Urembo, Michezo na Usafi - Vipaumbele vya Watanzania

Mzee Mwanakijiji

Platinum Member
Mar 10, 2006
33,478
40,000
Nimesoma habari kuwa Vodacom wamejitolea tena kudhamini mashindano ya urembo kwa mwaka huu na wametenga Shs; milioni 600 kwa ajili ya mashindano hayo ya kuonesha jinsi gani kina dada zetu wamejaliwa kwa kila hali ili hatimaye tuwe na binti mrembo kuliko wote walioshindana.

Sasa tulikuwa tunazungumzia mambo ya uchafu on the other thread na huko nyuma tuliwahi kuzungumzia ushindi wa Taifa Stars dhidi ya Burkinabe na watu wakachangiana Shs milioni 400 na upuuzi!

Sasa nilitaka kuhoji mambo mengi lakini hivi ni njia ipi ambayo Vodacom ingeweza kujitangaza kama kuwekeza hizo milioni 600 kwenye kampeni za Usafi kama vile "Safisha Tanzania na Vodacom"; "Kampeni ya Kusafisha Jijina Vodacom"

Tuna vipaumbele? Sekta binafsi na serikali na wananchi? Tunawezaje kuchagua vipaumbele vya Taifa...
 
MKJJ,

At the end of the day this is about marketing and sales.

Kuna psychology ya branding inatumika hapo, Voda waki sponsor urembo brand yao inakuwa automatically associated na uzuri, kuwa hip, kuwa cool, kuwa modern.

Michezo pia, kuwa tough, kuwa popular na hata kuwa victoriuos and at least resilient.

Kusafisha mji? Mitaro, uchafu, nzi na uchafu wote.nani anataka hilo.

Marketing is not that altruistic and prudent, if they can poison you to sell they will you know.
 


Nadhani kwa kuwa RA kachafuka na mdau mwenzake ni dhahiri kwamba wako wachafu kaa mitaro na makapi wangalianzia huko pia wangaliweza kujitangaza zaidi maana mwisho wa siku walengwa ni ni Watanzania so bora wadhamini mambo ambayo hayafikiriwi
 
Wakati Vodacom south Africa wanasifika kwa kudhamini researches mbali mbali za technologia na kuhakikisha vyuo vinabakiza wanafunzi wote wa mawasiliano na computers, economics nk ili baadaye wawe wasomi wazuri katika kuchangia maendeleo ya taifa, naona wamefika tanzania nchi ambayo naona imedhalaulika kweli kweli.

Lakini kwani Vodacom Tanzania ni akina nani?

Ni vizuri wajinga ndio waliwao.
 

Tumuulize Ephraim Mafuru ..... meneja masoko wa voda maana naona priority zake ziko mbali kabisaaaaaaa!
 
...at the end of the day,its all about profit na nani kawaambia vodacom wako pale kufanya charity work,wako responsible to there shareholder na kama tax wanalipa na ajira wanatoa thats enough,acha waweke advertising machine yao kwenye urembo maana ndio panapolipa,in economics its all good maana money spent,hiyo miji michafu imekosa hizo 600m lakini kumbuka waliopata ni sector ya urembo which is part of our total economy!
 
Tumuulize Ephraim Mafuru ..... meneja masoko wa voda maana naona priority zake ziko mbali kabisaaaaaaa!

mafuru Atakutolea siasa nyingi. Sana sana unajua hii ni kwa sababu hata viongozi wetu wamekaa sana kimashindano shindano, kiulimbende ulimbwende, lakini yote hayo ni katika kuficha wanayoyafanya. Wanaacha watanzania wakishangilia kwenye ulimbwende, na michezo wakati wao wakiFanya UFISADi.

Hizo zote nafikiri ziko katika strategy za makampuni kama VodaCom(TZ) ambayo kwa Tanzania imekamatwa na MAFISADI.
 


Tatizo wala si Vodacom, ni sisi Watanzania wenyewe.

Kama nchi ina muamko wa kisiasa na elimu Vodacom watajua tu na wataleta hayo mambo ya researches.Lakini sasa hivi wanaona watu wanaokuwa katika income bracket wanayoityaka wako zaidi katika urembo na michezo.

Socially responsible marketing is a very hot idea right now na kama kweli kuna market hawawezi ku i ignore.Tatizo sisi tunataka Vodacom ifanye kazi ya serikali kuwahimiza watu kuhusu elimu na usafi, hawawezi kufanya hivyo kama alivyosema best hapo juu kwa sababu hii si charity work au kazi ya serikali.

Hata unapomuona Reginald Mengi anapanda miti au kuhimiza vita dhidi ya ukimwi usifikiri anafanya charity work, mahesabu kibao katika biashara hata unapogawa una invest pia katika ioyo ya watu wakuone mzalendo na wazidi kununua bidhaa zako wakijifariji part inaenda kwenye mazingira.

