Iam really happy for you!
 

hongera, kila la heri Mzuzu na wengine wote mloomba.
 
Nimewachezea watu kibao Greencard lottery na baadhi wamepata....ila jamaa wako majuu hata salaam kwa mshikaji aliyewafanya wawe huko hakuna.Malipo kwa mungu na this time na mimi nimepata! tutakutana huko huko US! Kuhusu suala la kwa nini wabongo wengi hawashiriki,ninaweza kusema matatizo ni mengi ila kubwa ni lugha, uelewa na access ya information. sitaki kuamini kuwa ni access to internet kwa kuwa kucheza kwa kutumia internet tumeanza miaka michache iliyopita mimi nakumbuka nilianza kucheza wakati wa kutuma kwa posta na bado kulikuwa hakuna wanaocheza, ama wachache....pia nakubaliana na suala la watu kunyimana info...wakenya na wanigeria ikifika kwenye suala la kubebana na ma-harambee yao ni kiboko!! Mfano mzuri,Mimi nafanya kazi nchi fulani africa hii, tumetangaza kazi dunia nzima watu apply mpaka magazeti ya kibongo ila hakuna hata mmoja mbongo aliye-apply....ukiangalia applications ni wakenya, waganda, wazimbabwe kibao!! nani alaumiwe? licha ya mambo mengine, mimi nadhani watu wanaona uvivu kuongea kizungu! wanaona bora wakae bongo wapige kiswahili chao!!!
 
It is DV 2008;Fiscal year 2008 (Oct,1 2007 to Sept 30, 2008. Yes, ilichezwa 2006!
 
Mashaka matupu! hebu check vizuri.

Sorry its DV-2009 diversity immigrant program for fiscal year 2008!!! samahani for a mistake. Na barua imeandikwa March 25, 2008.
 
It must be the one played in 2008. Otherwise why get a letter in 2008 for lottery played in 2006? Doesnt make sense.

Congratulations!!!
 
Hakuna cha upendeleo wala nini, the plain truth is "watanzania hawachezi" hauwezi kushinda kama hauchezi na watz hatuchezi kwa wingi kama wakenya. Ukiwaona wakenya wanavyochakarika kucheza hii green card na wanacheza ukoo mzima ila watz ukiwaambia hata kupiga picha yenyewe inachukua miezi 10 mpaka mtu apate hiyo studio, watz hatuko aggressive hata kidogo huo ndio ukweli wenyewe!
 
It must be the one played in 2008. Otherwise why get a letter in 2008 for lottery played in 2006? Doesnt make sense.

Congratulations!!!

Thanks!! I actually send my entry on Oct-Nov 2007 for the first time, i was encouraged after reading the posts from Ogah and Masanja on this thread!

Thank you once again all that made me take a courage to put my entry on this
 
Thanks!! I actually send my entry on Oct-Nov 2007 for the first time, i was encouraged after reading the posts from Ogah and Masanja on this thread!

Thank you once again all that made me take a courage to put my entry on this

Sorry I meant 2007! Akili yangu sijui ilikuwa wapi. I'll definitely try next time.

All the best!
 
[That's what am talking about watz hatuko aggressive halafu tunapenda dezo kupita kiasi nimecheka niliposoma "eti wanatuma tiketi ya ndege" wanakuomba nini? usipokuja wewe Wanigeria na Wakenya watapata hiyo tiketi within a week, kwanini? they know what life is " U fight or U die"
Mi nimeshahangaika kuwashawishi marafiki na ndugu zangu kucheza hii green card mpaka nimechoka manake jambo ni lilelile hatuna motivation Bongo tamu, raha nyingi shida kiasi kalaghabaho!!!tutaishia hayo hayo wakati wenzetu wanapiga hatua!

 
jamani huu ni wangu ushauri. kwamba unapoamua kucheza bahati nasibu ili uweze kuondoka ulipotoka/ulipozaliwa basi ucheze kwa unyenyekevu mkubwa maana ni kweli nyumbani tuna matatizo makubwa tena makubwa ya kukatisha tamaa lakini ni jukumu letu kuyatatua hayo matatizo si kuyakimbia, iwapo tunacheza hizo bahati nasibu ili tuwe wamarekani bila kujali wajibu wetu kwa jamii ya nyumbani, basi tutakua hatujatimiza wetu inavyopaswa.
ndugu zanguni tumezaliwa na Afrika, tumekula nafaka zitokazo ndani ya udongo wake, tumekunywa maji yake, tumekula matunda yake, no matter ugumu na ubovu wa system yoyote huko nyumbani, wajibu wetu kwa afrika na watoto wake ni wetu. kama tunaenda marekani au wapi lakini tusiikimbie na kuisusa Afrika bali iwe ni changamoto kwetu kutumia nafasi hizo kutimiza wajibu wetu kwa Afrika.
ni hayo tu ndugu zanguni
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…