BAK
JF-Expert Member
- Feb 11, 2007
- 124,769
- 288,283
Ni kweli Obama kapagawisha watu. Lakini ni matusi sana kwa wamerika na raia wa dunia hii kusema kwamba eti akishindwa itakuwa pigo duniani kote. I hope wenye nchi hawatakusikia, maana wakikusikia wanaweza kubadili kabisa mawazo. Huu ni ujinga uliotukumba Tanzania mwaka 2005. Media ilijenga mazingira kwamba hakuna aliyefaa kuwa rais kwa nchi yetu isipokuwa JK. Ukweli ni kwamba bila Obama au MacCain, Marekani itakuwepo na dunia itakuwepo.
Mwenzako pia nilikumbwa na uwenda uwazimu mwanzoni kwamba Democrats wasingemsimamisha Fighter Hillary wasingeshinda, lakini ona leo Obama anavyotesa. With hindsight, naona ni sawa kabisa wana democrats kumpitisha huyu ndugu yetu agombee maana amewarudishia nyota yao.
Ifike mahala tuelewa kwamba mchango wa mtu mmoja ni mmoja tu, na ukiuondoa dunia haiwezi kugeuka!!
Naam narudia tena kusema Obama akishindwa itakuwa ni pigo kwa dunia. Hii hali ya uchumi tuliyokuwa nayo sasa hivi imesababishwa sana na ongezeko la mafuta ambayo demand yake iliongezeka sana kutokana na uvamizi wa Iraq, Kichaka hataki dunia iamini hivyo yeye anataka dunia iamini kwamba demand ya China na India ndiyo iliyosababisha hilo, lakini ukweli ni kwamba mahitaji ya mafuta duniani yaliongezeka sana baada ya uvamizi wa Iraq.
Ongezeko hilo kubwa la mafuta ndiyo limesabaisha uchumi wa dunia kuanguka maana bei ya mafuta ikiongezeka basi inaathiri bei ya kila kitu duniani. McOLd akishinda kuna uwezekani mkubwa akaedeleza sera za kichaka hivyo kuendelea na vita ya Iraq na si ajabu kuanzisha vita nyingine na Iran ambayo itasababisha bei ya mafuta ianze kupanda tena na hivyo kuathiri uchumi siyo tu wa Marekani bali wa dunia nzima kwa miaka ijayo. Kama hamtaki kuliona hilo la uvamizi wa Iraq lilivyochangia kwa kiasi kikubwa katika ongezeko la bei ya mafuta na hatimaye kuanguka kwa uchumi wa dunia mtajiju.