Sasa Vodacom tumeshindwa kuwabana wenyewe, hata mimi ningekuwa marketing manager nimepewa bottom line halafu watu wa Chuo Kikuu/ Wizara ya Elimu hawaleti proposals ila watu wa Miss Tanzania wanajaa kila siku ningekuwa na wakati mgumu kuwapa watu wa Chuo Kikuu au Jiji priority.
 
Mwanakijiji nani alikuambia tatizo la uchafu kwenye miji yetu ni hela? Mbona hata hao wanaoingoza hiyo miji hawajui kama ni michafu? Uchafu huko kwenye vichwa vya viongozi wetu na ndio tunatakiwa kuuondoa huko kwanza kabla ya kuanza kuisafisha hiyo miji. Otherwise nawaunga mkono Vodacom!
 

Vodacom kama wana nia Nzuri hawana haja ya kuiga mifano hii. Siku hizi nasikia hata mazoezi kwa vitendo kwa watanzania walipiga marufuku.
 
.. Uchafu uko kwenye vichwa vya viongozi wetu na ndio tunatakiwa kuuondoa huko kwanza kabla ya kuanza kuisafisha hiyo miji.

This could be the best quote of the week! yaani imekaa kiukweli ukweli kichizi! shukurani. You just made my day.
 

Hao viongozi wetu tunawachagua wenyewe tukijua uchafu ulioko kwenye vichwa vyao. Swali, je yawezekana na sisi wananchi vichwa vyetu vimejaa uchafu? Nauliza kwa sababu hawa viongozi wachafu tunawachagua kila chaguzi huku tukijua uchafu wao.....labda uchafu wa vichwa vyao ni reflection ya jamii inayowachagua....just thinking
 

wewe bwana mzee unapiga hadi ikulu kwa kweli .Ndiyo hivyo wachafu wanashiriki uchafu so figure out
 
Makodi na maushuru kedekede tunayolipa yanatosha kusafisha miji yetu, mbona miaka ya nyuma kulikuwa hamna Vodacom wala TIGO na jiji lilikuwa linang'ara? Viongozi wetu hawalioni suala la usafi kama priority. Makampuni yanapeleka pesa zao kwenye masuala ambayo kuna interest za wengi and Im afraid Usafi siyo moja ya mambo hayo.
 

Huko sawa mkuu

Hata kule South Africa kuna kitu sheria za nchi ndizo zinazosaidia. Baada ya utawala wa kibaguzi waliweka kitu kimoja walioko huko watanikosoa.

Walisema Makampuni hata yakilipa mishahara kiasi gani hayawezi kuwalipa watu kadri wanavyo taka(according to their investments in knowledge) bado vipato ni vidogo walicho hamua ni kwamba kunatakiwa Elimu, lazima pamoja na makampuni kulipa kodi yawekeze katika kuwasomesha wananchi.

Kwa hiyo mwisho wa mwaka unapeleka mahesabu umesomesha wangapi mwaka huu? Hiyo inaweza kukusaidia hata kupewa some insentive kwenye maswala ya kodi(tatizo hili ukiliweka kwetu itakuwaje). kuna kipindi Vijana hata walikuwa wanagomabiwa katika kupewa udhamini. Hasa hasa target ilikuwa katika makampuni ya madini yanayokuwa yanawaachia mashimo.
 

Mwakjj:

Sasa wao watakuwa wanafanya biashara au wanaongoza miji? Kumbuka michango yote ya makampuni ya biashara ni kwenye Brand Awareness na Brand value.

Kwa kutumia mashindano ya Urembo au Timu ya Taifa, brand yao inatangazwa nchi nzima na kuendelea. Kwa usafi, brand inabaki local.
 
warembo wengi hawana kazi, kupitia fani ya urembo wanaweza kujikimu na maisha hivyo kutojiingiza katika shughuli zingine chafu ambazo zinaweza hata kuhatarisha maisha yao na ya wengi.

Inapotokea kampuni ya kudhamini fani ya urembo ni vema kutoibeza kwani wanawezesha wengine ambao wanaona urembo ni fani yao.
 

Kakindo,

Capitalistic businesses main objective is to make profit for shareholders. All this other business about giving back to the community must be enforced, they will not hand it to you on a silver plate, you have to take it.

Ninachosema ni kuwa, kama Vodacom hawatoi kwa worthy causes kwa sababu hatuwabani huwezi kuwalaumu Vodacom, laumu sisi ambao hatuwabani.

Businesses will always try to get away with what they can, pay as little taxes as possible and maximize profit.Sielewi tunailaumu vipi kampuni ya kigeni inayofanya kazi kwetu chini ya sheria na statutes zetu, enforce the law and lobby for a more socially responsible and meaningful contribution.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…